CHADEMA chama Mbadala kwa CCM

CHADEMA chama Mbadala kwa CCM

MAAMKIZI YA AMANI KWAKO MKUU KABONDE.

Nashukuru kwa maoni yako mazuri, ila nashangaa kuona baadhi ya wana jamii waliojibu wanavyoshindwa kubaini hoja za kimantiki na kukimbilia udini.

Hoja niliyoitoa ni kwamba CHADEMA ni chama cha Kanisa, kwa maana ni Taasisi ya kisiasa ya KANISA. Haya wameyasema wakatoliki katika waraka wao rejea "Waraka wa kanisa katoliki Tanzania". Yawezekana Huna waraka huu.

Sasa hapa tutambue kuwa kumilikiwa na kanisa ni kitu kimoja, na udini ni kitu kingine. Mfano kuna hospitali nyingi hata za rufaa zinamilikiwa na kanisa, lakini watu wa dini zote hupata huduma kwa usawa bila ubaguzi.

Swali: Kwa hiyo mtu akisema Bugando ni hospitali ya Kanisa, ni udini???!, Bila shaka sio udini kwa sababu ni kweli hiyo ni Hospitali ya Kanisa.

Sasa waraka huo umebainisha madhumuni ya Taasisi hiyo ya kisiasa(CHADEMA) kwa KANISA. Ni udini na uchochezi wa hatari.

Kwa mantiki hiyo CHADEMA NIKATAMBUA SIO CHAMA MBADALA WA CCM KWA MASLAHI YA WATANZANIA NA TAIFA.
Inaonyesha jinsi gani huelewi hata huo waraka mwenyewe maana naona unasema tu maana hata kusoma hujawahi kabisa
 
CCM iko ngangari mkuu.
Kuing'oa lazima upinzani uache ubinafsi na kutafuta umoja wa wapinzani kwanza.
Mzee CCM siyo ngangari ila imejiimarisha kwa pesa nyingi wanazikwapua kutoka kwa wananchi. (kodi, VAT, kuuza mashirika, ardhi, migodi, na zile pesa za wahisani) wapo tayari hata kuua ili waendelee kuwa madarakani. lakini pia wanasaidiwa na ujinga wa Watanzania walio wengi kutojua haki zao. maana leo hii utamkuta mtu eti "Tunashukuru kwa Maisha bora kwa kila mtanzania huku hajui atakula nini, akienda Hospitali hapaiti dawa nyingine ila Mseto hata kama hana malaria, hawafahamu mabwanashamba na ni mkulima huku mbolea ikiwa imepanda kwa asilimia 500) kutoka 30,000- 150,000/-
jaribu kuona mipango ya kujiimarisha kukaa madarakani kwa kuuza kila kitu kwa wahindi, unadhani ndo ungangari huo.
Nadhani watanzania wakiamka tu basi kutawaka moto na utajua ccm siyo ngangari
 
Umeanza kwa kuonyesha kuwa CHADEMA ni chama cha Kidini, Sasa sema wewe mwenyewe kuwa nani mdini kati ya CHADEMA na vyama vingine, basi kama ndio hivyo CCM ndio Wadini?? Mbona uongozi wote wa juu ni waislam?? Acha kuongea masuala ya udini au CHADEMA ni chama cha kanisa wakati sio ukweli Mkuu, watu watakushangaa sana kuona unatoa tuhuma kama hizi wakati sio kweli

Mkuu Joshi, hayo maneno nimeyanukuu, sio yangu. Ni imani yangu kuwa kuna habari haijakufikia, nayo ni ile iitwayo Siri ya kiuchungaji" ambayo hubaki ndani ya Kanisa.
 
Mkuu Joshi, hayo maneno nimeyanukuu, sio yangu. Ni imani yangu kuwa kuna habari haijakufikia, nayo ni ile iitwayo Siri ya kiuchungaji" ambayo hubaki ndani ya Kanisa.
I Know it man, yaani tuache kuzungumza mambo ya udini katika vyama vya upinzania, yaani CCm wametumia hoja hiyo katika kuona kuwa CUF wanapoteza zao kwa hoja ya udini, lakini sio kweli, KWani kuna CUf ina watu wengi na wa dini mbalimbali, elewa kuwa kama wadini CCM ndio wadini wa kweli kweli
 
Nimesoma michango ya Mheshimiwa Josh Michael ktk thread hii, na nataka kumshukuru kwa analysis ya Chadema na maendeleo yake. Ni zaidi ya miaka 17 sasa tangu nilipokaa na wale Watanzania wazalendo tukaandika malengo na madhumuni ya chama hiki. Tangu mwanzo tuliamini kwamba ni lazima Chadema kiepuke kung'ang'ania viongozi wazee.

