CCM na Hatima Ya Bunge La Katiba

CCM na Hatima Ya Bunge La Katiba

Jambo lililo wazi hapa ni kuwa kwenye hilo bunge la katiba wajumbe wengi ni CCM,Je? Ma-CCM yatazingatia maslahi ya umma?na vip hao wajumbe watakapopitisha mambo yaliyo kinyume na wananchi,kwenye kura ya maoni bila daftari la wapigakura kurekebishwa,wananchi tutaweza kuipinga katiba hiyo ambayo bila hata ya kupiga ramli itakua imetokana na matakwa ya CCM?
 
CCM wamejidhihirisha wazi kuwa wako kichama zaidi kuliko kuwajali wananchi.Muungano waserekali 2 uliletwa na wao pasipo kuwashirikisha wananchi.Kwa sasa wananchi wanataka kuwa na muungano wa serekali 3 CCM kwa vile wanaangalia masilahi ya chama zaidi kuliko masilahi ya wananchi wanataka kuwalazimisha wananchi waendelee kuunga mkono muungano wa serekali 2 wakati umepitwa na wakati.Wanafikiri kuwa mwananchi bado ni yule wa zidum fikra sahihi za mwenyekiti wa CCM pasipo kutambuwa kuwa fikra hizo zimepitwa na wakati na sasa hivi zinazo dumishwa ni fikra sahihi za wananchi.Hapo ndipo wananchi wanaweza kutambua kuwa ni yupi yuko kwa ajili ya kuwapigania na ni yupi ambae yuko kwa ajili ya kujipigania mwenyewe ili kujineemesha yeye mwenyewe na familia yake.
 
Wanasiasa Bogus wanajifanya wao ndio Hati Miliki ya Tanzania!
 
Maneno meeengi lakini point yako hapa tukubali serikali tatu.lakini haya mambo huwezi kulazimisha,litakoloamliwa na wengi ndo hilohilo.
Hao wengi ni nani? Tume ya Jaji Warioba imekamilisha ukusanyaji wa maoni ya wananchi na 61% ya waliotoa maoni wanataka serikali tatu. Sasa wewe unataka wingi wa kitu gani hasa?
 
Toka mwanzo kabisa ccm ilijua inataka katiba ya aina gani na muungano wa serikali ngapi; hili lilidhihilishwa na jinsi sheria ya mabadiliko ya katiba ilivyopishwa na bunge lenye majority ya ccm legislators!! Ukiangalia compositiona ya hao wanaokwenda kwenye bunge la katiba ni hao wabunge wa bunge la JMT na hao wa baraza la wawakilishi pamoja na hao Rais atakaowateua ambao I ama sure ccm are at the moment involved in making sure kuwa hao wateule ni wale ambao ni sympathetic na views zao.

Kule kwenye bunge la katiba hawa wajumbe wa ccm watang'ang'ania muundo wa serikali mbili za muungano kulinda sera yao iliyopitwa na wakati; na watafanya hivyo wakijua kuwa Mwenyekiti wao hana ubavu wa kuwalazimisha kubadili huo msimamo na wanajua kabisa kuwa bila kubadili huo msimamo wa serikali mbili there wili be a stalemate na hivyo ndivyo wanavyotaka ili katiba mpya isipitishwe ili ile ya zamamani [1977] iendelee kutumika kwani it puts them in a better winning [ kumbuka ccm inajali kushinda chaguzi tu na sio maendeleo]position come the 2015 general elections tofauti na kama katiba mpya ikipitishwa!!! Wanakwenda kwenye bunge la katiba kudefend the Status quo na sio kuleta mabadiliko na ndio maana Kikwete akawaonya kuwa waende kwenye bunge na mtazamo wa kitaifa na sio kichama na kama katiba haitapitishwa yeye atakuwa kishaondoka na yuko kwao Msoga analima mihogo na fursa ya kupata katiba mpya kabla ya 2015 itakuwa imepotea!!! This is what some people predict to be a constitutional crisis awating this country.
 
Dah bandiko lina mshiko sana, nimeipitia fasta fasta kupata general view nikagundua kuna points nyingi zilizoshiba. Ngoja nipige msosi kwanza halafu nirejee tena niichimbue vizuri
 
Natamani CCM wakatae maoni ya wananchi tubaki na katiba ya zamani, halafu wanannchi waamue kuipiga chini CCM katika uchaguzi 2015.

CCM iwe upinzani ndani katiba hii, watajuta.
 
KWANINI CCM HAWANA HOJA
Awali nimeeleza makosa yanayosababisha mchakato kuwa mgumu na pengine kuleta tatizo katika bunge la katiba.

Mdhamini mmoja na wanachama wengi wa CCM wanaamini Warioba hakufanya la maana kuzuia muungano wa serikali 2 ubaki kama ulivyo.

