CCM na Hatima Ya Bunge La Katiba

CCM na Hatima Ya Bunge La Katiba

Hivi kwa nini watu wengine hawawezi kujadili hoja bila kuweka matakataka kama hayaaa (highlighted)!!!!!!! Du!! mambo ya aibu kabisa!!!!! taratibu mada inataka kugeuzwa.....

Sasa naona unataka kuuchafua huu uzi sio lazima kuchangia unaweza kubaki kuwa msomaji tu.

Lakini sio makosa yako inavyoonekana unaakili ya kuvuka barabara tu ili usigongwe na gari.

Hiyo habari ya kadinali Pengo hujaiona huku kwenye jukwaa la siasa au unajitoa ufahamu?

Au ndio zile sera musichanganye dini na siasa lakini upande mwingine ruksa kuchanganya dini siasa?
 
Asante sana Mchambuzi kwa tathmini hii. Ninaamini wengi kati ya wale wanaopiga kelele sana kuhusu mchakato wa Katiba Mpya na Serikali Mbili hawayajui haya, na pengine hata hawana uwezo wa kuyasoma na kuyaelewa. Ni ukweli mtupu ya kuwa waasisi wa Muungano Mwalimu Nyerere na Abeid Karume waliutengeneza Muungano kutokana na changamoto zilizokuwepo 1964, na waliuandaa mpango mzima kwa siri kubwa. Hata Abdulrahman Babu na Kassim Hanga hawakujua kitu gani kilikuwa kinaendelea. Kwa taarifa zilizopo ni kwamba walipewa salamu maalum za kupeleka China na Urusi. Wanafika huko walikokuwa wanatakiwa kwenda wanasikia BBC ya kuwa Tanganyika na Zanzibar zimeungana, ilikuwa changa la macho, ili wasije wakaleta maswali ambayo waasisi walikuwa hawana majibu.

Kwa sasa, miaka takriban 50 tangu kuundwa kwa Muungano, nyufa zimeanza kuonekana. Watanzania wa leo katika pande zote mbili wana maswali na matakwa yao ambayo yameshindwa kupatiwa ufumbuzi kupitia mfumo huu uliopo. Kwa mtu yeyote yule kutaka kulazimisha matakwa yake leo, kama walivyoweza kufanya waasisi wetu miaka karibia 50 iliyopita ni kujidanganya. Hata kama waasisi wa Muungano wangekuwa hai leo hii, ninaamini kabisa wasingeweza kuwaziba macho, masikio na midomo wananchi na kusema tunavyotaka sisi ndivyo itakavyokuwa. Changamoto za dunia zimebadilika, changamoto za ndani ya nchi zimebadilika, uwezo na upeo wa wananchi kuchanganua na kutoa mawazo yao umeongezeka, kwa kifupi watanzania wa leo sio wale wa 1964. Na ndiyo sababu katika hatua tuliyopo inabidi sote tushiriki kuipata Katiba tunayoikubali, ili tupate mfumo wa Serikali itakayoweza kukubalika na kutufanyia kazi sisi wananchi tunaoiweka madarakani. Huu sio wakati wa kutishana na kuambiwa 'Mtake, msitake, Katiba mpya itakuwa ya Serikali Mbili...'

Picha ama dhana aliyokuwa nayo Mwalimu ya kuwa na Serikali Mbili hapo awali iliweza kufanya kazi 1964. Ilipofika miaka ya sabini hata yeye alianza kuyaona mapungufu ya muundo huo, na akasimamia kuunganisha TANU na ASP mwaka 1977 na kuunda CCM kwa kuona kama hatua muhimu kuelekea kwenye serikali moja (?) Hata hivyo baada ya kuingia kwa mfumo wa vyama vingi, zoezi la kuendelea na mchakato wa kuziunganisha nchi hizi mbili ukarudi nyuma, hatukufanya mambo muhimu tuliyokuwa tunapaswa kuyafanya wakati ule ikiwa ni pamoja na kuunda Katiba Mpya, matokeo yake tumefikia mahali ambapo tunayumbishwa kutoka kila pembe, mvutano ndani ya chama tawala, mivutano kati ya vyama mbalimbali, mivutano kati ya Zanzibar na Tanzania Bara (?) na hata mivutano kati ya Zanzibar na Pemba. Tusipotuliza vichwa vyetu na kufanya maamuzi ya bsara ambayo kwa asilimia kubwa yatakuwa maamuzi ya walio wengi, hapatabaki Tanzania. Kwa kifupi siamini kama Tanzania itabaki kama watanganyika ambao ni wengi hawatasikilizwa matakwa yao!
 
Mkuu Mchambuzi nimekusoma hoja yako, kwa vile suala la katiba mpya halijawahi kuwepo kwenye ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi, lakini JK ameuanza mchakato bila kuihusisha CCM, then watairidhia katiba ya serikali tatu katika udharura ule ule ule wa kuanzishwa kwa mchakato huu , bila mabadiliko yoyote ya sera zao kisha ndio watabadili sera zao!.
Pasco.
 
Asante sana Mchambuzi kwa tathmini hii. Ninaamini wengi kati ya wale wanaopiga kelele sana kuhusu mchakato wa Katiba Mpya na Serikali Mbili hawayajui haya, na pengine hata hawana uwezo wa kuyasoma na kuyaelewa. Ni ukweli mtupu ya kuwa waasisi wa Muungano Mwalimu Nyerere na Abeid Karume waliutengeneza Muungano kutokana na changamoto zilizokuwepo 1964, na waliuandaa mpango mzima kwa siri kubwa. Hata Abdulrahman Babu na Kassim Hanga hawakujua kitu gani kilikuwa kinaendelea. Kwa taarifa zilizopo ni kwamba walipewa salamu maalum za kupeleka China na Urusi. Wanafika huko walikokuwa wanatakiwa kwenda wanasikia BBC ya kuwa Tanganyika na Zanzibar zimeungana, ilikuwa changa la macho, ili wasije wakaleta maswali ambayo waasisi walikuwa hawana majibu.

Kwa sasa, miaka takriban 50 tangu kuundwa kwa Muungano, nyufa zimeanza kuonekana. Watanzania wa leo katika pande zote mbili wana maswali na matakwa yao ambayo yameshindwa kupatiwa ufumbuzi kupitia mfumo huu uliopo. Kwa mtu yeyote yule kutaka kulazimisha matakwa yake leo, kama walivyoweza kufanya waasisi wetu miaka karibia 50 iliyopita ni kujidanganya. Hata kama waasisi wa Muungano wangekuwa hai leo hii, ninaamini kabisa wasingeweza kuwaziba macho, masikio na midomo wananchi na kusema tunavyotaka sisi ndivyo itakavyokuwa. Changamoto za dunia zimebadilika, changamoto za ndani ya nchi zimebadilika, uwezo na upeo wa wananchi kuchanganua na kutoa mawazo yao umeongezeka, kwa kifupi watanzania wa leo sio wale wa 1964. Na ndiyo sababu katika hatua tuliyopo inabidi sote tushiriki kuipata Katiba tunayoikubali, ili tupate mfumo wa Serikali itakayoweza kukubalika na kutufanyia kazi sisi wananchi tunaoiweka madarakani. Huu sio wakati wa kutishana na kuambiwa 'Mtake, msitake, Katiba mpya itakuwa ya Serikali Mbili...'

