Watanzania habarini! nchi inapita katika kipindi kibaya kwa vile kuna baadhi ya wananchi wanatumia vibaya uhuru wa nchi na demokrasia. KILA siku wanataka shwari, wao amani ni kikwazo kwao kukaribia jumba la magogoni. Mwaka jana walichukua fomu na kujaribu kulifikia JUMBA la Magogoni, hata hivyo watanzania wakawaacha kwenye mataa kwa vile sera zao za PANGU PAKAVU zikakataliwa na watz.
Wakaona maamuzi ya wananchi ni mabaya hivyo;-
1. Wakasusia hafla ya kutangazwa matokeo ya URAIS
2. Wakasusia sherehe za kuapishwa Rais na TV wakazima
3. Wakawahi Dodoma kupokea posho za Ubunge
4. Wakasusia hotuba ya ufunguzi wa Bunge iliyofanywa na RAIS
5. Wakavunja umoja na vyama vingine vya upinzani BUNGENI
6. Wakavuruga zoezi la uchaguzi wa Meya wa Jiji la Arusha
7. Wakazindua zoezi la maandamano endelevu nchini ANGENDA KUU IKIWA NI UFISADI NA KATIBA MPYA.
8. Wakatangaza wataendeleza maandamanoi nchini pamoja na Serikali ya CCM imekubali kuwepo na mjadala wa KATIBA na KUPIGA VITA UFISADI NDANI YA CCM NA SERIKALI.
9. Wakadandia MISIBA ILIYOTOKEA NYAMONGO.
HIZO NI VIASHIRIA VICHACHE JUU YA UENDESHAJE WA CHAMA FULANI CHA SIASA AMBACHO KINATAKA KUISHI KATIKA JUMBA LA MAGOGONI PASIPO KUTUMIA SANDUKU LA DEMOKRASIA.
TAFADHALI WATZ TUENDESHE MAOMBI KWA CHAMA HIKI KISICHO NA MTAZAMO WA UTAIFA NA TANZANIA KWANZA ILI WAONDOKANE NA STYLE YS SIASA WANAYOITUMIA KWANI INA MADHARA MAKUBWA KWA WANANCHI.
SINA HAJA YA KUTAJA CHAMA HUSIKA KWA VILE WANA JF WOTE WANAKIJUA CHAMA KINACHOENDA NJE YA MSTARI NA KOTOJALI MAMLAKA YA DOLA ILIYOPEWA RIDHAA NA WANANCHI.