Hoja ya kwamba ni gharama kwakweli ni ya kuchekesha sana.
Gharama kwa Tanganyika ni pale tu serikali ya shirikisho itakapoacha kuweka masharti ya uchangiaji kwa znz.
Hapo ndipo Mtanganyika atabeba mzigo, vinginevyo hakuna ongezeko la gharama hata kidogo.

CCM wameshindwa kuelewa kwa miaka 50 kumeundwa tume zaidi ya 5 kuhusu kero za muungano.Kumekuwa na wizara na kila aina ya ubabaishaji ambao haukutoa majibu ya tatizo.

CCM na serikali yake walikazania kuwapendeza wznz badala ya kutafuta suluhu ya kudumu.
Kila znz walipotaka jambo walitishia muungano.
Hiyo haikuwa suluhu hata kidogo, ilikuwa ni asprin tu ya kutuliza homa ya muungano.

Kwakuwa znz walionekana wameshikilia muungano kwa kutishia kila mara, hilo likaamsha curiosity kwa Watanganyika waliokuwa hawana tatizo na znz.

Watanganyika wakabaini wakati wamebeba mzigo mzito wa muungano znz walitumia muungano kama silaha ya kupata walichokitaka katika ku bargain.

Watanganyika wakagundua kumbe muungano ni pale mznz anapoihitaji Tanganyika baada ya hapo hakuna muungano.

Watanganyika wakagundua kuwa kumbe hata bunge la JMT halina nguvu kuliko BLW ambalo ndilo huamua hatima ya miswada ya Bunge la JMT.

Watanganyika wakaamshwa na kuonyeshwa kuwa kile wanachoambiwa wananyonya kumbe wananyonywa kupita kiasi.

Ndipo nguvu ya kurudi Tanganyika ikarudi bila CCM kujitambua.
Walidhani watu wapo usingizini, kuamka mataokeo ndio hayo ya serikali 3.

Ni kwa misingi hiiyo CCM hawana hoja kwasababu walikuwa na fursa miaka 50 hawakuweza leo wanahoja gani ya kushawishi kuwa serikali 2 ziatakuwa na maana.

Wakati huu Watanganyika wametambua hawana cha kupoteza serikali 2 hazitakubalika tena, huo ni ukweli na CCM ikijaribu itakumbana na hukumu ya 2015.Atakayebeba agenda ya kubadili mfumo bila kujali ni wa aina gani atakuwa na kiboko cha kuitandika CCM

Watu wanaishia kumlaumu Warioba tu, ukweli ,Warioba anaokoa muungano na ndicho alichofanya.Serikali 3 haziepukiki kwasababu moja haiwezekani hata kwa nini.

Watanganyika wanaitaka nchi yao, wamegundua kuwa hawana sababu za kupigizana kelele na nchi jirani. Nchi jirani ikitaka kuwa na mahusiano na Tanganyika ni kwa uwazi na haki sawa. Hapo CCM watawashwishi nini Watanganyika wakubali serikali 2?

In other words CCM watawashawishi nini Watanganyika kuwa muungano na znz ni muhimu na kuwa Watanganyika wapoteze tena kama ilivyokuwa miaka 50?
Kigumu zaidi ni kuwa Watanganyika wapo tayari kwa lolote watatishiwa na nini!



 
Muungano wetu uliundwa kwa njia ya legal manipulations and political expediency. Ndio maana muungano mpaka leo umejengwa chini ya shaky legal and political framework. Lakini kama nilivyojadili #1 , kwa vile uhalali wa serikali chini ya Mwalimu Nyerere haukutokana na katiba per se bali masuala mengine makuu matatu niliyojadili, kwa ilikuwa ni rahisi kufunika chemchem ya moto mkali uliokuwa unafukuta chini ya framework hizi hafifu za kisheria na kisiasa.

Tukumbuke kwamba kwa mwalimu nyerere, serikali mbili haikuwa ni final destination bali mpito kuelekea serikali moja aidha under his watch au kwa wale watakaomfuatia baadae. Lakini cha ajabu ni kwamba, waliomfuatia wana-treat mfumo wa serikali mbili kama ni the alpha and omega. Chama gani duniani kina sera static? Sera inatakiwa kuwa dynamic kuendana na nyakati, lakini hasa, kuendana na matakwa ya umma. Kwa ccm kung'ang'ania sera husika wakati umma haukubaliani na sera hiyo ni kitu cha ajabu sana kwa chama kikongwe kama ccm.

