CHADEMA imekosa Dira?

Does this article make any sense ama tunataka sasa kushusha hadhi ya forum kwa kuleta inssues ambazo ni below standard of this forum ? Hivi Masatu hoja ama post hii si ungaliweza kuandika kule kule ziliko za CUF ama CCM tukabana matumizi ?Ni mawazo yangu na swali tu si lazima ufuate ninavyosema mimi .

Lunyungu.

Article ya kusema kuwa Chadema wameshinda Biharamulo ina make sense?jee sio Below standard ya JF? WATU walivyokuwa hawana subra na wamejaa ushabiki WA CHADEMA wakajaza THANKS 71 habari isiyo na ukweli,wewe ukawa mtu wa pili kutuma maoni na ukasema hivi

"TAARIFA KAMILI NI KWAMBA CHADEMA WAMERUDIA MAMBO YA TARIME,CHADEMA IMESHINDA BIHARAMULO HABARI ZA UHAKIKA UNAWEZA KUPIGA SIMU +255787 474 707 KUJUA UKWELI".

UKAMALIZA KWA KUSEMA HONGERA CHADEMA.

UKAPEWA THANKS 21,ULIANDIKA HAYA WAKATI UKIJUA UNAONGOPA.

UONGO WAKO NA WENZAKO UKAWAPONZA GAZETI LA TANZANIA DAIMA WAKAKOPI HABARI KAMA ILIVYO KUMBE WAMEDANGANYWA KWA KUTEGEMEA HABARI YENU YA UPOTOSHAJI.

HABARI ZENU ZINA MAKE SENSE? MASATU KAULIZA CHADEMA WAMEKOSA DIRA? HUJAONA ALAMA YA KUULIZA SWALI?
 
Kufuatia kushindwa mfululuizo katika chaguzi ndogo za Busanda na Bihalamuro, chama cha "demokrasia" na maendeleo chadema kimepoteza dira sasa badala ya kukaa chini na kufanya tathmini ya kisanyansi mpaka kupelekea kushindwa katika chaguzi hizo, viongozi wa chama hicho hivi sasa wanamtafuta mchawi kwa kusingizia kuibiwa kura.

Madai kama haya yamekuwa yakitolewa na chama cha wananchi cuf katika chaguzi mbalimbali lakini chadema wamekuwa wakidai kuwa cuf ni walalamishi na sasa wimbo huo unaanza kuimbwa na chadema.

Ukweli ni Chadema kimekosa mikakati thabiti kuweza kuongoza na kubaki na kulala kila uchao, kilichobaki sasa kwa Chadema ni kurudi kwenye drawing board na kuanza upya huku wakijua siasa za Mwembe ya yanga za kulipua mabomu na kuvurumisha helikopta hazilipi na watanzania washawatukia kuwa ni chama cha kikabila na familia

Masatu pole sana nduguyu yangu.
Najua unakazi kubwa sana ya kuwaonyesha mabosi wako kuwa huwa una-post na kukilinda chama chako cha CCM-fisadi. Nilikuwa nategemea utoe post elimishi ila bado umejikita kwenye siasa za kiimla kama vile huoni yanayojiri Tanzania na umasikini wa kila kona baada ya sera za serikali ya CCM kushindwa baada ya kuwa madarakani kwa miaka zaidi ya 30.

CCM hawajakosa tu dira ila hawana mwelekeo wala haijui wanakwenda wapi, hawana uongozi wala hawala mipango ya kimaendeleo ya nchi zaidi ya mipingo ya kuiba kura kutumia NEC.

Chadema wana DIRA na mwelekeo mzuri sana, ni chama ambacho kinakuwa na kuwekeza mtaji wake kwa wananchi wote na kutumia rasilimali watu ili kuweza kumkomboa mwananchi aliyesahaulika baada ya kulipa kodi kwa mika 50 na kuliwa na kundi dogo. Chadema yenye demokrasia ya kweli lazima ipitie kwenye mikiki mingi ya siasa hasa hili la kudai kubadilika kwa Tume Ya Taifa ya Uchaguzi ni lazima kubadili mfumo mzima na uendeshaji wa NEC. Sisi kama Chadema tunaelewa hilo ni gumu sana kwa CCM kukubali kwani huu ndio muhimili wa ninyi washika pembe wa CCM mnapotegemea na kutoa lugha za kejeli na jeuri hata kudiriki kutukana wananchi.