Picha ama dhana aliyokuwa nayo Mwalimu ya kuwa na Serikali Mbili hapo awali iliweza kufanya kazi 1964. Ilipofika miaka ya sabini hata yeye alianza kuyaona mapungufu ya muundo huo, na akasimamia kuunganisha TANU na ASP mwaka 1977 na kuunda CCM kwa kuona kama hatua muhimu kuelekea kwenye serikali moja (?) Hata hivyo baada ya kuingia kwa mfumo wa vyama vingi, zoezi la kuendelea na mchakato wa kuziunganisha nchi hizi mbili ukarudi nyuma, hatukufanya mambo muhimu tuliyokuwa tunapaswa kuyafanya wakati ule ikiwa ni pamoja na kuunda Katiba Mpya, matokeo yake tumefikia mahali ambapo tunayumbishwa kutoka kila pembe, mvutano ndani ya chama tawala, mivutano kati ya vyama mbalimbali, mivutano kati ya Zanzibar na Tanzania Bara (?) na hata mivutano kati ya Zanzibar na Pemba. Tusipotuliza vichwa vyetu na kufanya maamuzi ya bsara ambayo kwa asilimia kubwa yatakuwa maamuzi ya walio wengi, hapatabaki Tanzania. Kwa kifupi siamini kama Tanzania itabaki kama watanganyika ambao ni wengi hawatasikilizwa matakwa yao!

Hiyo paragraph yenye wekundu ndio inaeleza kwa ufasaha jinsi kama nchi tulipoteleza na kupotea kuelekea vision ya nchi hizi mbili zilizoungana kushindwa kusonga mbele na kuwa nchi moja!! Badala ya kufanya mchakato wa katiba ambayo ingezileta hizi nchi mbili karibu zaidi ; marebisho ya katiba yakafanywa ambayo yalizitenga hizi nchi zaidi, kwa mfano kiongozi wa Zanzibar kutolewa kutokuwa makamu wa rais wa Muungano lilikuwa ni kosa kubwa ambalo halikuimalisha umoja!! Wazanzibar toka wakati huo wakajiona kama vile wanatengwa na wabara na kelele za kutaka mamlaka yao na mpaka kufanya marekebisho ya katiba yao ndio yakashika kasi!!!

Hapa tulipofika sasa juhudi zozote zitakazofanywa kama tunataka MUUNGANO wa kweli zilenge kuleta umoja na ushirikiano zaidi katika nyanja mbalimbali katika mfumo utakaokubaliwa hata kama ni wa mamlaka tatu!!
 
Mkuu Mchambuzi nimekusoma hoja yako, kwa vile suala la katiba mpya halijawahi kuwepo kwenye ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi, lakini JK ameuanza mchakato bila kuihusisha CCM, then watairidhia katiba ya serikali tatu katika udharura ule ule ule wa kuanzishwa kwa mchakato huu , bila mabadiliko yoyote ya sera zao kisha ndio watabadili sera zao!.
Pasco.
Mkuu Pasco,
Nimeshindwa kukupata vizuri. Je unajaribu kutueleza nini kitajiri kwa taarifa ulizonazo au hii ni kwa jinsi unavyo hypothesize?


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:


Kwanza nataka nikutahadharishe kitu kimoja, Unapo jadili na mimi Tafadhali usiingize mwingine ktk haya malumbano, unless unataka KUCHAFUA HUU UZI,

Unasema wewe umewapa mbinu WAZANZIBARI ZA KILA NAMNA ILI WAFANIKISHE HIO AZMA YAO, NAKUULIZA WEWE @nguruvi3 NANI KAKUOMBA HUO MSAADA?? Na wewe kama NANI wa kuwapa wazanzibari mbinu??
Hichi mi nakiita kiherehere! na upashkuna wa kucheza ngoma si yako!

Pili unasema MUUNGANO UNAKUATHIRI!

Hebu nijuze kidogo, wewe mbondei wa segera, na yule mpemba wa chake ANAE ATHIRIKA NA MUUNGANO HASA NI NANI?? Mbona Unatoa kauli bila kufikiri ndugu! AU ndio namna ya kutafuta sympathy kwa wanajukwaa??

Unantajia hao wajiitao waznz kuwa wametamka kuwa HUO MUUNGANO WANAUHITAJI, Na sababu pekee ulioirudia mara kwa mara ni KUTAKA ULINZI NA USALAMA! Nakuuliza Hao waznzibari Huo ulinzi wanaoutaka ni kwa kumhofu nani hasa??
au UNAMAANISHA wakijitenga Tanganyika Itawavamia??

Zanzibar adui yake ni TANGANYIKA! Na hakuna mwingine! Tena huyo Tanganyika NDANI YA MFUMO KRISTO!

Hao wanafiki wasemao kuwa ZNZBR Inahitaji Tanganyika kuilinda NI VIBARAKA TU AMBAO WAMEWEKWA HAPO KWA MASLAHI! Na hio ndio fikra ya wazanzibari wengi.

Hakuna hapo TZ asiyejua kuwa asilimia 99% ya WAZANZIBARI HAWATAKI MUUNGANO, Hao uliwataja hapo juu, ni ktk wale BLACK SHEEP, ambao ktk kila kundi la waungwana HUTOWAKOSA!

Wazanzibari Hawahitaji mtu kama wewe na Pasco kuwatetea kinafiki, na wakati huo huo Mnapenyeza maneno ya kuwadhalilisha na kuwaona hawanba maana sana!

na istoshe kwa mtu mwenye Upeo wa kawaida tu wa kufikiri akisoma mabango yako na yule mwenzako Pasco, Atagundua 100% kuwa NYINYI SIO WAPENDA HAKI HATTA KIDOGO! Bali ni watu wa kujaribu kupotosha ukweli halisi na kupenyeza propoganda za NYERERE {Mnajifanya kuuma huku mnapuliza.} huo unaitwa UNAFIKI. na ni mbaya kuliko UCHAWI.

WAZANZIBARI HAWAKUHITAJI WEWE WALA MTANGANYIKA YOYOTE KUWASAIDIA KUPIGANIA HAKI ZAKO,TENA HASSA WALE WALIO NDANI YA HUO MFUMO KRISTO!

Wewe kama ni mpenda haki, basi support KILE WANACHODAI WAZANZIBARI, Na SIO kujifanya kuwapa mbinu zako zisizo na mashiko.

Wapi ULIONA FISI AKAMFUNDISHA MBUZI JINSI YA KUTOROKA KWENYE JELA YA FISI WENZAKE??

NA mwisho!Labda lugha inakupa tabu kidogo MI SINA HAJA YA KUKUTISHA WEWE! bali nimekutahadharisha kuwa NAKUTAZAMA UNAVYOMWAGA PUMBA HAPA JUKWAANI UKIZIITA, "MAWAZO YANGU BINAFSI"!

Sasa Kila UTOAPO mawazo MABOVU basi uwe tayari KUKOSOLEWA! Na sio kunikaribisha kwako unipe panga!

Mi nimpige panga mtu mwenyewe yuko njia moja??

ILANI.
Shika heshima yako kuingiza jina la mzee Mohamed said ktk maongezi yangu mi na wewe, au sasa hivi utachukia huu uzi
!
Nimekusoma na wengine wamekusoma.Ahsante
 
Mkuu Pasco,
Nimeshindwa kukupata vizuri. Je unajaribu kutueleza nini kitajiri kwa taarifa ulizonazo au hii ni kwa jinsi unavyo hypothesize?


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Mchambuzi
Binafsi si weye pekee! mie mara zote hupata tabu sana kwa mijadala inavyokuwa inakuja na uchangizi wa Pasco.

Na mara aezaleta mwenyewe uzi na akaleta majibu potofu/ hata kushindwa utetea kile alichokiamini na kutushirikisha.

