CHADEMA chama cha kidalali na wapiga dili asema Dr. Slaa

CHADEMA chama cha kidalali na wapiga dili asema Dr. Slaa

Status
Not open for further replies.
Hashima yangu kwa Dr.Slaa haiwezi kufutwa kwa namna yoyote ile!
 
Katika hali isiyokuwa ya kawaida aliyekuwa katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dr. Wilbroad Peter Slaa amezionesha stakabadhi za malipo ambayo Lowassa aliyafanya ili kujiunga na chama hicho, Dr. Slaa amesema kuwa amefikia hatua hiyo ili kuwaonesha Watanzania kile kilichomfanya yeye kuondoka CHADEMA. Ameendelea kusema kuwa pia amesukumwa kufanya hivyo ili kuwaonesha wana CHADEMA waliokuwa wanambeza na kusema kanunuliwa ili mara nyingine wasirudie kusema mambo wasiokuwa na uhakika nayo.

Akiongea mbele ya vyombo vitatu vya habari akiwa mjini Austin, TX nchini Marekani ambako anachukua kozi fupi ya Sheria ili kujikumbusha vitu vilivyobadilika kwenye fani hiyo ambayo anatarajia kuanza kuifanyia kazi kuanzia Januari mwakani.

Nyaraka hizo za siri za CHADEMA zimezua gumzo kubwa nchini humo na watu wengi waliopata kuziona wameibeza sana CHADEMA na kuifananisha na chama cha Kidalali, chama cha wapiga pesa alisema Injinia Musa Kipao mkazi wa Tabata jijini Dar.
Sasa wewe unajitofautishaje na huyo doctor uliemtaja kabla hatujawapuuza wote kwa pamoja.
 
ukiona chama kizee kinatumia ukabila ujue kimekufa na watu wake wana akili za wafu
 
Alikuwa wapi kuzitoa muda wote mpaka asubiri leo hii ndio azitoe. Kama chadema kilikuwa ni chama cha kupiga dili, na yeye mwenyewe amekuwa kiongozi kwenye chama hicho kwa muda wote huo, inamaanisha hata na yeye alikuwa anapiga dili. Kama sivyo angeshajiondokea miaka mingi iliyopita.
 
Bora aendelee kusoma maana naona limebaki jina tuu dr ila uwezo kichwani unapungua kila siku zinavyozidi kwenda..
 
Yaani MTU anayetawaliwa na mke anaweza kuwa na uwezo wa kuongea la maana?
 
Weka documents mezani tofauti na hapo CCM mmepanic baada ya kuambulia 25% ya kura za urais.
Huyo dr bado hapo marekani bado anaishi kwenye apartment ya mzee mwanakijiji?
 
Siasa ya leo imewafagia watu sasa wanatafuta kick ivi kuna mafisadi wangapi wameiba hela na alitakiwa atoe ushahidi kama yuko fair mfano hazina hamna hela alitakiwa atuambie nani ametufanya masikini sio kubeza chadema atusaidii ila minamwona kama hana tofauti na hao mafisadi
 
Hayo aliyoongea angekuja ayasemee huku nyumbani Tz ndio tungejua ukweli, issue za chama cha Tz ww unaenda kuongelea USA:what:

I don't see any problem. Are there boundaries that demarcate where one can comment about politics in Tanzania? That you have to be in Tanzania only for your point to be valid! Preposterous!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom