CHADEMA chama Mbadala kwa CCM

CHADEMA chama Mbadala kwa CCM

Ebeana umejibuuu! CHADEMA inabidi wawe wanasoma alama za nyakati mapema. Mbowe anauzika ila JK anauzika zaidi but all in all it is a matter of timimng
 
CCM walitumia Pengo la Katiba na Sheria nyingine mbovu za Nchi Kwa ajili ya kushinda uchaguzi 2005
 
Kama ndio hivi na mambo yao, CCM wanapoteza mwelekeo wake na kushirikiana na Hata tume ya uchaguzi kuhujumu wapinzani
 
CCM walitumia Pengo la Katiba na Sheria nyingine mbovu za Nchi Kwa ajili ya kushinda uchaguzi 2005

Hakuna cha pengo wala mjomba wake.. Unganeni, ondoeni tofauti zenu mtaishinda CCM hata wakileta mchawi toka Sumbawanga..hawawezi kuiba kura zote, watajaribu lakini Umati utawasuta.. wataiba ngapi jamani wakati hesabu ya watu waliojiandikisha inajulikana na wapiga kura watajua walichagua chama gani.. Sidhani kama CCM inaomba ya Zimbabwe, Kenya au Iran yatokee..
Jipangeni acheni tofauti zetu za kulilia ruzuku hamjengi kitu... Asiyetaka kujiunga atolewe akapange jiwe lake CCM..
 
CCM wanapoteza mwelekeo wake

Nilidhani haya yanajulikana tangu enzi za KOLIMBA? Labda useme kuwa haya ya sasa ni dalili za kuwa kamwe CCM haiwezi kujisahihisha na kujikwamua katika mwenendo huu wa kuporomoka pamoja na Tanzania yetu

Omarilyas
 
Hakuna cha pengo wala mjomba wake.. Unganeni, ondoeni tofauti zenu mtaishinda CCM hata wakileta mchawi toka Sumbawanga..hawawezi kuiba kura zote, watajaribu lakini Umati utawasuta.. wataiba ngapi jamani wakati hesabu ya watu waliojiandikisha inajulikana na wapiga kura watajua walichagua chama gani.. Sidhani kama CCM inaomba ya Zimbabwe, Kenya au Iran yatokee..
Jipangeni acheni tofauti zetu za kulilia ruzuku hamjengi kitu... Asiyetaka kujiunga atolewe akapange jiwe lake CCM..
Hakuna mtu yoyote asiyejua kuwa CCM wanatumia Rasilimali za Tanzania kwa ajili yao, yaani watu, Magari hata Fedha za Taifa, Tazama Kagoda na mengine jinsi yalivyoweza kufanikisha ushinda wa CCM mwaka 2005, nani asiyejua kuwa mambo ya ajabu hata mikakati ya Wanamtandao jinsi walivyopiga kampeni hata vyombo ya habari?? Je wapinzani walipewa fursa sawa katika vyombo vya habari Tanzania?? Je Tume huru ya Uchaguzi inawasikiliza Wapinzani?? Wewe Kaka yangu Mkandala unajua vizuri sana jinsi na sheria gani?? Kulikuwa na Sheria mbaya sana hata zile za Takrima?? Na Sheria za MWaka 1977 ya uchaguzi
 
Je ni wangapi watasema na kudai mabadiliko haya ya sasa kati sio sisi wote
 
Ni fedha zetu ndio zilizoanzisha CCM na pia kuna haja ya kurudisha mali zote wanaodhi CCM na kurudisha serikalini na kufanya uwanja uwe sawa na watu wote na vyama vyote
 
Ni fedha zetu ndio zilizoanzisha CCM na pia kuna haja ya kurudisha mali zote wanaodhi CCM na kurudisha serikalini na kufanya uwanja uwe sawa na watu wote na vyama vyote