Ukimuuliza kwanini umeleta kitu kama hiki mbona hakipo sahihi..?! Akuambia kwasababu nami nimekikuta na nikaamua kukileta.

Wamuuliza tena, kwa taaluma yako ati ya uandishi tena waongeza "mahiri" ndivyo inakuruhusu kuokota vitu na kuleta hapa bila hata kujihoji mwenyewe kama mwanataaluma? Sasa mie hupata tabu sana juu ya mambo yake.

Pasco usinielewe vibaya kwa neno hili "HIYO NI TABIA YA KUNGURU", yeye hajali hujizolea kila akionacho hajali wana hana wa kuuliza.

Mchambuzi,
Labda tuzidi subiri huenda ana watu na watu wa kukujibu...!
 
Last edited by a moderator:
Wengi wapi unawaZungumzia wewe mwenzetu!? Ni wananchi elfu 37 au bunge la katiba watu mia sita?

Maneno meeengi lakini point yako hapa tukubali serikali tatu.lakini haya mambo huwezi kulazimisha,litakoloamliwa na wengi ndo hilohilo.
 
Mkuu Pasco,
Nimeshindwa kukupata vizuri. Je unajaribu kutueleza nini kitajiri kwa taarifa ulizonazo au hii ni kwa jinsi unavyo hypothesize?

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Mkuu Mchambuzi usichoelewa ni nini, hii sio hypothesis ni trend tuu, kama katiba mpya haijawahi kuwemo kwenye ilani ya CCM lakini imekuja kwa hati ya dharura, udharura huo huo ndio utakaotumika kupitisha katiba mpya ya serikali tatu na hivyo kuleta constitutional supremacy v/s party supremacy. Kutokana na kutawaliwa na chama kimoja kwa muda mrefu, wana CCM wengi bado wamelewa party supremacy ambapo chama ndicho kwanza kinatangulia serikali inatekeleza, bunge la katiba sio bunge la vyama, hata wana CCM wote wataoingia mule, hawaingii kwa u CCM wao, hivyo hakuna party caucuses mule, hivyo sasa ni katiba kwanza, kisha vyama vinajibadilisha kuendana na matakwa ya katiba mpya, yaani ndani ya setup ya katiba mpya CCM is as nothing as chama kingine chochote, wakati ndani ya bunge, CCM is everything kwa sababu ndio chama tawala.
Pasco
 
Mkuu Mchambuzi usichoelewa ni nini, hii sio hypothesis ni trend tuu, kama katiba mpya haijawahi kuwemo kwenye ilani ya CCM lakini imekuja kwa hati ya dharura, udharura huo huo ndio utakaotumika kupitisha katiba mpya ya serikali tatu na hivyo kuleta constitutional supremacy v/s party supremacy. Kutokana na kutawaliwa na chama kimoja kwa muda mrefu, wana CCM wengi bado wamelewa party supremacy ambapo chama ndicho kwanza kinatangulia serikali inatekeleza, bunge la katiba sio bunge la vyama, hata wana CCM wote wataoingia mule, hawaingii kwa u CCM wao, hivyo hakuna party caucuses mule, hivyo sasa ni katiba kwanza, kisha vyama vinajibadilisha kuendana na matakwa ya katiba mpya, yaani ndani ya setup ya katiba mpya CCM is as nothing as chama kingine chochote, wakati ndani ya bunge, CCM is everything kwa sababu ndio chama tawala.
Pasco

Kwahizi yamini wanazolishana serikali tatu tutegemee labda ubabe lakini kwa nia ya dhati CCM hawautaki muungano wa serikali tatu huo ndio msimamo wa wahafidhina wengi wa muungano huu. Humu pia wamejaa.
 
Kwahizi yamini wanazolishana serikali tatu tutegemee labda ubabe lakini kwa nia ya dhati CCM hawautaki muungano wa serikali tatu huo ndio msimamo wa wahafidhina wengi wa muungano huu. Humu pia wamejaa.
Mkuu Chamvinga, kwenye rasimu ya katiba suala la serikali 3 sio an option kusema wanaweza kuamua mbili au moja, hayo ndio matakwa ya Watanzania, sasa CCM watake wasitake that is it!, hatutengenezi katiba ya CCM , wala CCM ndani ya katiba mpya its just nothing as chama kingine chochote!. Kama ni kweli walidhamiria wish yao ni serikali mbili, they had a chance ku lobby ndani ya tume kabla ya rasimu ya pili. Kuhusu muungano bunge la katiba watajadili kuhusu muundo sio idadi ya serikali!. Serikali ni tatu, tuendeleze majadiliano kuanzia hapo!.
Pasco
 
Huyo Mchambuzi wako analeta thread/mnakasha ambao ndani yake pana elements/pattern ya kuhalalisha na ku-justify ule uharamia woote wa Nyerere na jinsi alivyotuadhibu Watanzania chini ya ile One Party Communist almost Juche System...khalafu wewe unangia hapa na kumwambia aondoke!? Aende wapi sasa!?

Hivi nyinyi Chadema mna maarifa japo kiduchu ya kuazima!?

Kwa mfano Mkuu Mchambuzi anajaribu kutuaminisha yakuwa ati wakti wa Mwalimu aka "Baba wa Taifa"...ya kwamba baadhi ya sababu kadhaa zilohalalisha ile Katiba ya kinyama ya wakti ule na kumfanza Nyerere bado awe "Halali"...ametaja ati ni Azimio la Arusha na uwepo wa ati wale alowaita ndo popular and Charismatic Leaders kama vile Nyerere!? Looh!

Sasa embu tupeni majina ya hao Viongozi walokua/waliowahi ati ndo kupendwa na Wananchi wakti,au ndo mna maana ya yule Nyerere!? Duh!

Kama kwa sifa za aina hiyo...hata Hitler,Kim Il Sung na Family yake,Saddam Hussein na Hafidh Al Assad mbona hawa woote nao walikua ni popular and charismatic Leaders!?

Hao Viongozi madhalimu woote,nao kama Nyerere tu yaani hawakuwa na tafauti kubwa mno! Na kwenye chaguzi takriban zoote ndani ya nchi zao,nao pia kama vile yule Nyerere...walikua wakipata taakriban 80-90% ya Kura!? Duh!

Badala ya Mkuu Mchambuzi kujaribu kuudanganya umma wa Watanzania na ulimwengu ati yakuwa wakti wa utawala wa kidhalimu wa yule Nyerere,Watanzania walikua Loyal!? Looh!

Kwanini hamtaki kusema kweli yakuwa wakti huo Wananchi/Watanzania woote walikua hawana option yoyote maskini dhidi ya utawala wa kimabavu wa yule Nyerere!?

Nafikiri yeye Nyerere ndo Kiongozi pekee katika nchi yetu alofanziwa majaribio ya kutaka kumpindua zaidi ya mara tatu,kama sikosei!? Sasa hiyo Loyalty asemayo huyo ajiitae ndo Mchambuzi iwapi hapo!?

Nafahamu kwa yakini yakuwa Mkuu Mchambuzi na takriban hao wenzie nyoote alowa-tag kwenye hii thread/mnakasha ni wenye mwelekeo,lengo,madhumuni na mtazamo mmoja naye! Si kitu kibaya mno,ndo maana hapa jamvini hazitakuwapo hoja zenye maana...sababu upinzani khalis hautakuwapo asilan,abadan!!

Nimechungulia baadhi ya michango ya Wanajamvi wenye kujimudu kimaarifa japo kiduchu hapa jamvini...si weye pimbi ujiitae Parameter lakini!

Kwa kifupi nimehuzunika kiduchu!

