Udhaifu upo vya vyote sio chadema tu. hata CCM tunawajua watu wengi tu wamepita kwa ruswa na sasa wengine ni mawaziri. Kinachotakiwa ni sisi wapiga kura mwakani tuamke na kuongeza idadi ya wabunge wa upinzani bungeni, CCM wanapata nguvu ya kupitisha mambo mengi ya kijinga bungeni kwa sababu wana wabunge wengi. Wakigundua wapo hatarini wanawaita wabunge wote wa CCM na kukaa kama kamati. Wajumbe mjue kura yenu ndio itakayo badilisha nchii kuwa na barabara nzuri, umeme,maji nk. hasa pale ambapo mikataba yote ya kifisadi itakapo badiliswa na pia mafisadi watapo acha uchafu wao. Nchii ni moja ya nchi tajiri sana kwa raslimali katika Afrika, lakini tusipo angalia maisha bora yatakua ndoto tu.Tafiti zimeonyesha kuwa nchi nyingi za Africa zenye raslimali ya asili ndizo zisizo na maendeleo ya kuridhisha(Resource rich are resource cursed countries). Mifano ni kama, DRC,Nigeria, Angora,Sudan,Liberia,Siera leone nk.,Sina hakika kama TZ tunaelekea huko au tutafika huko?,maana tafiti zinaonyesha madini yalichimbwa TZ ni 4% mpaka sasa. Nchi kama Botswana serikali ina hisa kwenye migodi ya Almasi na wakasaini mikataba ya 50,50%. Jiulize kinachotufanya sisi tusiwe na hisa kwenye migodi na kufanya tuwaachi wawekezaji tu nini?. Naishia hapo maana nina uchungu sana na serilkali hii ya CCM ilivyo fanya ubinafsishaji wa kifisadi na kuachi uchumi wote wageni na sisi kubakia washangiliaji tu, Kama kungekuwa na upinzani wenye nguvu bungeni wasingefanya hayo.