CCM msije mkatufikisha huku tafadhali

CCM msije mkatufikisha huku tafadhali

SEKRETARIETI KATOLIKI

MKUTANO WA MAASKOFU TANZANIA

P.O Box 2133

SIMU:022/2851075-7-8

022/2850047

022/2850017

FAX 022/2851133; 2850427

DOMAIN, TEC.CO.TZ

Barua pepe: ifo@tec.or.tz

DAR ES SALAAM TANZANIA

Idara: RAIS

Rejea: TEC/Pr.No.44/2025

WARAKA WA KICHUNGAJI KUSOMWA KATIKA PAROKIA ZOTE, VIGANGO, NA JUMUIYA NDOGO NDOGO ZOTE NCHINI TΑΝΖΑΝΙΑ KWA WEEK 10 MFULULIZO

Tarehe: Mei 2, 2025

"Heri wenye njaa na kiu ya haki, maana hao watashibishwa." (Mathayo 5:6)

Mwito wa Haki, Amani, na Uadilifu wa Kanisa

Ndugu wapendwa katika Kristo,

Neema na amani kutoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi daima.

Kwa masikitiko makubwa na hali ya wasiwasi wa haki, tunawaandikia leo kama maaskofu wenu na walezi wa maisha ya kiroho. Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) linatoa onyo kali kwa watawala dhidi ya jaribio lililoshindikana la mauaji ya Padri Dkt. Charles Kitima, Katibu Mkuu wa sasa wa TEC.

Kwa miaka mingi, Padre Kitima amelitumikia Kanisa na jamii kwa uaminifu kwa kuendeleza maadili ya ukweli, haki, heshima ya utu wa binadamu, na utawala bora, sambamba na mafundisho ya kijamii ya Kanisa. Kupitia mchango wake wa wazi kwa jamii, amekuwa mstari wa mbele kuwakumbusha wananchi wote wakiwemo viongozi juu ya wajibu wao wa kimaadili wa kulinda haki na maslahi ya wote.

Shambulio hili la kikatili siyo tu jaribio la kumdhuru mtu binafsi, bali ni shambulio la moja kwa moja dhidi ya wito wa kinabii wa Kanisa na misingi ya kidemokrasia inayopaswa kutamalaki katika jamii yoyote inayotafuta haki.

Wito wa Kanisa Katoliki na Tishio kwa Haki

Bwana wetu Yesu Kristo alifundisha kwamba, "Nanyi mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru." (Yohana 8:32). Kanisa, likiongozwa na ukweli huu, lina dhamira ya kudumu ya kutetea haki, uadilifu, na heshima ya kila maisha ya binadamu bila kujali dini, kabila au cheo chake

Juhudi za Padre Kitima za kuwaelimisha waamini na jamii kwa ujumla kuhusu uadilifu wa uchaguzi, haki za kikatiba, na uwajibikaji wa uongozi, zimeonekana kukwamisha mamlaka fulani. Maaskofu wa TEC wanaamini kwamba tukio hili ni juhudi ya makusudi ya
kulitisha Kanisa na kulinyamazisha katika wito wake wa kuhamasisha uelewa wa uraia na mabadiliko ya kisiasa.

Maamuzi ya Kiaskofu na Maelekezo kwa Waamini Kote Nchini

Katika tafakari ya kiroho na kwa kutekeleza wajibu wetu wa kiaskofu wa kuliongoza na kulilinda Kanisa, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania limeazimia kama ifuatavyo:

Mpaka pale Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itakapofanya yafuatayo:

Kukubali na kutekeleza mageuzi ya kina ya mfumo wa kisheria na uchaguzi;

Kuhakikisha usalama wa raia wote, wakiwemo viongozi wa dini wanaosema ukweli kwa amani;

Waamini wote Wakatoliki nchini Tanzania wanaelekezwa kujiepusha na shughuli zozote zitakazohusiana na uchaguzi mkuu ujao. Hasa:

1. Muumini wa Kanisa Katoliki asijitokeze kuchukua form ya kugombea au kukubali kuteuliwa kugombea nafasi ya udiwani, ubunge, au urais kupitia chama chochote cha siasa.

2. Wakatoliki kutoshiriki katika zoezi la kuhuisha daftari la wapiga kura.

3. Wakatoliki kutoshiriki wala kuhudhuria mikutano ya kampeni za kisiasa.

4. Wakatoliki kujizuia kushiriki kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Hatua hii ni msimamo wa amani na kimaadili, dhidi ya mfumo unaoonekana kuendeleza ukandamizaji na kukataa uwajibikaji. Hii siyo kujiondoa kwenye majukumu ya uraia, bali ni kitendo cha kiroho na cha kutafakari kwa kina dhidi ya ukosefu wa haki.

Manabii wa kale walielezea wazi hali kama hii. Nabii Isaya anasema: "Ole wao waandikao amri za uovu, na waandikawo maneno ya jeuri ili kuwanyima maskini haki zao." (Isaya 10:1-2)

Mwito wa Sala na Uangalizi

Tunawaalika watu wote wenye mapenzi mema ndani na nje ya Kanisa Katoliki kusimama nasi kwa mshikamano, sala, na utetezi wa amani. Tumuombe Mungu kwa ajili ya uponyaji kamili wa Padre Kitima, kwa haki kushinda, na kwa upya wa msingi wa maadili na demokrasia ya taifa letu.

Tunaliweka taifa letu mikononi mwa Mama Bikira Maria, Malkia wa Amani, na chini ya rehema na haki ya Bwana wetu Yesu Kristo.

Bwana awabariki na kuwalinda wote wanaotafuta amani na haki kwa jina lake.

Kwa huduma ya Kristo,

Askofu Eusebius Nzigilwa

Makamu wa Rais, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Imetolewa kuelekea Jumapili ya Nne ya Pasaka Mei 2, 2025
 
Mbona tushafika huko mkuu,au ulitaka uone nini uamini kama tumefika.
 
Polis wamepata ajali wananchi wamegoma kuwasaidia kisa ni polisi kutumika na serikali kukandamiiza wananchi...UgandaView attachment 3322516
Alooooooo! Ni hatari yaani wanalia Kwa maumivu lakini nasikia sauti ya mwanamke akisema wanalia Nini, wengine wasema wacha wakufe. Ni hatari sana.

Siku Moja mkoa Fulani wanajeshi walikuwa wanapita sasa walihitaji msaada Fulani katika eneo Hilo Ili waendelee na safari maana gari Yao ilipata hitilafu Fulani, raia walijitokeza Kwa ufindi wao na kikamilisha service ndani ya dakika Kumi. Lakini raia wema walisikika wakisema wangekuwa polisi tusingewasaidia kabisa na wangekoma.
 
Mi hua nawaza, ikitokea vita saiz, ule uzalendo wa wananchi kipindi cha Ile vita ya Kagera, utakuwepo hata kidogo?
Nani apigane vita za kisng ili wanasiasa wale mema ya nchi halafu baadae watuue ? Watapigana wao na watoto wao na uzuri Tanzania imepakana na nchi nyingi ni kutorokea tu nchi jirani.

Vita za kifala unawachia tu mafala
 
Ili polisi wetu wasifike huku wanasiasa wasiwaingilie.

Umeona Bashungwa MTU anyajipa picha ya upole kumbe ndo anawatumia polisi
Bashungwa amenisikitisha sana
Nimekumbuka msemo

Ukitaka kujuwa tabia ya mtu ngoja apate pesa
 
Sasa hivi inatakiwa hata misiba ya wanasiasa wa CCM na polisi tupunguze kiherehere cha kuhudhuria hawa jamaa ni wapuuzi sanaa hata kama ni jirani yako akili yake inawaza wewe ujichanganye akushughulikie na sio kukusaidia.
 
SEKRETARIETI KATOLIKI

MKUTANO WA MAASKOFU TANZANIA

P.O Box 2133

SIMU:022/2851075-7-8

022/2850047

022/2850017

FAX 022/2851133; 2850427

DOMAIN, TEC.CO.TZ

Barua pepe: ifo@tec.or.tz

DAR ES SALAAM TANZANIA

Idara: RAIS

Rejea: TEC/Pr.No.44/2025

WARAKA WA KICHUNGAJI KUSOMWA KATIKA PAROKIA ZOTE, VIGANGO, NA JUMUIYA NDOGO NDOGO ZOTE NCHINI TΑΝΖΑΝΙΑ KWA WEEK 10 MFULULIZO

Tarehe: Mei 2, 2025

"Heri wenye njaa na kiu ya haki, maana hao watashibishwa." (Mathayo 5:6)

Mwito wa Haki, Amani, na Uadilifu wa Kanisa

Ndugu wapendwa katika Kristo,

Neema na amani kutoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi daima.

Kwa masikitiko makubwa na hali ya wasiwasi wa haki, tunawaandikia leo kama maaskofu wenu na walezi wa maisha ya kiroho. Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) linatoa onyo kali kwa watawala dhidi ya jaribio lililoshindikana la mauaji ya Padri Dkt. Charles Kitima, Katibu Mkuu wa sasa wa TEC.

