CHADEMA ilipotosha umma taarifa ya Membe?

Jaribuni kutumia akili mlizopewa bure na mwenyezi Mungu. Siku mbili ama tatu kabla ya Membe kuema KUNA CHAMA FULANI kinafadhiliwa na nchi moja ya magharibi, Waziri mwenzake katika Baraza la Mawaziri na mwana CCM mwenzake alitamka wazi kuwa CHADEMA inafadhiliwa na nchi moja ya magharibi ili kuleta machafuko nchini. Kutumia akili uliyopewa na MUNGU ni pamoja na kujumlisha moja na moja ili kupata mbili badala ya kumi na moja! Mawaziri wawili wa Chama tawala wanatuambia kuwa kuna Chama kinafadhiliwa ili kuleta machafuko nchini, mmoja anataja wazi jina la Chama hicho na mwingine anadai kuwa taarifa imepelekwa kwenye vyombo vya usalama ili kupata udhibitisho wa taarifa hizo, akili yako inakuambiaje??? Umeishatafuniwa, basi hata kumeza tu mpaka umezewe??? Za mbayuwayu jumlisha na za kwako!

kweli akili ni nywele,ulichofanya ni zero transfer of knowledge! kama umesoma psychology utaelewa namaanisha nini?
 
hapa ni ushabiki zaidi ya hoja ya msingi...Kama mpokea habari ...Je Gazeti la Serikali linataka kufikisha ujumbe gani? Maana wanasema Chadema wamepotosha....swali wamepotosha nini na sahihisho lake ni lipi? Wanajamvi kumbukeni kuwa wakati wanatoa tamko huhusiana na kauli ya Mh. Membe walichambua vizuri kwa umakini na kujaribu kuinganisha na kauli ya waziri mwenzie kwa maana ya Mh. SS. Sasa kama kujibu wasema Sofia alikosea ili aunganishe na Chadema na wanahabari wengine ambao gazeti linasema watachukuliwa hatua baada ya uchunguzi wao kukamilika. Ni hayo tu kwa sasa.
 
Mnyika alisema kauli ya membe ina utata maana haijatajwa chama gani kinafadhiliwa. Kwa ilo jamaa,membe,anachanganyikiwa!

sasa kama hakutaja chama nyie mlitakaje? membe kama mwanadiplomasia aliyebobea hawezi kumention jina la chama publically na cdm hawana audacity ya kumfanya ataje jina la chama! wanausalama wanalifanyia kazi hilo na hatua zitchukuliwa! cdm walipasawa wapambane na bi sophia simba aliyewataja hadharani
 
Chadema wamezoea sana kuzidisha na kupotosha umma. hao hao walidanganya kuwa Mkuu wa Mkoa Shinyanga amefariki, na hao hao tena jana tu wamezua kuwa magufuri kajiuzulu. Na kesho watasema mengine.

hakika Chama hiki kimejaa wanafiki na waongo wakubwa sana katika kutaka kuleta balaa nchini.

Japo kuna uhuru wa kila raia kutoa maoni yake,, napata tabu pale watu wanapokuwa biased. Mwanajamvi mmoja alipata kunena kwamba "ushabiki wa kufumba macho na kusema ndio kwa kila kitu kinacho husu chadema" wa baadhi ya wana JF hapa ni utumwa mkubwa sana ambao inabidi kuuepuka! Huu unaoitwa "uanachama damu,chadema damu,ccm damu" ni utumwa wa ajabu maana una kuzuia hata kuuliza kitu pale unapo ona hakiendi vyema! Kama CDM walipotosha,, ieleweke hivyo na wakiri makosa badala ya kuendelea kung'ang'ania ubishi. Wengi tulihoji kwamba ni wapi Mh. Membe alipotaja CDM? Kuna vyama vingapi vya upinzani nchini? Mbona wengine hawakukurupuka kama CDM? Nadhani Mh. Membe anastahili kuombwa radhi na CDM.
 
umeona eeh? Sijui source yao ya habari huwa ni ipi? Slaa kipindi cha uchaguzi ashawahi kuzusha kuna contena lenye shahada za kupigia kura limekamatwa mahali,polisi kwenda wakakuta ni uzushi hakuna cha shahada wala nini! Hivi kwanini cdm wanamfeed kiongozi wao habari za uzushi? Hii inafanya watu kukosa imani nao
hapo kwenye blue CCM
 
Sikiliza vizuri kama una upofu wa masikio kauli ya Membe. Ametaja kuna chama kinafadhiliwa ........ lakini hakukitaja jina na mwisho alimalizia tumewaachia vyombo vya usalama kufuatilia hilo na kutoa taarifa kamili.

Kimsingi hakutaja jina na vile vyombo vya usalama vinalifanyia kazi na watatoa taarifa na hatua. Sasa Chadema Pupa za nini, Je hamjui kuwa mnajikanyaga wenyewe, kwanini mna react kama sio nyie.

Acheni ujinga huo, Tuache vyombo vya usalama vifanye kazi yake kiumakini na ufasaha.

Vipi Dr Magufuli kajiuzulu? uzushi mwingine huo.

Kwani CHADEMA walichisema ni nini? Wao walisema akitaje hicho chama na awataje hao wafadhili, basi! Shida hofu imewashika hasa baada ya Mama Simba kukurupuka na sasa mnatoa kauli zisizo na kichwa wala mkia. Umeita waandishi wa habari ukasema kuna chama kinafadhiliwa na balozi, basi watu watataka ufafanuzi na balozi zitataka ufafanuzi. Balozi zimeinuka juu na vile kabajeti ketu ni tembeza bakuli basi serikali imehaha. Semeni sasa!
 
Sikiliza vizuri kama una upofu wa masikio kauli ya Membe. Ametaja kuna chama kinafadhiliwa ........ lakini hakukitaja jina na mwisho alimalizia tumewaachia vyombo vya usalama kufuatilia hilo na kutoa taarifa kamili.

Kimsingi hakutaja jina na vile vyombo vya usalama vinalifanyia kazi na watatoa taarifa na hatua. Sasa Chadema Pupa za nini, Je hamjui kuwa mnajikanyaga wenyewe, kwanini mna react kama sio nyie.

Acheni ujinga huo, Tuache vyombo vya usalama vifanye kazi yake kiumakini na ufasaha.

Vipi Dr Magufuli kajiuzulu? uzushi mwingine huo.



Pole sana naona vichwa vyenu vinafangas.
 
unajua mkuu kuna msemo unaosema'ukirusha jiwe gizani atakayesema yalaaah ujue limempata" Membe hakutaja chama sasa kwnini cdm wakurupuke?? kwanini TLP,DP ama SAU wasilalamike? au wanajihisi nini? mwaka huu wataglue kweli

Viongozi wa CCM akiwamo Sophia Simba na Lipumba ndio walioitaja Chadema moja kwa moja na maswali ya waandishi yalilenga kwa Waziri Mhusika na Mambo ya Nje kutaka kujua kama ni sahihi kwa viongozi wa serikali kama Sophia Simba kuzungumzia mataifa ya nje kufadhili machafuko kupitia chama cha siasa alichokitaja, sasa Membe kwa kuwa aliyesema ni Waziri asingeweza kusema Waziri mwenzangu ni mwongo, bali alijibu kidiplomasia kwamba tutachunguza na ikithibitika tutatumia mikataba ya kimataifa kulishughulikia. Kwa upande wa Chadema kama chama cha siasa ambacho ndicho kunahusishwa na vurugu (rejea hotuba ya Rais) ndio wanaoamini (ni kweli) kwamba walengwa ni wao na hivyo kumtaka Waziri MWenye dhamana na mambo ya nje, ambaye ni Membe kutaja chama na nchi maana wanamuona Sophia Simba, kama mropokaji ambaye maneno yake hayawezi kubeba uzito unaostahili. Kwa mantiki hiyo, Membe hajakosea (Kwa maoni yangu) kwa kuwa yuko serikalini (Ambayo JK ni bosi wake na Sophia ni mwenzake) na Chadema nao hawajakosea maana ni chama cha siasa ambacho kimeonyesha kupambana hadi kuonekana kama chama cha fujo (kama ilivyokuwa CUF enzi zake).
 
sasa kama hakutaja chama nyie mlitakaje? membe kama mwanadiplomasia aliyebobea hawezi kumention jina la chama publically na cdm hawana audacity ya kumfanya ataje jina la chama! wanausalama wanalifanyia kazi hilo na hatua zitchukuliwa! cdm walipasawa wapambane na bi sophia simba aliyewataja hadharani

Hivi Sophia ni waziri wa serikali gani na Membe ni waziri wa serikali gani? Kauli ya waziri ni tamko la serikali. Ndio maana bungeni Spika husema serikali ni moja kwa hiyo waziri mmoja naweza kujibu au kusaidia kutoa jibu la wizara isiyo yake.
 
JAMANI SIONI TATIZO LA CHADEMA ila naomba majibu ya serikali kuhusiana na hoja za CDM kuhusiana na taarifa ya Membe kwenye vyombo vya Habari.

Kazi ya Serikali si kutetea viongozi waongo bali ni kubuni mikakati ya kutetea na kulinda maslahi ya Nchi na watu wake.
 
chama cha demokrasia na maendeleo pamoja na baadhi ya vyombo vya habari vinalaumiwa kupotosha taharifa ya waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa mh Benard Membe

Taharifa kamili
WIZARA ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, imesema baadhi ya vyombo vya habari pamoja na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), vilipotosha taarifa ya Wizara hiyo kuhusiana na chama kinachofadhiliwa ili kuleta machafuko nchini.

Imesema Waziri Bernard Membe hakutaja jina la chama wala nchi kinachofadhiliwa na nchi za Jumuiya ya Ulaya ili kuleta machafuko nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, John Haule amesema, Serikali itachukua hatua za kidiplomasia chini ya Mkataba wa Kimataifa wa Vienna kuhusu Mahusiano ya Kidiplomasia wa mwaka 1961, ikiwa itathibitisha nchi na chama hicho.

Haule amesema , Wizara imepokea taarifa za ujumbe wa simu za mkononi unaosambazwa kuwa baadhi ya nchi za Jumuiya ya Ulaya zinatuhumiwa kukifadhili chama cha siasa nchini ili kuleta machafuko na kwamba, raia wa nchi wanachama wa jumuiya hiyo wanakuwa na wasiwasi juu ya usalama wao.

“Tumepokea taarifa hizo na tumezipeleka kwenye vyombo vinavyohusika kwa uchunguzi na ikithibitika, Wizara itatoa taarifa,” amesema Haule leo.

Amesema, katika mkutano wa Waziri Membe alioufanya wiki iliyopita na waandishi wa habari, alijibu suala hilo bila kutaja jina la chama wala nchi inayofadhili, lakini Chadema kiliibuka na kumtaka Membe kuzitaja balozi hizo zinazofadhili chama hicho na kiasi cha fedha kinachotolewa



Kashanga,yatakushinda tu,kanyaga twende.
 
CCM kuwa waongo hakujustify CDM kupapatika na kudanganya!!!!

au unataka kusema uongo wa CDM una upako?

conclusion ya Membe ni kuwa vyombo vya usalama vinafuatilia na mwisho vitatoa majibu. kwa maoni yangu hakukuwa na haja ya CDM kulalama labda wangeishia tu kupambana na Sophy na kuacha habari ya Membe kuwa hawahusiki period

Wewe na Membe wote mna matatizo makubwa sana, Membe ni Decision Maker au hajui kazi yake? yaani CCM kila mtu hajui kazi aliyopewa sasa nchni mnaingoza vipi kwa nusu kibaba.

kitu chochote kinafika katika meza ya Decision Maker baada ya kufanyiwa uchambuzi na kuainisha chuya na Mchele ili Decision Maker afanye Decision sahihi, unataka kutwambia Membe ni mtoa Taarifa wa Vyombo vya Dola! unataka tuamini hivyo?! Kama unataka tuamini kuwa Membe siyo Decision Maker bali Mtoa taarifa kwa vyombo vya Dola je njia aliyotumia kuwapa taarifa vyombo vya Dola ndio njia sahihi kulingana na Upeo wako wewe na Membe?

Both are craps na nisingetegemea Kiongozi tena Waziri kutokujua majukumu yake kiasi hiki, angalia alafu twambie: -

  1. Kama Membe ni Waziri basi ni Decision Maker, maana yake jambo lolote linamfikia katika hatua ya mwisho kabisa ili kufanyike maamuzi kutoka na uchambuzi uliofanywa na wataalam wa Serikalini, kwa swala hili alipaswa kujitokeza kuongea baaada ya kupata taarifa sahihi kutoka katika vyombo vyote na hapo kama Decision Maker alikuwa anakuja kutoa maamuzi juu ya hili jambo na jinsi walivyolifanyia kazi na ushahidi uliopo na nini Serikali imeamu yaani Msimamo wa Serikali.
  2. Hili la pili unalotaka tuamini "Ashakum si Matusi" ni Upuuzi zaidi na inamdhalilisha zaidi; kuwa aliitisha waandishi wahabari kuwapa taarifa vyombo vya dola juu ya kuwepo kwa Chama kinachofadhiriwa ili kuvuruga amani ya nchni yetu, sasa vyombo vya dola upewa taarifa kwa njia ya "Press Conference?" inakuwaje waziri hajui njia sahihi ya kuwapa taarifa vyombo vya dola! huoni hajui lolote!
 
Viongozi wa CCM akiwamo Sophia Simba na Lipumba ndio walioitaja Chadema moja kwa moja na maswali ya waandishi yalilenga kwa Waziri Mhusika na Mambo ya Nje kutaka kujua kama ni sahihi kwa viongozi wa serikali kama Sophia Simba kuzungumzia mataifa ya nje kufadhili machafuko kupitia chama cha siasa alichokitaja, sasa Membe kwa kuwa aliyesema ni Waziri asingeweza kusema Waziri mwenzangu ni mwongo, bali alijibu kidiplomasia kwamba tutachunguza na ikithibitika tutatumia mikataba ya kimataifa kulishughulikia. Kwa upande wa Chadema kama chama cha siasa ambacho ndicho kunahusishwa na vurugu (rejea hotuba ya Rais) ndio wanaoamini (ni kweli) kwamba walengwa ni wao na hivyo kumtaka Waziri MWenye dhamana na mambo ya nje, ambaye ni Membe kutaja chama na nchi maana wanamuona Sophia Simba, kama mropokaji ambaye maneno yake hayawezi kubeba uzito unaostahili. Kwa mantiki hiyo, Membe hajakosea (Kwa maoni yangu) kwa kuwa yuko serikalini (Ambayo JK ni bosi wake na Sophia ni mwenzake) na Chadema nao hawajakosea maana ni chama cha siasa ambacho kimeonyesha kupambana hadi kuonekana kama chama cha fujo (kama ilivyokuwa CUF enzi zake).

Nadhani hapo penye wekundu panajieleza wazi. Mtu akisema tutachunguza,, ndiyo kataja CDM? Napata mashaka makubwa namna watu wanavyoweza kukurupuka tena viongozi kabisa.
 
watu wa Mungu tafadhalini sana tutumie lugha za staha katika kujenga hoja ili tusitoke kwenye mada kuu.
ukitumia matusi watu wataishia kukushusha thamani bure na kujaza tu posts kwenye hii thread.
hayo ya uzushi kuhusu kontena la kura,kifo cha RC shinyanga na la kusema Membe kawataja CDM watu wanajua ukweli ulivyo.
tusubiri uthibitisho wa wizara ili ukweli wa mambo ujulikane kwani ni mapema sana kwa yoyote kujihisi.
 
siamini kwanini hawa watawala wa ccm na wapambe wao humu wanashindwa kutumia common sense, wanatia aibu na kinyaa mno, ni upuuzi, utumbo kila kukicha, sikutegemea azomoke vile bila data then katibu wa wizara nae alambe matapishi ya membe, hawa watawala wamechoka juzi hapa tuliona kituko cha pinda juu ya magufuli ni utumbo juu ya utumbo, hivi kuna tofauti kati ya membe na sofia simba kinyazifa? Sasa huyo katibu analalama kitu gani? Membe hakutaja chama sofia alitaja hivi hii serikali wamekuwa wehu nini? Kimsingi wanatia kinyaa na kichefuchefu wanadhani watanzania ni wajinga wa kutupwa
 

  1. Kama Membe ni Waziri basi ni Decision Maker, maana yake jambo lolote linamfikia katika hatua ya mwisho kabisa ili kufanyike maamuzi kutoka na uchambuzi uliofanywa na wataalam wa Serikalini, kwa swala hili alipaswa kujitokeza kuongea baaada ya kupata taarifa sahihi kutoka katika vyombo vyote na hapo kama Decision Maker alikuwa anakuja kutoa maamuzi juu ya hili jambo na jinsi walivyolifanyia kazi na ushahidi uliopo na nini Serikali imeamu yaani Msimamo wa Serikali.

Wewe unaonekana una jazba,, tuliza moyo mkuu hapa ni hoja tu. Hapo penye rangi,, naona hukuelewa kwamba kilichompeleka Mh. Membe kwenye press conference haikuwa suala la CHADEMA. Hilo aliulizwa tu na mwandishi alipokuwa pale. Namnukuu Mnyika:
" Lakini jana (juzi) Waziri Membe aliulizwa kuhusu kuwapo kwa tuhuma za Balozi za Ulaya zinazowakilisha nchi zao hapa nchini kikifadhili chama kimoja cha siasa bila kukitaja, akajibu kuwa anafahamu suala hilo na vyombo vya usalama vinachunguza,"alisema Mnyika.

Sasa wewe kutuambia eti alipaswa kusubiri apate taarifa kutoka vyombo vyote kivipi? Ameulizwa swali la papo kwa papo na kama mwanadiplomasia aliyebobea,, akajibu vyema kwamba suala litachunguzwa bila kutaja chama chochote. Chadema wao wakawa wa kwanza kujitokeza na kupotosha umma kuhusu taarifa hii ya Membe.
 
Chadema wamezoea sana kuzidisha na kupotosha umma. hao hao walidanganya kuwa Mkuu wa Mkoa Shinyanga amefariki, na hao hao tena jana tu wamezua kuwa magufuri kajiuzulu. Na kesho watasema mengine.

hakika Chama hiki kimejaa wanafiki na waongo wakubwa sana katika kutaka kuleta balaa nchini.

writing in big font sizes does not justify your wrong statements
 
Back
Top Bottom