Uchaguzi 2020 CCM tumefanya makosa kwa miaka mitano. Hakuna wa kumlaumu, sasa tulinywe!

Mwingereza

JF-Expert Member
Jan 21, 2014
1,111
2,741
Kwa miaka mitano uwanja ulikuwa ni wetu. Tumewafunga minyororo ya miguuni, mikononi na hata shingoni huku midomo yao tumeyafunga kwa vitambaa. Uwanja ulikuwa ni wetu, tumewakejeli, tumewasimanga tumewaita kila haina ya majina huku wasiojulikana wakiwafanyia kweli bila kujulikana.

Tumewasweka lupango, tumewanunua kana kwamba ni mitumba. Tumetumia vyombo vya habari peke yetu. Tuliwazibia kila kona, ilikuwa ni CCM. Tumetembea vifua mbele huku tukijinasibu kama wana maendeleo. Polisi wamewatesa sana wana CHADEMA. Hawa jamaa wamekiona cha moto lakini bado wanapumua !

Tumeimba singeli za Stigllers Gorge, tumenunua midege, SGR, Flyovers, elimu bure, na kila haina ya maendeleo. Hatukuwa na kosa, tulikuwa weupe kama theluji bila kujua kwamba tulikuwa wachafu mithili ya nguruwe alijetumbukiza kwenye matope.

Ghafla bin vuu, maendeleo yote tuliyokuwa tunajivunia imegeuka kuwa kamba ya kutunyongea. Mwenyekiti wangu kakamatwa suruali chini Kibiti, "Anatoa Rushwa".

Maendeleo ya kujenga Uwanja wa ndege Kijijini Chato imegeuka kuwa kashfa ya karne.

Laiti tungalijua, tungewahacha hawa watu waongee, maana watu wangechoka mapema na hii mashambulizi yao isingekuwa kivutio kama ilivyo leo. Kwa hali iliyopo, ukigeuka kulia, watu wanataka kusikia nondo za Lisu. Kuhsoto wataka kumsikiliza Lissu. Kwenye daladala lissu, sehemu za starehe ni Lissu. Makanisani Lissu. Vijijini Lissu kila kona Lissu na Chadema.

Ingawa tumeziba vyombo vya habari kutangaza habari za Chadema, Instagram na mitandaoni ni hoja nzito za Lissu. Mbaya zaidi, muda wa kujitetea haitoshi nikiangalia miaka mitano na siku 60 za kampeni. hesabn haiku bali. Hatuwezi kutoboa

Mikutano yetu iliyokuwa Mubashara toka Ikulu, leo imegeuka kuwa Maigizo ya wana usalama kuchoma mahindi na bastola kiunoni. Maendeleo yetu ya Flyovers imekuwa Wapinzania kutaka kuuza Scrapper. Hoja mfu!

Bandugu kwa miaka mitano tumelikoroga. Sasa inabidi tulinywe. Mwaka huu kuiba kura ni kaa la moto na atakayethubutu anakwenda na maji.

Ama kweli majuto ni mjukuu!
 
Wapinzani wakijipanga vizuri wanaweza kusomba kura nyingi toka kwa wanaCCM. Watu wengi chamani hawapendi yanayoendelea mfano mzuri ni jinsi wajumbe walivyo wakata watu. Sasa hebu fikiria wanaccm wakitumia mfumo kama wa wajumbe.

Yaani kwenye kampeni wanajaa, rushwa wanachukua, wanapiga shangwe za nguvu, tisheti wanavaa ila kura wanawapa wapinzani. Nadhani wapinzani walifikirie hilo maana wajumbe wameonesha njia na nia.
 
Mwingereza,
Ili kufanikiwa lazima tufike mahali wakuu wa mikoa,wakuu wa Wilaya wateuliwe na Wananchi kama wabunge wanavyoteuliwa.pili lazima wakuu wote wa vyombo vya ulinzi na usalama waombe hizo nafasi na zitangazwe na wapitishwe na bunge.Vinginevyo tutaenda mbele tutarudi nyuma kila mwaka na mwisho Kuna atakayekuja kuiuza SGR mwaka 2030.
 
Wapinzani wakijipanga vizuri wanaweza kusomba kura nyingi toka kwa wanaCCM. Watu wengi chamani hawapendi yanayoendelea mfano mzuri ni jinsi wajumbe walivyo wakata watu. Sasa hebu fikiria wanaccm wakitumia mfumo kama wa wajumbe. Yaani kwenye kampeni wanajaa, rushwa wanachukua, wanapiga shangwe za nguvu, tisheti wanavaa ila kura wanawapa wapinzani. Nadhani wapinzani walifikirie hilo maana wajumbe wameonesha njia na nia.
Na hii ndivyo itakavyokuwa mwaka huu
 
Kwa miaka mitano uwanja ulikuwa ni wetu. Tumewafunga minyororo ya miguuni, mikononi na hata shingoni huku midomo yao tumeyafunga kwa vitambaa. Uwanja ulikuwa ni wetu, tumewakejeli, tumewasimanga tumewaita kila haina ya majina huku wasiojulikana wakiwafanyia kweli bila kujulikana...
Tulia wewee

Chama chetu cha Mapinduzi chajenga nchi
Chama chetu cha mapinduzi chabomoa nchi
 
Siamini kabisa. Tumewaburuza jamaa kwa miaka mitano leo tunaonekana kama mazwazwa hata kujitetetea hatuwezi tunabakia kuwatumia wakina TID. Shame on Polepole. Sijui walimuokota wapi !
Jamani, mwaka huu tukubaliane kufanya kampeni za kistaarabu, tunaomba jamani
 
Eti unasemaje?.Kuna waheshimiwa fulani waliacha nafasi zao za kazi wakaenda kuunga mkono juhudi uku wakitema cheche kua haijapata kutokea kama awamu hii ya asali na maziwa.Ilikua ni miaka ya wachache kujidai dai kila kona uku wengi wao wakiugulia.

Ila kwavile wakati sio milele hatimaye miaka mitano imeisha mambo yako vile vile tunaanza tena upya kuomba kuchaguliwa uku tukiona kumbe tuliyoyafanya bado hayatoshi pamoja nakujitanua kote kule.
 
Back
Top Bottom