Chadema imejipanga vizuri kupambana na dhuluma na proganda zenu, tupo mstari wa mbele kuelimisha wananchi na kuhakikisha tunajenga base nzuri iliyo huru na yenye demokrasia ya kweli isiyo ya kiimla wala ng'ang'anizi madarakani hata kuua kama mnavyofanya ninyi. Ni wajibu wa Chadema kuhakikisha wananchi wanajua nini wajibu wa serikali kwao baada ya wao kulipa kodi na kuchagua viongozi. Ni wajibu wa chadema kuwaelimisha wananchi hatari ya viongozi wanaoingia madarakani kwa kuiba kura, rushwa, ghiliba na aina yeyote ile ya dhuluma, hili ndio tunda na zao la ufisadi, rushwa na utawala mbovu uliojaa mikataba mibovu na utendaji mbaya na usiofaa. Ni lazima wananchi wajue hali hii haitokwisha bila kuachana na viongozi wanoingia utawalani kwa kutumia njia badhirifu.

CCM chama chako kimejikita kwenye dhuluma, ndio maana hata wewe unashabikia kwa sababu unafaidika na wizi huu, ila umesahau kuwa badala ya kupambana na Chadema wanaopigania haki pamoja na yako, ungegeuka uwaambie watawala wako kuwa hata sisi(CCM) tupo ndani ya hili behewa.
Behewa la barabara mbovu, hospitali mbaya, elimu duni, wizi wa maliasili yetu, mikataba mibovu nk. Waambie kuwa sote ni wahanga wa haya madhila.

Masatu miaka hamsini sasa bado hatuna Hospitali icon ya taifa, Masatu miaka 50 hatuwezi hata kukusanya kodi zetu, hatuwezi hata kusaini mikataba kwa ajili ya wananchi wetu kisingizio hatuna wataalamu.
Miaka hamsini bado kuna shule hazina waalimu, zahanati hazina dawa na wahudumu. Jiji halina maji na umeme wa uhakika, CCM haina mwelekeo dira wala majibu. CCM haina chakujivunia ilichokifanya inashindana kutoa ahadi na mtoto mwenye miaka 18. Je mzee wa miaka 50 hana alichokifanya bado anaahidi apewe muda zaidi afanye alichoaahidi miaka 40 iliyopita.
Masatu wageukie wenzako mwelezane ukweli, kilio chetu ni cha kweli na mabadiliko tunayoyataka ni ya kweli na tunaweza na tutafanya.CHADEMA ndio chama chenye dira na nia ya kweli kumboa mwananchi, chama cha wananchi wote na mali ya wote kipo kwa ajili ya wote kwa maendeleo na ulinzi wa mali asili zetu kwa ajili ya kizazi hiki na kizazi kijacho.
 
Kufuatia kushindwa mfululuizo katika chaguzi ndogo za Busanda na Bihalamuro, chama cha "demokrasia" na maendeleo chadema kimepoteza dira sasa badala ya kukaa chini na kufanya tathmini ya kisanyansi mpaka kupelekea kushindwa katika chaguzi hizo, viongozi wa chama hicho hivi sasa wanamtafuta mchawi kwa kusingizia kuibiwa kura.

Madai kama haya yamekuwa yakitolewa na chama cha wananchi cuf katika chaguzi mbalimbali lakini chadema wamekuwa wakidai kuwa cuf ni walalamishi na sasa wimbo huo unaanza kuimbwa na chadema.

