Hapana shaka kuwa inawezekana kabisa CCM wakatumia ile ya mwaka 2005 ya uchaguzi wa mazigaombwe maana hali halisi na wewe uliona na pia sitaki kuamini ndio sauti ya watu wengi wale kipindi cha kupiga kura waliipigia CCM, hapana kulikuwa na namna nyingine waliweza kufanya, Niambie na hao unasema kuwa hawajui mbona wabunge wengi wanatoka Vijijini na sio mijini kama wee unataka kujenga hoja yako
Mkuu tatizo la upinzani kila kitu wanakimbilia kusema wizi wa kura. Siku zote hawaangalii faults zao. Nitoe mifano.
CCM kwenye uchaguzi wa uraisi walishinda kwa about 80%. Upinzani wakagawana asilimia zilizo baki. Unataka kuniambia CCM waliiba kura kiasi gani mpaka kufikia 80%? Kama kweli CCM walishinda kwa dhuluma isinge tangazwa ushindi wa 80% kwa maana hiyo ingeonekana wizi wa dhahiri.
Hiyo ya wabunge kutoka vijijini au mjini inahusiana vipi mkuu?
1.Upinzani haifanyi kampeni majimbo yote na wala hawasimamishi wagombea katika kila majimbo. Hilo tayari limesha waweka katika disadvantage. CCM wana simamisha kila jimbo na just logic explanation will lead you to know that that would mean a better chance of getting more MP's.
2.Mkuu vyama vingi vya upinzani havija jikita vijijini vimejikita mijini. Asilimia kubwa ya Watanzania wanaishi in rural areas which means wangekuwa wana nguvu kijijini wangekua na idadi kubwa zaidi ya wabunge bungeni. Angalia Biharamulo walivyo shindwa. Na usikimbilie kusema CCM walicheza faulo kwa maana hata Chadema walitoa kauli za kama walivyoambia wanawake tutawapa chupi na sidiria.
3.Kama nilivyo sema post za nyuma kuwa kuna sehemu nyingi sana CCM inashinda on the basis of name recognition. Kila chama kina maeneo ambazo zina nguvu sana na maina mengi ya vijijini ni CCM ndiyo yenye nguvu. Unakuta watu wanaenda kupiga kura hawampigii mtu wanakipigia chama. Na kama nilivyosema kuna maeneo upinzani ni very weak au hawasimamishi kabisa mgombea.
4.CCM ina majority kwenye local governments. Which means unlike upinzani wao wanaweza kujipromote kwenye majimbo all year through. Wapinzani wengi ukiacha Chadema sasa kwa kuanzisha operesheni Sangala walikuwa wakifika vijijini wakati wa kampeni tu. Sasa watu wanashikilia local government wewe kuja tu wakati wa kampeni una muda gani wa kumake your case?
Tukubali au tukatae so far strategy za upinzani za kuattract voters hauja fanya kazi ipasavyo. Cha kwanza upinzani wanacho kimbiliaga kusema ni wizi wa kura. Yani wao wasipo shinda sehemu basi kuna wizi wa kura. Kama ni hivyo inakuaje baadhi ya majimbo wanashinda? Upinzani na supporters wake wanabidi wawe realistic sasa na waache kuwa fanatics wa kutetea chama tu na wajue they need a different approach. So far approach yao imefeli na bila hata facts and figures mtu unaliona hilo. What I'm saying is that upinzani wana hitaji short term goals na long term goals kukiondoa chama tawala.
WATU WAMESHINDWA KUSHIKA MAJORITY KWENYE LOCAL GOVERNMENTS, WAMESHINDWA KUCHUKUA MAJORITY BUNGENI SASA HUO URAISI WATASHINDAJE? WAANZE KWANZA KUCONCENTRATE CHINI NDIYO WAJE JUU NA HUO NDIYO USHAURI WANGU MKUBWA KWA UPINZANI.