Hata chadema wanatumia ruzuku kwa ajili ya helkopta ya mtu mmoja tu.
Chadema bado kuwa mbadala kina mapungufu mengi,mfano viti vya wabunge viti maalum Chadema hawana mfumo wa kuwatafuta zaidi ni jamaa wa karibu wa Chadema au watoto wa viongozi.pia hakuna mbunge wa kiti maalum hata mmoja toka ZNZ wakati CUF wana baraza la wanawake ambao wanawachagua wanawake wenzao,huko Chadema ni wanaume wanajiamulia kuweka watu wao.CCM wana jumuiya ya wanawake kuchagua.na wanashirikisha bara na visiwani. CHADEMA wanatoa mkoa mmoja na kabila moja.
 
Kwani CCM wapo vipi?? Mbona kuna Ndoa kibao kule Bungeni?? Mbona kuna watoto kibao wa vigogo, Sio sababu hiyo bwana mzee, the Tazama miundombinu ya Tanzania na tena utagemea nini?? Mbona SITTA ni SPIKA, MKEWE ni WAZIRI?? Mbona kuna ndoa kibao CCM??
 
Siasa ni kila siku hata kama CCM watakuja na mbinu nyingi sasa watu wanaanza kuelewa kabisa na pia itafika kipindi watu wataona ukweli, Ni kwamba Chadema wasiache kujenga watu wapya na sio masalio toka CCM na Kufanya kiwe makini na endelevu, You know Tatizo kubwa ni vyama vyetu vinabebwa na watu, Hata CCM kwa kiasi fulani walitumia mbinu ya Mafiga matatu na kuchagua Wabunge wengi toka CCM, Hivyo utaona haya Mwakani maana kati yao wanaweza wasirudi Bungeni, Hivyo nilikuwa nasema kuwa wengi katika vyama hivi hakuna Progressive plans na kufanya kiwe hai na sio mtu baada ya uchaguzi, Tazama hali ya uzalendo kati yao kaka yangu Mkandala, utaona na kujiuliza kuwa Chadema wanajitahidi kufanya hivyo. Kuna kila dalili za kufanya vizuri, then NCCR ya wakati ule ilikosa sustainable ya kuendelea kwasababu ni kwamba walikuwa wanafocus uchaguzi tu na vyama husika, Kuna haja ya kuwa na vyama kuwa tayari ya uchaguzi, Kwa kipindi chote hiki tuona na tumepima vyama vytu, tunawajua mamluki na hatimaye watapoteza au kufa natural Death kama vile vyama vingine, Lazima hata sio leo basi ni siku zizajo tuone au kupata vyama kama 2 vyenye nguvu Tanzania.

Usisahau kwamba huko nyuma tulikuwa na chama kimoja CCM! Kwa maana hiyo wapenda siasa wengi wako CCM na ndio hao ambao inabidi CHADEMA wafanye kazi ya ziada kuwafanya 'waokoke' na kuunga mkono CHADEMA na harakati zake.
 
Watu wanaogopa na Watu makini wanaogopa kuingia kwenye Siasa kwa ajili ya kuogopa Watu toka CCm, Siku inakuja na saa inakuja CCM utafika mwisho wao na wizi wa mali za umma, Kagoda, EPA, na Meremeta itakuwa mwisho wake. Mafisadi watakuwa mwisho wake
 
Watu wanaogopa na Watu makini wanaogopa kuingia kwenye Siasa kwa ajili ya kuogopa Watu toka CCm, Siku inakuja na saa inakuja CCM utafika mwisho wao na wizi wa mali za umma, Kagoda, EPA, na Meremeta itakuwa mwisho wake. Mafisadi watakuwa mwisho wake

Siyo kuogopa mkuu. Kuna watu hawapendi siasa. Ujue kwamba siasa ni interest kama interest zingine. Na kwa wale ambao wanapenda siasa CCM ndiyo imefanya kazi kubwa zaidi ya kuwa shawishi wajiunge na vyama vyao. Je recruiting system ya Chadema ikoje? Hatua gani wanazo chukua kuhakikisha wana nyakua vichwa vinavyo weza kusaidia chama chao? Au ni mpaka hao vichwa wenyewe waamue kuwafuata na kuomba wajiunge? Siasa na kama mchezo. Wachezaji nyota na chipukizi ndiyo wana paswa kutafutwa kwa udi na uvumba. Siyo kuchukua has beens wa vyama vingine au kuchukua watu ambao obviously hawata kisaidia chama kwa lolote.
 
