nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Monday, 16 May 2011
* Akomba wanachama wake 239
* Chiligati: Mamluki CCM kudhibitiwa
Na Ghati Msamba, Bunda
Gazeti la Uhuru
KIMBUNGA cha Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama, kimeitikisa CHADEMA, ambapo ngome yake imepata nyufa. Ngome ya CHADEMA imepata nyufa baada ya wanachama 239 kuihama na kujiunga na CCM, huku wakiponda kauli za kejeli na kuvuruga amani zinazotolewa na viongozi wa chama hicho.
Wanachama hao wapya wa CCM wamesema wameridhishwa na kasi ya maendeleo na utekelezaji wa Ilani ya CCM katika kuondoa kero za wananchi. Mukama akiwa katika siku ya kwanza ya ziara wilayani Bunda, kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Kata ya Kibara, wananchi hao walitangaza kujiengua CHADEMA na kujiunga na CCM. Katika mkutano huo, Mukama alisema CCM ndicho Chama pekee kinachoweza kusimamia rasilimali na kubadilisha maisha ya wananchi. Aliwaasa Watanzania kutokubali kurubuniwa na kuwasikiliza watu wanaopotosha ukweli kuhusu dhana ya CCM kujivua gamba kwa kuwatosa watuhumiwa wa ufisadi.
Katibu Mkuu alisema CCM ni taasisi kubwa, hivyo haiwezi kufa kirahisi kama wanavyoota wapinzani, hususan CHADEMA kwa kuwa ina viongozi wenye maadili ya uongozi. "Miaka 34 ya CCM ni mingi, hivyo ni lazima viongozi wabadilike na ndiyo dhana ya kujivua gamba ili kuleta mageuzi, kwani kwa kufanya hivyo ni kuonyesha ukomavu na umakini," alisema.
Alitumia fursa hiyo kuwataka wakuu wa wilaya mkoani Mara kusimamia kikamilifu fedha za miradi ya maendeleo ya wananchi zinazotengwa na serikali kwa halmashauri.
Katika mkutano huo, wazee wa Bunda wakiwakilishwa na Raphael Gurinja, walimuomba Mukama kurudi wilayani humo ili kusafisha siasa chafu na sumu iliyoenezwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa. Alisema Dk. Slaa amekuwa akieneza siasa chafu zenye mwelekeo wa kuvuruga amani nchini, hivyo kumuomba Mukama amfundishe siasa.
"Dk. Slaa anaeneza chuki wakati wenzake wanamwaga sera, sasa inabidi afundishwe jinsi ya kuhubiri sera na si siasa chafu," alisema Gurinja. Akikabidhi kadi kwa wanachama wapya, Mukama alisema wamechukua uamuzi sahihi kurejea CCM, kwani vyama vya upinzani havina sera. "Nawapongeza kwa uamuzi wa kujiunga na CCM. Kitendo hiki kimewaziba midomo wale wanaodai eti Chama hiki kinakufa, karibuni nyumbani," alisema.
Mukama pia alikabidhi kadi kwa wanachama wapya 175 wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) na kuwataka kuimarisha jumuia hiyo kikamilifu.
Katibu Mkuu Mukama yuko katika ziara ya siku nane mkoani Mara, ambapo pamoja na mambo mengine atahimiza uhai wa Chama. Mamluki CCM kudhibitiwa CCM imesema itahifadhi majina na kumbukumbu za wanachama wake nchini kwa kutumia mfumo wa kompyuta.
Hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa mageuzi ndani ya Chama, ambapo imewaagiza makatibu kukusanya kumbukumbu kutoka kwenye matawi na kuzipeleka makao makuu ya CCM, mjini Dodoma, ambako zitahifadhiwa. Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), John Chiligati, alisema hayo wakati akihitimisha ziara ya wajumbe wa sekretarieti mpya ya CCM.
Alisema utaratibu huo unatakiwa kukamilika kabla ya uchaguzi mkuu wa CCM na jumuia zake utakaofanyika mwakani. Chiligati ametoa miezi mitatu kwa makatibu kuwa wamewasilisha kumbukumbu na majina ya wanachama makao makuu kwenye Kitengo cha Oganaizesheni kinachosimamia uratibu wa masuala ya uchaguzi, uhai wa Chama na jumuia zake.
Alisema makatibu watapeleka wanachama hai kwa kulipa ada na wale ambao hawajalipa watatakiwa kutuma makao makuu kila yanapotokea mabadiliko, yakiwemo ya wanachama wapya, wanaoacha uanachama au kufariki dunia. Chiligati alisema utaratibu huo unalenga kukomesha uwepo wa wanachama mamluki na wa msimu wa uchaguzi, ambao hawana faida kwa uhai wa Chama.
Ziara ya wajumbe wa sekretarieti ya CCM iliyofanyika kwa siku sita katika maeneo mbalimbali mkoani Singida, iliwahusisha Chiligati, Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, Katibu wa NEC, Uchumi na Fedha, Mwingulu Nchemba na Katibu wa NEC, Oganaizesheni, Asha Juma Abdallah.
* Akomba wanachama wake 239
* Chiligati: Mamluki CCM kudhibitiwa
Na Ghati Msamba, Bunda
Gazeti la Uhuru
KIMBUNGA cha Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama, kimeitikisa CHADEMA, ambapo ngome yake imepata nyufa. Ngome ya CHADEMA imepata nyufa baada ya wanachama 239 kuihama na kujiunga na CCM, huku wakiponda kauli za kejeli na kuvuruga amani zinazotolewa na viongozi wa chama hicho.
Wanachama hao wapya wa CCM wamesema wameridhishwa na kasi ya maendeleo na utekelezaji wa Ilani ya CCM katika kuondoa kero za wananchi. Mukama akiwa katika siku ya kwanza ya ziara wilayani Bunda, kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Kata ya Kibara, wananchi hao walitangaza kujiengua CHADEMA na kujiunga na CCM. Katika mkutano huo, Mukama alisema CCM ndicho Chama pekee kinachoweza kusimamia rasilimali na kubadilisha maisha ya wananchi. Aliwaasa Watanzania kutokubali kurubuniwa na kuwasikiliza watu wanaopotosha ukweli kuhusu dhana ya CCM kujivua gamba kwa kuwatosa watuhumiwa wa ufisadi.
Katibu Mkuu alisema CCM ni taasisi kubwa, hivyo haiwezi kufa kirahisi kama wanavyoota wapinzani, hususan CHADEMA kwa kuwa ina viongozi wenye maadili ya uongozi. "Miaka 34 ya CCM ni mingi, hivyo ni lazima viongozi wabadilike na ndiyo dhana ya kujivua gamba ili kuleta mageuzi, kwani kwa kufanya hivyo ni kuonyesha ukomavu na umakini," alisema.
Alitumia fursa hiyo kuwataka wakuu wa wilaya mkoani Mara kusimamia kikamilifu fedha za miradi ya maendeleo ya wananchi zinazotengwa na serikali kwa halmashauri.
Katika mkutano huo, wazee wa Bunda wakiwakilishwa na Raphael Gurinja, walimuomba Mukama kurudi wilayani humo ili kusafisha siasa chafu na sumu iliyoenezwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa. Alisema Dk. Slaa amekuwa akieneza siasa chafu zenye mwelekeo wa kuvuruga amani nchini, hivyo kumuomba Mukama amfundishe siasa.
"Dk. Slaa anaeneza chuki wakati wenzake wanamwaga sera, sasa inabidi afundishwe jinsi ya kuhubiri sera na si siasa chafu," alisema Gurinja. Akikabidhi kadi kwa wanachama wapya, Mukama alisema wamechukua uamuzi sahihi kurejea CCM, kwani vyama vya upinzani havina sera. "Nawapongeza kwa uamuzi wa kujiunga na CCM. Kitendo hiki kimewaziba midomo wale wanaodai eti Chama hiki kinakufa, karibuni nyumbani," alisema.
Mukama pia alikabidhi kadi kwa wanachama wapya 175 wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) na kuwataka kuimarisha jumuia hiyo kikamilifu.
Katibu Mkuu Mukama yuko katika ziara ya siku nane mkoani Mara, ambapo pamoja na mambo mengine atahimiza uhai wa Chama. Mamluki CCM kudhibitiwa CCM imesema itahifadhi majina na kumbukumbu za wanachama wake nchini kwa kutumia mfumo wa kompyuta.
Hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa mageuzi ndani ya Chama, ambapo imewaagiza makatibu kukusanya kumbukumbu kutoka kwenye matawi na kuzipeleka makao makuu ya CCM, mjini Dodoma, ambako zitahifadhiwa. Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), John Chiligati, alisema hayo wakati akihitimisha ziara ya wajumbe wa sekretarieti mpya ya CCM.
Alisema utaratibu huo unatakiwa kukamilika kabla ya uchaguzi mkuu wa CCM na jumuia zake utakaofanyika mwakani. Chiligati ametoa miezi mitatu kwa makatibu kuwa wamewasilisha kumbukumbu na majina ya wanachama makao makuu kwenye Kitengo cha Oganaizesheni kinachosimamia uratibu wa masuala ya uchaguzi, uhai wa Chama na jumuia zake.
Alisema makatibu watapeleka wanachama hai kwa kulipa ada na wale ambao hawajalipa watatakiwa kutuma makao makuu kila yanapotokea mabadiliko, yakiwemo ya wanachama wapya, wanaoacha uanachama au kufariki dunia. Chiligati alisema utaratibu huo unalenga kukomesha uwepo wa wanachama mamluki na wa msimu wa uchaguzi, ambao hawana faida kwa uhai wa Chama.
Ziara ya wajumbe wa sekretarieti ya CCM iliyofanyika kwa siku sita katika maeneo mbalimbali mkoani Singida, iliwahusisha Chiligati, Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, Katibu wa NEC, Uchumi na Fedha, Mwingulu Nchemba na Katibu wa NEC, Oganaizesheni, Asha Juma Abdallah.