Viongozi wa ccm wanasahau kwamba mwalimu aliwahi kutamka kwamba iwapo umma utapinga muungano, hatowapiga mabomu bali kukubaliana na matakwa yao. Mwalimu alitetea mfumo wa sasa kwa hoja na uzalendo uliotukuka na bila ya partisan bias ya aina yoyote ndio maana pamoja na mapungufu ya mfumo husika, mambo yalijadilika na people lived with hopes. Leo wanasiasa wa ccm hawana hata chembe ya uzalendo kutetea mfumo uliopo; hawaonyeshi hata mapenzi kwa taifa lao la tanganyika, na mbaya zaidi, hawana hoja zaidi ya kejeli, mipasho, matusi na vitisho kwa wale wanaopinga serikali mbili kwa hoja; Leo umma umekataa mfumo uliopo, watawala hawapo mbali kupiga mabomu wananchi iwapo wataandamana kama matakwa yao ya mfumo wa muungano yatakataliwa na bunge la katiba.

Viongozi wa ccm wanasahau kwamba muungano ulikuwa ni wa kisiasa zaidi kuliko kiuchumi, na katika hiki wazanzibari got away with a lot kama Nguruvi3 anavyojadili kwa muda mrefu sana. Sasa watanganyika wamechoka na siasa za muungano ambazo haziwasaidii lolote na sasa wanataka uchumi uwe kipaumbele. Katika hili, baadhi ya viongozi wababaishaji ccm wanawatishia wananchi kwamba kiuchumi wataumia chini ya serikali tatu.

Wanasiasa wa aina hii hawawaelezi wananchi ukweli kwamba serikali mbili ndio mzigo zaidi kwa mwananchi, hasa mtanganyika kwani ni kwa mfumo wanaoutaka ccm, kwa kiasi kikubwa, mwananchi wa tanganyika ndiye anagharamia maisha ya mzanzibari na ya kwake kwa wakati mmoja; wanasiasa hawa wanaficha ukweli kwamba muundo wa serikali mbili umesababisha kuwepo kwa: *Wizara na taasisi zinazofanya kazi za muungano peke yake;
*zinazoshughulikia mambo ya Tanzania bara; na
*zinazoshughulikia mambo mchanganyiko yani ya muungano na yasiyo ya muungano.

Katika haya, hasa la tatu hapo juu, ni vigumu kutofautisha gharama za muungano na zisizo za muungano kwenye taasisi na idara husika.

Kwanini wanasiasa hawa wa ccm hawaelezi wananchi ukweli kwamba muungano ulikaa chini ya katiba ya muda kwa miaka karibia kumi na tatu kutokana na ugumu wa kuunda serikali moja? Kwanini hawaelezei umma kwamba miaka 12 baadae (1965-77) ndio TANU ikabuni muungano wa serikali mbili kwa imani kwamba muungano wa aina hiyo utawezekana tu chini ya one party state and one party constitution? Hii ndio maana nzima behind ndoa ya TANU na ASP;

Kama alivyoeleza Nguruvi3, wa kumlaumu sio jaji warioba bali ccm wenyewe kwa kutosoma alama za nyakati. Vinginevyo waseme kwamba warioba alikuwa nyuma ya sakata la kina Mzee Jumbe 1984; mzee mmoja mkongwe wa chama ananukuliwa akisema kwamba Jaji Warioba alikuwa kwenye G55 kwa kujificha kwa kumuogopa mwalimu. Kwa watu wenye akili na mapenzi kwa taifa lao, hizi ni breaking news na ni habari njema sana kwani wengi tulidhania warioba ameanza kukubaliana na hoja ya tanganyika baada ya kustaafu. Actually this makes him more credible for job, na hakika, unlike wakongwe wengine wa chama, he will be on the correct side of our history. Pamoja na hayo, je cha ajabu nini kwa mwanasheria (warioba)kuwa upande wa G55, ikizingatiwa kwamba muungano uliundwa chini ya legal manipulations? Ina maana mkongwe huyu wa ccm anayemshambulia warioba anataka kutuambia kwamba mwalimu alikuwa sahihi na mfumo uliopo? Kwa kweli angekuwa na hoja angalau ya kisiasa iwapo angesema kwamba warioba awali alikuwa pro two governments.

Historia tayari inaweka wazi kwamba miongoni mwa makosa na mapungufu makubwa ya Nyerere, moja wapo ilikuwa ni imano yake kwamba muungano wa serikali mbili unawezekana. Pengine aliamini hivyo kutokana na serikali yake kupata uhalali kutawala nje ya uhalali wa kikatiba kama nilivyojadili, suala ambalo kwa hilo siwezi mlaumu mwalimu. Lakini nitamlaumu kiongozi yoyote ambae bado anaamini katika formula ya serikali mbili ambayo ilijengwa kwa kutegemea uwepo wa one party state and one party constitution, serikali ambayo haikuhitaji katiba ya nchi kupata uhalali wa kutawala. Lakini miaka 50 baadae, kiongozi ambae anatetea muungano unaotawaliwa na legal manipulations and political expediency, huyo hatufai kwani anatupeleka kubaya kama taifa.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Muungano wetu uliundwa kwa njia ya legal manipulations and political expediency. Ndio maana muungano mpaka leo umejengwa chini ya shaky legal and political framework. Lakini kama nilivyojadili #1 , kwa vile uhalali wa serikali chini ya Mwalimu Nyerere haukutokana na katiba per se bali masuala mengine makuu matatu niliyojadili, kwa ilikuwa ni rahisi kufunika chemchem ya moto mkali uliokuwa unafukuta chini ya framework hizi hafifu za kisheria na kisiasa.

Mkuu mchambuzi hapa Tanzania kuna legal manipulations nyingi tu, sio kwenye kulinda muungano tu, nyingine hata zinakwenda kinyume kabisa na katiba yetu, lakini as long as CCM inazipenda zinaangaliwa tu. Lakini uzuri ni kuwa moto ukifukuta kwa muda mrefu, kama usipozimwa vizuri, basi matokeo yake yanakuwa mabaya.

Ukiangalia kwa sasa chokochoko zilizopo kwenye muungano kimsingi zinatokana na uriho wa madaraka wa watu wachache Zanzibar, na hasira ya wachache wa bara kutokana na kauli chafu za baadhi ya wanasiasa wa Zanzibar.

Bila kujali legality ya muungano, ni vizuri tukiangalia sababu ziliofanya uwepo muungano, kwanini Karume na Nyerere walikubaliana kuunganisha nchi wanazoongoza? Hili liwekewe wazi kwanza. Inawezekana kinachoandikwa na kusemwa, sio kilichopo, cha kweli bado wengi hatukijui. Tukikijua ndio tunaweza kukijadili wazi. Kama conditions zimebadilika na zinahitaji ndoa kuvunjika basi ielezwe wazi.

It is very possible that legal manipulations and coercive measures which have been taking place for decades have been done for the greater good.
 
Mkuu Bongolander, unaelekeza mjadala kuzuri kwa hoja zako kwamba:

Bila kujali legality ya muungano, ni vizuri tukiangalia sababu ziliofanya uwepo muungano, kwanini Karume na Nyerere walikubaliana kuunganisha nchi wanazoongoza? Hili liwekewe wazi kwanza. Inawezekana kinachoandikwa na kusemwa, sio kilichopo, cha kweli bado wengi hatukijui. Tukikijua ndio tunaweza kukijadili wazi. Kama conditions zimebadilika na zinahitaji ndoa kuvunjika basi ielezwe wazi.

It is very possible that legal manipulations and coercive measures which have been taking place for decades have been done for the greater good.

Mkuu Bongolander,

Kulikuwa na sababu tatu za kufanyika kwa muungano husika:
*Kwanza ni Panafricanism spirit.
*Pili Cold War Politics.
*Tatu, kuleta utulivu wa kisiasa kufuatia mapinduzi.

Sababu ya pili ikaja to overshadow sababu ya kwanza na ya tatu kwani ndio ilikuwa an immediate reason for the union to happen. Kwa maana nyingine, at the end, muungano ukazaliwa under the cold war womb.

Baada ya hilo kutokea, Mwalimu akajaribu sana kutumia mwanya huo to pursue his panafricanism dream huku na Karume nae akitumia mwanya huo to contain anti ASP fanatics. In the process, Mwalimu na Karume were both met with formidable challenges. ili kutimiza malengo yaliyowekwa, hapakuwa na jinsi zaidi ya sarakasi za legal manipulations and political expediency kwa matumaini kwamba pengine the weak political and legal frameworks zitaimarika, efforts which ended up futile.