Ukiangalia kiundani,wachangiaji woote mnamsifia yule Dictator Nyerere na utawala wake dhalim na kujaribu kumchafua mtu kama Rais wenu wa sasa Dr Kikwete...ambae katika kipindi kifupi mno cha utawala wake...pamoja na tafran na changamoto zoote zinazomkabili lakini amejitahidi mno kuimarisha mojawapao ya mambo makubwa vitu kama Democratic Institutions,freedom of speech and freedom of expression!

Nani alithubutu hata kuviota vitu kama hivyo wakti wa yule Nyerere!?

Mnaweza vipi nyinyi maharamia wa hoja,kuthubutu kuchangia tena ati kwa kuhalalisha makosa na nakma zoote yule Nyerere alizowafanzia Watanzania...lakini kwa unafiki ulotamalaki ndani ya nyoyo zenu,ati mnajaribu kuichafua CCM na Rais Dr Kikwete!? Looh!

Embu jaribuni kuwa objective na impartial japo kiduchu...kama kweli mwahitaji wangine wachangie kitaaluma na kuleta mazungumzo yenye uzalendo na tija kwa Taifa letu hili changa!

Yawaje leo hiyo CCM na Kikwete ati ndo wawe wabaya na history na Katiba yoote mwajaribu kuionyesha mapungufu makubwa!...kitu ambacho ni kweli,yaani kwa hili nakubaliana nanyi!?

Sasa yawezekana vipi hapa huyo Nyerere awe exonorated na asihusishwe/asizungumzwe kimapungufu kwayo au na huo muonao nyinyi yakuwa ndo uchafu/mapungufu ya hiyo CCM na hata chimbuko la haya yoote Taifa letu lipitiamo leo hii!? Kwani yeye Nyerere si ndo alokua mwasisi na mwandishi wa hiyo CCM na Pia Katiba iliyopo!?

Au kama si hivyo yakhusu nini basi nyinyi mum-glorify and/or glamourise kula kukacha mpaka kufikia kumwita ati Baba wa Taifa"!?

Nyinyi nyoote mkitajiwa tu yule Nyerere,hata kwa hoja zenye ukweli yakinifu...kwanini mwaruka Kimanga mpaka Salalah! Teeh! Teeh! Teeh!

Nimemsoma huyo Mchambuzi...ati anajaribu kutuhadaa hapa jamvini yakuwa mojawapo ya sifa kubwa za yule Nyerere ati alikua ni Pan-Afrikanist!? Looh!

Nyerere si ndo yule yule alionyesha ile Non Pan-Afrikanist views at International arenas/hadharani kwenye ule mgogoro wa Biafra...na mpaka kufikia kuingiza nchi yetu changa kwenye ule mgogoro mkali wa Nigeria...na kututia dosari la kuonekana Wazandiki na Wanafiki!?

Nguruvi3...anafahamu kiundani kabisa jinsi gani yule hasidi Nyerere alivyochangia kiundani kwa njia moja amma nyangine kuudhoofisha na mwishowe kuutokomeza ule Muungano wa awali hapo East Afrika-EAC!?

Sina haja asilan ya kujichosha mno kwa kutaja udhaifu na madhila kadhaa ili tujikumbushe tulipotoka na tusiwe wivi wa shukran.

Sasa kabla sijataja mangi kiundani...kwa hayo mawili kiduchu tu,kwanini mnajaribu kutuaminisha yakuwa huyo Nyerere ati alikua na sifa za Pan-Afrikanist!?

Nyerere alikua haamini asilan katika democratic institutions,democracy itself,freedom of speech/experssion...hii ni open secret kwenye World corridors of Politics...yaani kila mwenye akili na maarifa yake timamu anafahamu hili jambo!

Nyerere si ndo huyu huyu alokwenda kumsaidia yule haramia Albert Rene pale Seychelles(someone who was already implicated on systematic tortures and other Human Right abuses!) ili aendelee kuketi madarakani pale Seychelles...na Tanzania ikapeleka mpaka majeshi-JWZT kwa amri ya yule Nyerere!! Duh!

Kwa kifupi...Nyerere hakuwa intellectual capable wala hakuwa na integrity ya kupambana na nyakati/dunia mpya...yaani kwa kumsifia japo kiduchu,alishatambua yakuwa Watanzania tayari wameshaamka na wana fikara/mwamko mpya tena usio na woga asilan!

Kwa hiyo nyoote acheni au punguzeni kutuaminisha yakuwa ati Nyerere...aliamua tu kuachia kiti/nchi kwa mapenzi yake ya nchi/Taifa na Watanzania wenzie,au ati alikua akipenda/kuabudu mno Demokrasia!? Duh! Teeh! Teeh! Teeh!

Kwa kifupi...endeleeni tu na huo mchakato wenu wa Katiba hapa jamvini,lakini kila mtakapokua mwasema urongo,basi sisi tutakua twajawarekebisha kiduchu na kwenda zetu!

La si hivyo...yaani ikiwa twakaa tu kimya itakua hatuwatendei haki Watanzania wenzetu wangine,na pia itakua hata nyinyi pia hatukupendeni!? Maana akupendae ni yule akwambiae kweli!

Ahsantani sana!
 
Mkuu Wabara, kule nilijibu kila kitu mule mule kapitie tuu taratibu majibu yako utayakuta kule, hii mada ya Mkuu Mchambuzi ni mada serious, kama wewe bado unayo makando kando ya ile supu ya utumbo ule, uhifadhi unipakulie kwenye thread yangu nyingine yoyote tusiwajazie bure mainzi humu watu ambao sio wa ile biashara ya utumbo!. Nasisitiza hii mada ni very serious, wale wenzangu na mimi wa ile biashara ya utumbo tukutanie kule kule anga zangu, tusichafue anga za watu wakati mlengwa wenu ni mimi. Maswali yenu yote yasiohusika na hii mada, nirushieni kwenye thread yangu nyingine yoyote, sio humu!. Please !.
Pasco


Sasa hivi wewe Pasco...yataka wataka kutuaminisha ile mada/thread yako ilikua haina u-Serious kufananiza na hii ya Mkuu Mchambuzi!? Duh!

Umeshasahau yakuwa ile ilikhusu upotoshwaji wa kitaaluma/historia ulodhamiria kuufanza wewe na walokutuma...kumbuka history ya Zanzibar-1964 ilihusisha pamoja na mangi, mauaji ya raia/Wazanzibary kwa mahalaiki wasio na hatia wengi wao wakiwa wanawake na watoto waduchu!

Sasa hapo wewe wataka u-serious upi tena!?

Na kwenye civilized societies mtu wa fani/field yako...basi kufanza manipulation of information or lies...can amount to fraud which is a criminal offence!

Kwanini hutaki/hupendi kuwa responsible!? Dah!

Ahsanta.
 
Huyo Mchambuzi wako analeta thread/mnakasha ambao ndani yake pana elements/pattern ya kuhalalisha na ku-justify ule uharamia woote wa Nyerere na jinsi alivyotuadhibu Watanzania chini ya ile One Party Communist almost Juche System...khalafu wewe unangia hapa na kumwambia aondoke!? Aende wapi sasa!?

Hivi nyinyi Chadema mna maarifa japo kiduchu ya kuazima!?

Kwa mfano Mkuu Mchambuzi anajaribu kutuaminisha yakuwa ati wakti wa Mwalimu aka "Baba wa Taifa"...ya kwamba baadhi ya sababu kadhaa zilohalalisha ile Katiba ya kinyama ya wakti ule na kumfanza Nyerere bado awe "Halali"...ametaja ati ni Azimio la Arusha na uwepo wa ati wale alowaita ndo popular and Charismatic Leaders kama vile Nyerere!? Looh!

Sasa embu tupeni majina ya hao Viongozi walokua/waliowahi ati ndo kupendwa na Wananchi wakti,au ndo mna maana ya yule Nyerere!? Duh!

Kama kwa sifa za aina hiyo...hata Hitler,Kim Il Sung na Family yake,Saddam Hussein na Hafidh Al Assad mbona hawa woote nao walikua ni popular and charismatic Leaders!?

Hao Viongozi madhalimu woote,nao kama Nyerere tu yaani hawakuwa na tafauti kubwa mno! Na kwenye chaguzi takriban zoote ndani ya nchi zao,nao pia kama vile yule Nyerere...walikua wakipata taakriban 80-90% ya Kura!? Duh!

Badala ya Mkuu Mchambuzi kujaribu kuudanganya umma wa Watanzania na ulimwengu ati yakuwa wakti wa utawala wa kidhalimu wa yule Nyerere,Watanzania walikua Loyal!? Looh!

Kwanini hamtaki kusema kweli yakuwa wakti huo Wananchi/Watanzania woote walikua hawana option yoyote maskini dhidi ya utawala wa kimabavu wa yule Nyerere!?

Nafikiri yeye Nyerere ndo Kiongozi pekee katika nchi yetu alofanziwa majaribio ya kutaka kumpindua zaidi ya mara tatu,kama sikosei!? Sasa hiyo Loyalty asemayo huyo ajiitae ndo Mchambuzi iwapi hapo!?

Nafahamu kwa yakini yakuwa Mkuu Mchambuzi na takriban hao wenzie nyoote alowa-tag kwenye hii thread/mnakasha ni wenye mwelekeo,lengo,madhumuni na mtazamo mmoja naye! Si kitu kibaya mno,ndo maana hapa jamvini hazitakuwapo hoja zenye maana...sababu upinzani khalis hautakuwapo asilan,abadan!!

Nimechungulia baadhi ya michango ya Wanajamvi wenye kujimudu kimaarifa japo kiduchu hapa jamvini...si weye pimbi ujiitae Parameter lakini!

Kwa kifupi nimehuzunika kiduchu!

Ukiangalia kiundani,wachangiaji woote mnamsifia yule Dictator Nyerere na utawala wake dhalim na kujaribu kumchafua mtu kama Rais wenu wa sasa Dr Kikwete...ambae katika kipindi kifupi mno cha utawala wake...pamoja na tafran na changamoto zoote zinazomkabili lakini amejitahidi mno kuimarisha mojawapao ya mambo makubwa vitu kama Democratic Institutions,freedom of speech and freedom of expression!

Nani alithubutu hata kuviota vitu kama hivyo wakti wa yule Nyerere!?

Mnaweza vipi nyinyi maharamia wa hoja,kuthubutu kuchangia tena ati kwa kuhalalisha makosa na nakma zoote yule Nyerere alizowafanzia Watanzania...lakini kwa unafiki ulotamalaki ndani ya nyoyo zenu,ati mnajaribu kuichafua CCM na Rais Dr Kikwete!? Looh!

Embu jaribuni kuwa objective na impartial japo kiduchu...kama kweli mwahitaji wangine wachangie kitaaluma na kuleta mazungumzo yenye uzalendo na tija kwa Taifa letu hili changa!

Yawaje leo hiyo CCM na Kikwete ati ndo wawe wabaya na history na Katiba yoote mwajaribu kuionyesha mapungufu makubwa!...kitu ambacho ni kweli,yaani kwa hili nakubaliana nanyi!?

Sasa yawezekana vipi hapa huyo Nyerere awe exonorated na asihusishwe/asizungumzwe kimapungufu kwayo au na huo muonao nyinyi yakuwa ndo uchafu/mapungufu ya hiyo CCM na hata chimbuko la haya yoote Taifa letu lipitiamo leo hii!? Kwani yeye Nyerere si ndo alokua mwasisi na mwandishi wa hiyo CCM na Pia Katiba iliyopo!?

Au kama si hivyo yakhusu nini basi nyinyi mum-glorify and/or glamourise kula kukacha mpaka kufikia kumwita ati Baba wa Taifa"!?

Nyinyi nyoote mkitajiwa tu yule Nyerere,hata kwa hoja zenye ukweli yakinifu...kwanini mwaruka Kimanga mpaka Salalah! Teeh! Teeh! Teeh!

Nimemsoma huyo Mchambuzi...ati anajaribu kutuhadaa hapa jamvini yakuwa mojawapo ya sifa kubwa za yule Nyerere ati alikua ni Pan-Afrikanist!? Looh!

Nyerere si ndo yule yule alionyesha ile Non Pan-Afrikanist views at International arenas/hadharani kwenye ule mgogoro wa Biafra...na mpaka kufikia kuingiza nchi yetu changa kwenye ule mgogoro mkali wa Nigeria...na kututia dosari la kuonekana Wazandiki na Wanafiki!?

Nguruvi3...anafahamu kiundani kabisa jinsi gani yule hasidi Nyerere alivyochangia kiundani kwa njia moja amma nyangine kuudhoofisha na mwishowe kuutokomeza ule Muungano wa awali hapo East Afrika-EAC!?

Sina haja asilan ya kujichosha mno kwa kutaja udhaifu na madhila kadhaa ili tujikumbushe tulipotoka na tusiwe wivi wa shukran.

Sasa kabla sijataja mangi kiundani...kwa hayo mawili kiduchu tu,kwanini mnajaribu kutuaminisha yakuwa huyo Nyerere ati alikua na sifa za Pan-Afrikanist!?

Nyerere alikua haamini asilan katika democratic institutions,democracy itself,freedom of speech/experssion...hii ni open secret kwenye World corridors of Politics...yaani kila mwenye akili na maarifa yake timamu anafahamu hili jambo!

Nyerere si ndo huyu huyu alokwenda kumsaidia yule haramia Albert Rene pale Seychelles(someone who was already implicated on systematic tortures and other Human Right abuses!) ili aendelee kuketi madarakani pale Seychelles...na Tanzania ikapeleka mpaka majeshi-JWZT kwa amri ya yule Nyerere!! Duh!

Kwa kifupi...Nyerere hakuwa intellectual capable wala hakuwa na integrity ya kupambana na nyakati/dunia mpya...yaani kwa kumsifia japo kiduchu,alishatambua yakuwa Watanzania tayari wameshaamka na wana fikara/mwamko mpya tena usio na woga asilan!

Kwa hiyo nyoote acheni au punguzeni kutuaminisha yakuwa ati Nyerere...aliamua tu kuachia kiti/nchi kwa mapenzi yake ya nchi/Taifa na Watanzania wenzie,au ati alikua akipenda/kuabudu mno Demokrasia!? Duh! Teeh! Teeh! Teeh!

Kwa kifupi...endeleeni tu na huo mchakato wenu wa Katiba hapa jamvini,lakini kila mtakapokua mwasema urongo,basi sisi tutakua twajawarekebisha kiduchu na kwenda zetu!

La si hivyo...yaani ikiwa twakaa tu kimya itakua hatuwatendei haki Watanzania wenzetu wangine,na pia itakua hata nyinyi pia hatukupendeni!? Maana akupendae ni yule akwambiae kweli!

Ahsantani sana!

Mkuu wangu gombesugu nakusoma kwa saana !
Hii bakora umechapia huyo mjusi kafiri! Kama ni mtoto wa HALALI hawezi kurudi tena hapa!

Sasa anangalia mwenyewe! Ndo utajua hivi vizazi vya mitaani vimejaa humu!

Teh teh teh teh!

Ahsanta sanaaa!
 
Last edited by a moderator:
Huyo Mchambuzi wako analeta thread/mnakasha ambao ndani yake pana elements/pattern ya kuhalalisha na ku-justify ule uharamia woote wa Nyerere na jinsi alivyotuadhibu Watanzania chini ya ile One Party Communist almost Juche System...khalafu wewe unangia hapa na kumwambia aondoke!? Aende wapi sasa!? Hivi nyinyi Chadema mna maarifa japo kiduchu ya kuazima!? Kwa mfano Mkuu Mchambuzi anajaribu kutuaminisha yakuwa ati wakti wa Mwalimu aka "Baba wa Taifa"...ya kwamba baadhi ya sababu kadhaa zilohalalisha ile Katiba ya kinyama ya wakti ule na kumfanza Nyerere bado awe "Halali"...ametaja ati ni Azimio la Arusha na uwepo wa ati wale alowaita ndo popular and Charismatic Leaders kama vile Nyerere!? Looh! Sasa embu tupeni majina ya hao Viongozi walokua/waliowahi ati ndo kupendwa na Wananchi wakti,au ndo mna maana ya yule Nyerere!? Duh! Kama kwa sifa za aina hiyo...hata Hitler,Kim Il Sung na Family yake,Saddam Hussein na Hafidh Al Assad mbona hawa woote nao walikua ni popular and charismatic Leaders!? Hao Viongozi madhalimu woote,nao kama Nyerere tu yaani hawakuwa na tafauti kubwa mno! Na kwenye chaguzi takriban zoote ndani ya nchi zao,nao pia kama vile yule Nyerere...walikua wakipata taakriban 80-90% ya Kura!? Duh! Badala ya Mkuu Mchambuzi kujaribu kuudanganya umma wa Watanzania na ulimwengu ati yakuwa wakti wa utawala wa kidhalimu wa yule Nyerere,Watanzania walikua Loyal!? Looh! Kwanini hamtaki kusema kweli yakuwa wakti huo Wananchi/Watanzania woote walikua hawana option yoyote maskini dhidi ya utawala wa kimabavu wa yule Nyerere!? Nafikiri yeye Nyerere ndo Kiongozi pekee katika nchi yetu alofanziwa majaribio ya kutaka kumpindua zaidi ya mara tatu,kama sikosei!? Sasa hiyo Loyalty asemayo huyo ajiitae ndo Mchambuzi iwapi hapo!? Nafahamu kwa yakini yakuwa Mkuu Mchambuzi na takriban hao wenzie nyoote alowa-tag kwenye hii thread/mnakasha ni wenye mwelekeo,lengo,madhumuni na mtazamo mmoja naye! Si kitu kibaya mno,ndo maana hapa jamvini hazitakuwapo hoja zenye maana...sababu upinzani khalis hautakuwapo asilan,abadan!! Nimechungulia baadhi ya michango ya Wanajamvi wenye kujimudu kimaarifa japo kiduchu hapa jamvini...si weye pimbi ujiitae Parameter lakini! Kwa kifupi nimehuzunika kiduchu! Ukiangalia kiundani,wachangiaji woote mnamsifia yule Dictator Nyerere na utawala wake dhalim na kujaribu kumchafua mtu kama Rais wenu wa sasa Dr Kikwete...ambae katika kipindi kifupi mno cha utawala wake...pamoja na tafran na changamoto zoote zinazomkabili lakini amejitahidi mno kuimarisha mojawapao ya mambo makubwa vitu kama Democratic Institutions,freedom of speech and freedom of expression! Nani alithubutu hata kuviota vitu kama hivyo wakti wa yule Nyerere!? Mnaweza vipi nyinyi maharamia wa hoja,kuthubutu kuchangia tena ati kwa kuhalalisha makosa na nakma zoote yule Nyerere alizowafanzia Watanzania...lakini kwa unafiki ulotamalaki ndani ya nyoyo zenu,ati mnajaribu kuichafua CCM na Rais Dr Kikwete!? Looh! Embu jaribuni kuwa objective na impartial japo kiduchu...kama kweli mwahitaji wangine wachangie kitaaluma na kuleta mazungumzo yenye uzalendo na tija kwa Taifa letu hili changa! Yawaje leo hiyo CCM na Kikwete ati ndo wawe wabaya na history na Katiba yoote mwajaribu kuionyesha mapungufu makubwa!...kitu ambacho ni kweli,yaani kwa hili nakubaliana nanyi!? Sasa yawezekana vipi hapa huyo Nyerere awe exonorated na asihusishwe/asizungumzwe kimapungufu kwayo au na huo muonao nyinyi yakuwa ndo uchafu/mapungufu ya hiyo CCM na hata chimbuko la haya yoote Taifa letu lipitiamo leo hii!? Kwani yeye Nyerere si ndo alokua mwasisi na mwandishi wa hiyo CCM na Pia Katiba iliyopo!? Au kama si hivyo yakhusu nini basi nyinyi mum-glorify and/or glamourise kula kukacha mpaka kufikia kumwita ati Baba wa Taifa"!? Nyinyi nyoote mkitajiwa tu yule Nyerere,hata kwa hoja zenye ukweli yakinifu...kwanini mwaruka Kimanga mpaka Salalah! Teeh! Teeh! Teeh! Nimemsoma huyo Mchambuzi...ati anajaribu kutuhadaa hapa jamvini yakuwa mojawapo ya sifa kubwa za yule Nyerere ati alikua ni Pan-Afrikanist!? Looh! Nyerere si ndo yule yule alionyesha ile Non Pan-Afrikanist views at International arenas/hadharani kwenye ule mgogoro wa Biafra...na mpaka kufikia kuingiza nchi yetu changa kwenye ule mgogoro mkali wa Nigeria...na kututia dosari la kuonekana Wazandiki na Wanafiki!? Nguruvi3...anafahamu kiundani kabisa jinsi gani yule hasidi Nyerere alivyochangia kiundani kwa njia moja amma nyangine kuudhoofisha na mwishowe kuutokomeza ule Muungano wa awali hapo East Afrika-EAC!? Sina haja asilan ya kujichosha mno kwa kutaja udhaifu na madhila kadhaa ili tujikumbushe tulipotoka na tusiwe wivi wa shukran. Sasa kabla sijataja mangi kiundani...kwa hayo mawili kiduchu tu,kwanini mnajaribu kutuaminisha yakuwa huyo Nyerere ati alikua na sifa za Pan-Afrikanist!? Nyerere alikua haamini asilan katika democratic institutions,democracy itself,freedom of speech/experssion...hii ni open secret kwenye World corridors of Politics...yaani kila mwenye akili na maarifa yake timamu anafahamu hili jambo! Nyerere si ndo huyu huyu alokwenda kumsaidia yule haramia Albert Rene pale Seychelles(someone who was already implicated on systematic tortures and other Human Right abuses!) ili aendelee kuketi madarakani pale Seychelles...na Tanzania ikapeleka mpaka majeshi-JWZT kwa amri ya yule Nyerere!! Duh! Kwa kifupi...Nyerere hakuwa intellectual capable wala hakuwa na integrity ya kupambana na nyakati/dunia mpya...yaani kwa kumsifia japo kiduchu,alishatambua yakuwa Watanzania tayari wameshaamka na wana fikara/mwamko mpya tena usio na woga asilan! Kwa hiyo nyoote acheni au punguzeni kutuaminisha yakuwa ati Nyerere...aliamua tu kuachia kiti/nchi kwa mapenzi yake ya nchi/Taifa na Watanzania wenzie,au ati alikua akipenda/kuabudu mno Demokrasia!? Duh! Teeh! Teeh! Teeh! Kwa kifupi...endeleeni tu na huo mchakato wenu wa Katiba hapa jamvini,lakini kila mtakapokua mwasema urongo,basi sisi tutakua twajawarekebisha kiduchu na kwenda zetu! La si hivyo...yaani ikiwa twakaa tu kimya itakua hatuwatendei haki Watanzania wenzetu wangine,na pia itakua hata nyinyi pia hatukupendeni!? Maana akupendae ni yule akwambiae kweli! Ahsantani sana!
Mkuu Gombe, kitendo cha kulitaja jina la Nyerere mara 24 kwenye thread moja ni heshima tosha iwe kwa wema au kwa ubaya ni dhahir shayir mnamgwaya na kumha..sana!. Tena Wazejibari ndio wanatakiwa wamshukuru sana kwa muungano ule vinginevyo wangeendelea kujinjana kama kuku na hivi vitimbakwiri vizalia vya madhalimu walio jitimkia baada ya mapinduzi matukufu yale na kudai wajetimuliwa, saa hizi sijui hata wangekoholea wapi !, nawaona humu jinsi kamasi zinavyowatoka na kuzipaka humu kupitia keyboards zao!. Pasco.
 
Nilitaka jawaba la mfano kama huo. Maana kwako kupata zitu za maana kidogo yakuwia vigumu sana na hutoezapokea ukweli na kuukubali kattu. Kwa hivo tabia yako kama ni ya kumendea humu usiku wakti waja weshalala ndo niamini kuwa huna la maana au ndo "UBUNDI" na kuogopa maulizo ya wenye kujitambua? Yanini sasa uvamie uzi za wanzio na kuzipakaza yasofaa japo uzi zao nazo zimekitwa na kulazimisha watu kuamini wanacho kiamini wao?! Hapa ni pahala pa fikra huru, nakubalia na hilo, lakini yawapasa mfahamu kuwa uhuru huo si wa upande mmoya na kutokubali kukosolewa na wenye mtazamo tofauti na fikara zenyu ambao huenda wao ndo ukawa sahihi kuliko hayo yako. Shukraan kwa kunifuatiza na kupata somo japo huelewi!.
Ahasanta tuendeleze majadiliano na mnakasha huu kwa yale tuu yahusuyo.
 
Sasa hivi wewe Pasco...yataka wataka kutuaminisha ile mada/thread yako ilikua haina u-Serious kufananiza na hii ya Mkuu Mchambuzi!? Duh! 6 Umeshasahau yakuwa ile ilikhusu upotoshwaji wa kitaaluma/historia ulodhamiria kuufanza wewe na walokutuma...kumbuka history ya Zanzibar-1964 ilihusisha pamoja na mangi, mauaji ya raia/Wazanzibary kwa mahalaiki wasio na hatia wengi wao wakiwa wanawake na watoto waduchu! Sasa hapo wewe wataka u-serious upi tena!? Na kwenye civilized societies mtu wa fani/field yako...basi kufanza manipulation of information or lies...can amount to fraud which is a criminal offence! Kwanini hutaki/hupendi kuwa responsible!? Dah! Ahsanta.
Mkuu Gombe, naomba turejee kwenye mada kuu ya Mchambuzi msije mkaifikisha kule mlikonifikisha ile siku. Pasco
 
Ahasanta tuendeleze majadiliano na mnakasha huu kwa yale tuu yahusuyo.

Kwa kujivika uungwana wako wa kidharura na kinafiki, nakukumbusha tena maana ada ya mnaafiki ni kujisahau pia kwa kile alichokinena awali haya kama ni one second,

Kwa maneno hayo kubaliana nami kuwa "THREDS ZAKO NI ZA KIPUUZI/ HAZINA MAANA / UHAKIKA", kutokana na post yako #114 .

Jipange kwa ndia zangine nikutie fahamu za hakika ili ujiamini kwa huja popote pawapo na uwapo, si kutekesha na kusumbua watu wenye akli za maana katika vitu vya mizaha na upotoshwaji wa maksudi.
 



Wakuu,

kuna umuhimu kwetu sote kurudi kwenye mada iliyo mbele yetu badala ya kulumbana kwa hoja zisizo na maslahi kwa suala lililo mbele yetu. Iwapo tofauti yetu no mawazo na mitazamo, basi tufanye hivyo kwa hoja. Watu wengi sana wanatusoma humu kwa vile wanaipa JF heshima kubwa. Tujaribu kuilinda heshima hiyo kwa manufaa yetu sote.

Nikirudi kwenye mada, nianze na hoja ya mzee kisumo. Inaniwia vigumu sana kuelewa msingi wa hoja yake ni nini, hasa anapomshambulia jaji warioba na pia kusema kwamba - kama mfumo uliopo wa serikali mbili una matatizo, yanaweza rekebishwa. Naungana na mdau mmoja humu aliyehoji kwamba hivi kweli Kisumo na uzoefu wake wote haoni mfumo wa sasa una matatizo? Hata mwalimu aliwahi kukubali mara nyingi tu kuna matatizo lakini tofauti ya mwalimu na wazee wa sasa, mwalimu aliujadili muungano kwa hoja, uzalendo and in a non partisan fashion, hivyo kupelekea kero zilizopo kujadilika na pia watu kuishi kwa matumaini kwani no doubt, nyerere was a visionary, and "visionaries inspire".

Ni vigumu kuelewa kwanini peter kisumo na wengine wenye mtazamo wake ndani ya ccm wanamlaumu jaji warioba 2014 wakati:

1. Kwa mara ya kwanza suala la muundo wa muungano lilikitokeza kwa hisia kali mwaka 1984 katika kipindi kilichoitwa "kuchafuka kwa hali ya hewa".

2. Mwaka 1991, tume ya nyalali ikaja na kupendekeza serikali tatu.

3. Mwaka 1993, kikundi cha wabunge "G55" kikaja na hoja ya serikali tatu, na hii ilikuwa karibia miaka kumi baada ya sakata la mzee aboud jumbe. Lakini pamoja na hayo, peter kisumo anaruka matukio mawili ya awali na kujadili suala la G55 as if wao ndio walikuwa innovators wa hoja husika. Tukumbuke kwamba bunge liliridhia mfumo wa serikali tatu kufuatia hoja ya G55.

4. Mwaka 1999 ikaja kamati ya jaji kisanga, nayo ikapendekeza serikali tatu.

5. Vile vile ziliundwa tume nyingi kujaribu kutatua kero za muungano kama vile kamati ya amina salum ali, shelukindo na nyingine nyingi. Zote hazikuweza kutatua kera za muungano.

Tume ya warioba ni lazima ilijiridhisha na matukio yote haya kabla ya kukaa na kutengeneza hadidu rejea. Na kimsingi, hoja zilizotolewa mwaka 1984 (sakata la jumbe) hadi tume ya jaji kisanga, hoja hizi zinafanana, lakini muhimu zaidi, wakati wa maoni ya kitaasisi na mtu mmoja mmoja kwa tume ya warioba 2013, msingi wa hoja ukawa ni ule ule ulioanza miaka 20 iliyopita. Kwanini CCM hailioni hilo na badala yake baadhi ya makada wake wanamshambulia warioba na tume yake?

Binafsi nadhani katika viongozi wachache wenye busara waliobaki ccm, pamoja na mapungufu yao ya hapa na pale ni rais kikwete na samual sitta. Kikwete alisoma alama za nyakazi na kukubali sio tu kuanzisha mchakato wa katiba mpya, bali pia kuwaeleza wana ccm juu ya umuhimu wa kujiandaa kisaikolojia na kurudi kwa Tanganyika. Samuel sitta nae anastahili pongezi kwa kukiokoa ccm kule zanzibar ambako aliiwakilisha serikali katika halfa ya uzinduzi wa muswada wa mabadiliko ya katiba. Umma wa wazanzibari waliuchoma mswaada ule kwa sababu uliwazuia kujadili muungano. Iwapo serikali ingekuwa imetuma viongozi wengine kama kina nanihii badala ya sitta, leo tungekuwa tunaongea mengine.

Pia ni muhimu tutambue kwamba ni wazanzibari ndio waliosaidia kuweka shinikizo suala la muungano liwe sehemu ya muswada husika, hivyo kutoa fursa kwa Tanganyika kujadiliwa. Hakuna ushahidi sehemu yoyote kwamba wananchi wa Tanzania bara walikuwa wamejiandaa to revolt. Kwa maana nyingine, tukubali ukweli kwamba madai ya Tanganyika kwa wabara walio wengi yana uhusiano wa moja kwa moja na harakati za wazanzibari kudai autonomy yao, na ni harakati hizo ndio zimewazindua watanganyika wengi kutoka kwenye usingizi mzito. Kwa hilo, binafsi nawashukuru sana wazanzibari.

Nikijikita kwenye hoja yangu ya msingi katika bandiko hili, tutazame, je malalamiko makubwa ya wazanzibari juu ya muungano ni yepi?

1. Tanganyika inafaidika zaidi kuliko Zanzibar kwani chini ya mfumo uliopo, Tanganyika ndio Tanzania. Hoja hii imejadiliwa na tume ya warioba kwa hoja kwamba "Tanganyika imevaa koti la serikali ya muungano".

Je kuna ukweli katika hili? Binafsi nasema NDIO, ukweli upo tena mkubwa sana lakini utaugundua iwapo utafanikiwa kutambua kiini macho kilichopo. Kwa mfano:

Kwa mujibu wa katiba ya JMT (1977), chombo chenye mamlaka ya kusimamia masuala ya muungano ni serikali ya muungano. Lakini pia chombo chenye mamlaka ya kusimamia masuala yasiyo ya muungano (the so called "Tanzania Bara"), pia ni serikali ya muungano. Kama hadi hapa tupo sawa, tuendelee:

Kwa mantiki hiyo, ni serikali ya muungano ndio inayoshughulikia sana masuala kama vile ujenzi, uchukuzi, afya, kilimo, maji, maliasili na utalii,elimu, nishati na madini, na mengine mengi tu ambayo kimsingi ni ya Tanzania bara na sio ya muungano. Iwapo tupo sawa hadi hapa, tuendelee:

Wakati wa vikao vya bajeti ya bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania (chombo ambacho kipo kuwakilisha maslahi ya wa zanzibari na watanganyika equally), je:

*bunge hutenga siku ngapi kujadili masuala ya Tanzania Bara (Tanganyika)? Siku mbili hadi Nne. Je:
*bunge hutenga siku ngapi kujadili mambo ya muungano? Nusu siku hadi siku moja!

Suala lingine muhimu ni kwamba - maswali ya wabunge kuhusu mambo yanayowagusa sana wananchi (development and poverty issues) yanahusu zaidi Tanzania bara na mambo haya bungeni yanasimamiwa na waziri mkuu ambae hana mamlaka wala madaraka ya aina yoyote kwa zanzibar. Je haki za kimaendeleo za wazanzibari katika bunge la JMT chini ya mfumo wa sasa zinasimamiwa na nani?

Lalamiko lingine kubwa la wazanzibari dhidi ya mfumo wa serikali mbili ni kwamba - mambo ya muungano yamekuwa yakiongezeka na hivyo kuathiri "identity" na "autonomy" ya zanzibar na kupelekea znz kuwa katika hatari ya kumezwa. Lalamiko hili pia kwa mtazamo wangu lina mashiko, na tumeshajadili sana huko nyuma jinsi gani mkataba wa muungano (1964) ulichakachuliwa na kufikisha taifa katika sakata la jumbe la 1984.

Lalamiko lingine kubwa la wazanzibar ni kwamba Rais wao ameondolewa katika umakamo wa rais wa JMT. Mkataba wa muungano ulimtaja rais wa znz kuwa makamo wa rais katika kipindi cha mpito kuelekea katiba mpya, lakini kama tunavyoelewa, mchakato wa katiba hiyo haukutokea, ikaja katiba ya muda ya JMT (1965) ambayo ikiangiza chama cha TANU kwenye muungano kinyume na mkataba wa muungano (1964). Pamoja na mapungufu yote haya, rais wa znz akaendelea kuwa makamo wa rais mpaka pale weakness za legal and political framework za union zilipokuja kuwa dhahiri kufuatia mfumo wa vyama vingi. Muungano ambao Nyerere alieleza umma kwamba umeiga muungano wa uingereza ambayo inafuata a unitary form of government, miaka ya mwanzo ya tisini jaji bomani akapewa jukumu la kutatua kitendawili cha muungano ndani ya mfumo wa vyama vingi, akaja na solution ya mgombea mwenza kwa kuiga mfumo wa federation wa marekani ili kuepusha ccm na aibu ya kupata rais wa ccm upande wa bara na rais wa Upinzani upande wa zanzibar. Hapa tukabaki kujiuliza, ni muungano gani huu unaoazima elements za federation wakati tuliambiwa msingi wake ni unitary?Ni katika mazingira haya, rais wa znz akaondolewa kwenye umakamu wa rais wa JMT. Sasa cha ajabu nini hapa kwa znz kuanza kufukiria mchakato wa katiba yake ambayo lengo ni kulipa taifa lao madaraka kamili?

Upande wa bara nao una malalamiko mengi lakini muhimu ni pamoja na:

1. Zanzibar imebadili katiba yake na kuchukua madaraka ya jamhuri ya muungano kwa mfano kuelekeza sheria za muungano zilizopitishwa na bunge la JMT kupelekwa kwenye BLW. Kwa mantiki hii, katiba ya zanzibar sasa ipo juu ya katiba ya JMT, na tukumbuke hapa kwamba katiba ya JMT ndio katiba ya Tanzania bara au ukipenda Tanganyika. Kwahiyo maamuzi juu ya hali za maisha ya watanzania bara au ukitaka watanganyika milioni 43 kuanzia 2010 yapo mikononi mwa BLW linalowakilisha wananchi sio zaidi ya milioni moja na nusu.

Lalamiko la pili kubwa kwa upande wetu Bara ni kwamba - wananchi wetu hawana haki ya kumiliki ardhi znz wakati wenzetu wa znz wanayo haki hiyo tanzania bara au ukipenda Tanganyika.


Eneo lingine na malalamiko upande wa bara ni kwamba - zanzibar sasa imekuwa ni nchi huru, ina bendera yake wimbo wa taifa serikali yake na imeshabadili katiba yake ili ijitambue kama nchi wakati kwa mantiki hii Tanzania bara imeshapoteza utambulisho wake kwani katiba ya JMT inasema Tanzania ni nchi moja wakati katiba ya znz inasema Tanzania ni nchi mbili. Katika hili, kuna makosa gani kwa rasimu ya katiba kusema Tanzania ni nchi inayotokana na Tanganyika na zanzibar? Kwani ni dhahiri katika suala la utambulisho wao kama taifa, zanzibar haitarudi nyuma tena.

Nadhani haya ni baadhi ya mambo ambayo wawakilishi wetu kwenye bunge lijalo la katiba wakayakumbuka.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom