Salama ya CDM na Demokrasia ndani ya CDM ni lazima Zito Afukuzwe uanachama. vinginevyo CDM itaathirika sana kama itamwachia uanachama Zito. 1. Kubwa kuliko yote kukosoana ndani ya chama kutakufa kabisa na kila mmoja anajua athari za chama kutojikosoa. 2. Wanachama na wapenzi ama washabiki wa CDM watakaoonekana wako na Zito wataonekana wasaliti. 3. Kama inavyoaminika na wanachadema Zito anatumika na ccm. ccm hawataacha kumtumia Zito kuivuruga CDM. 4. Kuwepo kwa Zito kutabariki na kuzalisha makundi mengine yenye nia na malengo yaleyale ya kuivuruga CDM. 5. Zito anaonekana ni mtalaam wa siasa za kunyemeleana kuviziana ,Makundi na siasa za kibinafsi si rahisi akaacha harakati hizo