Leo, watetezi wa serikali mbili wanajisahau kwamba architect wake (mwalimu nyerere) didn't plan to make mfumo husika kuwa the alpha and omega bali kuwa wa muda mpaka mazingira yatakaporuhusu muungano wa serikali moja assuming kwamba nchi itaendelea kuwa under one party state na kuwa chini ya one party constitution. Hivyo ndivyo Mwalimu aliamini kwamba ndoto yake ya panafricanism itatimia.
Bongolander, hata mimi ni muumini wa serikali moja first and foremost lakini kwa vile naangalia vitu in practice zaidi, given the history plus the foundations of the said union, serikali moja haiwezekani and actually to adopt it itakuwa ni fast tracking ya kuvunja muungano kwani wanachokitaka zanzibar ni masuala ya autonomy, identity and self determination, masuala ambayo kimsingi ni haki yao. Tukija kwenye option ya pili ambayo ni serikali mbili, mfumo huu umeshindwa na hatuna haja ya kupoteza sana muda kufafanua tena na tena. Sasa iwapo nia ni kuimarisha na kuboresha muungano uliopo, njia pekee ni serikali tatu kwani hata kifanyike nini, kukarabati muungano kupitia serikali mbili ni jambo lisilowezekana kabisa given the history, legal foundation, na hatua ambayo mshirika mmoja wa muungano (zanzibar) amefikia kikatiba towards her autonomy, identity and self determination. Tumeshajadili sana logic behind serikali tatu, faida zake na kwanini mfumo huo ni njia pekee ya kuimarisha muungano vis a vis serikali mbili au moja. Lakini bado wapo wana ccm wanaoamini katika legal manipulations and political expediency kama njia ya kutafuta uhalali wa kutawala huku wakisahau kwamba uhalali wa serikali kutawala ulitokana na vyanzo tofauti kabisa na nje kabisa ya Katiba ya JMT (1977) kama nilivyojadili #1 . Isitoshe, walinzi wa kweli wa muungano wowote ule iwe ni ndoa ya mume na mke, ujirani, vijiji au nchi, walinzi wa kweli huwa ni wananchi, sio vyombo vya ulinza na usalama. Sasa iwapo wananchii walio wengi wameona kwamba njia pekee ya wao kuulinda na kuimarisha muungano ni kwa kuleta serikali tatu, kwanini hatutumii akili ndogo tu kuwapa imani zetu wananchi hawa juu ya ulinzi wao kwa muungano na taifa letu na badala yake tunataka kuendeleza ulinzi kupitia vyombo vya ulinzi na usalama kazi ambayo bila ya coercion imeshindikana for 50 years?



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mkuu mchambuzi hapa Tanzania kuna legal manipulations nyingi tu, sio kwenye kulinda muungano tu, nyingine hata zinakwenda kinyume kabisa na katiba yetu, lakini as long as CCM inazipenda zinaangaliwa tu. Lakini uzuri ni kuwa moto ukifukuta kwa muda mrefu, kama usipozimwa vizuri, basi matokeo yake yanakuwa mabaya.

Ukiangalia kwa sasa chokochoko zilizopo kwenye muungano kimsingi zinatokana na uriho wa madaraka wa watu wachache Zanzibar, na hasira ya wachache wa bara kutokana na kauli chafu za baadhi ya wanasiasa wa Zanzibar.

Bila kujali legality ya muungano, ni vizuri tukiangalia sababu ziliofanya uwepo muungano, kwanini Karume na Nyerere walikubaliana kuunganisha nchi wanazoongoza? Hili liwekewe wazi kwanza. Inawezekana kinachoandikwa na kusemwa, sio kilichopo, cha kweli bado wengi hatukijui. Tukikijua ndio tunaweza kukijadili wazi. Kama conditions zimebadilika na zinahitaji ndoa kuvunjika basi ielezwe wazi.

It is very possible that legal manipulations and coercive measures which have been taking place for decades have been done for the greater good.
Mkuu Bongolander ukitazama sample ya maoni ya tume ya Warioba utaona Watanganyika waliotaka serikali 3 ni wengi kuliko wanaotaka 2 au moja. Hii maana yake ni kuwa hakuna kikundi cha Watanganyika wenye hasira, bali kuna kundi ambalo limechoka na pengine kutafuta namna nyingine ya muungano.

Kwa upande wa znz nakubaliana nawe kwasababu upo mgawanyiko mkubwa sana ingawa unafichwa kwa kutumia maneno ya wznz wengi. Ukisoma maoni ya viongozi kama akina Sief Idd, Vuai, Seif Hamad na Jusa utaliona hilo.
Na kwa ukweli kuwa bado wanataka muungano uwe wa serikali 3 au mkataba ni ushahidi kuwa wanautaka muungano ingawa kuna kundi linaweka shinikizo tu.

Hakuna majibu ya kwanini Nyerere na Karume waliamua kuunganisha nchi hizi. Laiti yangekuwepo basi yangewekwa wazi na kundi moja kati ya matatu, kwanza lenye hasira, pili la uroho wa madaraka na tatu kinalosimama katika Pan Africanism.
Hoja za Mchunguzi hapo juu zinaweza kuwa na majibu au jibu.

Kwavile hakuna sababu kinachoonekana sasa hivi ni kama Tanganyika wanajua sababu na hivyo wanadhamana ya kulinda muungano. Ukweli ni kuwa Tanganyika imeubeba muungano kwa muda mrefu bila malalamiko. Hali imebadilika baada ya wznz kutumia fursa ya muungano kama pipi. Kwamba wakilia wanapewa pipi na wao wakalijua hilo.
Pili, Watanganyika kubeba mzigo pamoja na matusi juu. Hilo likajenga chuki.
Na kwavile walikuwa hawelewi mambo mengi na sasa wanayaelewa,uvumilivu umewatoka.

