CHADEMA, anzisheni TV/Radio Station!

CHADEMA, anzisheni TV/Radio Station!

Binafsi nimeshangaa pia! Kwa mshahara huu utaweza kuajiri na kuretain mtangazaji au DJ mahiri? Au ndo rate yao hapa mjini?

Kwa taarifa yako pale Clouds pamoja na mbwembwe zote kuna watu hawana mshahara kabisa.......ni sehemu ya mauzo kwa ajili ya kupatika dili zingine kama Mabwana, Majimama, na u-DC(mf.Kibonde)
 
Je radio yako ukitaka isikike nchi nzima?????

Ni very easy; ni suala la kuanzisha kituo kila baada ya km 150 (KAS/MASH/KUS/MAGH). Tanzania ina kama km za mraba 945,000. Kwa maana hiyo vitatakiwa kuanzishwa vituo 945,000/150 = 6,300!

Hapo ukizidisha na hiyo gharama (ya chini) anayo-propose mleta mada, jumla unapata kama 504,000,000,000 (bilioni 504) tu. Nadhani iko ndani ya uwezo.
 
Kwa taarifa yako pale Clouds pamoja na mbwembwe zote kuna watu hawana mshahara kabisa.......ni sehemu ya mauzo kwa ajili ya kupatika dili zingine kama Mabwana, Majimama, na u-DC(mf.Kibonde)


CHADEMA haina haja ya kuanzisha kituo cha redio maana redio zote za bwana asifiwe zinazisapoti CHADEMA, kuanzia redio tumaini, upendo, maria, wapo nk
 
Wakifungua redio hawa watasababisha mambo ya rwanda maana kama sasahivi tu wameanza ugaidi je wakipata redio
 
inaonekana bado una hangover ya jana
kanywe supu ndugu acha kujidhalilisha
Tnagu lini ukasikia hizi radio zikishabikia siasa??
CHADEMA haina haja ya kuanzisha kituo cha redio maana redio zote za bwana asifiwe zinazisapoti CHADEMA, kuanzia redio tumaini, upendo, maria, wapo nk
 
CHADEMA haina haja ya kuanzisha kituo cha redio maana redio zote za bwana asifiwe zinazisapoti CHADEMA, kuanzia redio tumaini, upendo, maria, wapo nk
......akili iliyooza/kufa ni mbolea ya umaskini.......................
 
Wakifungua redio hawa watasababisha mambo ya rwanda maana kama sasahivi tu wameanza ugaidi je wakipata redio

Ganja banah....hivi mkuu unatumiaga nini kufikiri
Una hangover bado au moshi wa marijuana umekujaa kichwani???
 
Mhe Mwenyekiti ameanzisha radio yake huko Marangu,sasa sijajua kwa nini amevutia kwake kwanza kabla maslahi ya Chama!hapo naomba mwongozo
 
Kupiga domo ni kazi rahisi sana kuliko kutenda, Chadema inaishia kilometer 150? tupe hesabu ya coverage ya nchi nzima.

Good idea. Radio inayoshika km 150 wanaweza kuanzisha CUF au CHAUSTA. Lkn CHADEMA inahitaji radio itakayokua na uwezo wa kufanya National Coverage.
 
hili jambo la radio tumeshalijadili sana hapa na hadi JOHN MNYIKA akatoa maelezo ya uongo na kweli ila hadi leo zimebaki ni ahadi kama zile za ccm na maisha bora
sent by nokia 3310
 
Kwa hapa Bongo!, piga ua garagaza ni vigumu sana kwa TCRA kutoa leseni kwa radio ya CHAMA (siasa). Panahitaji kazi ya ziada na tuseme ni kama haiwezekani. Je, tunaweza hata kuangalia nchi zingine, ni chama kipi kinamiliki vyombo vya habari kama radio direct?

Kwa siku hizi hata TCRA wakigundua tu unaanzisha radio yenye interest na siasa, au wewe ni mwana siasa, kazi sana kupata leseni.
 
Ni very easy; ni suala la kuanzisha kituo kila baada ya km 150 (KAS/MASH/KUS/MAGH). Tanzania ina kama km za mraba 945,000. Kwa maana hiyo vitatakiwa kuanzishwa vituo 945,000/150 = 6,300!

Hapo ukizidisha na hiyo gharama (ya chini) anayo-propose mleta mada, jumla unapata kama 504,000,000,000 (bilioni 504) tu. Nadhani iko ndani ya uwezo.

Unacheza wewe bilioni 504 wakati ofisi tu mmepanga vyumba vinne.
 
Kwa hapa Bongo!, piga ua garagaza ni vigumu sana kwa TCRA kutoa leseni kwa radio ya CHAMA (siasa). Panahitaji kazi ya ziada na tuseme ni kama haiwezekani. Je, tunaweza hata kuangalia nchi zingine, ni chama kipi kinamiliki vyombo vya habari kama radio direct?

