Wakuu,
kuna umuhimu kwetu sote kurudi kwenye mada iliyo mbele yetu badala ya kulumbana kwa hoja zisizo na maslahi kwa suala lililo mbele yetu. Iwapo tofauti yetu no mawazo na mitazamo, basi tufanye hivyo kwa hoja. Watu wengi sana wanatusoma humu kwa vile wanaipa JF heshima kubwa. Tujaribu kuilinda heshima hiyo kwa manufaa yetu sote.
Nikirudi kwenye mada, nianze na hoja ya mzee kisumo. Inaniwia vigumu sana kuelewa msingi wa hoja yake ni nini, hasa anapomshambulia jaji warioba na pia kusema kwamba - kama mfumo uliopo wa serikali mbili una matatizo, yanaweza rekebishwa. Naungana na mdau mmoja humu aliyehoji kwamba hivi kweli Kisumo na uzoefu wake wote haoni mfumo wa sasa una matatizo? Hata mwalimu aliwahi kukubali mara nyingi tu kuna matatizo lakini tofauti ya mwalimu na wazee wa sasa, mwalimu aliujadili muungano kwa hoja, uzalendo and in a non partisan fashion, hivyo kupelekea kero zilizopo kujadilika na pia watu kuishi kwa matumaini kwani no doubt, nyerere was a visionary, and "visionaries inspire".
Ni vigumu kuelewa kwanini peter kisumo na wengine wenye mtazamo wake ndani ya ccm wanamlaumu jaji warioba 2014 wakati:
1. Kwa mara ya kwanza suala la muundo wa muungano lilikitokeza kwa hisia kali mwaka 1984 katika kipindi kilichoitwa "kuchafuka kwa hali ya hewa".
2. Mwaka 1991, tume ya nyalali ikaja na kupendekeza serikali tatu.
3. Mwaka 1993, kikundi cha wabunge "G55" kikaja na hoja ya serikali tatu, na hii ilikuwa karibia miaka kumi baada ya sakata la mzee aboud jumbe. Lakini pamoja na hayo, peter kisumo anaruka matukio mawili ya awali na kujadili suala la G55 as if wao ndio walikuwa innovators wa hoja husika. Tukumbuke kwamba bunge liliridhia mfumo wa serikali tatu kufuatia hoja ya G55.
4. Mwaka 1999 ikaja kamati ya jaji kisanga, nayo ikapendekeza serikali tatu.
5. Vile vile ziliundwa tume nyingi kujaribu kutatua kero za muungano kama vile kamati ya amina salum ali, shelukindo na nyingine nyingi. Zote hazikuweza kutatua kera za muungano.
Tume ya warioba ni lazima ilijiridhisha na matukio yote haya kabla ya kukaa na kutengeneza hadidu rejea. Na kimsingi, hoja zilizotolewa mwaka 1984 (sakata la jumbe) hadi tume ya jaji kisanga, hoja hizi zinafanana, lakini muhimu zaidi, wakati wa maoni ya kitaasisi na mtu mmoja mmoja kwa tume ya warioba 2013, msingi wa hoja ukawa ni ule ule ulioanza miaka 20 iliyopita. Kwanini CCM hailioni hilo na badala yake baadhi ya makada wake wanamshambulia warioba na tume yake?
Binafsi nadhani katika viongozi wachache wenye busara waliobaki ccm, pamoja na mapungufu yao ya hapa na pale ni rais kikwete na samual sitta. Kikwete alisoma alama za nyakazi na kukubali sio tu kuanzisha mchakato wa katiba mpya, bali pia kuwaeleza wana ccm juu ya umuhimu wa kujiandaa kisaikolojia na kurudi kwa Tanganyika. Samuel sitta nae anastahili pongezi kwa kukiokoa ccm kule zanzibar ambako aliiwakilisha serikali katika halfa ya uzinduzi wa muswada wa mabadiliko ya katiba. Umma wa wazanzibari waliuchoma mswaada ule kwa sababu uliwazuia kujadili muungano. Iwapo serikali ingekuwa imetuma viongozi wengine kama kina nanihii badala ya sitta, leo tungekuwa tunaongea mengine.
Pia ni muhimu tutambue kwamba ni wazanzibari ndio waliosaidia kuweka shinikizo suala la muungano liwe sehemu ya muswada husika, hivyo kutoa fursa kwa Tanganyika kujadiliwa. Hakuna ushahidi sehemu yoyote kwamba wananchi wa Tanzania bara walikuwa wamejiandaa to revolt. Kwa maana nyingine, tukubali ukweli kwamba madai ya Tanganyika kwa wabara walio wengi yana uhusiano wa moja kwa moja na harakati za wazanzibari kudai autonomy yao, na ni harakati hizo ndio zimewazindua watanganyika wengi kutoka kwenye usingizi mzito. Kwa hilo, binafsi nawashukuru sana wazanzibari.
Nikijikita kwenye hoja yangu ya msingi katika bandiko hili, tutazame, je malalamiko makubwa ya wazanzibari juu ya muungano ni yepi?
1. Tanganyika inafaidika zaidi kuliko Zanzibar kwani chini ya mfumo uliopo, Tanganyika ndio Tanzania. Hoja hii imejadiliwa na tume ya warioba kwa hoja kwamba "Tanganyika imevaa koti la serikali ya muungano".
Je kuna ukweli katika hili? Binafsi nasema NDIO, ukweli upo tena mkubwa sana lakini utaugundua iwapo utafanikiwa kutambua kiini macho kilichopo. Kwa mfano:
Kwa mujibu wa katiba ya JMT (1977), chombo chenye mamlaka ya kusimamia masuala ya muungano ni serikali ya muungano. Lakini pia chombo chenye mamlaka ya kusimamia masuala yasiyo ya muungano (the so called "Tanzania Bara"), pia ni serikali ya muungano. Kama hadi hapa tupo sawa, tuendelee:
Kwa mantiki hiyo, ni serikali ya muungano ndio inayoshughulikia sana masuala kama vile ujenzi, uchukuzi, afya, kilimo, maji, maliasili na utalii,elimu, nishati na madini, na mengine mengi tu ambayo kimsingi ni ya Tanzania bara na sio ya muungano. Iwapo tupo sawa hadi hapa, tuendelee:
Wakati wa vikao vya bajeti ya bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania (chombo ambacho kipo kuwakilisha maslahi ya wa zanzibari na watanganyika equally), je:
*bunge hutenga siku ngapi kujadili masuala ya Tanzania Bara (Tanganyika)? Siku mbili hadi Nne. Je:
*bunge hutenga siku ngapi kujadili mambo ya muungano? Nusu siku hadi siku moja!
Suala lingine muhimu ni kwamba - maswali ya wabunge kuhusu mambo yanayowagusa sana wananchi (development and poverty issues) yanahusu zaidi Tanzania bara na mambo haya bungeni yanasimamiwa na waziri mkuu ambae hana mamlaka wala madaraka ya aina yoyote kwa zanzibar. Je haki za kimaendeleo za wazanzibari katika bunge la JMT chini ya mfumo wa sasa zinasimamiwa na nani?
Lalamiko lingine kubwa la wazanzibari dhidi ya mfumo wa serikali mbili ni kwamba - mambo ya muungano yamekuwa yakiongezeka na hivyo kuathiri "identity" na "autonomy" ya zanzibar na kupelekea znz kuwa katika hatari ya kumezwa. Lalamiko hili pia kwa mtazamo wangu lina mashiko, na tumeshajadili sana huko nyuma jinsi gani mkataba wa muungano (1964) ulichakachuliwa na kufikisha taifa katika sakata la jumbe la 1984.
Lalamiko lingine kubwa la wazanzibar ni kwamba Rais wao ameondolewa katika umakamo wa rais wa JMT. Mkataba wa muungano ulimtaja rais wa znz kuwa makamo wa rais katika kipindi cha mpito kuelekea katiba mpya, lakini kama tunavyoelewa, mchakato wa katiba hiyo haukutokea, ikaja katiba ya muda ya JMT (1965) ambayo ikiangiza chama cha TANU kwenye muungano kinyume na mkataba wa muungano (1964). Pamoja na mapungufu yote haya, rais wa znz akaendelea kuwa makamo wa rais mpaka pale weakness za legal and political framework za union zilipokuja kuwa dhahiri kufuatia mfumo wa vyama vingi. Muungano ambao Nyerere alieleza umma kwamba umeiga muungano wa uingereza ambayo inafuata a unitary form of government, miaka ya mwanzo ya tisini jaji bomani akapewa jukumu la kutatua kitendawili cha muungano ndani ya mfumo wa vyama vingi, akaja na solution ya mgombea mwenza kwa kuiga mfumo wa federation wa marekani ili kuepusha ccm na aibu ya kupata rais wa ccm upande wa bara na rais wa Upinzani upande wa zanzibar. Hapa tukabaki kujiuliza, ni muungano gani huu unaoazima elements za federation wakati tuliambiwa msingi wake ni unitary?Ni katika mazingira haya, rais wa znz akaondolewa kwenye umakamu wa rais wa JMT. Sasa cha ajabu nini hapa kwa znz kuanza kufukiria mchakato wa katiba yake ambayo lengo ni kulipa taifa lao madaraka kamili?
Upande wa bara nao una malalamiko mengi lakini muhimu ni pamoja na:
1. Zanzibar imebadili katiba yake na kuchukua madaraka ya jamhuri ya muungano kwa mfano kuelekeza sheria za muungano zilizopitishwa na bunge la JMT kupelekwa kwenye BLW. Kwa mantiki hii, katiba ya zanzibar sasa ipo juu ya katiba ya JMT, na tukumbuke hapa kwamba katiba ya JMT ndio katiba ya Tanzania bara au ukipenda Tanganyika. Kwahiyo maamuzi juu ya hali za maisha ya watanzania bara au ukitaka watanganyika milioni 43 kuanzia 2010 yapo mikononi mwa BLW linalowakilisha wananchi sio zaidi ya milioni moja na nusu.
Lalamiko la pili kubwa kwa upande wetu Bara ni kwamba - wananchi wetu hawana haki ya kumiliki ardhi znz wakati wenzetu wa znz wanayo haki hiyo tanzania bara au ukipenda Tanganyika.
Eneo lingine na malalamiko upande wa bara ni kwamba - zanzibar sasa imekuwa ni nchi huru, ina bendera yake wimbo wa taifa serikali yake na imeshabadili katiba yake ili ijitambue kama nchi wakati kwa mantiki hii Tanzania bara imeshapoteza utambulisho wake kwani katiba ya JMT inasema Tanzania ni nchi moja wakati katiba ya znz inasema Tanzania ni nchi mbili. Katika hili, kuna makosa gani kwa rasimu ya katiba kusema Tanzania ni nchi inayotokana na Tanganyika na zanzibar? Kwani ni dhahiri katika suala la utambulisho wao kama taifa, zanzibar haitarudi nyuma tena.
Nadhani haya ni baadhi ya mambo ambayo wawakilishi wetu kwenye bunge lijalo la katiba wakayakumbuka.
Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums