KUPOTEA...hivi unajua tafsir ya neno kupotea..??
Subiri shughuli yangu utaiona BUNGENI...MTANYOOOKA tu.
Kwa maana hiyo, basi hata wewe utafungwa, kwa sasa tunahitaji rais, kuna vigezo vya msingi vya kuvizingatia kama wananchi katika kumchagua rais, kwa mantiki hiyo inaonesha wewe hujaridhiwa na wagombea hawa wawili basi ungesimama wewe kugombea urais, tukuchague. Hata mzani huwa haulinganishi uzito kisawasawa bali hujaribu kuhsabiisha uzito wa jiwe na kitu kinachopimwa. Kwa maana hiyo hakuna kitu kilicho kamili, na hivyo hivyo tunafnya kwa mwanaadamu, hakuna aliye sahihi kisawasawa ila usahihi unazidiana, tumia akili za kuzaliwa. Wewe unatumia sana akili za shule, that's why
YERICKO NYERERE Anaishi katika uongo na uzushi, mpaka kila mmoja amemmpuuza, Mwanakijiji, Chahali na WATABE wengine wa maandishi yenye adili, wameikacha CHADEMA, bado CDM haijiulizi, inajivunia kuwa na YERICKO. Wasomi, watumishi, na wanataaluma wameikacha CHADEMA, bado CDM haijiulizi, wanajivunia madereva bodaboda.
Mwanz nilichosoma toka kwako ni uwezo wako wa kucheza na maneno.Sasa mimi nifungwe kwa kosa gani??
Na kwa kawaida uongozi hukurupuki, unapima uwezo ulionao kama unafit kwenye sox au viatu vya urais??
Waliokurupuka kwa nguvu kubwa ya pesa na maneno tumewaona namna walivyoendesha taasisi hiyo.Tumeshuhudia safari nyingi zisizo na tija.Tumeshuhudia familia ikifanya maamuzi badala ya taasisi.Hili ndilo lililo gufikisha hapa.
Jamani mwenye macho haambiwi tazama.Unaona mwenyewe tu.
Kumbe bado unaipenda CDM mbona unazidi kuifuatilia wakati umetimuliwa hii ni kama kuachana na mwenzi wako halafu unatoa siri,unadhani utapata kuungwa mkono kumbe unadharauliwa tu kwahiyo Juliana shoza wewe endeleza uliko si uliko tokaAMANI IWE JUU YENU ENYI WAJA WEMA WA BWANA MUNGU WANGU...!!
Katika muendelezo wa kuwafikirisha, nimeona leo niwaandikie kuhusu hali ya Upinzani na kampeni zinavyoendelea hapa nchini, ambapo hali ya sintofahamu ikiendelea kudhirihi kwa CHADEMA na Kambi yote ya Upinzani hapa nchini, wachambuzi mbalimbali, wasomi na waandishi wameendelea kuandika wakijaribu kuonyesha tatizo lililoikumba kambi hiyo, wengi wao wakisema FEDHA, vipande vya rupia vilivyoingia CHADEMA vimewafarakanisha. Nami Binafsi ktk muendelezo huo huo wa kuchambua hali hiyo nitaeleza CHANZO ama SABABU halisi ya SINTOFAHAMU inayoikumba kambi ya Upinzani.
Kwa Muhtasari sana, niseme CHANZO na SABABU HALISI ya Upinzani kukosa muelekeo na kufikia hapa tulipo ni OMBWE la UONGOZI katika kambi hiyo ikiongozwa na CHADEMA..Mimi niliwahi kuwa mwanachama wa CHADEMA, tena Kiongozi Mkubwa katika jumuiya yake ya Vijana, nilipata fursa ya kushiriki, kuhudhuria na kuchangia katika vikao na mikutano mikubwa, muhimu na nyeti ya Chama hicho.
Ilikuwa bayana kwetu kuwa, ilipofikia CHADEMA ilihitaji UONGOZI mpya utakaokuja na dira, maono na tafakuri mpya ambayo ingeki-transform chama hicho kuwa chama kamili cha siasa na kuondoa uongozi wa hamasa na mihemko ya kiuanaharakati..
Nikiwa ndani ya Vikao vya CHADEMA nikaliweka hili BAYANA kuwa tunalo ombwe la uongozi ndani ya CHADEMA, sikueleweka, nikaonekana natishia maslahi ya wakubwa na nafasi zao kwenye Chama, nikaonekana ADUI na nikapewa jina MSALITI.
Ukweli ni kwamba FEDHA ambayo leo imetajwa mara kadhaa kuwa ndio sababu kuu ya mfarakano ndani ya CHADEMA, imepata njia kutokana na Ukweli kuwa CHADEMA kuna Ombwe la Uongozi ambao umekosa Vision na Mission, ndio maana wakadhani FEDHA na UMAARUFU wa mtu ni mtaji wa wao kuingia Ikulu, wakasahau misingi, dhamira, imani na kiu ya Watanzania.
CHADEMA haina tabia ya kujitafakari, haijisahihishi, na wamezoea kuishi kimazoea, wanadhani kila siku ni jumapili na kila walisemalo watanzania watalikubali tu madhari limesemwa na wao, na kwamba kila muongeaji basi anasikilizwa. SIO HIVYO...!!
Leo waongeaji wa CHADEMA na WATETEZI wakuu kwenye mitandao ni YERICKO NYERERE, A man with 0.001 IQ, Anaishi katika uongo na uzushi, mpaka kila mmoja amemmpuuza, Mwanakijiji, Chahali na WATABE wengine wa maandishi yenye adili, wameikacha CHADEMA, bado CDM haijiulizi, inajivunia kuwa na YERICKO. Wasomi, watumishi, na wanataaluma wameikacha CHADEMA, bado CDM haijiulizi, wanajivunia madereva bodaboda.
Moja ya sifa ya Mwerevu, ni yule ambae haumwi na nyoka mara mbili, anayejikwaa akaanguka kisha asiishie kuangalia alipoangukia bali hugeuka kwa umakini na kutazama alipojikwaa, ni nini hasa kimemuangusha..Popularity ya CHADEMA na Upinzani imeshuka na inaendelea kushuka kwa kasi, HAWAJIULIZI.
Viongozi wameacha kuchangia hoja za msingi ndani ya Vikao, wameshikwa na woga na wengine wamesusa, Mwenyekiti Mbowe ambae Mimi binafsi nilishamuita ZERO tukiwa ndani ya Kikao changu cha Mwisho nikiwa KAMANDA wa CDM, ameendelea kwenda Mrama kwa kasi ya ajabu...kila jipya analoliamua ni baya kuliko la jana..
Kiukweli, tulipoanza discussion nilikuwa naona unakoelekea, na unaposimamia, ulisimamia katika kutaka mabadilko. Na ninaamini hvyo, sas basi, nimekuelewa vizuri, nieleze tu kwa kfiupi ni mabadiliko yapi uyatakayo wewe, sasa hivi hakutakuwa na misafara mingi ya nje, maana rais ajaye hana marafiki wengi nje, na wengini wanathubutu kusema #Magufuli hafai kuwa rais eti kwa sababu hajulikani nchi za nje, ina maana watanzania wenyewe wanapenda rais anayejulikana sana nje ili apapet safari nyingki za nje?
Kwa jinsi ninavyoona hata Kampeni zenyewe,ninaona hali ni ile ile,Magufuli kama ameshindwa kukemea MATUSI na KUDHALILISHA watu wengine sidhani kama anuweza wa kumkamata mtu yeyote na kumfungulia kesi.
Huyu ameenda Bariadi amempigia promo Chenge,amempigia promo Tiba kwa ufupi maana hawa ni wasafi sana kuliko yule anayedhalilishwa kwenye majukwaa yake.
Angeweza hata kwa kidogo kukemea ujinga labda ningemfikiria.Amechaguliwa na wenye pesa zao sababu wanajua weakness zake.
Kwangu bado sijapata RAIS wa kumpa kura mpaka sasa.Ila Mbunge wangu ninaye siku nyingi hana haja ya kuifuata kura yangu nitampelekea tu.