Kwa miaka mingi, Padre Kitima amelitumikia Kanisa na jamii kwa uaminifu kwa kuendeleza maadili ya ukweli, haki, heshima ya utu wa binadamu, na utawala bora, sambamba na mafundisho ya kijamii ya Kanisa. Kupitia mchango wake wa wazi kwa jamii, amekuwa mstari wa mbele kuwakumbusha wananchi wote wakiwemo viongozi juu ya wajibu wao wa kimaadili wa kulinda haki na maslahi ya wote.

Shambulio hili la kikatili siyo tu jaribio la kumdhuru mtu binafsi, bali ni shambulio la moja kwa moja dhidi ya wito wa kinabii wa Kanisa na misingi ya kidemokrasia inayopaswa kutamalaki katika jamii yoyote inayotafuta haki.

Wito wa Kanisa Katoliki na Tishio kwa Haki

Bwana wetu Yesu Kristo alifundisha kwamba, "Nanyi mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru." (Yohana 8:32). Kanisa, likiongozwa na ukweli huu, lina dhamira ya kudumu ya kutetea haki, uadilifu, na heshima ya kila maisha ya binadamu bila kujali dini, kabila au cheo chake

Juhudi za Padre Kitima za kuwaelimisha waamini na jamii kwa ujumla kuhusu uadilifu wa uchaguzi, haki za kikatiba, na uwajibikaji wa uongozi, zimeonekana kukwamisha mamlaka fulani. Maaskofu wa TEC wanaamini kwamba tukio hili ni juhudi ya makusudi ya
kulitisha Kanisa na kulinyamazisha katika wito wake wa kuhamasisha uelewa wa uraia na mabadiliko ya kisiasa.

Maamuzi ya Kiaskofu na Maelekezo kwa Waamini Kote Nchini

Katika tafakari ya kiroho na kwa kutekeleza wajibu wetu wa kiaskofu wa kuliongoza na kulilinda Kanisa, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania limeazimia kama ifuatavyo:

Mpaka pale Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itakapofanya yafuatayo:

Kukubali na kutekeleza mageuzi ya kina ya mfumo wa kisheria na uchaguzi;

Kuhakikisha usalama wa raia wote, wakiwemo viongozi wa dini wanaosema ukweli kwa amani;

Waamini wote Wakatoliki nchini Tanzania wanaelekezwa kujiepusha na shughuli zozote zitakazohusiana na uchaguzi mkuu ujao. Hasa:

1. Muumini wa Kanisa Katoliki asijitokeze kuchukua form ya kugombea au kukubali kuteuliwa kugombea nafasi ya udiwani, ubunge, au urais kupitia chama chochote cha siasa.

2. Wakatoliki kutoshiriki katika zoezi la kuhuisha daftari la wapiga kura.

3. Wakatoliki kutoshiriki wala kuhudhuria mikutano ya kampeni za kisiasa.

4. Wakatoliki kujizuia kushiriki kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Hatua hii ni msimamo wa amani na kimaadili, dhidi ya mfumo unaoonekana kuendeleza ukandamizaji na kukataa uwajibikaji. Hii siyo kujiondoa kwenye majukumu ya uraia, bali ni kitendo cha kiroho na cha kutafakari kwa kina dhidi ya ukosefu wa haki.

Manabii wa kale walielezea wazi hali kama hii. Nabii Isaya anasema: "Ole wao waandikao amri za uovu, na waandikawo maneno ya jeuri ili kuwanyima maskini haki zao." (Isaya 10:1-2)

Mwito wa Sala na Uangalizi

Tunawaalika watu wote wenye mapenzi mema ndani na nje ya Kanisa Katoliki kusimama nasi kwa mshikamano, sala, na utetezi wa amani. Tumuombe Mungu kwa ajili ya uponyaji kamili wa Padre Kitima, kwa haki kushinda, na kwa upya wa msingi wa maadili na demokrasia ya taifa letu.

Tunaliweka taifa letu mikononi mwa Mama Bikira Maria, Malkia wa Amani, na chini ya rehema na haki ya Bwana wetu Yesu Kristo.

Bwana awabariki na kuwalinda wote wanaotafuta amani na haki kwa jina lake.

Kwa huduma ya Kristo,

Askofu Eusebius Nzigilwa

Makamu wa Rais, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Imetolewa kuelekea Jumapili ya Nne ya Pasaka Mei 2, 2025
Mshana ninashida na wewe naomba kuongea na wewe
 
Back
Top Bottom