CHADEMA imeitekeleza nyumba ya Alphonce Mawazo?

CHADEMA imeitekeleza nyumba ya Alphonce Mawazo?

Habari yako mkuu sipingani na ww katika unachokieleza je umeshafanya mawasiliano na wale walioahidi? ili kujiridhisha na kutuletea taarifa bila kuegemea upande wowote maana maisha ya mtu hayaitaji unafiki au umbea kabisa, hivyo ningelishauri ungelifuatilia kwa pande zote mbili maana kwa upande wangu naona umeleta mada ya kinafiki kutaka kuonyesha upande fulani ni bora mwingine si bora, ili hali hapa unazungumzia maisha ya watu,tuwe makini katika uletaji wa habari, ni wazo tu.
umenena vyema mkuu.
 
Waungwana Poleni Na Majukumu ... 09/08/2016 Nilibahatika Kufanya Mazungumzo Na Mke Na Baadhi Ya Ndugu Wa Alphonce Mawazo ... Inasemekana Baada Ya Mazishi Viongozi Wa Chadema Walitoa Ahadi Kwa Familia Ya Alphonce Mawazo Ikiwemo Kuijengea Nyumba Familia Hiyo ... Kuwasomesha Watoto ... Kuinunulia Gari Familia Hiyo ... Na Kuwapatia Mtaji Wa Biashara Lakini Cha Ajabu Hadi Leo Viongozi Wa Chadema Hakuna Ahadi Yoyote Waliyoitekeleza ... Mimi Kama Mtanzania Mzalendo Kupitia Hii Thread Napenda Kuwakumbusha Viongozi Wa Chadema Wajitokeze Na Kwenda Kutekeleza Ahadi Walizoahidi Kwa Familia Ya Alphonce Mawazo ... !
Labda mm nikuulize tu ili kuweka kumbkumb sawa, hayo mazungumzo yenu yalitokana na nn?? uliitwa au ulijipeleka mwenyewe?? Na baada ya mazungumzo hayo ww binafsi ukionyesha kuguswa kwa hali ya juu ulichangia nn kwa familia hiyo....??? Hii ni habari ya 'kichochezi'
 
Waungwana Poleni Na Majukumu ... 09/08/2016 Nilibahatika Kufanya Mazungumzo Na Mke Na Baadhi Ya Ndugu Wa Alphonce Mawazo ... Inasemekana Baada Ya Mazishi Viongozi Wa Chadema Walitoa Ahadi Kwa Familia Ya Alphonce Mawazo Ikiwemo Kuijengea Nyumba Familia Hiyo ... Kuwasomesha Watoto ... Kuinunulia Gari Familia Hiyo ... Na Kuwapatia Mtaji Wa Biashara Lakini Cha Ajabu Hadi Leo Viongozi Wa Chadema Hakuna Ahadi Yoyote Waliyoitekeleza ... Mimi Kama Mtanzania Mzalendo Kupitia Hii Thread Napenda Kuwakumbusha Viongozi Wa Chadema Wajitokeze Na Kwenda Kutekeleza Ahadi Walizoahidi Kwa Familia Ya Alphonce Mawazo ... !
Ni kawaida kutelekezwa ni yalee ya Marehemu shelembi wa shinyanga kimya mpaka hivi leo
 
Mawazo alikufa kifo kibaya sana tena akitoka kwenye harakati za kujenga chama. Labda polisi kupitia uchunguzi wamehundua yaliyonyuma ya pazia kuhusu kifo kile.

Lkn tukumbuke kuwa ukifa hautakumbukwa utatelekezwa tu.

Tusubiri taarifa za ukuta tuone
walitoa ahadi ni vema wakaenda kuzitimiza
 
Wewe ni liongo kabla ya msiba kuisha wabunge wa chadema walichanga pesa zaidi ya milioni 100.

Kaulize kama hizo 100 Mil zimemfikia mjane wa Mawazo, zilivyopatikana tu zilichukuliwa na uongozi wa juu kwa kile kilichoitwa kulipa wanasheria na gharama za kumweka mwekiti mbowe pamoja na lowassa mwanza wakati wakishughurikia kesi ya maziko ya Mawazo
 
Mimi siyo mwanasiasa nawakumbusha tu
Kama sio mwanasiasa umeletaje Taarifa za kisiasa?wewe umesema umefanya mahojiano na mke wa marehemu Mawazo si ndivyo? Na kwa maana hiyo wewe ni mwandishi wa habari.Lengo la mahojiano hayo ilikuwa nini? Kama ilikuwa kujua kama ahadi ulizo zitaja zimetekelezwa ama la ,umeshindwaje kufanya mahojiano na walio ahidi? Kabla ya kuleta hapo? Na je mke wa Mawazo ndiye amekuomba umsemee hapa??
 
Sioni sababu ya watu humu kumshambulia na kumtukana mtoa mada.......
Uongo daima unazimwa na ukweli.....na uongo ukiachwa bila ya kuuzima utaaminika na watu kana kwamba ndio ukweli.........

Kama kweli CHADEMA walitoa ahadi hiyo kwa familia ya kamanda Mawazo na hawajatekeleza hata moja si jambo la kiungwana......njia pekee ya kumshushua mtoa mada ili aone haya ya kupost uongo siku nyingine ni kuumwaga ukweli wa jambo lenyewe......

Simamia kweli kwa kuwa kweli daima hutuweka huru.....
 
Back
Top Bottom