Hali hii ni matokeo ya serikali ya JK kuwa omba omba sana dunian
tumetukanywa au tumeambiwa ukweli!Tanzania bana inatukanwa na Israel, halafu inashambuliana yenyewe kwa yenyewe!
Nakuunga mkono.Tatizo letu mkuu hatujijui how irrelevant we are as a country.
jamani, tumedhalilika vya kutosha, tumenyanyswa na matamshi haya vya kutosha. Hatuwezi kuvumilia. Mimi kama mtanzania napendekeza tutangaze mgogoro na hiyo nchi sijui inaitwa Israel. Hiyo nchi haina maana yoyote katika medani ya maisha ya kila siku ya mtanzania. Nasi tuwaambie kuwa Israel si nchi muhimu Tanzania. kuomba radhi tu hakutoshi maji yakiisha mwagika hayazoleki. Huyu jamaa katamka haya maneno kutoka rohoni mwake hata akiomba radhi haitasaidia kesha tudharirisha. Cha muhimu tuangalie tumejikwaa wapi, kesho na mwingine atatamuka hivi hivi. Tatizo kubwa letu tumekuwa watu wa kuwasujudia hawa watu weupe. Mtu akisha kuwa mweupe sisi kila goti litapigwa sasa tukome. Kila siku tumebaki katika kushabikia siasa za maji taka basi.
North Korea ni jalala,jela kuu baada ya gaza.Mkuu SOBY, hata siku moja sintonunua fikra kama hizo!!!
Hizo wenzangu kazipelekeni hukooo!!! Kinachotufanya tuwe irrelevant ni nini hasa kama taifa? Labda kama kuna baadhi ya mambo ambayo wakuu wetu hutenda kinyume na matarajio ya ulimwengu hivyo kutufanya tusukumwe moja kwa moja jalalani.
Lakini hata tukihisiwa jalala, ni jukumu letu kukataa huo muonekano wa ujala machoni mwa ulimwengu kwa kuwa sisi tunawathamini sana tu tena kwa uzito wote hivyo ni matarajio yetu kurudishiwa heshma endapo hakina cha ajabu kilichofichama machoni mwetu wananchi.
Ishi!Eti aombe radhi ya nini?Nyie CHEDEMA,Tanzania haitoondokana na matatizo yake kwa kuombwa radhi na Israel.Sasa ni kweli Tanzania ni sawa na France au Uk kwa maslahi ya Israel?Sisi ni wa maana kwa Rwanda na Burundi,jamani kila nchi na class yao.Hata Dar ni ya maana kuliko Rukwa.
Na kwakweli heshima huwa hailazimishwi bali hutolewa kwa yule anaye heshimika.Hizo ni hisia za Israel,hata kama tukiwalazimisha waombe radhi,hizo zitabaki kuwa hisia zao siku zote!
aisee kumbe na wewe ni wa kule kwetu; aisee tupo wengi kumbe.Ishi!Eti aombe radhi ya nini?Nyie CHEDEMA,Tanzania haitoondokana na matatizo yake kwa kuombwa radhi na Israel.Sasa ni kweli Tanzania ni sawa na France au Uk kwa maslahi ya Israel?Sisi ni wa maana kwa Rwanda na Burundi,jamani kila nchi na class yao.Hata Dar ni ya maana kuliko Rukwa.
WE ACHA TUU MKUUUMy comrade Mnyika pole sana wote tunaumia.... Ila wakulaumiwa ni hao wanaojiita viongozi wa Tanzania!
Imagine a country as small as Israel, na jangwa lake lote; inatumia sehemu ndogo ya ardhi inauza matunda nje kwa faida kubwa!!! Tanzania pamoja na ardhi oevu yote iliyonayo inashindwa kulisha wilaya zake........ (naachia hapa nasikia machozi yananilengalenga....)
Nani asiyetudharau.... aliyetwambia tuwe mashoga.... ameishia wapi....!?
mwingine kaniambia "mapacha watatu.... jamani nchi hii.....!
huyu ndo bure kabisa pesa ya wizi anaiiita chenji hahhahhaa jamaa simtaki huyu duuu!Na kwakweli heshima huwa hailazimishwi bali hutolewa kwa yule anaye heshimika.
Mnyika kaweka vizuri kuwa sera zetu mbovu ndiyo msingi wa haya na iwapo Membe kama waziri mwenye dhamana anataka Tanzania iombwe radhi basi angalau ashauriane na wenzake kuhusu jinsi ya kubadili sera mbovu zinazotoa upendeleo kwa watu wa mataifa ya kigeni na kuwaacha wazawa katika aibu ya umasikini usiotazamika wala kutamanika.
Vinginevyo itabakia kama taarab tu na kujirusha huku ukifahamu kuwa ndani mwako huna thamani wala heshima katikati ya watu na jamii ila kwasababu unamdomo unaoweza kuimba basi inabidi ujifariji kwa jinsi hiyo.