Kauli Mbiu zetu:-
VIJANA: TAIFA LA LEO!
WATOTO: TAIFA LA KESHO!
KINA MAMA :WALEZI!
WAZEE: DHAMANA.

Najisikia vizuri sana kwamba vijana wazalendo, jasiri, wabunifu, wengi wao wakiwa wasomi wenye huruma na umma wa Watanzania wanaotumbukia deeper and deeper katika lindi la umaskini kila kukicha kwa sababu ya ufisadi, wanaongoza CHADEMA sasa. Uongozi unaoona uchungu kwamba maliasili zetu zinaporwa na wageni wakishirikiana na chama cha mafisadi kupitia serikali yao.

Licha ya kwamba kuna wanaosita kwamba hatuwezi kuchukua dola mwakani, ni tumaini langu kwamba Watanzania wataonyesha kuchukia kwao ufisadi kwa kutuunga mkono ili tuikomboe Tanzania. Mafisadi kwetu iwe ni mwiko.

Nimewashauri vijana waendelee na "OPERESHENI SANGARA" kila mkoa, ili kusimika chama na kusambaza ujumbe kwamba vita dhidi ya ufisadi itaweza kufanikiwa tu pale kizazi kipya kitakapotwaa dola. Na katika vita hii, hata ongezeko la Wabunge wenye msimamo huo ni kuimarisha wapiganaji.

Hakuna Kulala Mpaka Kieleweke.
 
Last edited:
Asante sana Baba yangu Mtei na pia ni matumaini yetu kuwa CHADEMA itakuwa imara sana na watu wote kuwa imara
 
Nashukuru kwa maoni yako mazuri, ila nashangaa kuona baadhi ya wana jamii waliojibu wanavyoshindwa kubaini hoja za kimantiki na kukimbilia udini.

Hoja niliyoitoa ni kwamba CHADEMA ni chama cha Kanisa, kwa maana ni Taasisi ya kisiasa ya KANISA. Haya wameyasema wakatoliki katika waraka wao rejea "Waraka wa kanisa katoliki Tanzania". Yawezekana Huna waraka huu.

Sasa hapa tutambue kuwa kumilikiwa na kanisa ni kitu kimoja, na udini ni kitu kingine. Mfano kuna hospitali nyingi hata za rufaa zinamilikiwa na kanisa, lakini watu wa dini zote hupata huduma kwa usawa bila ubaguzi.

Swali: Kwa hiyo mtu akisema Bugando ni hospitali ya Kanisa, ni udini???!, Bila shaka sio udini kwa sababu ni kweli hiyo ni Hospitali ya Kanisa.

Sasa waraka huo umebainisha madhumuni ya Taasisi hiyo ya kisiasa(CHADEMA) kwa KANISA. Ni udini na uchochezi wa hatari.

Kwa mantiki hiyo CHADEMA NIKATAMBUA SIO CHAMA MBADALA WA CCM KWA MASLAHI YA WATANZANIA NA TAIFA.

Mkuu kipengele gani hicho cha Huo unaouita Waraka? Maana mimi nina Nyaraka Mbili za katoliki hapa Moja Inaitwa ILANI na nyingine inaitwa Mpango wa kuhamasisha Huduma za kichungaji katika jamii kuelekea Uchaguzi mkuu 2010 na sioni Mahali popote kanisa lilipojihusisha na CHADEMA
 
Licha ya kwamba kuna wanaosita kwamba hatuwezi kuchukua dola mwakani, ni tumaini letu kwamba Watanzania wataonyesha kuchukia kwao ufisadi kwa kutuunga mkono ili tuikomboe Tanzania. Mafisadi kwetu iwe ni mwiko.

Nimewashauri vijana waendelee na "OPERESHENI SANGARA" kila mkoa, ili kusimika chama na kusambaza ujumbe kwamba vita dhidi ya ufisadi itaweza kufanikiwa tu pale kizazi kipya kitakapotwaa dola. Hakuna Kulala Mpaka Kieleweke.

Mzee Mtei kwa heshima na taadhima naomba kutofautiana nawe hapa.

Moja, nina uhakika unajua kuwa kuongoza nchi iliyo bora sio suala la umaarufu wa mtu ama oppurtunity kama ilivyo sasa na huu mtaji wa chuki za wananchi dhidi ya ufisadi. Hivyo basi itakuwa ni hatari kama watanzania wataangalia umaarufu wa mtu ama chuki zao dhidi ya ufisadi tu kukabidhi utawala wa nchi yetu kwa wengine. Ili kuwa na Tanzania iliyo njema ni muhimu kwa waliojimilikisha jukumu la kujenga utawala mbadala kutilia maanani ya ujenzi wa asasi katika vyama vyao ili kuepuka kuwalazimu wananchi kuchagua MAFISADI MBADALA wa UFISADI WA CCM.

Kwa maoni yangu hivi sasa ni muhimu sana watanzania kuvunja ukiritima wa CCM ndani ya vyombo vya maamuzi kwa kuchagua wabunge wa upinzani kwa wingi zaidi na kutumia miaka mitano inayofuata kujenga chama/vyama mbadala ambavyo vitakuwa chachu ya misingi imara inayosaidiwa na miundombinu yote muhimu ya utambuzi, utengenezaji na utekelezaji wa sera maradufu na zenye tija na mfumo wa utawala wenye kung'amua, kupambana na kutokomeza UFISADI bila ya kutetereka.

Kuhusu mafisadi nashauri muwe makini msiendeleze utamaduni unaojengeka ndani ya CCM wa mafisadi mbadala kutumia vita ya ufisadi kujivua dhambi zao za ufisadi na kujijengea ngome za kisiasa.....

Watanzania wanadeserve more than huu ujanjaujanja unaoendelea....

omarilyas
 
Hakuna haja ya kuunganisha vyama, Watu wachague chama makini. na pia kuna haja ya kuona kuwa ni nani anafaa kutuongoza Watanzania?? CHADEMA wanaweza pia,

Huu ubinafsi wenu ndio unaowafanya watanzania walie halafu mwisho waamue kulichagua jinamizi walilolizoea......

Omarilyas
 
Nimesoma michango ya Mheshimiwa Josh Michael ktk thread hii, na nataka kumshukuru kwa analysis ya Chadema na maendeleo yake. Ni zaidi ya miaka 17 sasa tangu nilipokaa na wale Watanzania wazalendo tukaandika malengo na madhumuni ya chama hiki. Tangu mwanzo tuliamini kwamba ni lazima Chadema kiepuke kung'ang'ania viongozi wazee. Kauli Mbiu zetu:-
VIJANA: TAIFA LA LEO!
WATOTO: TAIFA LA KESHO!
KINA MAMA :WALEZI!
WAZEE: DHAMANA.

Najisikia vizuri sana kwamba vijana wazalendo, jasiri, wabunifu, wengi wao wakiwa wasomi wenye huruma na umma wa Watanzania wanaotumbukia deeper and deeper katika lindi la umaskini kila kukicha kwa sababu ya ufisadi, wanaongoza CHADEMA sasa. Uongozi unaoona uchungu kwamba maliasili zetu zinaporwa na wageni wakishirikiana na chama cha mafisadi kupitia serikali yao.

Licha ya kwamba kuna wanaosita kwamba hatuwezi kuchukua dola mwakani, ni tumaini langu kwamba Watanzania wataonyesha kuchukia kwao ufisadi kwa kutuunga mkono ili tuikomboe Tanzania. Mafisadi kwetu iwe ni mwiko.

Nimewashauri vijana waendelee na "OPERESHENI SANGARA" kila mkoa, ili kusimika chama na kusambaza ujumbe kwamba vita dhidi ya ufisadi itaweza kufanikiwa tu pale kizazi kipya kitakapotwaa dola. Na katika vita hii, hata ongezeko la Wabunge wenye msimamo huo ni kuimarisha wapiganaji. Hakuna Kulala Mpaka Kieleweke.

Mzee MIMI sikuelewi.Vijana Gani unawazungumzia?Zitto Kabwe ndio kijana umemtosa na KUMPA mkweo Mbowe bila haya wala aibu.

Kafulillah umemtosa.

mara usinginzie kuwa kuna pesa za Mafisadi kwenye uchaguzi wa Chadema ili upitishe watu wako.

kisheria hukupaswa kushiriki kwenye kikao ambacho una mgongano wa kimaslahi.yaani kikao cha KUMTOA ZITTO ili ampishe Mtoto wako Mbowe.

swali la ziada wabunge wa viti maalum wa Chadema walipitishwa na kikao gani? kwanini ni watu wenye mahusiano na Kilimanjaro tu?

naona ujibu haya kwanza then nitakupa maswali mengine baadae.
 
Mzee MIMI sikuelewi.Vijana Gani unawazungumzia?Zitto Kabwe ndio kijana umemtosa na KUMPA mkweo Mbowe bila haya wala aibu.

Kafulillah umemtosa.

mara usinginzie kuwa kuna pesa za Mafisadi kwenye uchaguzi wa Chadema ili upitishe watu wako.

kisheria hukupaswa kushiriki kwenye kikao ambacho una mgongano wa kimaslahi.yaani kikao cha KUMTOA ZITTO ili ampishe Mtoto wako Mbowe.

swali la ziada wabunge wa viti maalum wa Chadema walipitishwa na kikao gani? kwanini ni watu wenye mahusiano na Kilimanjaro tu?

naona ujibu haya kwanza then nitakupa maswali mengine baadae.

Mkuu the Way Mzee Mtei alivyoandika na wewe Ulivyojibu inaonesha Dhahiri jinsi upeo wako wa Kuchambua Mambo ulivyo below the Negative line! Kutokana na Majibu yako wewe unaonekana ni

1: Mgomvi
2: Mchonganishi
3: Una Wivu
4: Siyo Mstaarabu
5: Huna Heshima wala Adabu
6: Mara nyingi huwa unayaonea Aibu Mabandiko yako ukikaa na kuyatafakari baada ya kuyarusha

Na hii inawezekana una Kaubongo Kadogo sana
 
Mbona mnachekesha,kwani CCM kimekufa.acheni porojo kajiandikisheni kura za serikali ya mtaa.mageuzi yaanzie huko.
 
hapana alichosema ni kweli kabisa,sio siri.

Mkuu Ustaarabu ni Jambo la Muhimu sana Mkuu, unaweza kuwa una Pointi Nzuri sana lakini Presentation yako ikamfanya mtu unayetaka kurespond aku ground hata kama anaona kwamba you have point. Hivyo ndivyo alivyo Kanda2
 
Mkuu the Way Mzee Mtei alivyoandika na wewe Ulivyojibu inaonesha Dhahiri jinsi upeo wako wa Kuchambua Mambo ulivyo below the Negative line! Kutokana na Majibu yako wewe unaonekana ni

1: Mgomvi
2: Mchonganishi
3: Una Wivu
4: Siyo Mstaarabu
5: Huna Heshima wala Adabu
6: Mara nyingi huwa unayaonea Aibu Mabandiko yako ukikaa na kuyatafakari baada ya kuyarusha

Na hii inawezekana una Kaubongo Kadogo sana
sijakuuliza wewe nimemuuliza huyu Mzee na yupo on line hivi sasa.mwache ajibu hajakuomba umjibie.
ndio maana nimemuuliza kidogokidogo kutokana na uzee wake.ulitaka nimpe heshima gani zaidi ya hii?
 
Issue za Uchaguzi wa Chadema umeisha , Mtei ana amini kwamba kizazi kipya kina nafasi .Zitto alikubali kwa mmoja hata kama aliona si sahihi lakini ni mpiganaji akaamua kusema tuendelee . Zitto kaingia Chadema ana miaka 16 hadi sasa , lakini leo ni mwana Chadema , Mbunge wa Kigoma na Mbunge wa vijana wote . Nadhani tusikia Mtei anasema nini . Pili kama kuna chama kina mwelekeo na kisiwe CUF ama CCM na TLP Chadema unganeni kuleta weight japokuwa swala la kuungana lina utata mno maana wengie unawapa nafasi na kesho wanajitoa na unabakia kupoteza kata , ama jibu , ama mtaa .
 
Mkuu the Way Mzee Mtei alivyoandika na wewe Ulivyojibu inaonesha Dhahiri jinsi upeo wako wa Kuchambua Mambo ulivyo below the Negative line! Kutokana na Majibu yako wewe unaonekana ni

1: Mgomvi
2: Mchonganishi
3: Una Wivu
4: Siyo Mstaarabu
5: Huna Heshima wala Adabu
6: Mara nyingi huwa unayaonea Aibu Mabandiko yako ukikaa na kuyatafakari baada ya kuyarusha

Na hii inawezekana una Kaubongo Kadogo sana

Loo hasira za nini? Hili ni jukwaa la siasa. Halina mkubwa wala mdogo. Hapa ukubwa na udogo ni wa hoja sio umri. Kijana anataka majibu basi apewe.
 
Back
Top Bottom