Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,024
- 9,442
Ndugu zangu Hivyo Ndivyo Hali Ilivyo kwa Sasa, Kasi ya Rais Samia kuwatumikia watanzania wa makundi yote,vyama vyote, Rika zote, jinsia zote, Kanda zote, Dini zote,makabila yote,maeneo yote na watu wa Hali zote bila ubaguzi wa aina yoyote kumeipoteza Chadema Katika Ramani ya siasa hapa nchini na kubakia chama Cha kurukia vimatukio vya kupita kama upepo.
Hii inatokana na kazi kubwa ya Rais Samia aliyoifanya ndani ya muda mfupi katika kuwatumikia watanzania, kila kundi na kila mtu kwa Sasa anamuona mama Samia kuwa Ni Rais wake, Ndio sababu ukienda secta binafsi utakuta anapongezwa kwa kuweka mazingira mazuri ya kiuwekezaji, ukienda kwa wafanyabiashara utakuta wanampongeza kwa kufanya mazingira ya biashara kuwa rafiki kwao.
Ukienda kwa wakulima utakuta anapongezwa kwa namna alivyo wasaidia wakulima kupungua kwa Bei ya mbolea na kupongezwa kwa bajeti ya Wizara ya kilimo kuongezeka, ukienda kwa wanafunzi wa vyuo vikuu utakuta wanampongeza kwa namna alivyowasaidia kupata Elimu baada ya kuwa wamepewa mkopo wa elimu ya juu, ukienda kwa wafugaji, wavuvi, wajasiriamali, bodaboda, machinga, watumishi wa umma, vijana, wazee,wakina mama wote utakuta wanampongeza Rais Samia kwa kuwasaidia katika shughuri zao na kuwawekea mazingira wezeshi.
Makundi haya ambayo yanamuunga mkono mama Samia Ndio yalikuwa Tegemeo la Chadema kuendeshea propaganda zake na kupandikiza chuki kwao ili waichukie CCM na serikali yake, Ndio maana ulikuwa ukiona makundi haya muda mwingi yanatupa lawama kwa serikali kuwa inayadidimiza kiuchumi, wafanyabiashara wakawa wanalia Sana kuwa wanakomolewa Sana katika suala Zima la ukadiliwaji wa kodi, hivyo wakawa wanawaunga mkono upinzani na hata kuwachangia fedha.
Lakini kwa Sasa baada ya Rais Samia kukaa na viongozi wa makundi Tofauti Tofauti ikiwemo viongozi wa machinga, kukaa na wachungaji, maaskofu, mashehe, vijana na wengine wengi na kuweza kuwasikiliza na kutatua kero zao na kutoa matumaini, Sasa makundi haya yamejenga Imani kubwa Sana kwa Rais mama Samia, yanamuunga mkono Rais kwa Sasa, yanamsikiliza na kumheshimu mh Rais kwa Sasa na yanajivunia Sana mama Samia kuwa Rais wao.
Hapa ndipo upweke wa chadema ulipoingilia maana kwa Sasa chadema imepuuzwa, haisikilizwi na mtu, haiungwi mkono na mtu, haifuatiliwi na watu Kama zamani, haina ushawishi kwa kundi lolote huku mitaani, Haina ngome ya kundi lolote au mkoa wowote, Haina mizizi yoyote kwa Sasa,imebaki Kama Tawi tu linaloelea na linalosubili kuangushwa na upepo mdogo tu, Chadema imekata Tamaa Sana, imejichokea,imepoteza mvuto kwa watanzania wa Rika zote.
Chadema kwa Sasa haina Sera Wala ajenda za kueleweka na wananchi, lakini kibaya zaidi Ni kuwa imekosa Dira na muelekeo hivyo kubaki inaenda tu Kama gari iliyokosa Taa usiku, Hii ni kutokana na kuwa mama Samia kabeba Sera na ajenda zote muhimu zenye kugusa maisha ya watanzania wa makundi yote na Rika zote na hivyo kuungwa mkono na makundi hayo yote.
Poleni Sana chadema, Ukurasa wenu ulishafungwa na watanzania, mizizi yenu ilishatupwa baharini,Huwezi kusimama Tena, wakati wenu ulishapita, Hamna namna zaidi ya kumuunga mkono Rais Samia kwa Sasa, msione aibu maana Wote Tupo na Samia, wote waliopoteza matumaini Sasa Wana matumaini na Imani na Rais Samia kuwavusha darajani, msishupaze shingo zenu maana mtaishia kuumia tu, watanzania hawana habari nanyi Tena ndio maana hawawasikilizi kwa lolote zaidi ya kuwapuuza tu na kuwaona wababaishaji, Huku Rais Samia akizidi kuchanja mbuga katika MIOYO ya mamillioni ya Watanzania.
Kazi iendeleee, mama Ametufikia na kuwafikia Watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti
Lucas Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
Hii inatokana na kazi kubwa ya Rais Samia aliyoifanya ndani ya muda mfupi katika kuwatumikia watanzania, kila kundi na kila mtu kwa Sasa anamuona mama Samia kuwa Ni Rais wake, Ndio sababu ukienda secta binafsi utakuta anapongezwa kwa kuweka mazingira mazuri ya kiuwekezaji, ukienda kwa wafanyabiashara utakuta wanampongeza kwa kufanya mazingira ya biashara kuwa rafiki kwao.
Ukienda kwa wakulima utakuta anapongezwa kwa namna alivyo wasaidia wakulima kupungua kwa Bei ya mbolea na kupongezwa kwa bajeti ya Wizara ya kilimo kuongezeka, ukienda kwa wanafunzi wa vyuo vikuu utakuta wanampongeza kwa namna alivyowasaidia kupata Elimu baada ya kuwa wamepewa mkopo wa elimu ya juu, ukienda kwa wafugaji, wavuvi, wajasiriamali, bodaboda, machinga, watumishi wa umma, vijana, wazee,wakina mama wote utakuta wanampongeza Rais Samia kwa kuwasaidia katika shughuri zao na kuwawekea mazingira wezeshi.
Makundi haya ambayo yanamuunga mkono mama Samia Ndio yalikuwa Tegemeo la Chadema kuendeshea propaganda zake na kupandikiza chuki kwao ili waichukie CCM na serikali yake, Ndio maana ulikuwa ukiona makundi haya muda mwingi yanatupa lawama kwa serikali kuwa inayadidimiza kiuchumi, wafanyabiashara wakawa wanalia Sana kuwa wanakomolewa Sana katika suala Zima la ukadiliwaji wa kodi, hivyo wakawa wanawaunga mkono upinzani na hata kuwachangia fedha.
Lakini kwa Sasa baada ya Rais Samia kukaa na viongozi wa makundi Tofauti Tofauti ikiwemo viongozi wa machinga, kukaa na wachungaji, maaskofu, mashehe, vijana na wengine wengi na kuweza kuwasikiliza na kutatua kero zao na kutoa matumaini, Sasa makundi haya yamejenga Imani kubwa Sana kwa Rais mama Samia, yanamuunga mkono Rais kwa Sasa, yanamsikiliza na kumheshimu mh Rais kwa Sasa na yanajivunia Sana mama Samia kuwa Rais wao.
Hapa ndipo upweke wa chadema ulipoingilia maana kwa Sasa chadema imepuuzwa, haisikilizwi na mtu, haiungwi mkono na mtu, haifuatiliwi na watu Kama zamani, haina ushawishi kwa kundi lolote huku mitaani, Haina ngome ya kundi lolote au mkoa wowote, Haina mizizi yoyote kwa Sasa,imebaki Kama Tawi tu linaloelea na linalosubili kuangushwa na upepo mdogo tu, Chadema imekata Tamaa Sana, imejichokea,imepoteza mvuto kwa watanzania wa Rika zote.
Chadema kwa Sasa haina Sera Wala ajenda za kueleweka na wananchi, lakini kibaya zaidi Ni kuwa imekosa Dira na muelekeo hivyo kubaki inaenda tu Kama gari iliyokosa Taa usiku, Hii ni kutokana na kuwa mama Samia kabeba Sera na ajenda zote muhimu zenye kugusa maisha ya watanzania wa makundi yote na Rika zote na hivyo kuungwa mkono na makundi hayo yote.
Poleni Sana chadema, Ukurasa wenu ulishafungwa na watanzania, mizizi yenu ilishatupwa baharini,Huwezi kusimama Tena, wakati wenu ulishapita, Hamna namna zaidi ya kumuunga mkono Rais Samia kwa Sasa, msione aibu maana Wote Tupo na Samia, wote waliopoteza matumaini Sasa Wana matumaini na Imani na Rais Samia kuwavusha darajani, msishupaze shingo zenu maana mtaishia kuumia tu, watanzania hawana habari nanyi Tena ndio maana hawawasikilizi kwa lolote zaidi ya kuwapuuza tu na kuwaona wababaishaji, Huku Rais Samia akizidi kuchanja mbuga katika MIOYO ya mamillioni ya Watanzania.
Kazi iendeleee, mama Ametufikia na kuwafikia Watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti
Lucas Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.