CHADEMA isipomvua Zitto uanachama...!

CHADEMA isipomvua Zitto uanachama...!

Mkuu siku 14 zilipaswa kuhesabiwa baada ya muda gani...Je unavyojuwa wewe uamzi ulitakiwa kutolewa siku ya kumi na tano au baada ya siku 14 kupita kikao kitaandaliwa cha kwenda kupitia utetezi wa wasaliti, je unajua walikata rufaa na rufaa yao imetupwa juzi.....
mkuu sina shaka kwamba wewe ni mmoja wa wazalendo wa kweli wa chadema lakini nimekupa taarifa kuwa Im not a politician!I know you are not too!
 
umetumwa na maccm hilo jambo ni la kamati kuu wewe hata halikuhusu kwanza huna hata kadi ya chama

kuiangusha ccm haukihitaji kadi ya ccm na pia kuikuza au kuiangusha chadema hakuhitaji kadi ya chadema....Im a just a simple citizen!
 
You dont know what you are talking about.
Mwaka 2005, ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza kukutana na kijana nguri wa siasa Zitto Zuberi Kabwe. Nakumbuka ilikuwa eneo maarufu kama Kontena pale chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Tulikuwa katika harakati za uchaguzi wa Serikali ya wanafunzi DARUSO.

John Mrema ndiye aliyenitambulisha kwa mwanasiasa huyu kijana na mahiri kwa siasa zake za kuvizia. Ulikuwa uchaguzi wa serikali ya wanafunzi, ambapo Mwita Waitara Mwikwabe ndiye aliyeibuka kidedea. Huyu alijifanya kuvaa nguo za kijani nje kumbe ndani ni gwanda.

Hata kabla ya mwaka huo (2005) nilikuwa nikimsikia Zitto jinsi anavyofanya siasa ndani ya UDSM wakati yeye sio mwanafunzi. Pia nikawa nasikia siasa hizo anazifanya hata vyuo vingine isipokuwa Mzumbe ambapo UVCCM ilikuwa imeweka mizizi.

ZITTO apingwe tu, tena sana.

Nadhani watu wanaweza kudhani nimeungana na Umbowe au Ubabu kumsema Zitto hasha, nilitokea kutopenda siasa za Zitto toka kale. Kwasababu nilimuona ni kijana mahiri na mweredi wa siasa lakini akiwapoteza vijana wengi sana nchini, tena wenye elimu zao.

1. Zitto amewafanya vijana wengi sana kujiunga na chama cha wajanja wajanja (CDM) wakati akijua chama hicho, sio chama kitakachowaletea maendeo watanzania, bali kukuza malalamiko na usanii.

2. Zitto aliwadanganya vijana wengi sana katika elimu ya juu, wakaingia katika migomo katika vyuo vyao. Wengine walifukuzwa na wengine walisimamishwa. Kisa ulikuwa ni mkakati wake wa kuimarisha Chadema.

3. Zitto amewapotosha vijana wengi, ambao sasa wanaona mbele giza, hawajui wafanye nini. Kwasababu aliwapa matumaini makubwa juu ya CDM wakati akijua sio chama cha siasa bali genge la wanasihasa

4. Zitto, baada ya kuwapotosha vijana wengi, sasa hataki kuwaambia ukweli, nini kilichomo ndani ya CDM, zaidi anafanya mipango ya kuwakimbia/kuwatelekeza.

5. Zitto amewafitinisha vijana na serikali yao. Ili waione CDM ni malaika.

Kwa dhati kabisa, Chadema mchapeni viboko vingi, tena vingi.
 
tatizo la mbwembwe za kijinga sema kufikia tarehe ngapi asipofukuzwa unajitoa uanachama ili siku ikifika niwe shaidi wake. Isije kuwa kama issue ya kuvua gamba.
 
Vyama vingine bwana!
Eti Zito Kabwe nae anaogopwa na Chama na wanachama zaidi ya million 5?
Eti Zito nae anataka kuwa Rais wa Tz?
Eti Zito nae anataka awe maarufu kuzidi CDM?
Kati ya mambo ambayo Mwl JKN hakuyapenda ni hayo na akikugundua ndo ulivo anakutoa haraka Sana chamani.
TOA ZITO NI MZIGO...CDM NI YA TZ SIO KIGOMA WALA ARUSHA PEKE YETU.
 
Mkuu mimi nitarudisha kadi ya CDM na kubaki kuwa yatima wa kisiasa, Zitto kafanya mabaya mengi sana hata hili la kumchafua Mbowe kahusika na soon tutaleta ushaidi humu.

Sipo tayari kuishi na nyoka nyumba moja.

Hivi Mbowe Kachafuliwa au kajichafua kwani alito...zewa yule mbunge kama zito kahusika ni kwamba kahusika kusema ukweli
 
Last edited by a moderator:
Natangaza rasmi kuwa Chadema isipomvua Zitto uanachama nitakuwa wa kwanza kuiviruga kupitia mtandao huu wa JF bila kujali lolote.
Nina details za kuvuruga chama zaidi ya Zitto.

Cc Crashwise

Kumbe we kirusi kikali kuliko virusi vyote vilivyowahi kutokea Chadema
 
Wakati Chadema wanamvua madaraka Zitto walisema hawajafuata utaratibu rasmi wa kawaida kwa sababu hilo ni jambo la dharura lililohitaji kufanyiwa maamuzi ya haraka sana. Hivi sasa unaisha mwezo tangu Chadema walipotoa siku 14 na hawana haraka yoyote ya kufanya maamuzi.

Je, ile dharura iliyowafanya wasifuate utaratibu wa kawaida wa kikatiba imeyeyuka vipi?

Chadema ni chama kinachoendeshwa katika misingi ya kilaghai...

Cc Pasco

Sawa kabisa mkuu
 
Back
Top Bottom