lusanje
JF-Expert Member
- Apr 7, 2013
- 312
- 98
Nazungumza kwa hisia kali sana na hasa baada ya kugundua tumepoteza muda sana wa kupigania chama dhidi ya mafisadi lakini bila ya manufaa yoyote.
Wana CHADEMA asilia tunatoa tamko hili;
TAMKO LA CHADEMA ASILIA NA MWENENDO WA KISIASA NCHINI.
1)Ni ukweli usiopingika kuwa tutakwenda kushindwa uchaguzi huu. Hivyo tujiandae kisaikolojia kukabiliana na matokeo hayo.
2) Tunahitaji kufanya mabadiliko mara baada ya uchaguzi kwa viongozi na makapi yote tuliyoyakaribisha ukawa.
3)Mara baada ya uchaguzi tutavunja rasmi UKAWA na kila chama kirudi kilipotoka na kujiunda upya.
4) Viongozi waliotuingiza kwwnye dili la kuwaleta ukawa ni lazima tuwachukulie hatua warudishe pesa walizopewa na tutawafukuza.
5) Tunakwenda kuwaomba Dr Slaa na Prof Lipumba warudi kuongoza jahazi. Kwani mwenyekiti bila wewe mambo yameshindikana. Hana fikra pevu.
6) Tutairudisha ajenda ya ufisadi mara baada ya mafisadi kusepa baada ya wao kumaliz mission yao.
7) Wote waliogeuka na ku support mafisadi tutawataka wajitatathmini na waachie ngazi kama hakuna maelezo ya kutosha
Umepishana na gari la mishahara