Watanganyika ni wavumilivu na kuwahukumu ni kuwaonea. Imefika mahali wanabeba serikali ya muungano na SMZ kwa pamoja. Maamuzi yanayowahusu Watanganyika inabidi yapate ridhaa BLW. Wanatoa kila wanachoombwa na hata zaidi ya hapo bila wao kunufaika na lolote kiuchumi, kijamii na hata kitamaduni. Kwamba wamekuwa ni donor peke yao, upande wa karume upo wapi?

Imefika mahali Znz wakataka bendera yao, wakataka wimbo wa taifa, serikali, bunge na mahakama. Wakati wakiwa na hivyo, wamekuwa wepesi sana wa kutumia fursa za muungano kwa jina tu bila kuwa na mchango mwingine wakichukua zaidi bila kuwekeza.

Sasa hivi wanataka kiti cha UN na hawataki hata uraia wa Tanzania.
Wanachokitaka ni kile chenye gharama ambacho hawana namna na ndio chanzo cha mkataba.
Hapo Watanganyika wanachaguo gani zaidi?

WZNZ hawataki hata hiyo 3, je nani anapaswa kusima upande wa Karume kwasababu wa Nyerere Watanganyika wamevumilia sana.

Mkuu 'it takes two to tango'. Tanganyika ita tango na nani?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mchambuzi #29
Wana CCM wanaosema serikali 3 ni mzigo hawajaweza kuonyesha mzigo huo ni upi.
Kwasasa hivi kuna kila kitu cha muungano na SMZ.

Yale ya muungano yanabebwa na Tanganyika, uzito wake hauonekani.
Serikali 3 ni kugawana mzigo kila mmoja abebe wake.
Of course bado Tanganyika itabeba mzigo lakini kuna unafuu kwa kiasi kikubwa sana.

Mfano, kuna wizara ya afya ya Tanzania inayomhudumia kila Mtanzania.
Kuna wizara ya afya ya SMZ inayomhudumia mzaznibar tu.
Muundo uliopendekezwa wizara ya afya itakuwa ya Tanganyika na SMZ kivyake.
JMT haitakuwa na wizara ya afya. Gharama zinaongezekaje hapo?
Kwamba kila nchi itawajibika ni kuongeza gharama huko?

Kuna wizara ya elimu ya Tanzania ikiwahusisha wznz na ya SMZ. Muundo unasema JMT haina wizara ya elimu bali kila nchi iwe na wizara yake. Hapo gharama zimeongezaje kwa kila mmoja kubeba jukumu lake?

Hoja kubwa ni kuwa CCM watoke na kuwaeleza watu, serikali 2 zipo miaka 50 na tume zaidi ya 5 zimeundwa matatizo yanazidi, je, kuacha serikali 2 kunaondoaje matatizo yanayojitokeza ambayo ni makubwa kuliko miaka 10 iliyopita.

Ni makubwa kwasababu Tanganyika imevunja ukimya na ipo kwa hatima yoyote.
Nani anaweza kuzima moto huo kwa kutumia bunduki au vifungo vya watu?

Wana CCM wajitokeze kueleza, kiuchumi Tanganyika inafaidika na nini hadi kudhani muungano ni muhimu sana kwa upande wao.

WanaCCM watoke na kuwaeleza Watanganyika gharama za kiuchumi zinazotokana na serikali 2 sasa zitafanywaje ili kuleta utangamano na kuondoa mzigo kwa Mtanganyika.

WanaCCM wajitokeze na waonyeshe hesabu wapi gharama zitakapoongezeka maana tumeanagalia maeneo yote hakuna mahali isipokuwa yapo maeneno yatakayopunguza gharama.

WanaCCM kama Kisumo waeleza baada ya kushindwa miaka 50 kuna kitu gani kipya watakachokifanya kwa maridhiano ya pande mbili, inanyonywa(kwa fikra tu) na inayobeba mzigo( kwa ukweli)

Na wanaCCM watoke watueleze badala ya serikali 2 wao walipendekeza nini na kifanywaje.
 
Daftari la kudumu la wapiga kura liboreshwe kabla ya bunge la katiba
 
ccm walichofanikiwa ni kujenga khoja batili kuwa matatizo ya nchi hii ni mfumo wa idadi za serikali......kwahiyo badala ya kuhoji uwajibikaji tunabakia kuzozana na idadi za serikali ambazo mwishowe ni akina nani wale na akina nani walale njaa. mtu wa kawaida hataathirika na idadi za serikali ziwe moja, mbili tatu au nne...............Kwa lugha ya Moi ni kuwa..............."masufuria yetu hayatajaa ugali na maharagwe kamwe" kwa idadi ya serikali.

Zanzibar itaendelea kujitutumua kuwa wao ni nchi lakini ambayo ipo kwenye makabrasha tu kwani hata bili halisi ya umeme hawawezi kuzilipa...................................ni wavivu hakuna mfano wake.
 
