Ritz
JF-Expert Member
- Jan 1, 2011
- 54,406
- 43,740
Mkuu gombesuguHuyo Mchambuzi wako analeta thread/mnakasha ambao ndani yake pana elements/pattern ya kuhalalisha na ku-justify ule uharamia woote wa Nyerere na jinsi alivyotuadhibu Watanzania chini ya ile One Party Communist almost Juche System...khalafu wewe unangia hapa na kumwambia aondoke!? Aende wapi sasa!?
Hivi nyinyi Chadema mna maarifa japo kiduchu ya kuazima!?
Kwa mfano Mkuu Mchambuzi anajaribu kutuaminisha yakuwa ati wakti wa Mwalimu aka "Baba wa Taifa"...ya kwamba baadhi ya sababu kadhaa zilohalalisha ile Katiba ya kinyama ya wakti ule na kumfanza Nyerere bado awe "Halali"...ametaja ati ni Azimio la Arusha na uwepo wa ati wale alowaita ndo popular and Charismatic Leaders kama vile Nyerere!? Looh!
Sasa embu tupeni majina ya hao Viongozi walokua/waliowahi ati ndo kupendwa na Wananchi wakti,au ndo mna maana ya yule Nyerere!? Duh!
Kama kwa sifa za aina hiyo...hata Hitler,Kim Il Sung na Family yake,Saddam Hussein na Hafidh Al Assad mbona hawa woote nao walikua ni popular and charismatic Leaders!?
Hao Viongozi madhalimu woote,nao kama Nyerere tu yaani hawakuwa na tafauti kubwa mno! Na kwenye chaguzi takriban zoote ndani ya nchi zao,nao pia kama vile yule Nyerere...walikua wakipata taakriban 80-90% ya Kura!? Duh!
Badala ya Mkuu Mchambuzi kujaribu kuudanganya umma wa Watanzania na ulimwengu ati yakuwa wakti wa utawala wa kidhalimu wa yule Nyerere,Watanzania walikua Loyal!? Looh!
Kwanini hamtaki kusema kweli yakuwa wakti huo Wananchi/Watanzania woote walikua hawana option yoyote maskini dhidi ya utawala wa kimabavu wa yule Nyerere!?
Nafikiri yeye Nyerere ndo Kiongozi pekee katika nchi yetu alofanziwa majaribio ya kutaka kumpindua zaidi ya mara tatu,kama sikosei!? Sasa hiyo Loyalty asemayo huyo ajiitae ndo Mchambuzi iwapi hapo!?
Nafahamu kwa yakini yakuwa Mkuu Mchambuzi na takriban hao wenzie nyoote alowa-tag kwenye hii thread/mnakasha ni wenye mwelekeo,lengo,madhumuni na mtazamo mmoja naye! Si kitu kibaya mno,ndo maana hapa jamvini hazitakuwapo hoja zenye maana...sababu upinzani khalis hautakuwapo asilan,abadan!!
Nimechungulia baadhi ya michango ya Wanajamvi wenye kujimudu kimaarifa japo kiduchu hapa jamvini...si weye pimbi ujiitae Parameter lakini!
Kwa kifupi nimehuzunika kiduchu!
Ukiangalia kiundani,wachangiaji woote mnamsifia yule Dictator Nyerere na utawala wake dhalim na kujaribu kumchafua mtu kama Rais wenu wa sasa Dr Kikwete...ambae katika kipindi kifupi mno cha utawala wake...pamoja na tafran na changamoto zoote zinazomkabili lakini amejitahidi mno kuimarisha mojawapao ya mambo makubwa vitu kama Democratic Institutions,freedom of speech and freedom of expression!
Nani alithubutu hata kuviota vitu kama hivyo wakti wa yule Nyerere!?
Mnaweza vipi nyinyi maharamia wa hoja,kuthubutu kuchangia tena ati kwa kuhalalisha makosa na nakma zoote yule Nyerere alizowafanzia Watanzania...lakini kwa unafiki ulotamalaki ndani ya nyoyo zenu,ati mnajaribu kuichafua CCM na Rais Dr Kikwete!? Looh!
Embu jaribuni kuwa objective na impartial japo kiduchu...kama kweli mwahitaji wangine wachangie kitaaluma na kuleta mazungumzo yenye uzalendo na tija kwa Taifa letu hili changa!
