Mwingereza
JF-Expert Member
- Jan 21, 2014
- 1,111
- 2,752
Muda siyo mrefu nimefika nyumbani kwangu, nikamkuta mamangu ambaye, mke wangu ambaye pia ni mtumishi, mdogo wangu wa kike wote wakiwa wananisubiri. Baada ya salamu, wakaniomba kadi yangu ya CCM. Kwa vile nilikuwa sijui nini kinaendelea, na kwa nia nzuri wakati navua viatu, nikamwambia mke wangu kadi ilipo. Akaenda kuichukua, akatoka nje akalimwagia mafuta taa na kuliwasha moto.
Cha ajabu, wote hapa nyumbani na hata wake za majirani, zoezi ilikuwa ni kuchoma kadi za CCM. Madai yahoo hawataki udikteta wa CCM. Inasemekana hapa kinondoni wamechoma kadi 120. Mabazo ni za CCM. Kila mwanamke alihakikisha amechoma kadi ya mumewe
Bila kuficha, mimi ni kada mkubwa wa CCM ingawa sijabahatika kwenye teuzi, ila nimekipigania chama tangu mwaka 89. Leo nyumba yangu hakuna kadi ya CCM na mke wangu ananitishia kwamba akiniona na watu wa CCM ananiachia mji na watu wangu wa CCM. Hii inaweza kiawa na madhara makubwa sana, hasa chama dola ikiwa kwenye wakati kama huu, kwani wanawake ndio wapiga kura wakubwa wa CCM.
Mimi ni mana CCM aliyebakia bila kadi.
Cha ajabu, wote hapa nyumbani na hata wake za majirani, zoezi ilikuwa ni kuchoma kadi za CCM. Madai yahoo hawataki udikteta wa CCM. Inasemekana hapa kinondoni wamechoma kadi 120. Mabazo ni za CCM. Kila mwanamke alihakikisha amechoma kadi ya mumewe
Bila kuficha, mimi ni kada mkubwa wa CCM ingawa sijabahatika kwenye teuzi, ila nimekipigania chama tangu mwaka 89. Leo nyumba yangu hakuna kadi ya CCM na mke wangu ananitishia kwamba akiniona na watu wa CCM ananiachia mji na watu wangu wa CCM. Hii inaweza kiawa na madhara makubwa sana, hasa chama dola ikiwa kwenye wakati kama huu, kwani wanawake ndio wapiga kura wakubwa wa CCM.
Mimi ni mana CCM aliyebakia bila kadi.