Nyie CHADEMA sikilizeni....amkeni sasa.
Anzeni kuwa mnafikiria kwa hatua kadhaa mbele.
Hatua zenye manufaa kwa mustakabali wa chama chenu na viongozi wenu.
Hivi nyie mna idara ya usalama kweli? Kama mnayo, iweje suala la ulinzi kwa Tundu Lissu mlikuwa hamjaona umuhimu wake?
Kwa nini Lissu hakuwa na ulinzi imara wa watu wenye silaha za moto?
Kwa kweli hapo mmeudondosha mpira. Na kama mna watu wanaohusika na usalama ndani ya chama chenu basi hamna budi kufanya maamuzi magumu na kuwatimulia mbali.
Haiwezekani kiongozi mkubwa kwenye chama kama Lissu asiwe na usalama wa kueleweka.
Sijui mlikuwa mnaitegemea serikali kwenye hilo!
Kiongozi wa juu tena mwenye mbwembwe na cheche kama Lissu kutembea tembea bila ulinzi wa maana ni upumbavu.
Ni upumbavu kwa sababu tayari yeye atakuwa ni mlengwa wa mashambulizi toka kwa wabaya wake. Anapotembea bila ulinzi anakuwa ni shabaha iliyo rahisi sana kuilenga.
Haiingii akilini kwa nini hadi siku ya lile tukio mlikuwa hamjampatia ulinzi huyo mwanasheria wenu mkuu.
Shame on you.
Hili chini ni bandiko lako kipindi kile ungosha haujakuathiri:
Hivi ni mimi tu au na wengine mpo mnaoona kama vile mambo yashamshinda huyu Magufuli?
Kuna hali fulani hivi naiona ambapo jamaa ni kama anaamka tu kila asubuhi na kutoa maamuzi ya kukurupuka kurupuka.
Yaani yeye ni amri tu....fanya hivi....fukuza huyu....twende kule...nk.
Yapo baadhi ambayo ni mazuri ambapo mtu unaona kabisa hapa nia ni nzuri lakini kuna mengine yenye ukakasi sana hadi kunifanya nianze kuhoji hekima na busara za huyo bwana!
---
Mimi ni mmoja wa watu wanaoamini kuwa rais wetu huyu, mheshimiwa mtukufu Dkt. John Pombe Joseph Magufuli si kiongozi mzuri hata kidogo, hususan katika ngazi ya urais.
Hilo nimekuwa nikilisema kwa muda mrefu sasa. Nakumbuka hata ile siku alipoteuliwa kuipeperusha bendera ya CCM nilisema hivyo humu humu JF.
Kwa kiasi fulani namkubali kwenye usimamizi lakini si kwenye uongozi. Hana kabisa haiba ya kiuongozi. Pia hana sifa za kuweza kuwa kiongozi mzuri.
Ni mtu mwenye jazba. Ana jeuri. Mwenye kuongea bila kufikiria athari za maneno yake[nyakati zingine]. Wengine wanasema eti kuwa hashauriki. Kwa ufupi ni mengi sana yanasemwa juu yake kiasi kwamba mengine ni vigumu kwa watu wa mbali kama sisi kujua kama ni ya kweli au la. Hivyo kwa sisi wa mbali tunaenda na yale tuyaonayo na tuyasikiayo toka kwake yeye mwenyewe.
Sasa kwa jinsi vile mambo yanavyoenda sasa hivi kuna kila dalili huenda nchi imeshamshinda kuiongoza. Hivyo ndivyo niuonavyo mwelekeo.
Hata ndani ya chama chake ukiangalia vizuri utaona nyuso nyingi tu za manung'uniko toka kwa wakereketwa. Wengi wao siku hizi wanashindwa hata kumtetea. Wapo kimyaaaa utadhani wagonjwa. CCM hawana furaha kabisa.
Naamini asipojiangalia na kujifanyia tathmini basi hiyo kazi itamshinda kabla hata hajafikia nusu ya muhula wa hii miaka mitano.
Niliwahi kuandika kuhusu 'a police state'. Jikumbushe....