CHADEMA mmekuwaje tena???

CHADEMA mmekuwaje tena???

Mambo hadharani hakuna chama hapo ila ni genge la wajanja wachache waliojiunga na kuanzisha kikundi chao.kwa mwendo huo mlio nao hamtoweza kamwe kuingia magogoni.

mnajifanya mnapigania democracy kumbe mnapigania matumbo yenu,Big up ZITO ZUBERI KABWE MWANA MWANDIGA umeamua kujiweka pembeni na siasa za maji mataka.:smile-big:wana uana wenyewe kwa wenyewe.
hasan kazukamwe mtot wa kigoma na zito wake sijui mnaendesha siasa za namna gani, full ukabila na ukanda, alf ww operation kimbunga inahitaji ikukumbe urudi kwenu burundikwenye asili y akwenu
 
Ni mapambano baina Chadema Kanda ya Ziwa Vs Chadema Moshi-Arusha.

unaongelea kanda ya ziwa ipi? ziwa magharibi au z.victoria? kama ni z.victoria huku cdm inatisha na inaukubali uongozi uliopo.acha kuandika bila kutafiti,yaani upo nyuma ya keyboard daresalama halafu unaongelea kanda ya ziwa! wewe kweli juha.
 
unaongelea kanda ya ziwa ipi? ziwa magharibi au z.victoria? kama ni z.victoria huku cdm inatisha na inaukubali uongozi uliopo.acha kuandika bila kutafiti,yaani upo nyuma ya keyboard daresalama halafu unaongelea kanda ya ziwa! wewe kweli juha.
Na wewe ukileta ngebe utazimwa kama walivyozimwa hawa wa kanda ya ziwa akina Amani Kabouru, Chacha Wangwe, Zitto Kabwe, Samson Mwigamba, John Shibuda, Mkosamali, Shitalamba, Kafulila nk. Salama yako ni kuendelea kuwa Msukule.
 
Tatzo wengne hawaelewi. Kazi kumponda zitto tu kisa anasifiwa na maccm.kwani yeye aliomba asifiwe? Siku tundu lissu akisifiwa na maccm naye mtasema anatumiwa? Tunachonganishwa nasisi tunakubali.

Mkuu fanya tafakuri kwa kina,hivi kwa akili zako unaamini kabisa kwa sisas za Tanzania,na kwa chuki za ccm kuichukia CHADEMA,hivi unaona ni jambo jepesi tu wakatoka huko watokako hao CCM wakamsifia kiongozi mahiri wa CDM kama anaijenga CDM?
CCM wanamsifia yule wanaemtumia.kama hujui siasa za bongo acha kuandika vitu usivyovijua.
 
Hii habari ilikuwemo humu ikatolewa

[wanabidii] UFISADI WA ZITTO ZUBERI KABWE

Wednesday, October 30, 2013​
kauli yake inadhihirsha tabia zake za kisaliti.​
anataka kuficha maovu yake ya kupokea Million 250 CRDB na zile Dolla laki 2 na ushee kupitia German.​
Huyu bwana ni msaliti na kwa wajuzi wa mambo mtaona ni kwanini hakuandamana na dr slaa wakati wa kampeni za urais​
CCM wana mtumia na walishamtumia siku nyingi na innafaa atemwe cheo chake kabla ya 2015 atakiangamiza chama.​
Zito your finished man, nlikuamini lakini baada ya kusoma post inayokuhusu wewe sina imani nawe kanisa​
Umethamini hela kuliko maisha ya sisi walalahoi tunaotegemea ukombozi wa kweli......​

Riporti ya siri inaeleza ukweli 23/6/2008 saa 07:52 ulikutana na kina Wassira na mtu wa usalama wa Taifa sea cliff​
30/6/2008 Ulipokea mshiko wako CRDB Bank kiasi 250Tsh Million.​
Kisha Jumatano ya tarehe 16/12/2009 majira ya saa 13:12 za mchana​
kwa Ujerumani akaunti namba .............................,​
ziliingizwa dola za kimarekani 266,000 pesa hizi katika​
uchunguzi zimebainika kuwa zilitoka Tanzania katika Benki ya​
NMB Dar katika akaunti namba​
.............................. ... yenye jina la TSA,​

Fedha hizo alizichukua ili kutoa taarifa za siri za chadema na aliezipokea kwa niaba yake huko germani ni mwana mama alisoma nae nae akapewa Dola 25,000 kama ahsante...kweli tanzania hatuna wazalendo​

wakatoa na evidence hii Mfano tarehe 7/9/2010 siku ya jumanne saa 11:21 asubuhi,​
...............kupitia namba yake ya simu ya kiganjani​
......................, alimpigia Zitto kupitia simu ya kiganjani namba​
.............................. waliongea mambo mengi japo kwa muda mfupi, na​
jambo kubwa lilikuwa ni "vipi kuna kipya ndani ya Chadema?"​
Zitto alijibu "yapo mengi lakini hayana impact kwa ccm"​

LISEMWALO LIPO NA KAMA HALIPO LAJA.

