CHADEMA isipomvua Zitto uanachama...!

CHADEMA isipomvua Zitto uanachama...!

Natangaza rasmi kuwa Chadema isipomvua Zitto uanachama nitakuwa wa kwanza kuiviruga kupitia mtandao huu wa JF bila kujali lolote.
Nina details za kuvuruga chama zaidi ya Zitto.

Cc Crashwise
Mbona Chadema imeishavurugwa siku nyingi.
 
Zitto na wenzake watoeni haraka siku kumi na nne tayari, msifikiri mara mbili kuhusu kumvua uanachama. Mkimrudisha atarekebisha makosa aliyofanya na wasaliti wake watakuja smart zaidi ili kuua chama na hapo itakuwa 2015, bora sasa hivi muwatoe huyo ambaye hamjamjua kwanza sio tishio na bora awe mmoja kuliko wawe wengi.

Msikubari kushauriwa, katiba ndio msingi na simamieni katiba. . . mtaonesha kuwa hamuwezi ongoza nchi na mtakuwa hamfuati katiba kama CCM, hatutaweza ona tofauti na wenzenu wa CCM na huo pia ni mtego wao mkimwacha watawavaa.

Kama Zitto na wenzake wanapendwa na watu na ni maarufu waunde chama chao au wahamie chama ambacho watu watawafuata, wanang'ang'ania nini? ebu jiulizeni !!!! Ebo !

ni hayo tu yangu.

Mkuu siku 14 zilipaswa kuhesabiwa baada ya muda gani...Je unavyojuwa wewe uamzi ulitakiwa kutolewa siku ya kumi na tano au baada ya siku 14 kupita kikao kitaandaliwa cha kwenda kupitia utetezi wa wasaliti, je unajua walikata rufaa na rufaa yao imetupwa juzi.....
 
Binafsi nimekuwa pamoja na CDM tokea 2007 nikiwa chuoni lakini kwa mara ya kwanza ntarudisha kadi na sitakuja kupiga kura tena katika siasa za nchi hii

Kama mtaamua kumuona ZZK ni bora zaidi ya chama,ni bora zaidi ya maiti ya Mwandosi,ni bora kuliko maiti za Arusha,ni bora kuliko Katiba basi mwacheni ila msije kuilaumu halaiki pale historia itakapokuwa inareveal.

mwandosi ndiyo kwenye siasa za tanzania.
 
wenzako wamejadili usiku na mchana wameshindwa wamefanya vikao mpaka dubai wamekwama wewe unaleta ushauri wako mwepesi hapa.

Kamati gani ilikaa Dubai, acha kujitoa fahamu...
 
Mkuu siku 14 zilipaswa kuhesabiwa baada ya muda gani...Je unavyojuwa wewe uamzi ulitakiwa kutolewa siku ya kumi na tano au baada ya siku 14 kupita kikao kitaandaliwa cha kwenda kupitia utetezi wa wasaliti, je unajua walikata rufaa na rufaa yao imetupwa juzi.....

mtahangaika sana lakini mwisho wake mtakuja kujuta hamtaamini zitto ni kiboko yenu.
 
Usiwaze kuiua chadema kwa ufinyu wa fikra ila jitahidi kuwaza hivyo kwa tafkuri kubwa inayovuka mipaka ubinafsi wako wa roho na akili.
 
Ni kweli kabisa Mh. Zitto Kabwe hana budi kufukuzwa kabisa kwenye chama kwani amejisahau na kuona KITU (pesa) ni bora kuliko UTU (Watanzania) wakiwemo ndugu zake wa karibu (mjomba, shangazi, bibi, babu na wengine), mimi naamini CHADEMA ni chama makini hivyo kitafuata taratibu zote kikatiba za kumvua Zitto uanachama
 
Kama unaujua uozo wa cdm tuweke wazi au unashinikiza kiaina?
 
Sidhan kama chadema wanaweza kumvua uanachama Zito coz ndo kichwa chao pale!

Sent from my BlackBerry 9790 using JamiiForums
 
Mods ,......naileta mada hii kwa mara ya pili kwa kuwa mada niliyoleta mara ya kwanza ikiwa na maudhui ya namna hii mliifuta au kuunganisha bila kunitaarifu!

WanaJf wenzangu mimi sio mwanasiasa na sipendi hadaa za wanasiasa...nimeamua kuwa muwazi .....kama chadema haitamvua uanachama zitto kabwe basi mimi nitakuwa mmoja wa wafuasi wa buku 7 katika kueneza propaganda chafu dhidi ya chadema kupitia mtandao huu wa Jf au mtandao wowote ule unaofaa!Im not bluffing!nategemea kuanza mchakato huu mwanzoni mwa mwezi february mwaka 2014.
Cc to Crashwise
 
Last edited by a moderator:
Du zitto mwingine huyu kama sixgate. Uongozi busara na uvumilivu. Namini CC/KK wako makini wanaangalia amalize option zake zote ndio wamteremshe akiwa mwepesi. Naomba asiwe mwepesi
 
Who cares! Anza hata leo mkuu! Ni sawa na kutishia kuideki bahari! Huna lolote wewe.
 
nakubaliana na wewe kwenye hoja ya kutaka msaliti avuliwe uanachama. ni matumaini yangu kuwa ngazi ya maamuzi haitatuangusha.aidha sikubaliani na mpango wa kuivuruga cdm kama haitamvua uanachama huyu msaliti na kundi lake lote.
nikushauri uchukue msimamo wangu wa kiungwana wa kuondoka chamani ikiwa watamsamehe
 
Hayo ni maamuzi ya kamati kuu wamfukuze au wasimfukuze ila mimi nitaheshimu.
huwezi kuivuruga chadema wewe dhaifu!!
walijaribu akina sixgates sembuse wewe papeti
 
Last edited by a moderator:
thanks God hii mada imerudi...kwa kuwa ilifichwa.some creatures are very serious...mimi ni among them!
 
Back
Top Bottom