Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 97,115
- 136,850
Hiki chama kikuu cha upinzani baada ya uchaguzi wa 2015, badala ya kuendelea kukua, sasa ni dhahiri kabisa kuwa hakifanyi hivyo bali kimedumaa, kinazidi kudumaa, na kimedhoofu sana.
Wengi wetu tiliona jinsi chama hicho kilivyoendelea kustawi baada ya uchaguzi wa 2010. Kati ya 2010 hadi 2015 chama kilikua, kilistawi, hadi kikawa tishio la kweli dhidi ya CCM na kukifanya chama hicho tawala kulazimika kufanya mabadiliko na kimsingi kukiri kwamba ufisadi ni tatizo kubwa.
Sasa toka 2015 mpaka hivi sasa hiki chama ni kama kimechanganyikiwa kabisa. Hakijui hata kifanye nini. Kutwa kucha kinapoteza wanachama wake wanaohamia CCM. Kinapoteza wabunge, madiwani, na kadhalika.
Wenye chama, kwa mujibu wa kauli na matendo yao, wanaona eti hakuna tatizo. Mbunge akikihama na kwenda CCM, wenye chama wanakuja na majibu yaliyo 'formulaic'. Oh...kanunuliwa huyo...oh wamenunuliwa hao.
Kwa mtindo huu, hadi kufikia 2020, kama hicho chama hakitajitafakari na kufanya mabadiliko, basi kitaingia katika huo uchaguzi mkuu kikiwa dhoofu kushinda wakati mwingine wowote ule.
Kuhusu CUF, ACT, TLP, UDP, na wengineo, who really gives a damn about them? Vimefubaa.
Naisubiri kwa hamu Oktoba nione nani mwingine atayeitosa CHADEMA na kuhamia CCM.
Yours very truly,
Big Bad Wolf.
Wengi wetu tiliona jinsi chama hicho kilivyoendelea kustawi baada ya uchaguzi wa 2010. Kati ya 2010 hadi 2015 chama kilikua, kilistawi, hadi kikawa tishio la kweli dhidi ya CCM na kukifanya chama hicho tawala kulazimika kufanya mabadiliko na kimsingi kukiri kwamba ufisadi ni tatizo kubwa.
Sasa toka 2015 mpaka hivi sasa hiki chama ni kama kimechanganyikiwa kabisa. Hakijui hata kifanye nini. Kutwa kucha kinapoteza wanachama wake wanaohamia CCM. Kinapoteza wabunge, madiwani, na kadhalika.
Wenye chama, kwa mujibu wa kauli na matendo yao, wanaona eti hakuna tatizo. Mbunge akikihama na kwenda CCM, wenye chama wanakuja na majibu yaliyo 'formulaic'. Oh...kanunuliwa huyo...oh wamenunuliwa hao.
Kwa mtindo huu, hadi kufikia 2020, kama hicho chama hakitajitafakari na kufanya mabadiliko, basi kitaingia katika huo uchaguzi mkuu kikiwa dhoofu kushinda wakati mwingine wowote ule.
Kuhusu CUF, ACT, TLP, UDP, na wengineo, who really gives a damn about them? Vimefubaa.
Naisubiri kwa hamu Oktoba nione nani mwingine atayeitosa CHADEMA na kuhamia CCM.
Yours very truly,
Big Bad Wolf.
Mbowe, of course