CCM wapinga matokeo ya Serikali za mitaa Sumbawanga

CCM wapinga matokeo ya Serikali za mitaa Sumbawanga

Naona katibu alikuwa anatoa sababu akiwa anakata gogo..
 
Hahaaa!! Huyo katibu ni mjinga na mjanja sana. Ameshaambiwa na watu CCM makao makuu watamtimua kwa kuwa ameshindwa kupambana na CHADEMA ipasavyo hivyo hana mbinu mbadala zaidi ya kujitetea kijinga.
Poor CCM.

Huko anatoka Waziri mkubwa(mtoto wa mkulima), ndiye atakuwa ametoa amri ya shinikizo hilo! inasemekana huko Dar(Chanika) kwenye mtaa anakoishi inasemekana amekataa kuongozwa na Chadema, Sembuse kwenye jimbo analotoka!
 
Alitegemea matokeo yafanane kila mwaka?inaelekea bado haamini kilichotokea.Haya mapingamizi ya kishenzzi na ya kupotezeana muda inabidi yaongelewe kwenye katiba mpya.Kuwepo na vigezo vya mapingamizi,sio tu mtu anaweka pingamizi heti matokeo hayafanani na ya uchaguzi uliopita wakati wanaosimamia ni wao,polisi ni wao,uchakachuaji ni wao,sasa anafikiri kura zilijipiga na hazikupugwa na watu?

Shame on them!
 
Wangekuwa wameshinda wao wangeenda kupinga nini subiri mwaka huu mtafungua kesi mpaka mbinguni
 
Akiongea na waandishi wa habari, katibu wa CCM mkoa amesema hawakubaliani na matokeo hayo kwa vile hayaendani na matokeo ya jumla waliyopata kwenye uchaguzi kama huo mwaka jana ki-mkoa ambayo ni asilimia 69.

Chanzo: ITV habari za saa.

My take; Hivi hajui mambo huwa yanabadilika, wananchi (CCM) wa mwaka jana si wa leo?

Faiza Foxy......tafadhali jitokeze haraka sana huyu katibu ana zongwa mno.
 
Hivi huyu katibu wa ccm mkoa ni mzima kweli?
Hivi ni kweli hajui kwamba siasa inabadilika kila siku?
Hivi alidhani wananchi wa Sumbawanga watakuwa mbumbumbu kila siku?
Nadhani kichwa cha katibu huyu kimegoma kufikiri kama vilivyo vichwa vya viongozi wengi wa ccm.

Mkuu kuna wakati Pc inakwambia Mozilla or Word is not responding.

Plz close the program or wait!! Nadhani brain ya huyu M/kiti ni mgando!
 
Back
Top Bottom