jogi
JF-Expert Member
- Sep 25, 2010
- 25,558
- 25,322
Kwa muda mrefu sana nimekuwa nikimchunguza huyu John Magale Shibuda nyendo zake na misimamo yake katika katika jamii. Nimegundua kuwa huyu bwana ni gamba damudamu tena lililo na mshipi hadi kiunoni! Nia kubwa ni kuviza harakati za CHADEMA katika ukombozi wa taifa maskini Tanzania!
Kwa kipindi kirefu tangu ajiunge na CHADEMA alijitahidi sana kuivuruga kwa misimamo ya kimagamba na alikuwa na intimate relation na CCM pamoja na wakuu wa magamba. Amejaribu kutikisa kiberiti amekuta kimejaa, amejaribu kupanda chuki za kifirauni ndani ya CHADEMA akashindwa na sasa ana mkakati wa siri na kagenge kadogo kutoka CDM na CCM wenye ya kuipunguza nguvu CHADEMA, bahati yake mbaya ame-prove failure!
My take;
CHADEMA pungezeni mawasiliano naye kabsa, ikiwezekana muwekeni kando kwakuwa hana nguvu ya kushindana nanyi pamoja jitihada zake zote!
ulikokatia kuni ndiko wenzio walikokati kamba!!!!