CCM wafanyia mkutano kituo cha polisi

CCM wafanyia mkutano kituo cha polisi

Dah hata msaada aliotoa katika kituo hicho mnaudhihaki mbona hamna jema kwenu hicho kituo kafanikisha kukifanyia renovation kawawekea hadi ac na kiyoyozi madirisha ya Vioo na Seli yenye choo
 
Mahanga kufanyia mkutano kituo cha Polisi si ajabu kwa mtu yeyote anayeishi maeneo hayo ya Tabata Shule kwani watu wengi wa maeneo hayo hawamtaki na zaidi ya 85% wazee kwa vijana hawakumpigia kura kwa hiyo kufanya hivyo ilikuwa ni njia mojawapo ya kujihami kwani uwezekano wa kuzomewa au kufanyiwa vurugu lazima ungejitokeza.
Itakuwa labda ndie aliesaihidia kujengwa kwa kituo hicho.
 
ndo mana tunasema polisi ya Tanzania haina cha zaidi ila kumsikiliza IGP Mwigulu Nchemba... Policcm... kuna siku watafanyia mkutano TBC.... TBCCM
 
Last edited by a moderator:
Hiki chama ni aibu tupu mara kifanyie mikutano sokoni, mara stendi leo kituo cha polisi ila aibu mweee
 
Au ana hofu kwa vile aliiba masanduku ya kura ? Maana hata vibaka wakizidiwa hukimbilia polisi .
 
Huyo Mahanga ameenda hapo kituoni kwenda kulipa fadhila kwa policcm jinsi walivyomuokoa na aibu ya karne,kwenye uchaguzi wa 2010.

Si mnakumbuka kwenye uchaguzi huo,jinsi alivyokamatwa red handed na mabox ya kura feki,hadi akafikishwa kwrnye kituo cha polisi cha Buguruni, lakini kama kawaida yao mapoliccm yakapotezea kiaina,ushahidi huo wa beyond reasonable doubt.

Kwa maana hiyo Mahanga,ana kila sababu za kufanyia mikutano yake kwenye vituo vya polisi,kwani bila vituo hivyo kuupotezea ushahidi huo wa dhahiri wa kukamatwa na kura hizo feki,anajua dhahiri kuwa hivi leo asingekuwa anaitwa mheshimiwa mbunge!!
 
Haongei na wananchi wa Tabata, bali anaongea na Magamba wenzake wa CCM
 
Kwa mtindo huu kazi kweli kweli hi sasa ndio policcm narudia tena policcm
 
Muwe wavumilivu, 2015 si mbali. Mkumbuke tu kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura. Hawa dawa yao mbona kidogo tu..!
 
Dah hata msaada aliotoa katika kituo hicho mnaudhihaki mbona hamna jema kwenu hicho kituo kafanikisha kukifanyia renovation kawawekea hadi ac na kiyoyozi madirisha ya Vioo na Seli yenye choo

Unafahamu tofauti ya ac na kiyoyozi au unaropoka tu ili uingize buku saba?
 
Sasa Mahanga anaishije kama digidigi ndani ya jimbo analoliongoza ikiwa hana confidence ya kukutana na wananchi anaowawakilisha bungeni? Huu uroho wa madaraka ndio chanzo cha maccm kuiba kura na kulazimisha kuongoza watu wasiowakubali.
 
Muwe wavumilivu, 2015 si mbali. Mkumbuke tu kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura. Hawa dawa yao mbona kidogo tu..!

Mkuu,

Sisitiza kulinda kura pia! Magamba hayana aibu. Tukumbuke pia serikali ya ccm huwa kuna watu hawapendi wakose bungeni na uwagharimia kwa njia yoyote..we should be able to spot them! Tuayajue hayo majimbo na kura zetu zilindwe kwa nguvu zote!
 
Jamani mwacheni kakimbilia sebuleni kuficha uozo wake akijua ukimkosoa tu unawekwa chumban(Ndani) si ndo policcm hyo??
 
Labda waliogopa kumwagiwa tindikali, maana yale magaidi yemeachiwa huru kule Tabora
 
Huyu ndie aliyekimbia na masanduku ya kura na Polisi wakawa wanamwangalia tu. Na Leo anafanyia mkutano kituoni wanamwangalia tu, kesho hatujui atafanya nini
kesho atakwenda kufunga mkutano chadema usiendelee kwa kushirikiana na polis!
 
Back
Top Bottom