Kulikuwa na sababu tatu za kufanyika kwa muungano husika:
*Kwanza ni Panafricanism spirit.
*Pili Cold War Politics.
*Tatu, kuleta utulivu wa kisiasa kufuatia mapinduzi.

Mchambuzi kama kweli hizi ndio sababu za muungano naweza kusema zilikuwa weak sana. Lakini nina wasiwasi sana na muungano as per articles of union, bado sijui how much was US was involved in it and for what reason, if any. Lakini kama hizo sababu tatu kweli ndio sababu za muungano, haukufaa wakati ule, haufai sasa na hautafaa kamwe. Inawezekana kuwa Tanganyika has wasted alot for that.

Kwa upande wa bara sioni kama kuna issue sana kuwa nje ya muungano, hasa ukizingatia watu kama Seif Sharif Hamad wanaona kuwa Zanzibar si part ya Afrika ni part ya arabuni, better let them be
 
...

Kwa upande wa znz nakubaliana nawe kwasababu upo mgawanyiko mkubwa sana ingawa unafichwa kwa kutumia maneno ya wznz wengi. Ukisoma maoni ya viongozi kama akina Sief Idd, Vuai, Seif Hamad na Jusa utaliona hilo.
Na kwa ukweli kuwa bado wanataka muungano uwe wa serikali 3 au mkataba ni ushahidi kuwa wanautaka muungano ingawa kuna kundi linaweka shinikizo tu.

...

Mkuu, kwa heshima na taadhima, hapo kwenye red. Unaweza ukawa sahihi au usiwe sahihi.

Tatizo wahafidhina wa CCM wameugeuza huu muungano kama kama kitu kisichotakiwa kuhojiwa na wananchi. Kwa CCM, pengine baada ya vitabu vitukufu, kinachofuata kwa utukufu ni Muungano. Pengine ndio maana hata sheria ya mabadiliko ya Katiba haikutoa uhuru wa kutosha kwa wananchi kuujadili muungano kwamba sharti mojawapo liwe "kuulinda muungano".

So, katika mazingira kama hayo wanasiasa uliowataja (na wengineo) hawana option, hata kama HAWAUTAKI MUUNGANO, inakuwa vigumu kwao kuwa wawazi na badala yake wanajiegemeza kwenye vijisababu kama "muungano wa mkataba" na vinginevyo. Mkuu, nani haogopi "kesi ya uhaini"?

The best option, kama ambavyo ilishawahi kujadiliwa humu, ilitakiwa wanachi waulizwe, right from beginning; wanautaka muungano? Kama ndio, muungano wa aina gani? Baada ya majibu hayo, mchakato wa Katiba Mpya ya JMT ungefuata lakini bahati mbaya hilo halikufanyika.

Hivyo, kama wananchi hawatapewa wanachokitika kwa maana ya muundo wa muungano, I can see, agenda ya muungano itaendelea kuwa agenda ya kudumu miaka nenda miaka rudi na huenda ikatupelekea siko kama taifa.
 
Kuna hoja ya kwamba waliotoa maoni katika rasimu ya katiba mpya ni wachache kwa kulinganisha na idadi ya watanzania na kwahiyo vyama viruhusiwe kuchakachua rasimu ya katiba. Jamani mbona wakati wa uchaguzi wanaopiga kura ni wachache na kwahiyo kura za ushindi ni chache zaidi kwa kulinganisha na idadi ya watanzania na hatubishi! Tuheshimu utaratibu wa kidemokrasia tunaojiwekea na tusiwe na "double Standards". Kinachofanyika sasa ni kampeni ya vyama vya siasa ku-indoctrinate wananchi wafuate matakwa yao (yaani wananchi kwa ujumla wao na vyama vikiwamo hawana akili tosha). Angalizo kali hapa ni pale watakapo badili yaliyomo katika rasimu ya Katiba Mpya na kuifanya isiwe katiba iliyotokana na maoni ya watu bali ya kundi fulani sawa hii tuliyonayo ambayo, pamoja na uzuri wake, haina uhalali rasmi kwa sababu inatokana na serikali ya chama tawala. Mwisho tutarudi kule kule baada ya gharama yote hii kutumika.
Pili kuna hili kwamba kura za maoni zisipokidhi vigezo zinaweza kupelekea katiba ya sasa ikaendelea. Hili likitokea ni uongozi utakuwa umeshindwa kutuongoza kufikia lengo la kuwa na katiba mpya. Hainingii akilini kwamba kura za maoni zikatae mabadiliko yote katika rasimu isipokuwa pale ambapo muundo (format) wa kutafuta/kupiga kura uwe umeundwa kulenga hilo litokee, yaani tutakavyo takiwa kujibu wakati wa kura kuhusu rasimu. Format isiruhusu hili kutokea na haipashwi kutokea kama rasimu imetokana na maoni ya watu.
 