Siyo kuogopa mkuu. Kuna watu hawapendi siasa. Ujue kwamba siasa ni interest kama interest zingine. Na kwa wale ambao wanapenda siasa CCM ndiyo imefanya kazi kubwa zaidi ya kuwa shawishi wajiunge na vyama vyao. Je recruiting system ya Chadema ikoje? Hatua gani wanazo chukua kuhakikisha wana nyakua vichwa vinavyo weza kusaidia chama chao? Au ni mpaka hao vichwa wenyewe waamue kuwafuata na kuomba wajiunge? Siasa na kama mchezo. Wachezaji nyota na chipukizi ndiyo wana paswa kutafutwa kwa udi na uvumba. Siyo kuchukua has beens wa vyama vingine au kuchukua watu ambao obviously hawata kisaidia chama kwa lolote.
Hapana Siasa zinawahusu maisha yao kila siku, Hali ngumu ni kwasababu ya wanasiasa wetu, Kila kitu kina connection za tabia hizi na kwasababu hiyo ndio maana CCM wanatumia mianya kama hii kubana demokrasia
 
Tunahitaji mabadiliko makubwa sana hasa Bungeni Dodoma Mwakani na tena Kiburi cha CCM kiweze kwisha na kwa kuwa hakuna sehemu ambapo CCM wanatumia kwa wingi wao kama ni bungeni!! Chagua CHADEMA
 
Tunaweza kuwashinda mafisadi kwa watu wenye moyo safi kujitokeza kugombea CHADEMA mwaka huu na mwakani
 
Kwani CCM wapo vipi?? Mbona kuna Ndoa kibao kule Bungeni?? Mbona kuna watoto kibao wa vigogo, Sio sababu hiyo bwana mzee, the Tazama miundombinu ya Tanzania na tena utagemea nini?? Mbona SITTA ni SPIKA, MKEWE ni WAZIRI?? Mbona kuna ndoa kibao CCM??

MAMA SITTA hakupitishwa na mume wake spika kuwa mbunge na waziri.alipitishwa kwenye vikao vya jumuiya halali ya chama.

mama ANNA KILANGO MALACELA alipitia mchakato mkali jimboni SAME MASHARIKI akiwa na wapinzani kama Daniel Yona na NANCY KABOYOKA na hatimaye mama MALECELA akawa mshindi akifuatiwa na Nancy na YONA kushika nafasi ya Tatu.kuna Marehemu Amina Chifupa alipigana kupitia jumuiya ya vijana na kuwa mtu wa pili hiyo ndio tiketi yake ya kuingia bungeni.
Vita KAWAWA kachukua fomu na kuingia jimboni kushindana na wengine.

Chadema hakuna chaguzi au ridhaa iliyofanywa na wanachama wa chadema kuwachagua wabunge wao kama Lucy owenyA,GRACE KIWELU,ANNA KOMU. hao walipewa nafasi hizo za viongozi wa Chadema kila mtu kataja mtu wake akawa mbunge hilo ni kosa na udhaifu mkubwa hakiwezi kuwa chama mbadala kwa kutokuwa na taratibu ndogo tu kama hii ya kuhakiksha equal policy inafanyiwa kazi na wanachama wa Chama.
 
Kuna kamati mbalimbali katika Chama za Ndani, Umeweza kupata habari za CCM baada ya kuandikwa kwenye vyombo vya habari, ukweli kuwa wao nao walipitishwa na kugombea nafasi hizo kutokana na watu wengine nao
 
Back
Top Bottom