CHADEMA imedumaa na wale wengine wamefubaa kabisa

CHADEMA imedumaa na wale wengine wamefubaa kabisa

Haya nenda kamuulize jiwe kwanini anawakubali hao wanao hama kutoka cdm na kuwapitisha bila kupingwa kwenye chama chake,huyo Mbowe naye ni binadamu kama wewe anahitaji kuishi maisha kama wewe yaani hata aibu huoni?
Mkuu whatever the case, tuache kuwasaidia viongozi wa Chadema na unnecessary excuses. Kinachoendelea kinaichafua Chadema na aina ya watu hasa viongozi walionao. Huwezi kupoteza wabunge kwa kasi namna hii tena kwa stupid reasons alafu tuache kujiuliza viongozi wamechukua hatua gani kuzuia ujinga kama huu.

Viongozi wa Chadema wanahitaji pressure kubadilika na bila nguvu yetu kwa pamoja kuwataka kuwajibika na kujenga upya uelekeo wa chama wataendelea kudeka kupitia utetezi wenu ambao daima unaishia kulaumu wanaohama tu.

Labda siku Mbowe mwenyewe atakaposema anaunga mkono juhudi ndio tutakuwa na mjadala wa maana.
 
Umevurugwa wewe na una macho lkn huoni na una masikio lkn husikii
Mkuu whatever the case, tuache kuwasaidia viongozi wa Chadema na unnecessary excuses. Kinachoendelea kinaichafua Chadema na aina ya watu hasa viongozi walionao. Huwezi kupoteza wabunge kwa kasi namna hii tena kwa stupid reasons alafu tuache kujiuliza viongozi wamechukua hatua gani kuzuia ujinga kama huu.

Viongozi wa Chadema wanahitaji pressure kubadilika na bila nguvu yetu kwa pamoja kuwataka kuwajibika na kujenga upya uelekeo wa chama wataendelea kudeka kupitia utetezi wenu ambao daima unaishia kulaumu wanaohama tu.

Labda siku Mbowe mwenyewe atakaposema anaunga mkono juhudi ndio tutakuwa na mjadala wa maana.
 
Mnajifanya hamnazo yanayoendelea hamyaoni.

Ata fisi alipenda sana mkono wa binadamu uanguke lakini ndiyo hivyo.

Chadema itaendelea kuwepo .
 
Ni mpuuzi tu asiyeona hujuma zinazofanywa na utawala wa CCM ili kuvidhoofisha vyama vya upinzani hapa nchini.
 
Hiki chama kikuu cha upinzani baada ya uchaguzi wa 2015, badala ya kuendelea kukua, sasa ni dhahiri kabisa kuwa hakifanyi hivyo bali kimedumaa, kinazidi kudumaa, na kimedhoofu sana.

Wengi wetu tiliona jinsi chama hicho kilivyoendelea kustawi baada ya uchaguzi wa 2010. Kati ya 2010 hadi 2015 chama kilikua, kilistawi, hadi kikawa tishio la kweli dhidi ya CCM na kukifanya chama hicho tawala kulazimika kufanya mabadiliko na kimsingi kukiri kwamba ufisadi ni tatizo kubwa.

Sasa toka 2015 mpaka hivi sasa hiki chama ni kama kimechanganyikiwa kabisa. Hakijui hata kifanye nini. Kutwa kucha kinapoteza wanachama wake wanaohamia CCM. Kinapoteza wabunge, madiwani, na kadhalika.

Wenye chama, kwa mujibu wa kauli na matendo yao, wanaona eti hakuna tatizo. Mbunge akikihama na kwenda CCM, wenye chama wanakuja na majibu yaliyo 'formulaic'. Oh...kanunuliwa huyo...oh wamenunuliwa hao.

Kwa mtindo huu, hadi kufikia 2020, kama hicho chama hakitajitafakari na kufanya mabadiliko, basi kitaingia katika huo uchaguzi mkuu kikiwa dhoofu kushinda wakati mwingine wowote ule.

Kuhusu CUF, ACT, TLP, UDP, na wengineo, who really gives a damn about them? Vimefubaa.

Naisubiri kwa hamu Oktoba nione nani mwingine atayeitosa CHADEMA na kuhamia CCM.

Yours very truly,

Big Bad Wolf.
hahahahaha! CHADEMA ya sasa imezidi kuimalika zaidi. mfano kwenye mkutano ya kampeni Monduri na Ukonga, tulishuhudia maelfu ya watu kuliko ilivyokuwa 2015
 
CCM imebaki kulazimisha kupendwa.wakati CDM inakimbiliwa na watu kwa mapenzi yao toka moyoni.
 
Ujinga ni kushindwa kuona na kutambua mazingira ya kisiasa ambayo wenye dola wmeyaweka/wamejiwekea ili kudhoofisha upinzani. Mikutano ya kisiasa wanafanya wao wakifanya wengine wanakamatwa,Live coverage ni kwa mtu mmoja tu hasa TBC wengine hata vyombo vya habari vinawaogopa sababu vyombo vyenyewe vimebanwa. Kuna mengi ya kihuni yanayoendelea ambayo kama huna akili utaona ni sawa.
Kinachonishangaza ni jinsi watu wanavyoshangilia uonevu, inaonyesha kuwa pamoja na miaka mingi kupita bado tunaweza kutobolewa miguu na tukafungwa minyororo kama enzi za utumwa.
 
Angekuwepo angenunulika,MTU masikini hawezi kuwa mwanasiasa mzuri.
Dr Slaa hana msimamo wowote ndio maana wale aliokuwa anawapinga akiwamo Magufuli kuwa atamfunga akiingia madarakani kwa ufisadi wa nyumba za serikali alioufanya akiwa waziri wa nyumba

Angekuwa ana msimamo wa kiuanaharakati asingeweza kwenda kuungana na wale wanaodhulumu haki za raia
 
Back
Top Bottom