Siwezi kukupinga moja kwa moja katika hoja yako, ingawa nitakupinga kukifananisha CHADEMA na baadhi ya vyama vya upinzani vilivyotangulia katika mapambano ya ukombozi dhidi ya CCM. Nazungumzia kukifananisha vyama KAMA NCCR 1995, CUF 2000-2005, na hata TLP. Nasema nitakupinga kwa hili kutokana na mikakati ya kichama waliyokuwa nayo wapinzani wa zama hizo. Vyama vilikuwa na mipango mibovu sana, ni kweli vilikuwa ni vyama vya msimu kwani siasa zao zilikuwa zikifanywa siku miaka michache sana (1 au 2) kabla ya uchaguzi. Katika mdahalo uliofanyika kwenye hotel ya Moven Peak Dar es salaam, mwaka 2010 siku moja kabla ya uchaguzi ukiwashirikisha wagombea urais kasoro wa CCM ambae alikatazwa na chama chake. Katika mdahalo huo Dr. Slaa aliulizwa na mwandishi wa habari, kuwa CHADEMA kinamatumaini makubwa sana ya kushinda uchaguzi wa kesho, je mkishindwa mtachukua hatua gani? Dr. Slaa pamoja na mambo mengine aliyomweleza mwandishi yule, alimweleza pia huo ndio utakuwa mwanzo mzuri wa kuijenga CHADEMA na kuifanya iwafikie watu tangu kwenye ngazi ya msingi. Kauli yake ile ilionekana walipoanzisha operations mbalimbali za chama. Mfano operation sangara, Movement for Change M4C, operation vua gamba vaa gwanda, sera ya majimbo ambayo inaonyesha kufanikiwa. Lakini pia kuelekeza nguvu kubwa kwa vijana ambao ndio kizazi cha vyama vingi. Nikisema hivyo namaanisha kwa kijana aliezaliwa mwaka 1992 kipindi mfumo wa vyama vingi unaasisiwa atakuwa ametimiza miaka ya kumuwezesha kupiga kura kufikia 2015. Huku ndiko wanapowekeza CHADEMA. Lakini pia wapo waliosema kuwa CHADEMA kama kingeshindwa 2010 basi kingekufa kama vyama vilivyotangulia vya upinzani lakini huu ni mwaka 2013 na kasi ya mabadiliko inazidi kuwaingia watanzania na ndiyo maana nikakwambia KUKIFANANISHA CHADEMA NA VYAMA VINGINE VYA UPINZANI NCHINI NI KUTOITENDEA HAKI. Ni vyema ungeifananisha na vyama vya upinzani vya Zambia na Kenya ambavyo vilifanikiwa kuviangusha vyama vikongwe kutokana na mikakati yake katika kuimarisha vyama vyao na hatimaye kuwapatia ukombozi kutoka kwa wakoloni weusi kama CCM. Chamsingi niwaombe viongozi wa CHADEMA waendelee na kasi hii na wasikatishwe tamaa na watu wachache wasioitakia mema Tanzania.