Ukweli ni Chadema kimekosa mikakati thabiti kuweza kuongoza na kubaki na kulala kila uchao, kilichobaki sasa kwa Chadema ni kurudi kwenye drawing board na kuanza upya huku wakijua siasa za Mwembe ya yanga za kulipua mabomu na kuvurumisha helikopta hazilipi na watanzania washawatukia kuwa ni chama cha kikabila na familia

Mwanawasu inawezekana kweli chadema imekosa dira, lakini je ni chama gani chenye dira?Bila shaka unataka kutueleza kuwa ccm ndicho chenye dira.Ccm hii hii unayotaka kutuaminisha kwamba ina dira si ndiyo katibu mkuu wake alisema tena hadharani kwamba imekosa dira?au umemsahau marehemu Horace Kolimba, huyu si alikuwa katibu mkuu wa ccm na akatamka bayana kwamba chama kimekosa dira, matokeo yake mkamkolimba. Au nawewe unaogopa kufanyiwa ukolimba kwahiyo inabidi ufe na tai shingoni huku moyoni ukisononeka?
Hivi masatu wale ndugu zako kule nyambono wamefaidika nini na CCM?
Kutokana na hiyo dira ya ccm, kuna matumaini gani ya kuinua maisha ya ndugu zako wa bwasi ambao wamekuwa wakiogelea kwenye lindi la umaskini kwa miaka yote tangu tupate uhuru?hiyo dira ya ccm itawanufaisha lini watu wa kisorya?
 
Kufuatia kushindwa mfululuizo katika chaguzi ndogo za Busanda na Bihalamuro, chama cha "demokrasia" na maendeleo chadema kimepoteza dira sasa badala ya kukaa chini na kufanya tathmini ya kisanyansi mpaka kupelekea kushindwa katika chaguzi hizo, viongozi wa chama hicho hivi sasa wanamtafuta mchawi kwa kusingizia kuibiwa kura.

Madai kama haya yamekuwa yakitolewa na chama cha wananchi cuf katika chaguzi mbalimbali lakini chadema wamekuwa wakidai kuwa cuf ni walalamishi na sasa wimbo huo unaanza kuimbwa na chadema.

Ukweli ni Chadema kimekosa mikakati thabiti kuweza kuongoza na kubaki na kulala kila uchao, kilichobaki sasa kwa Chadema ni kurudi kwenye drawing board na kuanza upya huku wakijua siasa za Mwembe ya yanga za kulipua mabomu na kuvurumisha helikopta hazilipi na watanzania washawatukia kuwa ni chama cha kikabila na familia

Duh! Hii kali!!! Ama kweli mtu akipenda chongo huita kengeza. Chama gani kiko kwenye decline kama siyo CCM. Tuwe objective katika ku-analyse issues. CHADEMA sasa hivi kinapata 45+ kwenye chaguzi, hayo ni mafanikio makubwa sana na sasa hivi wana-CCM wanajua kabisa Wadanganyika si mambumbu na ndiyo maana wanaweweseka na kinachoweza kutokea 2010. SERA KUU YA CCM NI UFISADISM

"USHINDI WA KIMBUNGA KWA CCM BILA POLISI, JESHI, TUME YA UCHAGUZI na RUSHWA" ni NDOTO ZA ALINACHA"
 
Masatu pole sana nduguyu yangu.
Najua unakazi kubwa sana ya kuwaonyesha mabosi wako kuwa huwa una-post na kukilinda chama chako cha CCM-fisadi. Nilikuwa nategemea utoe post elimishi ila bado umejikita kwenye siasa za kiimla kama vile huoni yanayojiri Tanzania na umasikini wa kila kona baada ya sera za serikali ya CCM kushindwa baada ya kuwa madarakani kwa miaka zaidi ya 30.

CCM hawajakosa tu dira ila hawana mwelekeo wala haijui wanakwenda wapi, hawana uongozi wala hawala mipango ya kimaendeleo ya nchi zaidi ya mipingo ya kuiba kura kutumia NEC.

Chadema wana DIRA na mwelekeo mzuri sana, ni chama ambacho kinakuwa na kuwekeza mtaji wake kwa wananchi wote na kutumia rasilimali watu ili kuweza kumkomboa mwananchi aliyesahaulika baada ya kulipa kodi kwa mika 50 na kuliwa na kundi dogo. Chadema yenye demokrasia ya kweli lazima ipitie kwenye mikiki mingi ya siasa hasa hili la kudai kubadilika kwa Tume Ya Taifa ya Uchaguzi ni lazima kubadili mfumo mzima na uendeshaji wa NEC. Sisi kama Chadema tunaelewa hilo ni gumu sana kwa CCM kukubali kwani huu ndio muhimili wa ninyi washika pembe wa CCM mnapotegemea na kutoa lugha za kejeli na jeuri hata kudiriki kutukana wananchi.

