Ex Spy
JF-Expert Member
- Jan 15, 2007
- 213
- 1,726
Ingawa uchaguzi wa kura za maoni CCM umeshafanyika na mbunge anayeshikilia kiti hicho ndugu Abdulkarim Sha au BULJI alimshinda OMAR KIMBAU lakini katika kuonyesha kutoridhishwa kwa maamuzi ya Kidemokrasia yaliyofikiwa na wana-kisiwa cha Mafia, Omar Kimbau ameamua kukata rufaa kwa madai kuwa daftari la Kilindoni lilibadilishwa na pia kawalalamikia PCCB kuwa hawafanyi kazi zao kadiri inavyotakiwa huku akijisifia kuwa wajumbe wote wa CCM wa PWANI wako MFUKONI MWAKE.
Haya ni baadhi ya maelezo niliyoyapata toka Mafia kwa wana-CCM:
1. Ukweli ni kuwa PCCB makosa yaliyoyafanya ni kutomkamata Omar Kimbau ambaye amekuwa akijisifia kuwa PCCB hawana ubavu wa kumkamata
2. Uchaguzi umekwisha salama na wana Mafia wametoa maamuzi kuwa Shah aendelee kuwa mbunge wao
3. Uhusiano wa CUF na OMAR KIMBAU utapelekea CCM kukikosa kisiwa cha Mafia kwani kitendo cha mashabiki wa Omari ambao ni CUF kumpigia kura kinaweza kubackfire na CUF ikaingia madarakani kwa mgongo wa OMARI KIMBAU
4. Kitendo cha DC wa Mafia bwana MANGOCHIE MANZIE kunyamaza kimya kwenye hili sakata ni kithibitisho rasmi kuwa kweli alikuwa anamshabikia mwana mama kwa jina la HAFSA ambaye anafanyakazi kwenye mooja ya jumuia za Umoja wa Mataifa jijini DAR
5. Kwa sababu DC hayupo Mafia, Polisi wamekuwa wakikamata watu hovyo kwa amri ya Omari Kimbau kinyume na sheria
6. Kitendo cha Katibu Mkuu CCM bwana YUSUF MAKAMBA kutoa amri uchaguzi ufanyike Mafia bila kufuata taratibu za Chama ni kithibitisho tosha kuwa sheria inapindwa ili kulazimisha Omari Kimbau ashinde.
7. Kikao cha Chama wilayani kimeamua Uchaguzi usirudiwe sasa iweje MAKAMBA atoe amri tuu pasipo fuata taratibu? Na Kama hali ikiendelea hivi sisi tuko tayari kwa lolote lile INCLUDING kurudisha kadi za CCM na kuwapa CUF kura zetu.
8. Mwisho ningependa kuwafahamisha wakuu wa Usalama kuwa kama hali ya uonevu haitoangaliwa ma makini damu itakuwja kumwagika kwani sisi tushachoka na hatuwezi kuendelea kuwa watumwa wao mwaka nenda rudi.
9. Msimamo wetu wa kutopiga kura uko pale pale na tungeomba MAAMUZI YETU yaheshimiwe.
10. Tunalaani vikali kitendo cha Katibu Mkuu Makamba kuingilia chaguzi zinazoendelea na tunapenda kumfahamisha kuwa ndiyo anakipeleka chama shimoni kabisa.
Haya ni baadhi ya maelezo niliyoyapata toka Mafia kwa wana-CCM:
1. Ukweli ni kuwa PCCB makosa yaliyoyafanya ni kutomkamata Omar Kimbau ambaye amekuwa akijisifia kuwa PCCB hawana ubavu wa kumkamata
2. Uchaguzi umekwisha salama na wana Mafia wametoa maamuzi kuwa Shah aendelee kuwa mbunge wao
3. Uhusiano wa CUF na OMAR KIMBAU utapelekea CCM kukikosa kisiwa cha Mafia kwani kitendo cha mashabiki wa Omari ambao ni CUF kumpigia kura kinaweza kubackfire na CUF ikaingia madarakani kwa mgongo wa OMARI KIMBAU
4. Kitendo cha DC wa Mafia bwana MANGOCHIE MANZIE kunyamaza kimya kwenye hili sakata ni kithibitisho rasmi kuwa kweli alikuwa anamshabikia mwana mama kwa jina la HAFSA ambaye anafanyakazi kwenye mooja ya jumuia za Umoja wa Mataifa jijini DAR
5. Kwa sababu DC hayupo Mafia, Polisi wamekuwa wakikamata watu hovyo kwa amri ya Omari Kimbau kinyume na sheria
6. Kitendo cha Katibu Mkuu CCM bwana YUSUF MAKAMBA kutoa amri uchaguzi ufanyike Mafia bila kufuata taratibu za Chama ni kithibitisho tosha kuwa sheria inapindwa ili kulazimisha Omari Kimbau ashinde.
7. Kikao cha Chama wilayani kimeamua Uchaguzi usirudiwe sasa iweje MAKAMBA atoe amri tuu pasipo fuata taratibu? Na Kama hali ikiendelea hivi sisi tuko tayari kwa lolote lile INCLUDING kurudisha kadi za CCM na kuwapa CUF kura zetu.
8. Mwisho ningependa kuwafahamisha wakuu wa Usalama kuwa kama hali ya uonevu haitoangaliwa ma makini damu itakuwja kumwagika kwani sisi tushachoka na hatuwezi kuendelea kuwa watumwa wao mwaka nenda rudi.
9. Msimamo wetu wa kutopiga kura uko pale pale na tungeomba MAAMUZI YETU yaheshimiwe.
10. Tunalaani vikali kitendo cha Katibu Mkuu Makamba kuingilia chaguzi zinazoendelea na tunapenda kumfahamisha kuwa ndiyo anakipeleka chama shimoni kabisa.