masopakyindi
Platinum Member
- Jul 5, 2011
- 18,409
- 14,116
Mambo yameanza kunuka. Hata Yesu aligeukwa na baadhi ya wafuasi wake kwa matamanio ya kidunia. Yaani pamoja na ushahidi wote wa CHADEMA kupeleka magari, baadhi ya wabunge na kutoa michango ya kifedha kwa ODM, leo wanageuka? hatari. Na huo ufafanuzi mbona hawajatoa viongozi wa CDM kwenye vyombo vya habari? maana ninavyowafahamu kwa kupenda sifa wangeitisha press conference.
halafu, hayo madai si ya leo au jana. yalikuwepo hata kabla ya uchaguzi haujafanyika. leo mmeona maji yameanza kuwafika shingoni na ni siku moja tu kabla ya matokeo ya mwisho kutangazwa hapo tarehe 8.3.2013 asubuhi mnaanza kuwakana ODM na kusingizia kuwa CCM ndiyo wana ushirika na ODM. Hivi inaingia akilini?
halafu barua yenyewe ina utata;
- kama ulikuwa ni mwaliko wa kichama, ingepaswa uandikiwe uongozi wa chama cha mapinduzi. halafu kwa kawaida barua za organizations hazimlengi mtu. hivyo kwa kitendo cha kumuandikia mtu tena kwa kumtaja, Waziri wa Ujenzi, John Pombe Magufuli, bila shaka ni mpango ambao umeandaliwa na watu ambao upeo wao katika barua za kiofisi ni finyu na ninaamini kuwa hao ni viongozi wa CHADEMA ambao hawatumii hata chembe ya akili yao kufikiria.
- inawezekana vipi Mkutano ufanyike tarehe 7/12/2012 halafu barua ya mwaliko iandikwe tarehe 5/12/2012. kwa maoni ya haraka, barua hiyo kama ingekuwa ni ya kweli ingewafikia walengwa baada ya tukio. hata kama utatumia fax, lazima kuna taratibu za kiofisi mpaka barua kufikia mlengwa na kufanyiwa kazi kwa wakati.
-udhaifu mwingine wa barua hiyo ni kuwa maudhui ya barua yenyewe haieleweki.je ilikuwa ni kukialika chama cha mapinduzi kuimarisha nguvu za ODM au ilikuwa ni nini?
-halafu utata mwingine ni kitendo cha barua kukosa kumbukumbu namba. hata kwa watu waliosoma hadi darasa la saba tu bila shaka wana uelewa kuwa barua ya kiofisi tena ya chama ambacho kipo madarakani lazima iwe na Kumbukumbu Namba. kwa hiyo barua iliyotolewa inakosa hadhi na ndipo tunapoamini kuwa imeandaliwa na wafuasi wa CHADEMA ambao wengi wao uelewa wao ni mdogo katioka mambo ya kiofisi na huenda ni hawa waliopata alama 0 kwenye mitihani ya kidato cha nne au wale waliochora zombi na messi:amen:
kwa ujumla nimeona kichefuchefu baada ya kuiona hiyo barua na kitendo cha kujinasibisha kuwa imeandikwa na ODM
......
Mkuu mfa maji haachi kutapa tapa!