Hakuna mahali ambapo nimeainisha kama Dr.Slaa ni adui wa CDM,pili tulikaririshwa kwamba viongozi wazuri ni lazima watoke CCM.Lakini hii ilikuwa ile CCM yenye UZALENDO wa hali ya juu.
Magufuli alimpigia Promo Chenge na Tibaijuka.Na wale wabunge ambao leo wanatoa pesa ili kupata ubunge kesho watatoa pesa ili kupata uwaziri,unarudi na kusema RUSHWA na UFISADI utaisha ndani ya CCM ni ndoto mtu aotayo MCHANA.
Kwa trend iliyopo hakuna Kiongozi atakayetoka CCM akaweza kuipiga vita RUSHWA,ingewezekana hilo kufanyika kama CCM kwenye mchujo wangewatoa wote waliotoa RUSHWA ili kupata kugombea UBUNGE.
Ingewezekana tu kama ingewatoa wote wabadhirifu wa mali za umma,wala rushwa,mafisadi ambao hadi leo wako ndani ya CCM.
Kama nasema kama CCM ingewaondoa wote kabisa wote walioingia kwenye kinyang'anyiro cha ubunge kwa rushwa ndogo au kubwa hii ni pamoja na Mtoto wa Mkulu,Nape Nauye kwenye ubunge hakika Mwanz ungenishawishi kuipigia kura CCM
Hii ni pamoja na Magufuli mwenyewe asingekuwepo kwenye kinyang'anyiro maana ameshindwa kuongoza wizara iliyokithiri kwa rushwa,ubadhirfu,wizi ,ufisadi nk nk leo atawezeje kutuaminisha kwamba ataweza kuondo RUSHWA kwenye TAIFA lenye wizara zaidi ya 30,hakika naweza kuwa sina PHD lakini hii haihitaji PHD kuona kwamba hata huyu hawezi..
Tuliaminishwa Mkapa ni Mr Clean alipokuwa akipigiwa debe na JKN mwisho wa siku ametoka akiwa MCHAFU kuliko choo cha wanafunzi kilichojaa.
Tukaaminishwa tena kwamba huyu anayetoka madarakani ni muadilifu,Mzalendo nk nk lakini leo UCHAFU wote unamuelea,wizi wa mali za umma ESCROW,Uuzaji na umikaji wa UDA kwa familia ya Mkullu,hii yote inaletea ukakasi.
Ni bora safari hii tuwape wapinzani,tena kwa kura za kishindo kabisa,hatuhitaji vita ya walionacho na wasio nacho,nawassa watanzania wenzangu,wakati ndiyo sasa TUBADILIKE,CCM imetosha,kama kula wacha na UPINZANI ule.