issenye
JF-Expert Member
- Feb 2, 2011
- 3,781
- 5,205
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimemtaka Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, kuitaka Serikali ya Israel kuwaomba radhi Watanzania kutokana na kauli ya Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo, Ehud Barak, kudai kuwa Tanzania si nchi ya muhimu wala ya maana.
Aidha, chama hicho kupitia Kurugenzi yake ya Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa kimemtaka Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi, kueleza iwapo hatua hiyo ndiyo msingi wa mahusiano yaliyopo kati ya nchi hizo, hasa ikizingatiwa kuwa serikali imekuwa ikieleza kwamba Tanzania ina mahusiano mazuri ya kiulinzi na Israel.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa wa CHADEMA kupitia mtandao wake wa kijamii.
Waziri Barak alifanya mahojiano na Radio Israel na kutoa kauli ambayo imenukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari vya nchi hiyo kuwa Tanzania si nchi ya muhimu wala ya maana hata kufikia hatua ya kuilinganisha na eneo ndani ya Libya linaloitwa Tripolitania.
Mnyika alisema kupuuzwa huku kwa nchi yetu katika medani ya kimataifa kunatokana na sera mbovu ya mambo ya nje chini ya utawala wa sasa wa Chama cha Mapinduzi (CCM).
"Tanzania imepoteza heshima katika siasa za dunia kutokana na diplomasia yetu kujikita katika kuomba omba kimataifa; pamoja na kuwa kimaneno na maandishi serikali inazungumza kuhusu diplomasia ya kiuchumi, kivitendo mahusiano yetu yamejengeka katika misingi ya utegemezi, kupungua kwa urari wa kibiashara na kuachia mianya ya uporwaji wa rasilimali," alisema.
Alieleza kuwa kauli ya Waziri Barak ni muendelezo wa mataifa mbalimbali kuifanya Tanzania na baadhi ya nchi nyingine za Afrika kukosa heshima wala sauti katika siasa za kimataifa kama ambavyo serikali za Uingereza na Marekani zilivyoweka masharti yenye mwelekeo wa ukoloni mamboleo kuhusu masuala ya ushoga na usagaji.
"Barua pekee ya Balozi wa heshima wa Tanzania nchini Israel, Kasbian Nuriel Chirich, kwenda kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel, Avigdor Lieberman ya kulaani matamshi hayo na kumkaribisha mwakilishi wa Israel kutembelea Tanzania haitoshi kuifanya serikali ya nchi hiyo kutambua athari za kidiplomasia za kauli iliyotolewa," alisema Mnyika.
Mbunge huyo alieleza kuwa wakati wa uongozi wa awamu ya kwanza wa hayati Mwalimu Julius Nyerere, Tanzania ilikuwa na heshima na sauti kimataifa si tu katika jitihada za ukombozi kusini mwa Afrika bali pia katika mahusiano ya kisiasa, kiuchumi na kijamii baina ya nchi za Kusini na mataifa mengine duniani.
Kutokana na hali hiyo, alisema iwapo hatua hazitachukuliwa kurejesha heshima na sauti ya Tanzania kimataifa, maamuzi mengi yatafanyika yenye athari kwa wananchi wengi bila ushiriki wao thabiti kama yanayoendelea hivi sasa kuhusu Mikataba ya Kiuchumi na Nchi za Jumuia ya Ulaya (EPA) yenye madhara kwa wakulima na wenye viwanda nchini.
"Ni wakati sasa kwa Watanzania kuendelea kuunganisha nguvu ya umma kusimamia uwajibikaji na kufanya mabadiliko ya kimsingi ya kiuongozi, kisera na kimfumo ya kitaifa, ili kurejesha nafasi na heshima ya Tanzania kimataifa katika mazingira ya sasa ya ushindani wa kiuchumi, kiulinzi, kijamii na kisiasa," alisema.
Source: Mimi mwenyewe mwana CHADEMA
Aidha, chama hicho kupitia Kurugenzi yake ya Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa kimemtaka Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi, kueleza iwapo hatua hiyo ndiyo msingi wa mahusiano yaliyopo kati ya nchi hizo, hasa ikizingatiwa kuwa serikali imekuwa ikieleza kwamba Tanzania ina mahusiano mazuri ya kiulinzi na Israel.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa wa CHADEMA kupitia mtandao wake wa kijamii.
Waziri Barak alifanya mahojiano na Radio Israel na kutoa kauli ambayo imenukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari vya nchi hiyo kuwa Tanzania si nchi ya muhimu wala ya maana hata kufikia hatua ya kuilinganisha na eneo ndani ya Libya linaloitwa Tripolitania.
Mnyika alisema kupuuzwa huku kwa nchi yetu katika medani ya kimataifa kunatokana na sera mbovu ya mambo ya nje chini ya utawala wa sasa wa Chama cha Mapinduzi (CCM).
"Tanzania imepoteza heshima katika siasa za dunia kutokana na diplomasia yetu kujikita katika kuomba omba kimataifa; pamoja na kuwa kimaneno na maandishi serikali inazungumza kuhusu diplomasia ya kiuchumi, kivitendo mahusiano yetu yamejengeka katika misingi ya utegemezi, kupungua kwa urari wa kibiashara na kuachia mianya ya uporwaji wa rasilimali," alisema.
Alieleza kuwa kauli ya Waziri Barak ni muendelezo wa mataifa mbalimbali kuifanya Tanzania na baadhi ya nchi nyingine za Afrika kukosa heshima wala sauti katika siasa za kimataifa kama ambavyo serikali za Uingereza na Marekani zilivyoweka masharti yenye mwelekeo wa ukoloni mamboleo kuhusu masuala ya ushoga na usagaji.
"Barua pekee ya Balozi wa heshima wa Tanzania nchini Israel, Kasbian Nuriel Chirich, kwenda kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel, Avigdor Lieberman ya kulaani matamshi hayo na kumkaribisha mwakilishi wa Israel kutembelea Tanzania haitoshi kuifanya serikali ya nchi hiyo kutambua athari za kidiplomasia za kauli iliyotolewa," alisema Mnyika.
Mbunge huyo alieleza kuwa wakati wa uongozi wa awamu ya kwanza wa hayati Mwalimu Julius Nyerere, Tanzania ilikuwa na heshima na sauti kimataifa si tu katika jitihada za ukombozi kusini mwa Afrika bali pia katika mahusiano ya kisiasa, kiuchumi na kijamii baina ya nchi za Kusini na mataifa mengine duniani.
Kutokana na hali hiyo, alisema iwapo hatua hazitachukuliwa kurejesha heshima na sauti ya Tanzania kimataifa, maamuzi mengi yatafanyika yenye athari kwa wananchi wengi bila ushiriki wao thabiti kama yanayoendelea hivi sasa kuhusu Mikataba ya Kiuchumi na Nchi za Jumuia ya Ulaya (EPA) yenye madhara kwa wakulima na wenye viwanda nchini.
"Ni wakati sasa kwa Watanzania kuendelea kuunganisha nguvu ya umma kusimamia uwajibikaji na kufanya mabadiliko ya kimsingi ya kiuongozi, kisera na kimfumo ya kitaifa, ili kurejesha nafasi na heshima ya Tanzania kimataifa katika mazingira ya sasa ya ushindani wa kiuchumi, kiulinzi, kijamii na kisiasa," alisema.
Source: Mimi mwenyewe mwana CHADEMA