NIWAULIZE MOOD KWANINI WALITOA HABARI NZIMA ISIACHWE IKASOMWA NA JF TUKAMPIMA ZITO????


nlibahatika kukariri chache.

kwa sasa ipo WANABIDII BLOG: [wanabidii] UFISADI WA ZITTO ZUBERI KABWE
 
Mtei alipomkabidhi uenyekiti Bob Makani, katiba ikabadilishwa na kikaingizwa kipengele cha ukomo wa vipindi viwili. Alipokabidhiwa Mbowe uenyekiti, kipengele hicho kikafutwa bila kushirikisha wanachama katika maamuzi hayo!!!​
 
Hakika CDM imefanya vijana wengi wakaajiriwa pale lumumba. Bila cdm mngelipwaje akina Ze marco Lizabon Simiyu Yetu.
 
Sasa mnayumba;mnapoteza mwelekeo. Nyinyi tunawategemea kama wapinzani wakuu Tanzania. Wabunge wenu 49 Bungeni Dodoma wanafanya kazi inayotukuka na kukonga nyoyo za watanzania wengi.Wabunge wenu ni watetezi,wajenzi wa hoja,waibua mijadala ya kujenga Taifa,walinda maslahi ya nchi,hawayumbishwi haraka na sifa nyinginezo wazistahilizo viongozi wa kupigiwa mfano. Lakini chamani ni tofauti.

Iweje myumbishwe na masuala madogo madogo ya kisiasa kirahisi namna hiyo? Kweli nawaambia, mtatingishwa na wapinzani wenu kirahisi msipojirekebisha. Kiukweli, mmepambana vya kutosha. Kuanzia kuitwa chama cha kikabila,kikanda,kidini na kigaidi. Mapambano hayo mkayashinda. Sasa wanatumiwa watu kufitisha viongozi chamani. Wanatumiwa akina Zitto,Shibuda na sasa Samson Mwigamba. Hawa wanatumiwa tu.Wanachorwa kwenu kama wasaliti na waropokaji. Nanyi mnaelekea kuamini. Mtasambaratika kiuongozi.

Kwa Zitto ilitosha kauli yake kuwa 'anachonganishwa na viongozi wake na aachwe afanye siasa'. Kwa Shibuda inatosha kunyamaa kama mfanyavyo. Kwa Mwigamba, yatosha kusimamia tamko lenu la kichama la Kanda ya Kaskazini na taratibu nyingine kufuata. Milango hii hatari kwenu ifungwe haraka. Laasivyo, itaingiza maadui na uadui.

Sasa mnashupaliwa kuhusu Katiba ya chama. Itoshe kusema kuwa mtanzania yeyote mwenye ushahidi wa ubatili wa Katiba ya CHADEMA aende na nyaraka zake kwa Msajili wa Vyama vya Siasa kuilalamikia.Msajili atafuata sheria.Atashughulikia suala hilo haraka na hadi mwisho wake.Jaji Mutungi anamsubiri mtanzania huyo!

CHADEMA niwaambie, kuna watu hapa Lumumba na Ofisi nyingine wamenunuliwa 'Ipads' na 'Iphones' kupambana nanyi mtandaoni. Hasa hapa JF. Watawalia muda wenu na kuwasimamisha. Mkichelewa kuchukua hatua,mipango yenu mingi itakwama.Mtadhoofu.Wapenda demokrasia kama mimi tutabaki na huzuni kuu.Tunahitaji upinzani bora nchini ili CCM yetu ifanye bora zaidi.Tunahitaji CCM yetu ibanwe ili itoe matunda vutizi.

Kwa kifupi, CHADEMA hamna haja ya kuchonganishwa kila kukicha. Please, do not expose your weak points easily. Wanaotajwa watajwe;wanayosema yaripotiwe;anayelalama alalame lakini CHADEMA songeni mbele mjenge demokrasia. Tunatarajia mechi kali ya kisiasa hapo 2014 na 2015. CHADEMA beware!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

@Dr.W.Slaa
 
Kumekuwa na misigano mingi inayoendelea katika mitandao ya kijamii hususan katika masuala ya posho na mashambulizi baina ya mtu na mtu mfano ni Zitto na Lema sasa, kinachonisikitisha ni kuona viongozi wa juu wamekaa kimya hawalioni hili dk wewe ni mtendaji wa chama hawa wapo chini yako jitokeze utuambie kama huu ndiyo mfumo mpya wa chama uliochaguliwa na kupitishwa na kwanini kama si mfumo rasmi haikemewi
 
Unataka waongee kwenye mtandao nao au kwenye magazeti? hii itasaidia nini? malumbano ni kukua na kama hakuna matusi malumbano yaendelee
 
Kumekuwa na misigano mingi inayoendelea katika mitandao ya kijamii hususan katika masuala ya posho na mashambulizi baina ya mtu na mtu mfano ni Zitto na Lema sasa, kinachonisikitisha ni kuona viongozi wa juu wamekaa kimya hawalioni hili dk wewe ni mtendaji wa chama hawa wapo chini yako jitokeze utuambie kama huu ndiyo mfumo mpya wa chama uliochaguliwa na kupitishwa na kwanini kama si mfumo rasmi haikemewi

Ugonvi wa jiran unakuhusu nn?Fanya mambo yanayokuhusu ili cku isikupite kwa kuhangaikia yasiyokuhusu.
 
Back
Top Bottom