Yawaje leo hiyo CCM na Kikwete ati ndo wawe wabaya na history na Katiba yoote mwajaribu kuionyesha mapungufu makubwa!...kitu ambacho ni kweli,yaani kwa hili nakubaliana nanyi!?
Sasa yawezekana vipi hapa huyo Nyerere awe exonorated na asihusishwe/asizungumzwe kimapungufu kwayo au na huo muonao nyinyi yakuwa ndo uchafu/mapungufu ya hiyo CCM na hata chimbuko la haya yoote Taifa letu lipitiamo leo hii!? Kwani yeye Nyerere si ndo alokua mwasisi na mwandishi wa hiyo CCM na Pia Katiba iliyopo!?
Au kama si hivyo yakhusu nini basi nyinyi mum-glorify and/or glamourise kula kukacha mpaka kufikia kumwita ati Baba wa Taifa"!?
Nyinyi nyoote mkitajiwa tu yule Nyerere,hata kwa hoja zenye ukweli yakinifu...kwanini mwaruka Kimanga mpaka Salalah! Teeh! Teeh! Teeh!
Nimemsoma huyo Mchambuzi...ati anajaribu kutuhadaa hapa jamvini yakuwa mojawapo ya sifa kubwa za yule Nyerere ati alikua ni Pan-Afrikanist!? Looh!
Nyerere si ndo yule yule alionyesha ile Non Pan-Afrikanist views at International arenas/hadharani kwenye ule mgogoro wa Biafra...na mpaka kufikia kuingiza nchi yetu changa kwenye ule mgogoro mkali wa Nigeria...na kututia dosari la kuonekana Wazandiki na Wanafiki!?
Nguruvi3...anafahamu kiundani kabisa jinsi gani yule hasidi Nyerere alivyochangia kiundani kwa njia moja amma nyangine kuudhoofisha na mwishowe kuutokomeza ule Muungano wa awali hapo East Afrika-EAC!?
Sina haja asilan ya kujichosha mno kwa kutaja udhaifu na madhila kadhaa ili tujikumbushe tulipotoka na tusiwe wivi wa shukran.
Sasa kabla sijataja mangi kiundani...kwa hayo mawili kiduchu tu,kwanini mnajaribu kutuaminisha yakuwa huyo Nyerere ati alikua na sifa za Pan-Afrikanist!?
Nyerere alikua haamini asilan katika democratic institutions,democracy itself,freedom of speech/experssion...hii ni open secret kwenye World corridors of Politics...yaani kila mwenye akili na maarifa yake timamu anafahamu hili jambo!
Nyerere si ndo huyu huyu alokwenda kumsaidia yule haramia Albert Rene pale Seychelles(someone who was already implicated on systematic tortures and other Human Right abuses!) ili aendelee kuketi madarakani pale Seychelles...na Tanzania ikapeleka mpaka majeshi-JWZT kwa amri ya yule Nyerere!! Duh!
Kwa kifupi...Nyerere hakuwa intellectual capable wala hakuwa na integrity ya kupambana na nyakati/dunia mpya...yaani kwa kumsifia japo kiduchu,alishatambua yakuwa Watanzania tayari wameshaamka na wana fikara/mwamko mpya tena usio na woga asilan!
Kwa hiyo nyoote acheni au punguzeni kutuaminisha yakuwa ati Nyerere...aliamua tu kuachia kiti/nchi kwa mapenzi yake ya nchi/Taifa na Watanzania wenzie,au ati alikua akipenda/kuabudu mno Demokrasia!? Duh! Teeh! Teeh! Teeh!
Kwa kifupi...endeleeni tu na huo mchakato wenu wa Katiba hapa jamvini,lakini kila mtakapokua mwasema urongo,basi sisi tutakua twajawarekebisha kiduchu na kwenda zetu!
La si hivyo...yaani ikiwa twakaa tu kimya itakua hatuwatendei haki Watanzania wenzetu wangine,na pia itakua hata nyinyi pia hatukupendeni!? Maana akupendae ni yule akwambiae kweli!
Ahsantani sana!
Hii bayana yako ni ulimbo tosha, ninaamini kabisa watu wamefyonza Ilm.
Last edited by a moderator: