CCM yatamba kuzoa majimbo, kata 2015

CCM yatamba kuzoa majimbo, kata 2015

Informer

Platinum Member
Joined
Jul 29, 2006
Posts
1,629
Reaction score
6,812
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kimejipanga kuhakikisha wanarejesha majimbo yote kiliyoyapoteza katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015 kwa kuwa kimeshabaini sababu za kupoteza majimbo na kata katika uchaguzi uliopita.

Hayo yalibainishwa juzi na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Bara, Mwigulu Nchemba, wakati akizungumza kwenye kikao maalumu cha Halmashauri Kuu ya CCM wilaya ya Ilemela, jijini hapa.

“Tumeshagundua sababu za kupoteza baadhi ya maeneo ni ugomvi tu baina yetu. Sasa tumekuja na kaulimbiu mpya ya ‘Umoja ni Ushindi’, anayesubiri CCM ishindwe atazeeka sana bila kuona hivyo,” alisema.

Kwa kuwa kikao hicho kiliwashirikisha watendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Ilemela, Mwigulu alisema wapo watu wanaoacha kuitumikia Serikali iliyopo madarakani wakidhani kuwa kuna Serikali nyingine itaingia madarakani hivi karibuni.

Aliwataka viongozi wa CCM wasisite kuchukua hatua na kukemea kwa kile wanachotaka kitekelezwe na watendaji kwa mujibu wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi.

“Waliopo Serikalini wanatekeleza mkataba wa Serikali inayoongoza nchi, tukifuata hilo Tanzania tutapiga hatua na tunapoisimamia Serikali hatupaswi kulaumiwa na mtu, kwani tunaisimamia ilani ya CCM itekelezwe,” alisema Naibu Katibu Mkuu huyo wa CCM.

Nchemba alisema kinachoigharimu Tanzania ni baada ya uchaguzi kumalizika, halafu watu kuanza uchaguzi mwingine badala ya kuchapa kazi ya kuwatumikia wananchi.

“Uchaguzi ukiisha tujenge kasumba ya kuacha kampeni na maandamano ya kila siku na kuingia kazini kuwatumikia wananchi, si mmeona wenyewe baada ya uchaguzi wa Marekani kumalizika watu wanafanya kazi na sio kuzungumzia uchaguzi tena,” alisema.

“Haiwezekani siku zote ziwe za kampeni. Tutafanya lini kazi, siku zote kuwa za kampeni zinawafanya watumishi wa serikali kushindwa kugawa muda wa kuwatumikia wananchi?” Alihoji.


Katika kikao hicho maalumu, Nchemba aliwagawia wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM wilaya makabrasha ya maazimio ya Mkutano Mkuu wa Nane wa Taifa na Hotuba ya Mwenyekiti wa CCM Taifa, Jakaya Kikwete, kama vitendea kazi vyao.

Chanzo: HabariLeo | Imeandikwa na Grace Chilongola, Mwanza | Jumapili, 23 Desemba 2012
 
Huyu Mwigulu ana hali mbaya sana jimboni kwake. Sasa sijui watayazoa majimbo gani ikiwa la kwake tu amelishindwa!?
 
Inawezekana akawa na hali mbaya jimboni kwake lakini jamaa ni kichwa
 
Lazima watambe kwa kuwa TUME ya UCHAGUZI ni yao na wanafanya makusudi kutotuletea KATIBA itakayosimamia haki ya TAIFA hili. (Sikustushwa na source ya habari hii pia)
 
Inawezekana akawa na hali mbaya jimboni kwake lakini jamaa ni kichwa

daa mwigulu kichwaa??? Acha kumkashifu migulu wewe? Kichwa cha nini kobe au chura make ule weupe alionao kichwani sio wa kawaida
 
Sio Mara ya Kwanza hawa Jamaa kujipa Matumaini, Kabla ya Uchaguzi wa 2010 walitamba kurudisha majimbo yote ila ilikuja kuwa tofauti,

CCM hawazungumzii kuondoa kero za wanananchi kabla ya 2015, wao wanazungumzia kurudisha majimbo,
 
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kimejipanga kuhakikisha wanarejesha majimbo yote kiliyoyapoteza katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015 kwa kuwa kimeshabaini sababu za kupoteza majimbo na kata katika uchaguzi uliopita.

Hayo yalibainishwa juzi na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Bara, Mwigulu Nchemba, wakati akizungumza kwenye kikao maalumu cha Halmashauri Kuu ya CCM wilaya ya Ilemela, jijini hapa.

“Tumeshagundua sababu za kupoteza baadhi ya maeneo ni ugomvi tu baina yetu. Sasa tumekuja na kaulimbiu mpya ya ‘Umoja ni Ushindi’, anayesubiri CCM ishindwe atazeeka sana bila kuona hivyo,” alisema.

Chanzo: HabariLeo | Imeandikwa na Grace Chilongola, Mwanza | Jumapili, 23 Desemba 2012

Kuota ndoto si kupata. Asubiri muziki mnene 2015, wakitumia wakuu wa mikoa, wilaya, wakurugenzi, polisi, usalama wa taifa na tume ya uchaguzi patanuka!. Wao wanatafuta kukomboa majimbo si kuwaondoa watanzania ktk lindi la umeskini!
 
