VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Sasa mnayumba;mnapoteza mwelekeo. Nyinyi tunawategemea kama wapinzani wakuu Tanzania. Wabunge wenu 49 Bungeni Dodoma wanafanya kazi inayotukuka na kukonga nyoyo za watanzania wengi.Wabunge wenu ni watetezi,wajenzi wa hoja,waibua mijadala ya kujenga Taifa,walinda maslahi ya nchi,hawayumbishwi haraka na sifa nyinginezo wazistahilizo viongozi wa kupigiwa mfano. Lakini chamani ni tofauti.
Iweje myumbishwe na masuala madogo madogo ya kisiasa kirahisi namna hiyo? Kweli nawaambia, mtatingishwa na wapinzani wenu kirahisi msipojirekebisha. Kiukweli, mmepambana vya kutosha. Kuanzia kuitwa chama cha kikabila,kikanda,kidini na kigaidi. Mapambano hayo mkayashinda. Sasa wanatumiwa watu kufitisha viongozi chamani. Wanatumiwa akina Zitto,Shibuda na sasa Samson Mwigamba. Hawa wanatumiwa tu.Wanachorwa kwenu kama wasaliti na waropokaji. Nanyi mnaelekea kuamini. Mtasambaratika kiuongozi.
Kwa Zitto ilitosha kauli yake kuwa 'anachonganishwa na viongozi wake na aachwe afanye siasa'. Kwa Shibuda inatosha kunyamaa kama mfanyavyo. Kwa Mwigamba, yatosha kusimamia tamko lenu la kichama la Kanda ya Kaskazini na taratibu nyingine kufuata. Milango hii hatari kwenu ifungwe haraka. Laasivyo, itaingiza maadui na uadui.
Sasa mnashupaliwa kuhusu Katiba ya chama. Itoshe kusema kuwa mtanzania yeyote mwenye ushahidi wa ubatili wa Katiba ya CHADEMA aende na nyaraka zake kwa Msajili wa Vyama vya Siasa kuilalamikia.Msajili atafuata sheria.Atashughulikia suala hilo haraka na hadi mwisho wake.Jaji Mutungi anamsubiri mtanzania huyo!
CHADEMA niwaambie, kuna watu hapa Lumumba na Ofisi nyingine wamenunuliwa 'Ipads' na 'Iphones' kupambana nanyi mtandaoni. Hasa hapa JF. Watawalia muda wenu na kuwasimamisha. Mkichelewa kuchukua hatua,mipango yenu mingi itakwama.Mtadhoofu.Wapenda demokrasia kama mimi tutabaki na huzuni kuu.Tunahitaji upinzani bora nchini ili CCM yetu ifanye bora zaidi.Tunahitaji CCM yetu ibanwe ili itoe matunda vutizi.
Kwa kifupi, CHADEMA hamna haja ya kuchonganishwa kila kukicha. Please, do not expose your weak points easily. Wanaotajwa watajwe;wanayosema yaripotiwe;anayelalama alalame lakini CHADEMA songeni mbele mjenge demokrasia. Tunatarajia mechi kali ya kisiasa hapo 2014 na 2015. CHADEMA beware!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Iweje myumbishwe na masuala madogo madogo ya kisiasa kirahisi namna hiyo? Kweli nawaambia, mtatingishwa na wapinzani wenu kirahisi msipojirekebisha. Kiukweli, mmepambana vya kutosha. Kuanzia kuitwa chama cha kikabila,kikanda,kidini na kigaidi. Mapambano hayo mkayashinda. Sasa wanatumiwa watu kufitisha viongozi chamani. Wanatumiwa akina Zitto,Shibuda na sasa Samson Mwigamba. Hawa wanatumiwa tu.Wanachorwa kwenu kama wasaliti na waropokaji. Nanyi mnaelekea kuamini. Mtasambaratika kiuongozi.
Kwa Zitto ilitosha kauli yake kuwa 'anachonganishwa na viongozi wake na aachwe afanye siasa'. Kwa Shibuda inatosha kunyamaa kama mfanyavyo. Kwa Mwigamba, yatosha kusimamia tamko lenu la kichama la Kanda ya Kaskazini na taratibu nyingine kufuata. Milango hii hatari kwenu ifungwe haraka. Laasivyo, itaingiza maadui na uadui.
Sasa mnashupaliwa kuhusu Katiba ya chama. Itoshe kusema kuwa mtanzania yeyote mwenye ushahidi wa ubatili wa Katiba ya CHADEMA aende na nyaraka zake kwa Msajili wa Vyama vya Siasa kuilalamikia.Msajili atafuata sheria.Atashughulikia suala hilo haraka na hadi mwisho wake.Jaji Mutungi anamsubiri mtanzania huyo!
CHADEMA niwaambie, kuna watu hapa Lumumba na Ofisi nyingine wamenunuliwa 'Ipads' na 'Iphones' kupambana nanyi mtandaoni. Hasa hapa JF. Watawalia muda wenu na kuwasimamisha. Mkichelewa kuchukua hatua,mipango yenu mingi itakwama.Mtadhoofu.Wapenda demokrasia kama mimi tutabaki na huzuni kuu.Tunahitaji upinzani bora nchini ili CCM yetu ifanye bora zaidi.Tunahitaji CCM yetu ibanwe ili itoe matunda vutizi.
Kwa kifupi, CHADEMA hamna haja ya kuchonganishwa kila kukicha. Please, do not expose your weak points easily. Wanaotajwa watajwe;wanayosema yaripotiwe;anayelalama alalame lakini CHADEMA songeni mbele mjenge demokrasia. Tunatarajia mechi kali ya kisiasa hapo 2014 na 2015. CHADEMA beware!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam