Ujue nilichojifunza leo, ni kwamba wewe Lizaboni, una uelewa mkubwa sana, lakini kuna wakati huwa unaamua kuondoa uelewa wako ili kucheza ngoma ya akina Mwigulu Nchemba. Yaani hoja uliyoijenga hapa imekaa vizuri sana, kwamba CHADEMA na CCM wote ni watanzania, na kila tunachokifanya ni kwa ajili ya watanzania, whether ni CCM au ni CHADEMA wote wana haki sawasawa ya kushika madaraka na kuongoza nchi. Kwahiyo hatuna haya ya kuchukiana kibinadamu bali tushindane kwa hoja. Na yeyote kati yetu akiwa na hoja nzuri basi asikilizwe. Hii ni message mhimu sana kwa
Mwigulu Nchemba. Huwa anadhani wapinzani ni watu wa kutoka nchi jirani, na wakiongea jambo anawachukulia kwamba ni wageni wanaoingilia mambo ya ndani ya watanzania.
Mimi binafsi sina mtizamo huo. Bali nilichojaribu kukieleza katika post yangu ni ukweli kwamba CHADEMA wana dira, na si kweli kwamba hawana dira kama ambavyo wewe unataka kutusadikisha. Kama wasingekuwa na dira, ni dhahiri wasingeweza kutoa mawazo kwa chama tawala na yakakubaliwa.