Nashukuru kwa mawazo na mchango wako..
Kuna wakati lazima tujifunze kuwa wakweli na tuuzungumze ukweli wote, sio kwa kuficha ficha, sio kwa kuoneana haya wala si kwa kusimangana bali kwa nia njema ya kujenga.
Yericko Nyerere - A story teller kumtaja hadharani kuwa ana IQ ndogo sio tusi..,kuna wakati nilikuwa nae kwenye group moja ya WhatsApp akawa kila asubuhi na jioni analeta taarifa za uzushi na uongo, na mkimkosoa leo asubuhi jioni anarudia tena kuwaletea kisa kingine..nikamwambia wazi kuwa shida aliyokuwa nayo ni UWEZO mdogo wa UBONGO wake..sio tusi ni UKWELI.
Kama kweli mdogo wangu unaju kuwatusi watu jaribu kumuita Nape matusi uliyokuwa ukiyatoa au unayoyatoa kwa kwa Yeriko tuone hata kama utaruhusiwa kuvaa hata shati la kijani
Ama kuhusu MBOWE, kabla ya hapo, naomba nikuthibitishie kuwa hakuna mtu ambaye hakuwahi kutofautiana na MBOWE katika uendeshaji wa Chama kwa muda mrefu kuliko mimi pale ambapo alitenda sawasawa, nilisimama kila wakati kwenye vikao vyetu, nikatanguliza neno SHUKRANI Mwenyekiti umetuvusha kwa hili na hili, nilimsifu katika kila jema, lakini bahati mbaya sana kwa Wafalme wetu hawajui kuwa kuna kusifiwa na kukosolewa..kwao kukosolewa ni kuvunjiwa heshima...
Pia jaribu kumtukana Mwenyekiti JK kama ambavyo ulimtukana Mbowe ndipo utaona rangi zote. Si kuwa kila aliyekaa kimya ndani ya chama au taasisi anakubalina kila kitu na viongozi wa juu. Tatizo hapa ni kuwatusi wakubwa zako na ninavyokufahamu tayari umeshang'atwa na nyoka hata ujani utuogopa. Laiti kama waliokulea wangekuacha uendelee na tabia ya kuwatusi viongozi wako usingeweza kuwa kiongozi unayejisisfia kuwa. Big UP CDM for bringing you!!!
Siku ya Kwanza kabisa kutofautiana na MBOWE ni siku ambayo VIJANA WAWILI wa BAVICHA walipotakiwa kwenda UGANDA kwa mafunzo ya Kiungozi na Utawala (PYPA), Mimi na Mwenyekiti(HECHE) tukapanga wawakilishi wetu, ambao ni Vijana wapambanaji ambao tumekuwa tukiwatumia kwa muda mrefu bila kuwalipa fadhila yeyote, tukadhani nafasi ya kuwaendeleza, kuwaandaa imefika, tukapendekeza majina yao..SIKUAMINI kilichotokea.
Siku tatu kabla ya Safari, yaliletwa MAJINA ya watu ambao siwajui, sikuwahi kuwaona popote pale katika mapambano na harakati za BAVICHA, nikaambiwa watakwenda hao badala ya wale tuliowapitisha Mimi na Mwenyekiti (Moja ya jina nililoletewa ni JOHN MALLYA - Ambaye kwa sasa ndio mwanasheria wa Chama) BINAFSI nilipingana na MBOWE katika hili, tena wazi wazi...nikihoji UHALALI wa John Mallya na Mwenzake kwenda kwenye mafunzo hayo
Lakini kama hilo halitoshi, wakati kuna mfarakano na mvutano mkubwa wa kimtazamo ndani ya Chadema 2012, kuhusu kutosha kwa Mwenyekiti katika nafasi yake..Binafsi nilieleza kwa hoja ndani ya Kikao kwanini nadhani MBOWE asiendelee kwenye nafasi hiyo na badala yake ZITTO achukue kijiti..nilitoa sababu na vigezo (ambavyo kama itabidi nitavisema hapa siku moja) Huu ukawa ndio mwanzo wa VITA kamili kati yangu na MBOWE na TIMU yake.
Nilivumilia mengi mpaka kufikia hatua hiyo ya kumuiya ZERO ndani ya Kikao, na actually ni baada ya kuja na barua (fake) eti ya kukihujumu Chama, nikamwambia ikiwa Mwenyekiti u with all resource that U have bado unakubaliana na uzushi uliomo ndani ya barua hiyo na umefanya maamuzi based on that piece of sh&***t then wewe ni ZERO...ilikuwa hakuna namna nyingine ya maelezo, isipokuwa kuuweka UKWELI ninaouamini mbele ya wote.
Sikia, I believe on myself na naendelea kuona kuwa i'm an asset popote pale nilipo, the good thing CCM nimeaminiwa, nikakubaliwa na nikaruhusiwa kufanya na kutenda ninachokiamini....nimepelekwa shule, nimepelekwa darasa la itikadi ya CCM, nikapikwa upya namna bora ya kufanya siasa, nikaondolewa Uhanaharakati nikafundishwa siasa..nikajaribiwa na nikafuzu.
Hizo shule siku hizi ni short courses, tulikuwa tunahudhuria miezi 12 ili kuwa mwanachama wa CCM ya wakulima na wafanyakazi. Toka ikengeuke na kuwa ya wafanyabiashara uanachama ni vodafasta ndio maana Merehemu Kolimba halideclare openly kuwa CCM imepoteza dira na mwelekeo.
watanzania wa sasa wanachotaka ni mabadiliko na sio blah blah za chama fulani, na ninashukuru sana hata mgombea wenu amelitambua hilo ndio maana ana behave kama mgombea binafsi. Huo ni ushindi mkubwa kwa M4C japokuwa ni kweli baadhi ya makamanda wake wamejitosa baharini na kuliwa na mamba!!
Imani yao kwangu ni kubwa, ninachokiandika hapa kuhusu CHADEMA, kama ningekiandika nikiwa CHADEMA kuhusu CCM ningefukuzwa CHAMA, kwa sababu maamuzi yao yanazingatia zaidi mihemko na hisia.
Na ndivyo ilivyo....na ndivyo walivyo....wanaamua bila KUFIKIRI.