CHADEMA, Ludovick Rwezahula anaangamia mahabusu, utu uko wapi?

CHADEMA, Ludovick Rwezahula anaangamia mahabusu, utu uko wapi?

Status
Not open for further replies.
My Future Investment..................., YES!!! Now you are.

NCHEMBA.JPG

Mwigulu ana moyo wa utu sana. Ingawa ana mapungufu mengine ya kibinadamu, lakini ana utu.
 
Nani kasema anapata shida huko Mahabusu!!?? Mtu anapiga simu kwa demu wake mpaka wakati wa longa longa jamani!! Kinachomsumbua si kingine bali aibu ya waliomtuma. Sio huyo Naibu Katibu Mkuu wala Wanashomire wenzake washirikishwa wote wana aibu kibao ndio maana wanamuogopa lakini yuko fine tu mahabusu. Mpaka mara ya mwisho alikuwa kashapewa kama Mil 2 hivi nasikia lakini akikubali masharti ya Bwana wake atamaliziwa mpaka zifike Mil 30 eti. Ila mkataba wake pamoja na mambo mengine ulikuwa una malipo ya kila mwezi kwa familia yake nasikia ni kama laki 7 hivi Mwigulu anatoa kwa mke wake ili mambo yaweze kwenda. Mkataba ni wa miezi 4 hadi 5 toka kukamatwa kwake. Kwa hiyo Hammy-D usijitie ujinga wakati dili unalijua barabara!! Watamtoa tu usijali ngoja tusahausahau na kesi ya Tabora iende ende kidogo waone kama dili litawezekana au la. Unaweza kudanganya watu wote kwa muda fulani tu sio wakati wote Kaka.
 
Nadhani cha kufahamu hapa ni kwamba Je nyaraka hizo zinazotakiwa Mahakamani zinatakiwa kutolewa na ndugu zake au chama.kama ni ndugu basi hakuna haja ya kuibebesha CDM lawama.
Hata hivyo,swala la kumdhamini mtu si jambo dogo. Jamaa akitoka akakuchomoka,mashitaka yanahamishiwa kwako wangu. Kama Ludo aliweza kufanya usaliti wa namna ile,nani anaweza kumwamini na kumdhamini?
Nadhani,huko aliko ni mahali salama sana kwake kuliko sehemu nyingine yoyote coz jamii inamhukumu kama msaliti na akija uraiani anaweza kuambulia kifo cha mawe.
Kama tu ndugu zake wa damu,mke,wazazi hawataki kuonyesha ushirikiano. Wewe kama nani ujifanye unataka kusaidia?unauchungu naye sana?unamjua vema kuliko wao?
 
Mwambie Boss wake Mwigulu Nchemba amkumbuke akamtoe jela. Jana alikuwa Taifa anakikipiga dhidi ya wabunge wa Simba na aliibuka kidedea 4-3. Ingekuwa Enzi za Umkontwe we Sizwe adhabu yake ni "Fire Necklace" i.e. Tairi la Moto Shingoni. Ebo!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Moderators, threads kama hizi ni za kijinga.

Kwenye video hii Mwigulu anasema mwenyewe anatamka kuwa alimtuma kurekodi mkanda, akampa vitendea kazi, na kisha akakabidhi kanda.

Mkanda huu ndio sababu ya yeye kuwa ndani.

Sasa moderators, kama jukwaa hili bado linataka kujikita katika ukweli, hii thread inapaswa kufutwa hapa.

Mnaendekeza propaganda za kitoto sana, ambazo hazitujengi kama taifa bali zinatujengea chuki kati ya wananchi.



cc. Paw, Invisible
 
Last edited by a moderator:
Nadhani ludovick akae huko jela milele, sababu tangu amekamatwa hakuna tena taarifa taka zinazovuja toka Chadema
 
CHADEMA ni mchungaji mwema anayewajua kondoo wake,unaona ni jinsi gani inavyawapigania makada wake waliowekwa ndani kwa sababu kukipigania chama.rudovick mlimutumia nyinyi msimtelekeze hata kama ka dili kamewagomea.
 
Tumeanza na mungu tutamaliza na mungu, malipo duniani, bado mwigulu na vibaraka wengine....... Coming soon!!!!! Mnafikiri tanzania ni watu wenye akili ndogo?????
 
Nani kawaambia ludovick anateseka huko aliko? Mmesahau wakati alitakiwa awe mahabusu walisahau na simu yake ileendelea kupigia watu kadhaa. Naaamini hayuko mahabusu, amepelekwa Leo iliakashiriki kesi. Na kwa upande mwingine hata ningekuwa mimi salama yangu ni keko kuliko huku mtaani. Tunapoteza muda kuijadili hii hoja.
 
kma kosa lake lilikuwa ni kuibua siri ya mikakati ya kishetani ya CHADEMA dhidi ya waandishi wa habari, basi nadhani kuna siku mwanga wa mungu utamuangazia kwa sababu alifanya vile kwa maslahi mapana ya taifa.
kinachonifurahisha kuhusu hili sakata la lwakatare ni jinsi wana chadema wanavyojiumauma na kujikanganya kuhusu ile video. naona sasa wamehama kutoka kwenye'' VIDEO FAKE'' mpaka kwenye 'LUDOVIC MSALITI'''.
Mwisho wa hili sakata uko wazi.. LWAKATARE ATAFIA JELA KAMA MFUNGWA na LUDOVIC atasalimika.
just stay tuned

Mkuu usijitie uzuzu kwa makusudi, very simple Ludo msaliti zaidi ya Yuda kwa kushiriki kutengeneza video feki ya ugaidi ambayo hata mahama kuu imeikataa..hulioni hilo au mahaba na chama yamekuzidi uwezo!!!!
 
Hio ndio CHADEMA yenye kauli mbiu"tumeanza na Mungu na tunamaliza na Mungu".Huyo Mungu anaefundisha lipa baya kwa baya maradufu ni yupi?maneno ya nabii isa mwenyewe yani yesu amesema"samehe saba mara sabini"."akupigae shavu lakushoto basi mgeuzie na la kuume".

Lakini CHADEMA mnaona sahihi kabisa kumuhukumu Rudo.Mungu ni mwenye huruma na ndio maana pamoja na makosa ye2 bado tunaishi,Dr mpaka sasahivi anaishi na kima.da yeye anaona ni sahihi kabisa tena anafika hatua yakwenda na kima.da hata Izrael hija
 
hapa naona udhaifu mkubwa sana kufanywa na kiongozi wa juu wa taasisi.
hivi katika 'mpango nyeti' kama huu aliwezaje kumtumia mtekelezaji pesa kwa simu yake bila kushtuka kuwa itajulikana kirahisi na kurahisisha ushahidi!?


Hilo sio tatizo, Ndio maana hadi leo hajawahi kuitwa kuthibitisha na huenda hatoitwa milele. Yuko juu ya sheria zote duniani kwa wakati huu, Mwacheni anywe maji ya faraja ya muda mfupi wa duniani.
Hata hivyo ukiangalia chaguzi zote si ndio hao hao husambaa mitaani na kugawa 5,000 na vipande vya kanga?. Hata hivyo huyo alipewa dau la kutosha sana.
 
Halfu imekaa vibaya....sasa ajishuhudie mwenyewe kwanini alichukua mkanda yeye ila hakureport polisi kabla ya wewe Mwigulu?Halafu k umwekea dhamana huwezi kwa vile unajidai huusiki kumtuma.....
 
hivi chama kinaweza kumdhamini mtuhumiwa? Sijawahi kusikia hii kitu, wataalamu embu nielewesheni kwa hili?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom