CHADEMA jifanyieni tathmini

CHADEMA jifanyieni tathmini

Yeah, No strikes now. How did you fix that?

Kinda simple...

On the desktop version...

Click edit...

Highlight the struck content...

upload_2017-9-10_22-15-22.png


Then click on that italicized T [with the little 'x' to the side...second from left on the tool bar] to remove the formatting.

Click 'Save Changes' and you're done!
 
Nyie CHADEMA sikilizeni....amkeni sasa.

Anzeni kuwa mnafikiria kwa hatua kadhaa mbele.

Hatua zenye manufaa kwa mustakabali wa chama chenu na viongozi wenu.

Hivi nyie mna idara ya usalama kweli? Kama mnayo, iweje suala la ulinzi kwa Tundu Lissu mlikuwa hamjaona umuhimu wake?

Kwa nini Lissu hakuwa na ulinzi imara wa watu wenye silaha za moto?

Kwa kweli hapo mmeudondosha mpira. Na kama mna watu wanaohusika na usalama ndani ya chama chenu basi hamna budi kufanya maamuzi magumu na kuwatimulia mbali.

Haiwezekani kiongozi mkubwa kwenye chama kama Lissu asiwe na usalama wa kueleweka.

Sijui mlikuwa mnaitegemea serikali kwenye hilo!

Kiongozi wa juu tena mwenye mbwembwe na cheche kama Lissu kutembea tembea bila ulinzi wa maana ni upumbavu.

Ni upumbavu kwa sababu tayari yeye atakuwa ni mlengwa wa mashambulizi toka kwa wabaya wake. Anapotembea bila ulinzi anakuwa ni shabaha iliyo rahisi sana kuilenga.

Haiingii akilini kwa nini hadi siku ya lile tukio mlikuwa hamjampatia ulinzi huyo mwanasheria wenu mkuu.

Shame on you.

1. hana ulinzi wakati hata gwajima ana ulinzi!!
2.alifuatiliwa sana , idara yao ya intelijinsia ililala, au haipo
3. hawana hela za dharura yanapotokea majanga, michango ndio inatembezwa
 
Tundu Lisu anajiamini sana kwa sababu anamiliki kijibastola fulani hivi cha kichina

ambacho ukitaka kufyatua lazima ukigonge kama zile redio za zamani zenye mende, na kakifyatuka kanaishia mita 12 tu!!
 
1. hana ulinzi wakati hata gwajima ana ulinzi!!
2.alifuatiliwa sana , idara yao ya intelijinsia ililala, au haipo
3. hawana hela za dharura yanapotokea majanga, michango ndio inatembezwa

Natumaini hili tukio limewaamsha sasa.

Ni lazima wafanye tathmini na mabadiliko.
 
Nyani Ngabu,

..walinzi wenye bunduki/bastola??

..what if wakimjia na ma rpg?

..na sidhani kama wataruhusiwa kuwa na ulinzi wa aina hiyo.

..kwamba walitaka kumuua mchana kweupe, tena eneo la makazi ya viongozi, inaonyesha jinsi gani hao wauaji wanavyofanya ukatili wao kwa kujinafasi, na bila wasiwasi wowote.
 
zikoje mkuu, naweza kukutajia idadi ya watu saba tena wachungaji wenye ulinzi mkali nchi hii

kubali tu

Hao wachungaji wamewahi kuikosoa serekali na mungu wa nchi hii?
 
Nyani Ngabu,

..walinzi wenye bunduki/bastola??

Ndiyo.

Walinzi wenye silaha [armed security guards].

..what if wakimjia na ma rpg?

Then there will be a firefight.

It's better to be armed than not to be.

..na sidhani kama wataruhusiwa kuwa na ulinzi wa aina hiyo.

Kwa nini wasiruhusiwe?

Kama raia wa kawaida tu wanaruhusiwa kuwa na/ kumiliki silaha za moto kwa nini kiongozi mkubwa wa chama cha kisiasa na mbunge asiweze kuwa na walinzi binafsi wanaobeba silaha za moto?

Kama hawataruhusiwa [nasadiki unazungumzia kuruhusiwa na serikali] basi serikali yenyewe ilibebe hilo jukumu. Itoe ulinzi kwa viongozi ambao maisha yao yako hatarini na/au ambao wamesharipoti kuwa maisha yao yapo hatarini.

Na ikitokea serikali ikakataa kabisa kutoa ruhusa ya walinzi binafsi kubeba silaha au yenyewe kutoa ulinzi basi lolote litakalotokea kwa huyo muombaji serikali itawajibika moja kwa moja kwa asilimia 100.

..kwamba walitaka kumuua mchana kweupe, tena eneo la makazi ya viongozi, inaonyesha jinsi gani hao wauaji wanavyofanya ukatili wao kwa kujinafasi, na bila wasiwasi wowote.

Hilo ni kweli....na nadhani unachodokeza hapo ni kwamba serikali inahusika, siyo?
 
Aisee nadhani waikuwa wakimpa ulinzi ila hawakutarajia kitu kama hiki, mwenyewe sikutarajia mbunge na mpinzani maarufu kuliko wote wa Magufuli kupigwa risasi kwenye akiwa kwenya makazi ya mawaziri
Walinzi hupewa watu wenye roho zakikatili only like magufuli,bashite and nowdayz lipumba .........
 
Acha kufikiri kischana zaidi unaambiwa wenye cheche ndio wa nahitaji ulinzi wengine hawana madhara.

mmmnh

inamaana viongozi wote/wabunge wote walindwe???

si wapo bungeni,wenye itikadi tofauti,

Mtu anayeongoza jimbo kwa ticket ya CCM,alindwe sababu katika jimbo lake,kuna walio na itikadi tofauti??ya ukawa kwa mfano
 
Nyani Ngabu,

..sidhani kama cdm wanaweza ku-dictate kwamba serikali iwapatie ulinzi.

..hawa watu hawawajibiki popote pale. Hata wakisema uongo au kukosea hakuna mahali wanawajibika.

..nikupe mfano mdogo. TL aliitisha press conf na kusema mambo makubwa mawili. Moja, polisi na usalama wa taifa wanamfuatilia. Mbili, ndege ya serikali imekamatwa Canada.

..Sasa msemaji wa serikali amejibu kuhusu ndege kukamatwa. Lakini igp anasema hana habari za TL kusema wapo watu wanamfuatilia.

..Kwa hiyo mpaka hapo utaona wako watu hawasemi ukweli na hakuna mtu wa kuwawajibisha.

..kwa kweli mimi siamini kama CDM wanaweza kutendewa haki. Naona kama vile aliyepaswa kuwa mwamuzi na mtoa haki ameamua kuchukua upande. Na upande wenyewe siyo CDM.

NB.

..sijasema kwamba serikali inahusika. Lakini suala kwamba TL amenusurika kuuwawa ktk eneo ambalo linapaswa kuwa na wanausalama linapaswa kutolewa maelezo.
 
Mbona na nyie hampambani na hali yenu na mnaitegemea polisi iwakamate walohusika?

Nyie wafuasi hamna akili kabisa.

Mnachojua na mnachoweza ni kuzungusha mikono tu.
Ivi polisi leo ni wa Ccm?ingekua hivo leo mahakama ya kenya ingetoa ule ukweli?tuakikishie kua polisi ni wa Ccm.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nyani Ngabu,

..sidhani kama cdm wanaweza ku-dictate kwamba serikali iwapatie ulinzi.

..hawa watu hawawajibiki popote pale. Hata wakisema uongo au kukosea hakuna mahali wanawajibika.

..nikupe mfano mdogo. TL aliitisha press conf na kusema mambo makubwa mawili. Moja, polisi na usalama wa taifa wanamfuatilia. Mbili, ndege ya serikali imekamatwa Canada.

..Sasa msemaji wa serikali amejibu kuhusu ndege kukamatwa. Lakini igp anasema hana habari za TL kusema wapo watu wanamfuatilia.

..Kwa hiyo mpaka hapo utaona wako watu hawasemi ukweli na hakuna mtu wa kuwawajibisha.

NB.

..sijasema kwamba serikali inahusika. Lakini suala kwamba TL amenusurika kuuwawa ktk eneo ambalo linapaswa kuwa na wanausalama linapaswa kutolewa maelezo.

Ngoja kwanza...

Hapo kuhusu IGP...nilivyomwelewa mimi ni kwamba Lissu hakutoa/ hakupeleka taarifa rasmi kwa jeshi kuwa kuna watu wanamfuatilia.

Hivyo ndivyo nilivyomwelewa IGP.

Lissu kusema alivyosema kwenye mkutano ule na waandishi wa habari kunaweza kuchukuliwa kuwa ni mojawapo ya porojo za kisiasa kwenye majukwaa ya kisiasa.

Lakini unapopeleka taarifa rasmi kwenye chombo kama polisi, suala zima linachukua sura tofauti kabisa.

Kwa hiyo si ajabu IGP alikuwa anamaanisha katika muktadha huo.

Swali ni je, Tundu Lissu alipeleka taarifa rasmi polisi au aliishia kusema vile kwenye ule mkutano tu?
 
Acha kufikiri kischana zaidi unaambiwa wenye cheche ndio wa nahitaji ulinzi wengine hawana madhara.

Nyie ndio mnaskuma wabunge wakae kama midoli bungeni,na sio actively kutatua matatizo yanayotukabili,

nilichokua namaanisha,ni kwamba,tuko itikadi tofauti,wengine kuwa tofauti huko wanatafsiri ni uadui,

watu wa hivyo ndio nimewatolea mfano,mtu anaweza kuwa yeye ni CCM wakati kiongozi wake ni UKAWA,ila they don't want to tolerate each other,then what follows,God knows what.

Halikuwepo swala la ulinzi ,kwa CCM wala Upinzani,

May be there was no need then,ila sasa hivi kwa mambo yanavyokwenda inabidi muwaongezee posho Zaidi wawalipe walinzi wao,

Airee!
 
Ngoja kwanza...

Hapo kuhusu IGP...nilivyomwelewa mimi ni kwamba Lissu hakutoa/ hakupeleka taarifa rasmi kwa jeshi kuwa kuna watu wanamfuatilia.

Hivyo ndivyo nilivyomwelewa IGP.

Lissu kusema alivyosema kwenye mkutano ule na waandishi wa habari kunaweza kuchukuliwa kuwa ni mojawapo ya porojo za kisiasa kwenye majukwaa ya kisiasa.

Lakini unapopeleka taarifa rasmi kwenye chombo kama polisi, suala zima linachukua sura tofauti kabisa.

Kwa hiyo si ajabu IGP alikuwa anamaanisha katika muktadha huo.

Swali ni je, Tundu Lissu alipeleka taarifa rasmi polisi au aliishia kusema vile kwenye ule mkutano tu?

..I agree.

..Swali langu ni, polisi walichukua hatua gani?

..Siamini kwamba taarifa kama ile inahitaji kuwa rasmi ili IGP aifuatilie.

..Na mawasiliano ya TL si yanadukuliwa. Na " mcha mungu" ndiye aliyetoa siri hiyo.

..Sasa inabidi yatolewe maelezo kama ktk udukuzi uliokuwa ukifanyika hawakuona mawasiliano ambayo TL alikuwa akilalamika kwamba kuna watu wanamfuata kila anapokwenda?
 
..I agree.

..Swali langu ni, polisi walichukua hatua gani?

..Siamini kwamba taarifa kama ile inahitaji kuwa rasmi ili IGP aifuatilie.

..Na mawasiliano ya TL si yanadukuliwa. Na " mcha mungu" ndiye aliyetoa siri hiyo.

..Sasa inabidi yatolewe maelezo kama ktk udukuzi uliokuwa ukifanyika hawakuona mawasiliano ambayo TL alikuwa akilalamika kwamba kuna watu wanamfuata kila anapokwenda?

Kuna sababu kwa nini zipo njia zilizo rasmi za kutoa taarifa polisi.
 
Ngoja kwanza...

Hapo kuhusu IGP...nilivyomwelewa mimi ni kwamba Lissu hakutoa/ hakupeleka taarifa rasmi kwa jeshi kuwa kuna watu wanamfuatilia.

Hivyo ndivyo nilivyomwelewa IGP.

Lissu kusema alivyosema kwenye mkutano ule na waandishi wa habari kunaweza kuchukuliwa kuwa ni mojawapo ya porojo za kisiasa kwenye majukwaa ya kisiasa.

Lakini unapopeleka taarifa rasmi kwenye chombo kama polisi, suala zima linachukua sura tofauti kabisa.

Kwa hiyo si ajabu IGP alikuwa anamaanisha katika muktadha huo.

Swali ni je, Tundu Lissu alipeleka taarifa rasmi polisi au aliishia kusema vile kwenye ule mkutano tu?
Ukimsikiliza IGP vizuri ni kama anatumia fursa ya kuripoti kukwepa ukweli

1. IGP na Mkuu wa Usalama walitajwa na TL. Hawa ni viongozi wa umma si wa kisiasa. Kuhusishwa tu na thuma kama hizo kulitosha wao kufanya jambo, kujitokeza na kueleza kwa namna yoyote iwe kukanusha au kumtaka TL athbitishe madai yake, hawakufanya lolote

2. Polisi wanasema hawawezi kutumia vyombo vya habari kupokea madai. Ni kweli lakini tujiulize pia, wanapata wapi muda wa kufuatilia watu katika mitandao ambayo ni sehemu ya vyombo vya habari kwa zama hizi? Kama ni porojo kama za TL kwanini wanakamata watu

3. Wakati Polisi wakikana kupata habari kupitia mikutano na waandishi, Polisi hao hao wanamtafuta Mashinji na dereva wa TL kwa kutumia vyombo vya habari.
Ni wakati gani vyombo vya habari ni muhimu au si muhimu kwao

4. Kuna Wabunge akiweno Nape wamepeleka taarifa rasmi kuhusu kufuatiliwa, nini kimetokea!
 
Back
Top Bottom