NyepesiNyepesi
Member
- Mar 8, 2011
- 47
- 9
Hii ni tahadhari kwa viongozi na wanachama wa chadema.
Baada ya tume ya uchaguzi kugawanya baadhi ya kata na majimbo ya uchaguzi mwaka jana, chama cha chadema kililazimika kuteua viongozi wa muda kukaimu nafasi za uongozi katika kata na majimbo mapya hadi hapo uchaguzi mkuu utakapokuwa umekwisha. Na baada ya kukamilika kwa zoezi la uchaguzi mkuu, uongozi wa chadema taifa umetoa maelekezo ya kufanyika kwa chaguzi za kidemokrasia ili kupata viongozi watakaoshikilia madaraka hadi 2014 utakapofanyika uchaguzi mkuu wa chama.
Kutokana na mwitikio mkubwa wa wananchi kujiunga na chadema na kuiunga mkono, aidha kwa kuchukua kadi na kuwa wananchama ama kwa kuwaunga mkono kwa wingi sana wanapoitisha maandamano na mikutano katika maeneo mbalimbali ya nchi, chama tawala ccm kimeingiwa na uwoga wa kuondolewa madarakani mwaka 2015. Pamoja na mikakati mbalimbali wanayoipanga ili kuidhoofisha chadema, mojawapo ni kupandikiza watu wao ndani ya chadema ili iwe rahisi kwao kujua kwa undani mipango na mikakati ya chadema lakini pia wawatumie watu wao hao kujipenyeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kupitia chadema na hivyo kuisaidia ccm kushinda uchaguzi mkuu ujao kwa hao mapandikizi yao kufanya hujuma dhidi ya chadema.
Sasahivi kuna wimbi kubwa sana la watu kumiminika ndani ya chadema kuchukua kadi za uanachama na moja kwa moja kugombea nafasi za uongozi, wengi wao ndio hao waliotumwa na ccm ili baadae wasaidie kuchafua hali ya hewa ndani ya chadema na kuihujumu. Kwahiyo nawatahadharisha wanachadema muwe makini sana mnapofanya uchaguzi. Kwa hapa Dar es salaam nimeambiwa kuna chaguzi ndogo katika majimbo ya ukonga na segerea pamoja na baadhi ya kata katika majimbo hayo.
Katika jimbo la ukonga kwa mfano, kuna watu kadhaa ambao wamejiunga na chadema hivi karibuni na moja kwa moja wameingia kwenye kinyang'anyiro cha uongozi wa jimbo. Mojawapo ni Mchungaji mmoja(jina kapuni) aliyegombea ubunge jimbo la ubungo mwaka jana 2010 kwa tiketi ya chama cha UDP lakini sasahivi amehamia chadema na mojakwa moja amejitosa kuwania uongozi jimbo la ukonga. Uongozi wa chadema muwe macho na mchungaji huyo atawavuruga, taarifa zaidi ni kwamba mwaka jana alishiriki kumpigia kampeni mgombea ubunge jimbo la ukonga kwa tiketi ya CUF, sasa hayo mapenzi na chadema yametoka wapi ndani ya miezi michache?? huyu ni wa kuangaliwa sana atawavuruga. Mwingine ni kijana mmoja, mdogo wake na mbunge mmoja wa viti maalum ccm mkoa wa iringa, kabla ya hapo alikuwa diwani wa viti maalum ukonga. Huyu kijana amejiunga na chadema mwezi wa sita na moja kwa moja amejaza fomu ya kuwania uongozi wa bavicha jimbo la ukonga, huyu naye ni kuangaliwa sana asije akakihujumu chama. Kuna vijana wengine wawili mwanamke na mwanaume, mmoja wao mwanaume alijaribu kujipenyeza kugombea nafasi ya uongozi(ukatibu) bavicha taifa kutokea jimbo la ukonga lakini bado hakijaeleweka. Uongozi wa taifa uwe makini na kijana huyo, amejiunga na chadema wakati wa kuelekea uchaguzi mkuu wa bavicha. Mwanamke bado hajaweka dhamira yake hadharani lakini ameanza kujipitisha kwa viongozi wa kata ambao ndio wapiga kura katika uchaguzi wa jimbo na pia anaonekana "kumteka" kiongozi mmoja wa jimbo.
Mwisho kabisa namalizia kwa kuwataka tena wanachadema kuwa makini na mamluki wa ccm na vyama vingine wataivuruga chadema, kila mmoja anashuhudia jinsi shibuda anavyowakoroga, kila mmoja anakumbuka jinsi yule mamluki wa ccm alivyokihujumu chama kule singida kwenye uchaguzi mkuu mwaka jana,na mifano kwa kweli ni mingi sana kila mmoja mahali pake ana ushuhuda.
Jambo la muhimu ni kujipa muda kwanza kuwapima hawa wanachama wapya hasa wanaotokea vyama vyengine ili kujiridhisha kama ni wa ukweli ama ni wa "kichina", nadhani mnanielewa vizuri. Kazi kwenu chadema. Hakuna chuki binafsi katika hili bali ni tahadhari kwa viongozi wa chama changu ili wawe makini na mamluki!!
Nawasilisha na kuwatakia weekend njema.
Baada ya tume ya uchaguzi kugawanya baadhi ya kata na majimbo ya uchaguzi mwaka jana, chama cha chadema kililazimika kuteua viongozi wa muda kukaimu nafasi za uongozi katika kata na majimbo mapya hadi hapo uchaguzi mkuu utakapokuwa umekwisha. Na baada ya kukamilika kwa zoezi la uchaguzi mkuu, uongozi wa chadema taifa umetoa maelekezo ya kufanyika kwa chaguzi za kidemokrasia ili kupata viongozi watakaoshikilia madaraka hadi 2014 utakapofanyika uchaguzi mkuu wa chama.
Kutokana na mwitikio mkubwa wa wananchi kujiunga na chadema na kuiunga mkono, aidha kwa kuchukua kadi na kuwa wananchama ama kwa kuwaunga mkono kwa wingi sana wanapoitisha maandamano na mikutano katika maeneo mbalimbali ya nchi, chama tawala ccm kimeingiwa na uwoga wa kuondolewa madarakani mwaka 2015. Pamoja na mikakati mbalimbali wanayoipanga ili kuidhoofisha chadema, mojawapo ni kupandikiza watu wao ndani ya chadema ili iwe rahisi kwao kujua kwa undani mipango na mikakati ya chadema lakini pia wawatumie watu wao hao kujipenyeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kupitia chadema na hivyo kuisaidia ccm kushinda uchaguzi mkuu ujao kwa hao mapandikizi yao kufanya hujuma dhidi ya chadema.
Sasahivi kuna wimbi kubwa sana la watu kumiminika ndani ya chadema kuchukua kadi za uanachama na moja kwa moja kugombea nafasi za uongozi, wengi wao ndio hao waliotumwa na ccm ili baadae wasaidie kuchafua hali ya hewa ndani ya chadema na kuihujumu. Kwahiyo nawatahadharisha wanachadema muwe makini sana mnapofanya uchaguzi. Kwa hapa Dar es salaam nimeambiwa kuna chaguzi ndogo katika majimbo ya ukonga na segerea pamoja na baadhi ya kata katika majimbo hayo.
Katika jimbo la ukonga kwa mfano, kuna watu kadhaa ambao wamejiunga na chadema hivi karibuni na moja kwa moja wameingia kwenye kinyang'anyiro cha uongozi wa jimbo. Mojawapo ni Mchungaji mmoja(jina kapuni) aliyegombea ubunge jimbo la ubungo mwaka jana 2010 kwa tiketi ya chama cha UDP lakini sasahivi amehamia chadema na mojakwa moja amejitosa kuwania uongozi jimbo la ukonga. Uongozi wa chadema muwe macho na mchungaji huyo atawavuruga, taarifa zaidi ni kwamba mwaka jana alishiriki kumpigia kampeni mgombea ubunge jimbo la ukonga kwa tiketi ya CUF, sasa hayo mapenzi na chadema yametoka wapi ndani ya miezi michache?? huyu ni wa kuangaliwa sana atawavuruga. Mwingine ni kijana mmoja, mdogo wake na mbunge mmoja wa viti maalum ccm mkoa wa iringa, kabla ya hapo alikuwa diwani wa viti maalum ukonga. Huyu kijana amejiunga na chadema mwezi wa sita na moja kwa moja amejaza fomu ya kuwania uongozi wa bavicha jimbo la ukonga, huyu naye ni kuangaliwa sana asije akakihujumu chama. Kuna vijana wengine wawili mwanamke na mwanaume, mmoja wao mwanaume alijaribu kujipenyeza kugombea nafasi ya uongozi(ukatibu) bavicha taifa kutokea jimbo la ukonga lakini bado hakijaeleweka. Uongozi wa taifa uwe makini na kijana huyo, amejiunga na chadema wakati wa kuelekea uchaguzi mkuu wa bavicha. Mwanamke bado hajaweka dhamira yake hadharani lakini ameanza kujipitisha kwa viongozi wa kata ambao ndio wapiga kura katika uchaguzi wa jimbo na pia anaonekana "kumteka" kiongozi mmoja wa jimbo.
Mwisho kabisa namalizia kwa kuwataka tena wanachadema kuwa makini na mamluki wa ccm na vyama vingine wataivuruga chadema, kila mmoja anashuhudia jinsi shibuda anavyowakoroga, kila mmoja anakumbuka jinsi yule mamluki wa ccm alivyokihujumu chama kule singida kwenye uchaguzi mkuu mwaka jana,na mifano kwa kweli ni mingi sana kila mmoja mahali pake ana ushuhuda.
Jambo la muhimu ni kujipa muda kwanza kuwapima hawa wanachama wapya hasa wanaotokea vyama vyengine ili kujiridhisha kama ni wa ukweli ama ni wa "kichina", nadhani mnanielewa vizuri. Kazi kwenu chadema. Hakuna chuki binafsi katika hili bali ni tahadhari kwa viongozi wa chama changu ili wawe makini na mamluki!!
Nawasilisha na kuwatakia weekend njema.