Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,014
- 144,372
Nashangazwa sana na sifa za kinafiki CCM wanazoompa Dr. Slaa leo hii wakati ni CCM hawa hawa walimuita muongo na mzushi wakati alipokuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA.
Isitoshe, ni CCM hawa hawa kupitia serikali ya Kikwete, walimpiga Dr. Slaa virungu wakati wa maandamano ya CHADEMA mkoani Arusha na hata aliekuwa mchumba wa Dr. Slaa nae hakusalimika pamoja na wanachama na viongozi wengine wa CHADEMA.
Kama kuna mwenye ushahidi wa viongozi wa CCM na serikali yake kumsifia Dr. Slaa wakati yuko CHADEMA auweke hapa tuondoe ubishi.
Hata hivyo, muda umetusaidi kugundua kuwa Dr. Slaa naye hakuwa akipinga sera na matendo ya CCM kutoka moyoni, bali alikuwa akifanya vile kutetea kibarua chake kwani mpinzani wa kweli huwezi kurudi CCM wakati CCM ni ile ile kwa sera na matendo yako.
Angekuwa serious, angetafuta chama kingine lakini sio kwenda kutumia serikali ya chama kilekile alichokuwa anakipinga na hivyo hakuwa na tofauti na viongozi wa CHADEMA waliompokea Lowassa kama kweli hiyo ndio ilikuwa hoja yake kuu.
CCM acheni unafiki tena unafiki wa kiwango cha SGR katika swala hili. Msitufanye wajinga na hatuna kumbukumbu.
Isitoshe, ni CCM hawa hawa kupitia serikali ya Kikwete, walimpiga Dr. Slaa virungu wakati wa maandamano ya CHADEMA mkoani Arusha na hata aliekuwa mchumba wa Dr. Slaa nae hakusalimika pamoja na wanachama na viongozi wengine wa CHADEMA.
Kama kuna mwenye ushahidi wa viongozi wa CCM na serikali yake kumsifia Dr. Slaa wakati yuko CHADEMA auweke hapa tuondoe ubishi.
Hata hivyo, muda umetusaidi kugundua kuwa Dr. Slaa naye hakuwa akipinga sera na matendo ya CCM kutoka moyoni, bali alikuwa akifanya vile kutetea kibarua chake kwani mpinzani wa kweli huwezi kurudi CCM wakati CCM ni ile ile kwa sera na matendo yako.
Angekuwa serious, angetafuta chama kingine lakini sio kwenda kutumia serikali ya chama kilekile alichokuwa anakipinga na hivyo hakuwa na tofauti na viongozi wa CHADEMA waliompokea Lowassa kama kweli hiyo ndio ilikuwa hoja yake kuu.
CCM acheni unafiki tena unafiki wa kiwango cha SGR katika swala hili. Msitufanye wajinga na hatuna kumbukumbu.