Ila mwisho MABADILIKO ndani ya CCM ni ndoto mpaka watambue maovu na makosa yao ya msingi kabisa.Kwa sasa bado sana,ila kuna siku inakuja watajua.
Kama unaona mbunge ndiye atakayekukidhia hatja zako zote za kiraia, basi, ila kama siyo, umepata hasara
Hata baada ya matokeo ya TWAWEZA bado watasimama majukwaani waseme UKAWA tutachukua nchi..
Ni kweli, hii ni forum kila mtu ana uhuru na nafasi ya kuzungumza ila tu tusichupe mipaka
Kwa jinsi ninavyoona hata Kampeni zenyewe,ninaona hali ni ile ile,Magufuli kama ameshindwa kukemea MATUSI na KUDHALILISHA watu wengine sidhani kama anuweza wa kumkamata mtu yeyote na kumfungulia kesi.
Huyu ameenda Bariadi amempigia promo Chenge,amempigia promo Tiba kwa ufupi maana hawa ni wasafi sana kuliko yule anayedhalilishwa kwenye majukwaa yake.
Angeweza hata kwa kidogo kukemea ujinga labda ningemfikiria.Amechaguliwa na wenye pesa zao sababu wanajua weakness zake.
Kwangu bado sijapata RAIS wa kumpa kura mpaka sasa.Ila Mbunge wangu ninaye siku nyingi hana haja ya kuifuata kura yangu nitampelekea tu.
Ila mwisho MABADILIKO ndani ya CCM ni ndoto mpaka watambue maovu na makosa yao ya msingi kabisa.Kwa sasa bado sana,ila kuna siku inakuja watajua.
Nadhani kweli watanzania tunahitaji kuelimishwa kwenye issue za haki za msingi za uraia na somo la uraia.Kutokana na sentensi yako nimeona umuhimu wa watanzania kupata elimu hii.
Kwa kawaida wabunge wananguvu kubwa kuliko rais na serikali yake,maana hawa ndiyo wanaoifuatilia serikali na kuhakikisha matakwa ya msingi ya sheria na haki za raia zinafuatwa.Hivyo ninaujua umuhimu wa wabunge rafiki.Anyway ninaona uelewa wetu uko tofauti sana.
Hilo swala unalolisema la Magufuli kumpigia debe Chenge nina wasi wasi nalo, sijawahi sikia, na kuhusu mabadiliko, kama hayatapatikana ndani ya CCM usitegemee mtu ambaye alikuwa CCM akaondoka CCM kwa sababu ya utovu wa maadili ndiye aje kuleta nabadiliko ya aina yoyote akiwa nje ya CCM, Hilo halipo,
Michezo inayochezwa na UKAWA ni ya pata potea, watanzania tusipokuwa makini tutajutia, mara kumi ya majuto ya CCM, maana kumejaa watu ambao kwanza hawaaminiki tena kutokana na kauli zao, kuanzia wenyeji mpaka wageni,Mbowe ndiye aliyeapa kuwa EL akiingia CDM labda yeye awe amekufa, Slaa alikuwa rafiki mzuri wa CDM leo amekuwa adui, Lissu alimuweka EL kwenye list of shame, Mnyika na Mdee ndio walikuwa wakemeaji wakuu wa ufisadi na kumu attack EL. Leo hii VICE VERSA IS TRUE, what if hawa watu wakapata nchi, itakuwa vice versa is true or false?. Bora uruke maji ukanyage matope, kuliko kuruka maji ukakanyage kinyesi.
Usijifanye una elimu sana wewe, kama shule nimeenda na elimu nimeipata, ila nguvu ya wabunge kama kweli ipo tungeiona pale bungeni wabunge wa kambi pinzani walipokuwa wakimkeme ufisadi wa ENL halafu leo wapo kimya, nguvu yao ya kukemea ipo bungeni tu ama?
Waliishia tu kususa vikao, wananchi wanaumia halafu mwisho wa siku wanatuambia maadui wa haki, wala rushwa na mafisadi ndio wamekuwa mabadiliko, fikiri sana shilingi ina pande mbili.