Hata mkisema vipi. Mwigulu ni kichwa sana na ni mwiba mkali sana unaochoma upinzani hasa CDM. Mwigulu amejitahidi kujibu hoja za wapinzani kwa umakini mkubwa sana. Nampongeza Mwigulu na kumhakikishia kuwa sisi vijana tuko pamoja naye.
 
Mwigulu, Marekani hawachakachui uchaguzi watu wanapata viongozi wanao wafaa na walio wachagua hivyo huridhika na kuendelea kuchapa kazi, kumbuka wakati wa Bush na Al Gore kule Florida? Kulijitokeza dalili za uchakachuaji malumbano yaliendelea hadi haki ilipopatikana mahakamani. Acheni kujificha kwenye kivuli cha uzalendo baada ya kutenda maovu, hapo ulipo moyoni unajua kabisa kuwa serkali yako mwaka 2010 iliingia madarakani kwa dhuluma za uchakachuaji halafu bila aibu unataka watu wasahau wachape kazi chini ya serkali isiyo chaguo lao!!
 
Sijawahi kuona kiongoz mbovu kama mwigulu ktk nchi hii, he iz just a ****
 
Watarudisha kama alivyorudisha la arumeru yeye na lusinde.
 
[FONT=courier
new]CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kimejipanga kuhakikisha
wanarejesha majimbo yote kiliyoyapoteza katika uchaguzi mkuu ujao wa
mwaka 2015 kwa kuwa kimeshabaini sababu za kupoteza majimbo na kata
katika uchaguzi uliopita.
[/FONT]

Hayo yalibainishwa juzi na Naibu Katibu Mkuu
wa CCM Tanzania Bara, Mwigulu Nchemba, wakati akizungumza kwenye kikao
maalumu cha Halmashauri Kuu ya CCM wilaya ya Ilemela, jijini
hapa.


“Tumeshagundua sababu za kupoteza baadhi ya
maeneo ni ugomvi tu baina yetu. Sasa tumekuja na kaulimbiu mpya ya
‘Umoja ni Ushindi’, anayesubiri CCM ishindwe atazeeka sana bila kuona
hivyo,” alisema.


Kwa kuwa kikao hicho kiliwashirikisha
watendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Ilemela, Mwigulu alisema wapo watu
wanaoacha kuitumikia Serikali iliyopo madarakani wakidhani kuwa kuna
Serikali nyingine itaingia madarakani hivi karibuni.


Aliwataka viongozi wa CCM wasisite kuchukua
hatua na kukemea kwa kile wanachotaka kitekelezwe na watendaji kwa
mujibu wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi.
[FONT=courier
new]
[/FONT]
“Waliopo Serikalini wanatekeleza mkataba wa
Serikali inayoongoza nchi, tukifuata hilo Tanzania tutapiga hatua na
tunapoisimamia Serikali hatupaswi kulaumiwa na mtu, kwani tunaisimamia
ilani ya CCM itekelezwe,” alisema Naibu Katibu Mkuu huyo wa
CCM.


Nchemba alisema kinachoigharimu Tanzania ni
baada ya uchaguzi kumalizika, halafu watu kuanza uchaguzi mwingine
badala ya kuchapa kazi ya kuwatumikia
wananchi.


“Uchaguzi ukiisha tujenge kasumba ya kuacha
kampeni na maandamano ya kila siku na kuingia kazini kuwatumikia
wananchi, si mmeona wenyewe baada ya uchaguzi wa Marekani kumalizika
watu wanafanya kazi na sio kuzungumzia uchaguzi tena,”
alisema.


“Haiwezekani siku zote ziwe za kampeni.
Tutafanya lini kazi, siku zote kuwa za kampeni zinawafanya watumishi wa
serikali kushindwa kugawa muda wa kuwatumikia wananchi?”
Alihoji.


Katika kikao hicho maalumu, Nchemba aliwagawia
wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM wilaya makabrasha ya maazimio ya
Mkutano Mkuu wa Nane wa Taifa na Hotuba ya Mwenyekiti wa CCM Taifa,
Jakaya Kikwete, kama vitendea kazi vyao.

Chanzo: HabariLeo | Imeandikwa na Grace Chilongola,
Mwanza | Jumapili, 23 Desemba 2012

onyesha na dhibitisha una akili timamu kwa kutochagua magamba 2015.
 
Wana jamvi ni ukweli usiopingika kwamba chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kitapoteza majimbo mengi kiliyoyapata 2010 kutokana na misuguano ndani y chama hiko ambayo inazidi kukibomoa chama hiko.
 
Hoja yako inaelea ipi maana majimbo yapi unayoongelea na kwanini uyapoteze na je itapata majimbo mangapi zaidi.
 
Dah! hapa kazi ipo. Umekurupuka!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
WASIOSOMA NI CHAKULA CHA WASOMI
 
Wana jamvi ni ukweli usiopingika kwamba chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kitapoteza majimbo mengi kiliyoyapata 2010 kutokana na misuguano ndani y chama hiko ambayo inazidi kukibomoa chama hiko.
pro-chadema watakuwashia moto! haya! wakati wao wanadhani watapata urais wewe unawatabiria kupoteza majimbo? sasa hivi watakuambia wewe uko nyuma ya mgogoro unaofukuta ndani ya chama.ngoja waje!
 
Back
Top Bottom