Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,434
- Thread starter
- #41
Nguruvi3, Rutashubanyuma dudus, Makucha
CCM bado ina amini kwamba bado inaweza kufanya ukarabati mkubwa wa mfumo wa serikali mbili. Ni vigumu kuelewa kama ukarabati huo utafanywa na mchina au nani, lakini kilicho dhahiri ni kwamba given the history, legal and political foundations na maamuzi ya znz kwa mujibu wa katiba yake ya 2010, CCM inapoteza tu muda kudanganya wananchi, pengine for political expediency.
Nguruvi3 alitaka kujua hoja za ccm juu ya faida ya serikali mbili. Ebu tujaribu kulitazama hilo, katika muktadha wa ukarabati wa kichina to sustain serikali mbili:
Maeneo mawili makubwa yatahitaji mabadiliko: kwanza ni kuwa na mambo ya kutosha kwenye orodha ya ya muungano including issues za economy and development. Lakini hili likifanyika, matokeo yake ni kuzidisha malalamiko kwa wazanzibari kwamba hadhi na utambulisho wao kama taifa unapotea. Kwa upande mwingine, ukarabati uki involve kupunguza mambo mengi ya muungano, serikali ya muungano itaishia kushughulika zaidi na mambo ya Tanganyika, na katika hili, zanzibar itaona kwamba Tanganyika ndio muungano wenyewe. Lakini vile vile given mwamko wa watanganyika hivi leo, watanganyika nao wataona si haki nao wasiwe na uhuru wa kuendesha mambo yao kama ilivyo kwa zanzibar.
Eneo la pili linalo hitaji ukarabati wa kichina ili to sustain serikali mbili utahitaji:
Kuondoa mgongano na mgogoro wa kikatiba. Hapa maana yake ni kwamba Zanzibar kubadili katiba yake ili Tanganyika na zanzibar ziwe ni sehemu za nchi moja badala ya kuwa nchi kamili shiriki za muungano. Iwapo Tanganyika na zanzibar zitakuwa ni nchi kamili, haitawezekana kwa nchi moja kuwa na hadhi na uhuru wake na kuacha nchi nyingine isiwe na hadhi and autonomy yake.
Kwa kutazama haya mawili, ukarabati wa kichina wa ccm kwa muungano utakuwa ni mgumu. Ni kwa mantiki hii, solution pekee ni serikali tatu ili kila upande uwe na hadhi sawa ambapo kila upande utashughulikia mambo nje ya muungano huku serikali ya muungano ikibaki na machache ambayo yanaunganisha Taifa. Nje ya hapo, kama alivyopata tamka Nguruvi3, tuvunje jahazi na kila mtu achukue mbao zake, vinginevyo tutaingia kwenye machafuko.
Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
CCM bado ina amini kwamba bado inaweza kufanya ukarabati mkubwa wa mfumo wa serikali mbili. Ni vigumu kuelewa kama ukarabati huo utafanywa na mchina au nani, lakini kilicho dhahiri ni kwamba given the history, legal and political foundations na maamuzi ya znz kwa mujibu wa katiba yake ya 2010, CCM inapoteza tu muda kudanganya wananchi, pengine for political expediency.
Nguruvi3 alitaka kujua hoja za ccm juu ya faida ya serikali mbili. Ebu tujaribu kulitazama hilo, katika muktadha wa ukarabati wa kichina to sustain serikali mbili:
Maeneo mawili makubwa yatahitaji mabadiliko: kwanza ni kuwa na mambo ya kutosha kwenye orodha ya ya muungano including issues za economy and development. Lakini hili likifanyika, matokeo yake ni kuzidisha malalamiko kwa wazanzibari kwamba hadhi na utambulisho wao kama taifa unapotea. Kwa upande mwingine, ukarabati uki involve kupunguza mambo mengi ya muungano, serikali ya muungano itaishia kushughulika zaidi na mambo ya Tanganyika, na katika hili, zanzibar itaona kwamba Tanganyika ndio muungano wenyewe. Lakini vile vile given mwamko wa watanganyika hivi leo, watanganyika nao wataona si haki nao wasiwe na uhuru wa kuendesha mambo yao kama ilivyo kwa zanzibar.
Eneo la pili linalo hitaji ukarabati wa kichina ili to sustain serikali mbili utahitaji:
Kuondoa mgongano na mgogoro wa kikatiba. Hapa maana yake ni kwamba Zanzibar kubadili katiba yake ili Tanganyika na zanzibar ziwe ni sehemu za nchi moja badala ya kuwa nchi kamili shiriki za muungano. Iwapo Tanganyika na zanzibar zitakuwa ni nchi kamili, haitawezekana kwa nchi moja kuwa na hadhi na uhuru wake na kuacha nchi nyingine isiwe na hadhi and autonomy yake.
Kwa kutazama haya mawili, ukarabati wa kichina wa ccm kwa muungano utakuwa ni mgumu. Ni kwa mantiki hii, solution pekee ni serikali tatu ili kila upande uwe na hadhi sawa ambapo kila upande utashughulikia mambo nje ya muungano huku serikali ya muungano ikibaki na machache ambayo yanaunganisha Taifa. Nje ya hapo, kama alivyopata tamka Nguruvi3, tuvunje jahazi na kila mtu achukue mbao zake, vinginevyo tutaingia kwenye machafuko.
Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Last edited by a moderator: