CHADEMA: Israel ituombe radhi

CHADEMA: Israel ituombe radhi

PIPIJOJO hapa hoja si Mh Mnyika,hoja hapa ni kauli ya Israeli,naona umepost mara nyingi nyingi huku ukim-point Mnyika.
Nimegundua wewe ni mmoja au ni sehemu ya waliochangia sisi tunadharauliwa kiasi hiki,maana hakika wewe ni mfuasi wa Magamba-CCM.na haya yote ni matokeo ya CCM.kwa kuwa nina hasira ngoja niachane na hii kitu
 
Hayo ni mawazo yako finyu, TZ ni muhimu sana kuliko uongo mnaolishwa na viongozi wa vyama vyenu.
Kwa taarifa unajitukana mwenyewe.

Nawe kwa taarifa yako Tanzania ni muhimu kwa wazungu kuchuma rasilimali na kuiacha hoi bin taabani
 
Rafiki wa kweli ni yule anaekuambia ukweli, Israel wametuambia ukweli kuliko wale wanao tuambia uchumi wetu unapaaaaaaaaa wakati tuna pigika mpaka hata pesa ya kulipa wafanyakazi hatuna.....

Crackpot...
 




Kabla hujakurupuka you should Ask what i do for a living ...!? Am a Doctor holding bachelor of MD & Surgery .... unajuwa toka 2005 mpaka sasa nimeokoa maisha ya watu wangapi hospitali ....! kama weye ni jobless na huna umuhimu hapa duniani ni kivyako na siwezi nikakubaliana na kauli za huyo mpuuzi kwa mimi ni sawa na karatasi la toilet mimi kama mtanzania nina umuhimu wangu kama sio kwake basi kuna watu wengine ... pumbav sana huyo barak #%&@


usimlaumu huyo kaka...I own a PhD and I somehow contribute internationally in my area of specialisation...

Despite my good international reputation, i RARELY INTRODUCE MYSELF AS A TANZANIAN!!!!! i am not happy of this....

i rarely do so since just after my introduction the debate turns around to me that ...so you are there...are you happy with what is going on up back home??? e.t.c.....

it gets to the point you fail to be proud of our mother land.....SHAME UPON US!
 
Kwanza Israel katusaidia kutuonyesha u-kondoo wetu.... UKWELI UTABAKI KUWA UKWELI.. hata tujitutumue vipi..!!! Mwingine anamuushisha Nyerere..!!! Enzi za Nyerere upuuzi wote uaotudharaurisha usingekuwepo!!! watu mnagawa dhahabu bure kwa majahili bado msidharaulike!!!! Hata wasiosema wanatudharau zaidi ila wanaona wanyamaze ili....... (people might not notice the difference).... Mtu mzima miaka 50 bado hata kutambaa hawezi!!! Kalaaniwa au ni zezeta.... SAMAHANI KAMA NIMEKUKWAZA
Nilikuwa ninampango wa kuendelea kuchangia kwenye thread hii lakini baada ya kuona badiko hili naona umemaliza kila kitu....Asante sana
 
FIDIVIN,hapo umekosea watu wanafanya kazi na wanalipa kodi,hata asie na ajira wanalipa kodi ,watanzania wote tunalipa kodi katika njia tofauti,lakini kuna kodi tunazolipa kila mtu kila unaponunua mahitaji,achilia mbali wafanyakazi wanaolipa kodi ya PAYE.

Lakini swali linabaki palepale kwanini tunadharauliwa hivi katika anga za kimataifa?mimi binafsi nakubaliana na huyu jamaa aliesema wa-Tanzania ni vilaza,maana mambo mengine yanayopelekea tudharaulike yanatokana na watanzania wenyewe kushabikia mi viongozi inayotoka chama kinachofuga mafisadi,milafi ya pesa, inaendekeza rushwa na wala haina jipya katika uongozi wao,na inaliongoza taifa kwa mazoea, miviongozi haina creativity.

Viongozi inawaza wizi tu,haina fikra mbadala,sasa ninapokubali watanzania ni vilaza ni kuendelea kuichagua hii mijitu au ni kuendelea na chama cha magamba.hata wanaoijiita wamesoma hapa TZ tena hao ndo vilaza wakubwa, hawana jipya anaebisha aniambie amefanya nini au anafanya nini kuiondoa nchi hii katika hali mbaya ya umasikini na ufisadi unaoimaliza nchi?kazi kujipendekeza tu wala hawajiamini hata kidogo na ni waoga wa maisha.

leo hii tunadharaulika wakati watu wanaosababisha wapo wala hakuna juhudi za makusudi za kutaka kuondoka huko,na bado tutasikia nchi nyingine itaibuka na lake.
 
Tazameni hizi comments kutoka sehemu nyingine za dunia kuhusu Tanzania.
Nadhani tatizo la kutoheshimika kwetu ni kubwa na sii la kufanyia mzaha.

Quote:


[TD="class: alt2"] Originally Posted by Margot Life expectancy in Tanzania is about 48 years.. They have massive problems with AIDS and Malaria.

Its NOT a tourist destination for Zionists or anyone else.

[/TD]

It should be a tourist destination for conservatives. Tanzania has almost no government or governnment spending. It's a private sector paradise.

I hear, tho, that the despot-in-chief has given away large chunks of Tanzania to Israeli speculators in exchange for a few airplanes and cars.
 
Hilo dege la jeshi lina uafadhali, hawa mapacha watatu Richmondi, dowanz na symbioni tunao miaka nenda miaka rudi mkuu wa kaya katuambia hata hawajui!! Lakini anatetea walipwe tuuu pesa yao. Jifanye wewe ni balozi unayewakilisha nchi yako hapa TZ halafu waziri Mkulo anakujia kukuomba uchangie kwenye bajeti yake ya mwaka ujao!! Katika mazingira kama haya nani atakuheshimu? Tunastahili kudharaulika na nchi zingine. Naungana na wachangiaji wengine kwamba wanaostahili kutuomba radhi ni sisiemu iliyotengeneza na kutekeleza sera ambazo zimetufikisha hapa.

Ni aibu sana.

Hao mnao waita watawala wameweka pamba zao masikioni hawataki kusikia hiyo kitu.
 
hivi tunaposema dar sio itigi... tunakosea?? au msaki sio kambi ya fisi pia tunakosea sio?

na kweli, kweli kabisa yani kweli tunategemea Membe atawaaambia jamaa watuombe radhi? na hata akisema wataomba?

kwa hiyo kwa Dar,Itigi ni irrelevant...
 
John Mnyika kwa nini hushangai Waziri wa ulinzi wa Israel ndiye anazungumzia sera za nje badala ya waziri husika wa mambo ya nje wa Israel ambaye tuna uhakika anajua vema zaidi mambo hayo? hapa kuna namna!!!!

Au anadhani sisi ni nchi ya Kiislamu? Maana alivyotaja.. TanzaNIA,MauritaNIA,TripolitaNIA.....
 
Kwani Israel imeongea uongo? Kama dege la kijeshi linatua nchini na Usalama wa Taifa wapo na linapakia Twiga na kupaa tena bila rais kujua hii nchi ina maana kweli?


Kama hawajui wamiliki wa Dowans/Richmond waliosababisha Waziri wake mkuu kujiuzulu................tehe tehe tehe! INAUMA SANA!
 
Si kweli kwamba kila kinachosemwa na wazungu ni cha kweli. Mnyika kwa taarifa yako tu Marekani ni taifa tajiri sana duniani lakini ndio pia mkopaji namba moja duniani kwa maana ya thamani ya deni la ndani na nje.

Inavyoonyesha we na Mnyika 'hamkukutana barabarani'
 
Hivi sasa tuna madini ya Urenium ni muhimu sana katika mambo ya ulinzi na utengenezaji wa silaha na nishati. Nasikia Israel walionyesha nia tukakataa. Huyu waziri kuna jambo linamuuma

Ehud ameshakataa kuomba radhi! Kama uranium ipo tubadilishane na tehran kwa matreka (kilimo kwanza) ya kizuka ya kuzuka tutakuja wauzia msosi! 😛
 
kwani hawa washenzi israel tunafaidika nao kitu gani? yote haya ni huyu mbumbu kikwete...
 
Tanzania bana inatukanwa na Israel, halafu inashambuliana yenyewe kwa yenyewe!
Kwa hiyo unataka pawe na umoja kati ya wapenda haki na mafisadi?watashea common interest ipi?
 
Sikutegemea kitu kama hiki kutoka kwa Mnyika.. Mwenyewe unasema sera mbovu za ccm zimetufikisha hapa bado unalaumu kwa Waisrael kusema hatuna umuhimu mkubwa kwao?! Halafu kuna watu humu wamekomaa kuwa Barrak amewatukana!

Wabongo wengi wana mazoea ya kukimbilia kwenye 'kichaka cha kutukanwa' Yeyote anayedai Tz imetukanwa alete hapa hilo tusi neno kwa neno tulione. Tunaweza kusema bila kusita kuwa Ureno, Tuv-aimag (huko Mongolia) na Uzbekistan hazina umuhimu kwa Tz kama zilivyo Canada, Norway/Denmark? China nk.

Ajabu kuna raia wa nchi mojawapo watapiga makelele kuwa wametukanwa!! Haya tuonyesheni umuhimu wa Tanzania kwa Israel...
 
Back
Top Bottom