CCM wafanyia mkutano kituo cha polisi

CCM wafanyia mkutano kituo cha polisi

Hii ni kuokoa gharama za kuwasafirisha polisi kwenda kwenye mkutano ikiwa ungefanyika mbali na hapo.Nawapenda CCM wanajua kuokoa pesa za walipa kodi.
 
Kile ambacho tunalalamika kila siku na kutoa ushahidi lakini serikali inapuuza.

Chama cha Mapinduzi wakiongozwa na Mbunge wa jimbo la Segerea na Naibu waziri Makongoro Mahanga wamefanyia mkutano kwenye mlango wa kituo cha Polisi kana kwamba hakuna viwanja vingine.

Polisi wakashindwa kufanya kazi zao magamba yamejaa mlangoni.

Hivi CHADEMA wangefanya vile mlangoni mwa polisi ingekuwaje? hebu wadau angalieni Picha mseme wenyewe
tatizo nini kufanya mkutano kwenye eneo la polisi ?
 
Dah hata msaada aliotoa katika kituo hicho mnaudhihaki mbona hamna jema kwenu hicho kituo kafanikisha kukifanyia renovation kawawekea hadi ac na kiyoyozi madirisha ya Vioo na Seli yenye choo

Hata kama alitoa msaada si alishakabidhi?

Ina maana angekuwa katoa msaadaa hospitali angekuwa huru kwenda kufanyia mkutano hapo?!
 
Ukitaka kukosoa uwe msafi!

Of all the things, that is the best you can do!!...It was an error(typing error) unless someone persist in it to be a mistake.

Nilimaanisha Kupenda nchi na Si 'jupenda' nchi! Na kiswahili sanifu ni huwa 'mnakimbilia' wapi na si "MNAKIMBILIAGA" wapi.

Now, Back to the topic!

Ukiwabana hata typo error kwao ni point of argument!
 
Magamba walikuwa na hofu kwamba wakifanyia eneo lingine watazomewa!
Yalikuja tabata kimanga yakazomewa mkuu ndio maana yakaona yakafanyie mkutano polisi post tabata shule....bwahahaaaaa
 
kama chadema wanafanyia mikutano yao kanisani. kusa gan ccm kufanyia mkutano mahali ambapo kuna ulinzi wa kutosha
 
Ukiangalia kwa makini picha yaonesha bwana mahanga hakuwa na uhakika wa usalama kwenye mkutano wake hasa ikikumbukwa alikamatwa na masanduku ya kura alizochakachua, mtu wa namna hiyo anajua asivyo na wa kuwahutubia hivyo kuhofia anaweza kuadhibiwa kwa wizi muda wowote hali inayopelekea kuufuata ulinzi mlangoni!

Alikuwa "mzalendo" mzalendo ya CCM, ya wizi wa kura! na wizi mwingine, manaake kwa CCM mzalendo ni reciprocal ya Mzalendo halisi!
 
“The world will not be destroyed by those who do evil, but by those who watch them without doing anything” -ALBERT EINSTEIN
 
Wakati nasoma uzii huu Radioni kulikuwa kunaimbwa ule wimbo "......mbona majanga......mbona majanga....." Nikaiangalia picha hii nikajikuta naangua kucheko mwenyewe. mbona majanga!!
ImageUploadedByJamiiForums1375790181.993446.jpg
 
kama chadema wanafanyia mikutano yao kanisani. kusa gan ccm kufanyia mkutano mahali ambapo kuna ulinzi wa kutosha

Mkuu hili neno lako na baadhi ya watu kama nyie ndo mnaovuruga taifa hili, sometimes you dont have to look far for you to notice a fool, keep it up
 
Huyu jamaa watu huwa wakimfata na shida zao anawaambia hana mda kwanza hana shida na kura zao yeye pesa yake ndo iliyompa Ubunge!!na anajigamba kwamba 2015 atapita tu hata wasipompa kura.
 
Kweli magamba wanavituko ha ha ha ameenda karibu na ulinzi si huyu wanasema alikimbia na masanduku ya Kura?
 
ni jambo la kawaida....ingelikuwa upinzani hasa chadema hawa kandamizwi na polis.
 
Back
Top Bottom