CCM Kubadili Jina ili Kupata Mvuto.

CCM Kubadili Jina ili Kupata Mvuto.

tena wakibadilisha jina ndiyo siku yao ya kufa itawadia
 
Wanajivua gamba mpaka jina! Wanafikiri kobe ukamuita duma atakimbia,wasituzingue.
 
Hata hivyo neno "MAPINDUZI" limekuwa likinichanganya sana....! Lakini hivi ni lini mgonjwa akabatizwa kuahirisha kifo chake?
 
Jaman jaman,kweli ccm wamepoteza kabisa, kujivua gamba hakijawatosha!ushauri wangu kwa kuwasaidia ccm wajiite NYERERE PARTY itawasaidia kuwakamata akina fulan japokuwa wamepungua cku hizi,yaani wale wanaosema Njomba,Mkapa kapata Unyerere.
Wakijiita hivyo mimi nitaanza kupinga na kwenda mahakamani, maana wapo watu wanaoitwa hivyo lakini sio wana CCM.....!
 
hivi kusingetokea 'Mapinduzi ya Zanzibar' hili jina Chama cha 'Mapinduzi' kuna mtu hata angefikiri kuwa liwe jina la chama?
 
wameona mbali! Wamejua cdm kitakuwa chama tawala ndoo maana wanaandaa chama kingine cha upnzani.
 
Habari za ndani za na za kiintelijensia nilizozipata zinasema, Chama Cha Mapinduzi (CCM), kinampango wa kubadili jina hilo, ili kukiletea mvuto wake wa asili kwa wananchi.
Habari hizo zinazidi kudai kuwa, mchakato utawakilishwa katika siku ya kuadhimisha miaka 50 ya uhuru, na mipango ya kutoa mapendekezo ya jina mbadala litakalotumiwa utaanza rasmi ili ikiwezekana litumike katika uchaguzi ujao.

Hali hiyo inatokana na CCM kupoteza umaarufu hivyo kutishia uwezekano wa kupotea katika ulimwengu wa kisiasa ifikapo mwaka 2025.

Hivi sasa CCM inadai kutumia nguvu na rasilimali nyingi katikai kuuza sera zake kwa wananchi, kitu ambacho ni tofauti na chama kikuu cha upinzani CHADEMA.

Tatizo sio jina ila mtazamo wao wa kuweka maslahi mbele kwa mafisadi badala ya walalahoi.
 
mmmmh,vpi kuhusu rangi nayo wabadili?,maana siku hzi nguo zenye rangi ya njano na kijani hazinunuliki kabisa hata kama si ya magamba!.
wamesababisha hata marefa kuichukia timu ya Yanga msimu huu.
 
Labda el shabab! Katibu mkuu aliyevuliwa gamba alisema anakwenda kuwaandalia makao. Je ni wapi huko? Ni swala la wakati tu sasa. Bye bye
 
Sishangai kwa sababu waliwahi kuita rushwa takrima !!!!!!!!!
 
Hivi si walisha badili jina hawa? Kwani magamba ni jina la chama gani?
1.ccm ni jina la ubatizo .
2.magamba ni jina la kipaimara .
3.maiti ndo jina la mwisho kupewa
 
Hata kama wangejiita MALAIKA hatutawasahau kwa mabaya yote waliyokwisha kutufanyia(wananchi),Kama vidonda vitapona basi makovu yake tutakuja kuwaonyesha wajukuu zetu.
 
Habari za ndani za na za kiintelijensia nilizozipata zinasema, Chama Cha Mapinduzi (CCM), kinampango wa kubadili jina hilo, ili kukiletea mvuto wake wa asili kwa wananchi.
Habari hizo zinazidi kudai kuwa, mchakato utawakilishwa katika siku ya kuadhimisha miaka 50 ya uhuru, na mipango ya kutoa mapendekezo ya jina mbadala litakalotumiwa utaanza rasmi ili ikiwezekana litumike katika uchaguzi ujao.

Hali hiyo inatokana na CCM kupoteza umaarufu hivyo kutishia uwezekano wa kupotea katika ulimwengu wa kisiasa ifikapo mwaka 2025.

Hivi sasa CCM inadai kutumia nguvu na rasilimali nyingi katikai kuuza sera zake kwa wananchi, kitu ambacho ni tofauti na chama kikuu cha upinzani CHADEMA.

hata wakibadili wanachama wake si lolote si chochote tutawakataa tu
 
Back
Top Bottom