Amani iwe nanyi nyote.
Naomba niwakumbushe udugu wangu chadema, awamu ya nne mlipiga sana kelele kuwa kuna ufisadi, nchi haikuwa na Rais tunahitaji Rais Dikteta naomba niseme ukweli niliungana na CHADEMA, na katika uchaguzi niliisaidia kweli kweli kwa mapenzi ya kutoka moyoni
Mungu si Athumani tukaletewa jiwe, mwamba kweli kweli, ghafla tukashuhudia hakuna uhuru wa habari! utekaji kila kona, watumishi wakapauka na nataka niseme ukweli kura nilimpa Lissu na nilimpambania hadi kwa ndugu zangu.
Ila Mungu si mzee Hassan katikati ya giza katuletea mama, msikivu ndani ya miezi mitatu nyoyo zimetua, matumaini yamefufuka.
Mama msema kweli katwambia uchumi wetu umeyumba tupige kazi tuukuze, leo mnataka kuleta ngebe, ndani ya miezi mitatu mnataka katiba, hii ni sawa na kuoa mke kisha ndani ya mwezi unamdai mtoto hata mimba huchukua miezi 9 kuzaliwa.
Hayo mnayoyafanya ndo yalisababisha tuletewe jiwe, safari hii hatukubali, tutaenda taratibu na mama.
Naomba niwakumbushe udugu wangu chadema, awamu ya nne mlipiga sana kelele kuwa kuna ufisadi, nchi haikuwa na Rais tunahitaji Rais Dikteta naomba niseme ukweli niliungana na CHADEMA, na katika uchaguzi niliisaidia kweli kweli kwa mapenzi ya kutoka moyoni
Mungu si Athumani tukaletewa jiwe, mwamba kweli kweli, ghafla tukashuhudia hakuna uhuru wa habari! utekaji kila kona, watumishi wakapauka na nataka niseme ukweli kura nilimpa Lissu na nilimpambania hadi kwa ndugu zangu.
Ila Mungu si mzee Hassan katikati ya giza katuletea mama, msikivu ndani ya miezi mitatu nyoyo zimetua, matumaini yamefufuka.
Mama msema kweli katwambia uchumi wetu umeyumba tupige kazi tuukuze, leo mnataka kuleta ngebe, ndani ya miezi mitatu mnataka katiba, hii ni sawa na kuoa mke kisha ndani ya mwezi unamdai mtoto hata mimba huchukua miezi 9 kuzaliwa.
Hayo mnayoyafanya ndo yalisababisha tuletewe jiwe, safari hii hatukubali, tutaenda taratibu na mama.