Chadema imejipanga vizuri kupambana na dhuluma na proganda zenu, tupo mstari wa mbele kuelimisha wananchi na kuhakikisha tunajenga base nzuri iliyo huru na yenye demokrasia ya kweli isiyo ya kiimla wala ng'ang'anizi madarakani hata kuua kama mnavyofanya ninyi. Ni wajibu wa Chadema kuhakikisha wananchi wanajua nini wajibu wa serikali kwao baada ya wao kulipa kodi na kuchagua viongozi. Ni wajibu wa chadema kuwaelimisha wananchi hatari ya viongozi wanaoingia madarakani kwa kuiba kura, rushwa, ghiliba na aina yeyote ile ya dhuluma, hili ndio tunda na zao la ufisadi, rushwa na utawala mbovu uliojaa mikataba mibovu na utendaji mbaya na usiofaa. Ni lazima wananchi wajue hali hii haitokwisha bila kuachana na viongozi wanoingia utawalani kwa kutumia njia badhirifu.

CCM chama chako kimejikita kwenye dhuluma, ndio maana hata wewe unashabikia kwa sababu unafaidika na wizi huu, ila umesahau kuwa badala ya kupambana na Chadema wanaopigania haki pamoja na yako, ungegeuka uwaambie watawala wako kuwa hata sisi(CCM) tupo ndani ya hili behewa.
Behewa la barabara mbovu, hospitali mbaya, elimu duni, wizi wa maliasili yetu, mikataba mibovu nk. Waambie kuwa sote ni wahanga wa haya madhila.

Masatu miaka hamsini sasa bado hatuna Hospitali icon ya taifa, Masatu miaka 50 hatuwezi hata kukusanya kodi zetu, hatuwezi hata kusaini mikataba kwa ajili ya wananchi wetu kisingizio hatuna wataalamu.
Miaka hamsini bado kuna shule hazina waalimu, zahanati hazina dawa na wahudumu. Jiji halina maji na umeme wa uhakika, CCM haina mwelekeo dira wala majibu. CCM haina chakujivunia ilichokifanya inashindana kutoa ahadi na mtoto mwenye miaka 18. Je mzee wa miaka 50 hana alichokifanya bado anaahidi apewe muda zaidi afanye alichoaahidi miaka 40 iliyopita.
Masatu wageukie wenzako mwelezane ukweli, kilio chetu ni cha kweli na mabadiliko tunayoyataka ni ya kweli na tunaweza na tutafanya.CHADEMA ndio chama chenye dira na nia ya kweli kumboa mwananchi, chama cha wananchi wote na mali ya wote kipo kwa ajili ya wote kwa maendeleo na ulinzi wa mali asili zetu kwa ajili ya kizazi hiki na kizazi kijacho.


Mijineno miiiingi no substance blah blah tupu! rudi darasani kajifunze hebasu kwanza toka kujitawala ni miaka 48 na sio 50.

Ukisha pass hesabu za kujumlisha na kutoa njoo tukate issue....
 
Mwanawasu inawezekana kweli chadema imekosa dira, lakini je ni chama gani chenye dira?Bila shaka unataka kutueleza kuwa ccm ndicho chenye dira.Ccm hii hii unayotaka kutuaminisha kwamba ina dira si ndiyo katibu mkuu wake alisema tena hadharani kwamba imekosa dira?au umemsahau marehemu Horace Kolimba, huyu si alikuwa katibu mkuu wa ccm na akatamka bayana kwamba chama kimekosa dira, matokeo yake mkamkolimba. Au nawewe unaogopa kufanyiwa ukolimba kwahiyo inabidi ufe na tai shingoni huku moyoni ukisononeka?
Hivi masatu wale ndugu zako kule nyambono wamefaidika nini na CCM?
Kutokana na hiyo dira ya ccm, kuna matumaini gani ya kuinua maisha ya ndugu zako wa bwasi ambao wamekuwa wakiogelea kwenye lindi la umaskini kwa miaka yote tangu tupate uhuru?hiyo dira ya ccm itawanufaisha lini watu wa kisorya?

Ooh really? kwa hiyo maneno ya marehemu yashakuwa msahafu... hang on a minute... tunae marehemu mwingine anaitwa Chacha Wangwe yeye alisema Chadema ni chama cha kikabila na familia nae mka mkolimba! how about that?
 
Mugo"The Great";514193 said:
Duh! Hii kali!!! Ama kweli mtu akipenda chongo huita kengeza. Chama gani kiko kwenye decline kama siyo CCM. Tuwe objective katika ku-analyse issues. CHADEMA sasa hivi kinapata 45+ kwenye chaguzi, hayo ni mafanikio makubwa sana na sasa hivi wana-CCM wanajua kabisa Wadanganyika si mambumbu na ndiyo maana wanaweweseka na kinachoweza kutokea 2010. SERA KUU YA CCM NI UFISADISM

"USHINDI WA KIMBUNGA KWA CCM BILA POLISI, JESHI, TUME YA UCHAGUZI na RUSHWA" ni NDOTO ZA ALINACHA"


Well if we go by the same scenario tokea uchaguzi mkuu uliopita CCM wameongeza jimbo la Bihalamuro baada ya kulipoteza 2005. Je chadema wameongeza jimbo gani? work it out ni nani baina ya CCM na Chadema ana decline.

Wahenga wanasema "nearly never killed a bird" mmeshindwa na mtaendelea kushindwa!
 
Mijineno miiiingi no substance blah blah tupu! rudi darasani kajifunze hebasu kwanza toka kujitawala ni miaka 48 na sio 50.

Ukisha pass hesabu za kujumlisha na kutoa njoo tukate issue....

Huwa JF hoja kwa hoja kama unakimbia kujibu hoja wewe kimbia nafikiri lugha niliyotumia ni rahisi jibu hoja.Ahadi nimesema za miaka 40. Je Chama chako CCM kimekwisha toa ahadi ngapi mpaka leo hakuna mlichotekeleza zaidi ya kuzidisha wizi na kupora mali.

Masatu, je ni maeneo gani zaidi ya wizi unajivunia serikali ya CCM? nimekwambia hatuna hata hospitali moja ICON ya Taifa, barabara mbovu, shule waalimu hakuna watoto wana kaa vumbini. Jibu hayo mimi sio mtu wa mipasho.
 
^^ Mwenye macho ahambiwi tazama... tararila za hakuna hiki, kile kiko vile, pale pamekuwa hivi ni aina tu ya mipasho
 
Well if we go by the same scenario tokea uchaguzi mkuu uliopita CCM wameongeza jimbo la Bihalamuro baada ya kulipoteza 2005. Je chadema wameongeza jimbo gani? work it out ni nani baina ya CCM na Chadema ana decline.

Wahenga wanasema "nearly never killed a bird" mmeshindwa na mtaendelea kushindwa!

From CCM perspective kuongeza jimbo ni mafanikio(hii ni kweli) lakini from another angle CCM inapoteza umaarufu ndio maana ushindi wa 80-90% sasa hivi haupo. Unajua mti unaweza kuwa mmoja lakini ukiambiwa uelezee ulivyo itategemea na angle uliyopo. Kwako wewe kuongeza jimbo ni mafanikio (you are entitled to it) na kwangu mimi kupungua kwa %age ni sign ya decline. That's why katika kupima performance kuna A+, A, A-, B+, B n.k.

Lakini amini usiamini "ENZI ZA CHAMA KUSHIKA HATAMU aka UTAMU ZINATOWEKA"
 
masatu jibu hoja usilumbane kwa kutumia vina na nahau za mipasho eleza kisayansi nini kimekufanya uone na utuaminishe kuwa chadema haina dira
 
Huwa JF hoja kwa hoja kama unakimbia kujibu hoja wewe kimbia nafikiri lugha niliyotumia ni rahisi jibu hoja.Ahadi nimesema za miaka 40. Je Chama chako CCM kimekwisha toa ahadi ngapi mpaka leo hakuna mlichotekeleza zaidi ya kuzidisha wizi na kupora mali.

Masatu, je ni maeneo gani zaidi ya wizi unajivunia serikali ya CCM? nimekwambia hatuna hata hospitali moja ICON ya Taifa, barabara mbovu, shule waalimu hakuna watoto wana kaa vumbini. Jibu hayo mimi sio mtu wa mipasho.

Masatu miaka hamsini sasa bado hatuna Hospitali icon ya taifa, Masatu miaka 50 hatuwezi hata kukusanya kodi zetu, hatuwezi hata kusaini mikataba kwa ajili ya wananchi wetu kisingizio hatuna wataalamu.


Chadema wana DIRA na mwelekeo mzuri sana, ni chama ambacho kinakuwa na kuwekeza mtaji wake kwa wananchi wote na kutumia rasilimali watu ili kuweza kumkomboa mwananchi aliyesahaulika baada ya kulipa kodi kwa mika 50 na kuliwa na kundi dogo.

Hayo maneno ya nani?
 
Kama tunaanza kulumbana humu ndani haisaidii chochote. mimi nadhani kuchambua hoja ni mhimu sana. Kwanza CHADEMA wanapashwa kukaa chini na kujiuliza kwanini wanakua na washabiki wengi lakini votes zinakua ndogo? Je kuna mkono wa mtu during votes counting? je do they trust their agents? How about their network at village levels? na P.R za wagombea woa zikoje huko majimbona? Kwanini watu wengi wanajiandikisha kupiga kura lakini wanao turn up ku vote ni nusu tuu? kwanini watu wanakua waoga kupiga kura?
 
Kitendo cha CHADEMA kutangaza kimeshinda uchaguzi wa B'mulo kupitia kwa wapambe wake ni kipimo tosha kuwa chama hicho kimekosa Dira.
 
Angalau CHADEMA wanathubutu kuitikisa CCM sasa. Tuuangalie tu mfumo wa sasa wa uwakilishi BUNGENI. Huu wa aliyeshinda hata kwa kura moja anatangazwa mshindi hata kama waliojitokeza kupiga kura hawafiki nusu ya WALIOJIANDIKISHA inaacha maswali mengi kuliko majibu. Tuangalie mifumo mingine ya kuchaguana duniani ikoje.
Hakuna TIJA kwa TAIFA kuwa na BUNGE linalofanana na mfumo wa utawala wa chama kimoja.
Kama kuna haja ya kuendelea na viti maalum mtu kama MBASA wa Biharamulo au MAGESA wa Busanda walistahili kupewa nafasi hizo.
 
Angalau CHADEMA wanathubutu kuitikisa CCM sasa. Tuuangalie tu mfumo wa sasa wa uwakilishi BUNGENI. Huu wa aliyeshinda hata kwa kura moja anatangazwa mshindi hata kama waliojitokeza kupiga kura hawafiki nusu ya WALIOJIANDIKISHA inaacha maswali mengi kuliko majibu. Tuangalie mifumo mingine ya kuchaguana duniani ikoje.
Hakuna TIJA kwa TAIFA kuwa na BUNGE linalofanana na mfumo wa utawala wa chama kimoja.
Kama kuna haja ya kuendelea na viti maalum mtu kama MBASA wa Biharamulo au MAGESA wa Busanda walistahili kupewa nafasi hizo.
Mfumo wa kuchaguliwa kwa kura za wananchi ndio sahihi, viti maalumu ni kumwongezea tu mwanchi mzigo usio na maana.Wananchi wa kada zote wanatakiwa wawe na elimu ya kutosha ya uraia na uwakilishi na nini maana ya kura zao. Hili CCM inaliogopa kwani uelewa wa mpiga kura ni kaburi la CCM.
 
Hivi kwani ni CHADEMA peke yake iliyoshindwa katika uchaguzi wa Biharamulo??
 
Back
Top Bottom