Kwa siku hizi hata TCRA wakigundua tu unaanzisha radio yenye interest na siasa, au wewe ni mwana siasa, kazi sana kupata leseni.

sidhani kama chadema wanaulazima wa kuanzisha kituo cha radio,itakuwa ni matumizi mabaya tu ya rasilimali,zilizopo zinatosha kabisa labda kama nanyi mmevimbewa kama mlivyofanya huko bungeni muanzishe tv ya bunge wakati tbc zipo mbili zote zinaendeshwa kwa kodi ya masikini,kama si kuwachezea watz ndiyo nini hiki au kwa vile wamezoea kuambiwa watz wakarimu vichwa vinajaa maji wakati rasilimali zinasombwa! zinahamishwa
 
Kupiga domo ni kazi rahisi sana kuliko kutenda, Chadema inaishia kilometer 150? tupe hesabu ya coverage ya nchi nzima.
Nadhan hakuna redio ya FM hapa nchini inayocover eneo lote la nchi hii kilomita za mraba 945 isipokuwa redio yenye coverage kubwa kuliko zote (RFA) imesimika mitambo yake kila makao makuu ya mikoa yote ta Tanzania bara (mikoa 25) hivyo unaweza kuzdisha mara 25 unapata jawabu lililokaribu na ukweli na izingatwe kuwa gharama za studio haziwezi kuwa kila mkoa maana unaweza kuwa na studio moja tu au mbili na mobile kwa ajili ya matukio ya live. Pia mleta maada amesahau kuwa pia kama unataka kuwa na redio inayorusha matangazo muda wote ni lazma uwe na power backup hasa kwa ajli ya stesheni mama na studio yake. hivyo generator ya 10kVA kwa master redio na 20kVA kwa studio maana studio itakuwa na viyoyozi na mitambo mingine isiyotaka hata skunde moja isiyo na umeme hivyo umuhimu wa UPS pia ni mkubwa sana! Lakini all in all UMUHIMU WA CHADEMA KUWA NA REDIO NI MKUBWA MNO KULIKO KITU CHOCHOTE. Nadhani viongozi wamelemaa na redio za makada wa CCM ambao utakapofika wakati wa kampeni wakaamliwa na chama(CCM) kuwa wasitangaze habari zozte za CHADEMA ndipo viongozi wangu watakapogundua umuhimu wa kuwa na kituo cha redio na tayari watakuwa wamechelewa! Nawashauri wafikirie nje ya box maana kuna watu walishawahi kuahidi kutoa seti ya kituo kimoja cha kuanzia (Friends of CHADEMA USA) lakini ahadi haikufuatiliwa. Tusubiri mzee wa richmonduli anayejua kutumia media apewe rungu muone wenye vituo watakavyopewa amri za vitisho vya kufungiwa ilimradi tu wamtangaze yeye na marufuku kwa wengine na hasa CHADEMA. Tuwe na uwezo wa kuiona kesho mapema kabla matendo ya kesho hayajatuathiri. Mtoa hoja ana hoja na tusiihujumu kwa ushabiki bali tuongezee kwenye mapungufu ili tuiboreshe na hatimaye viongozi wetu wakaona umuhimu unaoonekana kwa kila anayejua mwenendo wa siasa za nchi yetu
 
Ni very easy; ni suala la kuanzisha kituo kila baada ya km 150 (KAS/MASH/KUS/MAGH). Tanzania ina kama km za mraba 945,000. Kwa maana hiyo vitatakiwa kuanzishwa vituo 945,000/150 = 6,300!

Hapo ukizidisha na hiyo gharama (ya chini) anayo-propose mleta mada, jumla unapata kama 504,000,000,000 (bilioni 504) tu. Nadhani iko ndani ya uwezo.
dudus
Si kweli, ukitaka kuwa na coverege ya nchi nzima unachotakiwa kufanya ni kuomba leseni almost kila mkoa, au kwa mikoa miwili au mitatu inategemeana na wingi wa radio station kila mkoa.

Baada ya hapo unahitaji booster station. (Ina transmitter, receiver na antena zake let say na mnara) So hapa bei yake inaweza kuwa kama Transmitter ya 2 KW inakaribia milion 19, na set zake za STL zinaweza fika up to 10milion, na mnara ni kama 5Milion, ada ya TCRA milion 2. Jumla ni kama 37milion kila booster mara mikoa hata 15 hivi. Hizi bei nimekadiria tu nipo kitandani ustake serious sana inaweza kupungua sana zaidi ya hapo.
 
Last edited by a moderator:
Kwa hapa Bongo!, piga ua garagaza ni vigumu sana kwa TCRA kutoa leseni kwa radio ya CHAMA (siasa). Panahitaji kazi ya ziada na tuseme ni kama haiwezekani. Je, tunaweza hata kuangalia nchi zingine, ni chama kipi kinamiliki vyombo vya habari kama radio direct?

Kwa siku hizi hata TCRA wakigundua tu unaanzisha radio yenye interest na siasa, au wewe ni mwana siasa, kazi sana kupata leseni.
Hata CCM haina redio isipokuwa makada wa ccm ndio wamiliki kisheria wa redio uhuru kwa ufadhiri wa CCM lakini kila mwenye akili timamu anajua uhuru redio ni ya ccm. Hivyo kisheria vyama vya siasa haviruhuswi kumiliki redio lakini vinweza kumiliki kupitia makada wake. Jamani hata RPF waliingia Rwanda kwa propaganda za redio yao hata waasi wa seleka wamepindua CAR wakiwa na redio hata kama usjiri unakuwa wa watu binafsi
 
Mshahara 250, 000/=??????

Mkuu,
Mimi nimetoa hiyo price kwa lengo la local radio ya wilayani au mkoani kwa wafanyakazi wenye certificate ambao pia hulipwa commission kutokana na ukusanyaji wa matangazo. Mfano:-

Analipwa Tshs 250,000/= kwa mwezi.
Analipwa 30% commission kwa kila tangazo.
Kwa mwezi analeta matangazo yenye thamani ya Tshs 1,000,000/= 30% yake itakuwa kama laki 3.

hivyo jumla kwa mwezi ni kama ana Tshs 550,000/= Hata mwalimu wa serikali mwenye degree sidhani kama anafika hapa au kuzidi sana hapa.

 
Back
Top Bottom