CCM Yakwama kuzindua Kampeni Kalenga leo

CCM Yakwama kuzindua Kampeni Kalenga leo

La muhimu kwa CDM ni kupiga kampeini hilo la MAGAMBA kushindwa kuzindua ni kitu ingine, wanatafuta mkakati wa kuja nao ikiwa ni pamoja na kununua kadi za wapiga kura, kuweni waangalifu na mjaribu kupita chini kwa chini kuzuia hii hali lasivyo ..................
 
Niliwaambia Chadema humu jamvini, CCM sio wajinga kiasi hicho wanafanya mipango ya chini kwa chini na kwa jimbo la Kalenga ambalo sehemu kubwa ni Iringa vijijini wanawategemea zaidi mabalozi wa nyumba kumi kuwarubuni wapiga kura, kuwatisha na hata kununua viparata vyao(Vitambulisho vya kupigia kura). Kuweni makini makamanda hakuna kubeza hata hatua moja ya hao manyang'au.
 
KILASI kwani shule umemaliza? Kama umemaliza basi hongera sana! Nashukuru kwa kukubali ukweli kuwa Godfrey ndio mbunge tarajali kinachosubiriwa ni kura tu!

Kila mtu Kalenga anajua Godfrey ndio mbunge wao na moto wa kuotea mbali! Hata Grace wenu anajua wazi na sasa ndio utakuwa mwisho wake wa kukishabikia CDM!

Kwa Kalenga Kama kumsukuma mlevi hivi!
nani ka kwambia nasoma shule.mi na ishi tu.nadhani unaye mjua siyo mimi
 
Sawa lakini cha moto mtakiona soon! Asikimbie mtu humu maana mnakuwa Kama wagonjwa na visingizio lukuki!

Vipi mtani leo upo zamu? Kwani wenzako hawaonekani wamekuachia Jukwaa peke yako au zile tablet mali ya chama leo wiki end hazitumiki zimefungiwa pale Lumumba?
 
Katika hali ya kushangaza chama cha CCM kimeshindwa kuzindua kampeni zake katika jimbo la Kalenga leo kama walivyotangaza awali.

Badala yake wamesema uzinduzi utafanyika siku nyingine itakayotangazwa.

Inadaiwa mbali na sababu nyingine mojawapo ni kutokana na mgombea wake kutokukubalika jimboni humo.Mgombea huyo wa CCM Godfrey Mgimwa alikuwa akiishi Uingereza na ameoa mke wake Mzungu raia wa huko huko.Pia wananchi wa Kalenga wanadai walimfahamu siku ya mazishi ya baba yake.

Inawezekana pia Ahirisho hilo linatokana na Katibu Mkuu wa Chadema Dr Wilbroad Slaa kuzindua kwa kishindo kikubwa kampeni za chama chake hapo jana Jumamosi huku akisindikizwa na Chief wa Kabila la Wahehe Abdu Sapi Mkwawa.

Tatizo uwa mnakurupuka sana kwa thread zisizo na Mashiko.
Toka mda mrefu CCM walisema Tar 23 watafanya Mkutano wa Kwanza wa Kampeni lakini sio Uzinduzi.

Uwe unafuatilia wala sio kukurupuka!
 
Kuna Mgimwa mwingine naibu waziri, je anaundugu na marehemu?
 
Au wanataka kumuoza ndoa ya mkeka kwanza ili awe na mke mhehe?
 
Tatizo uwa mnakurupuka sana kwa thread zisizo na Mashiko.
Toka mda mrefu CCM walisema Tar 23 watafanya Mkutano wa Kwanza wa Kampeni lakini sio Uzinduzi.

Uwe unafuatilia wala sio kukurupuka!

huo mkutano wa kwanza unaousema wewe umefanyika???? na kama umefanyika twambie umefanyikia wapi na ulikuwa na agenda zipi?????
kajipange upya,huu upuuz wako uliokuja nao umebuma!!!
 
Hawana jipya maccm kwakua hutumia ndoto kama ahadi kwa wananchi na kushindwa kutekeleza. Kwanza mgombea hata kiswahili au kihehe hajui atapigeje kampeni? Na kingereza si wote wanajua.mwache ale koz ya lugha ya kiswahili kwanza.
 
Katika hali ya kushangaza chama cha CCM kimeshindwa kuzindua kampeni zake katika jimbo la Kalenga leo kama walivyotangaza awali.

Badala yake wamesema uzinduzi utafanyika siku nyingine itakayotangazwa.

Inadaiwa mbali na sababu nyingine mojawapo ni kutokana na mgombea wake kutokukubalika jimboni humo.Mgombea huyo wa CCM Godfrey Mgimwa alikuwa akiishi Uingereza na ameoa mke wake Mzungu raia wa huko huko.Pia wananchi wa Kalenga wanadai walimfahamu siku ya mazishi ya baba yake.

Inawezekana pia Ahirisho hilo linatokana na Katibu Mkuu wa Chadema Dr Wilbroad Slaa kuzindua kwa kishindo kikubwa kampeni za chama chake hapo jana Jumamosi huku akisindikizwa na Chief wa Kabila la Wahehe Abdu Sapi Mkwawa.
Huyo chief ni tapeli tena mwizi kama dr slaa hatuwezi tukakaa hapa jamvini kujadili mkwawa copy.
 
Back
Top Bottom