Wakuu Nguruvi3, Bongolander,

Kuhusiana na hidden agenda juu ya muungano, hoja ya msingi ni kwamba muungano ulizaliwa katika kipindi ambacho kulikuwa na mjadala mkali juu ya panafricanism na kwa upande mwingine, dunia ilikuwa inapita katika thickness of the cold war. Be what it may, its is quite obvious kwamba birthmark ya muungano wetu hadi leo inabebwa na cold war kuliko panafricanism au kitu kingine chochote.

Iwapo tupo sawa hadi hapo, nadhani pia tutakubaliana kwamba muungano wetu is the only living and surviving example ya "political association" miongoni mwa sovereign states barani africa. Mkazo hapa ni "political association - suala ambalo miaka 50 baadae bado linawapa wakati mgumu sana viongozi wa nchi huru za africa kufanikisha a true political federation". Hata kwa dunia nzima, hilo limefanikiwa sehemu chache sana kama marekani na kwingine. Kutokana na hili, ni kawaida kwa watu to cite muungano wetu kama mfano wa panafricanist unity au mfano wa its failure. Swali linalofuatia ni je:

*Should our union pamoja na structure yake be cited as an exemplar of panafricanist unity? CCM wapo tayari kabisa kwa dhati kutetea hilo as we head towards regional integration?

Binafsi nadhani muungano wa aina hii is a threat to all countries in the region that wish to pursue ndoto ya mwalimu on panafricanism based on an incremental approach (kupitia regional blocks kwanza kabla ya bara zima kuungana unlike Nkrumah ambae alitaka a fast track/radical approach. Kwa mtazamo wangu, muungano wetu is an illustration of CCM's failure to move forward the panafricanism agenda na kuwa mfano wa kuigwa barani africa.

Mwalimu nyerere was a visionary leader, no doubt, na kama ilivyo kwa visionaries wote, legacy yake ipo kwenye vision kuliko practice. As it has been argued "vision inspires, practice teaches". Miaka 50 ya muungano, ccm can no longer inspire us given mwalimu's vision, lakini muhimu zaidi, watanganyika have learnt through practice. As Nguruvi3 puts it rightly, enough is enough.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Makucha,
Bandiko #38 una hoja ya msingi kuhusiana na uwezekano wa kura ya maoni kuturudisha kwenye katiba ya zamani. Kura ya maoni ni vizuri tuitazame in relative terms (pande zote za muungano) sio absolute terms (kwa Tanganyika tu). Nasema hivi kwa sababu naamini kwamba kuchakachua kura ya maoni upande wa zanzibar itakuwa ngumu kwani kule tayari msimamo wao unaeleweka tofauti na tanzania bara ambapo bado kuna loopholes za kuchezea iwapo nia itakuwa ni kuaminisha umma kwamba watanganyika wengi wameamua otherwise.

Nikijikita na upande wa zanzibar - wakati tume ya warioba inakusanya maoni ya wananchi znz, tume ilibaini kwamba haitakuwa rahisi tena kubadili katiba ya znz kuifanya znz kuonekana kuwa sehemu ya jamhuri ya muungano badala ya kuwa sura ya nchi kamili. Mabadiliko hayo - yani ya kutoitambua znz kama moja ya nchi shiriki za muungano yatahitaji tena kura ya maoni na ni dhahiri matokeo yake yatapinga hilo kwa nguvu kubwa. Na ndio maana kwa tathmini ya tume ya warioba kufuatia kusikiliza maoni ya wa znz, ikawa dhahiri kwamba pendekezo la kuifanya znz isionekane kama moja ya nchi shiriki za muungano litapingwa vikali kwenye kura ya maoni.

Kwa maana hii, iwapo kura ya maoni upande wa bara itakataa kurudi kwa Tanganyika na kutufanya tuendelee na katiba ya mwaka 1977, katiba ya zanzibar itakuwa ni supreme kwa katiba ya 1977 na maamuzi mengi juu ya maisha ya watanganyika yatategemea BLW linaamua nini. Hali hii italeta machafuko makubwa upande wa bara na sasa kuzaa "usisi na uwao" na hatimaye kuvunja muungano. Kwa maana hii, hatima ya muungano ipo mikononi mwa ccm, hasa viongozi wakaidi kama nilivyojadili kwenye bandiko #1 . Ni muhimu wakaacha kutumia visingizio vingine vya kisiasa na pia kushutumu tume ya warioba wakati chanzo cha mgogoro wa muungano kwa miaka 50 sasa ni msimamo wa CCM na chanzo cha kuvunjika kwa muungano itakuwa ni msimamo huo huo wa ccm.






Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom